You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Ilidaiwa kwamba maaskofu walikuwa badala ya mitume. Kwa namna fulani uaskofu
ulitokana na mitume, yaani maaskofu waliwekwa na mitume kuwa watawala katika kanisa
na mamlaka ya utawala wao ilihusisha kuhubiri na kuitetea Injili.
Umoja Wa Ibada
Ibada mbalimbali zilizokuwa zikifanywa na kanisa kwa pamoja zilisaidia kukuza umoja wa
kanisa na kutokea kwa viongozi wenye mamlaka. Kulikuwa na ibada mbalimbali ambazo
zilifanywa na kanisa, baadhi ya ibada hizo ni ibada ya ubatizo na ibada ya meza ya
Bwana. Pia kanisa liliadhimisha sikukuu mbalimbali ambazo pia kwa namna fulani
zilichangia kukuza umoja wa kanisa.
H. MABISHANO YA KITHIOLOJIA.
Mabishano ya kitheolojia yalikuwa ni majadiliano ya mafundisho na mitazamo mbalimbali
ya kitheolojia na kiuongozi iliyokuwa ikiibuliwa na baadhi ya viongozi wa kanisa.
Kutokana na kutofautiana mitazamo juu ya hoja Fulani za kitheolojia mababa wa kanisa
walibishana na kuitisha mikutano ili kuweza kutoa suluhu juu ya tofauti hizo za
kimafundisho na kitheolojia. Kundi la walioshindwa katika mikutano hiyo lilihukumiwa na
kuitwa wazushi na kisha kutengwa na kanisa.
Mabishano ya kithiolojia yalisababishwa na mitazamo mbalimbali ambayo wakristo
walikuwa nayo juu ya Yesu Kristo. Baadhi ya mitazamo hiyo ni .
Uungu wa Yesu Kristo.
Wakristo wa awali walimpa Yesu heshima kwa kumwita majina mbalimbali kama vile
Masihi, Kurios, Kritos na Logos.
Jina la Logosi lilitokana na falsafa za kigiriki, Kutokana na falsafa hizo Logos ilikuwa ni
njia ya Mungu kufanyika mwili na kukaa na watu hapa duniani. Hivyo wakristo wa awali
walimtambua Yesu kama Mungu.
Kristo kama Logosi.
Katika kipindi cha karne ya pili na ya tatu karibu wanazuoni wote wa kikiristo
walifundisha kwamba Kristo alikuwa ni Logos. Kulikuwa na mwanazuoni moja aliyeitwa
Yustini Shahidi ambae aliweka mkazo kuwa Logos alikuwa ni Mungu wa pili.
Wanazuoni wengine waliweka mkazo katika umoja wa Yesu.Walikubali kwamba Logos
amefanyika kuwa mwili katika Yesu Kristo lakini alikuwa ni Mungu halisi, Mungu
mwana ndiye aliyefanyika mwili, si Mungu wa pili. Kulingana na mtazamo waYustini ni
dhahiri kwamba alikana ubinadamu wa Yesu. Yesu kama Logos alikuwa Kweli Mungu
na mwanadamu kweli.
Monarchianism. Dhana ya Mungu mmoja.
Kulikuwa na wanazuoni wengine waliopinga mafundisho ya kumhusisha Yesu na Logos
kwa sababu jambo hili lilielekea kupinga imani yakuwa Mungu ni mmoja. Wanazuoni
31