21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Ilidaiwa kwamba maaskofu walikuwa badala ya mitume. Kwa namna fulani uaskofu

ulitokana na mitume, yaani maaskofu waliwekwa na mitume kuwa watawala katika kanisa

na mamlaka ya utawala wao ilihusisha kuhubiri na kuitetea Injili.

Umoja Wa Ibada

Ibada mbalimbali zilizokuwa zikifanywa na kanisa kwa pamoja zilisaidia kukuza umoja wa

kanisa na kutokea kwa viongozi wenye mamlaka. Kulikuwa na ibada mbalimbali ambazo

zilifanywa na kanisa, baadhi ya ibada hizo ni ibada ya ubatizo na ibada ya meza ya

Bwana. Pia kanisa liliadhimisha sikukuu mbalimbali ambazo pia kwa namna fulani

zilichangia kukuza umoja wa kanisa.

H. MABISHANO YA KITHIOLOJIA.

Mabishano ya kitheolojia yalikuwa ni majadiliano ya mafundisho na mitazamo mbalimbali

ya kitheolojia na kiuongozi iliyokuwa ikiibuliwa na baadhi ya viongozi wa kanisa.

Kutokana na kutofautiana mitazamo juu ya hoja Fulani za kitheolojia mababa wa kanisa

walibishana na kuitisha mikutano ili kuweza kutoa suluhu juu ya tofauti hizo za

kimafundisho na kitheolojia. Kundi la walioshindwa katika mikutano hiyo lilihukumiwa na

kuitwa wazushi na kisha kutengwa na kanisa.

Mabishano ya kithiolojia yalisababishwa na mitazamo mbalimbali ambayo wakristo

walikuwa nayo juu ya Yesu Kristo. Baadhi ya mitazamo hiyo ni .

Uungu wa Yesu Kristo.

Wakristo wa awali walimpa Yesu heshima kwa kumwita majina mbalimbali kama vile

Masihi, Kurios, Kritos na Logos.

Jina la Logosi lilitokana na falsafa za kigiriki, Kutokana na falsafa hizo Logos ilikuwa ni

njia ya Mungu kufanyika mwili na kukaa na watu hapa duniani. Hivyo wakristo wa awali

walimtambua Yesu kama Mungu.

Kristo kama Logosi.

Katika kipindi cha karne ya pili na ya tatu karibu wanazuoni wote wa kikiristo

walifundisha kwamba Kristo alikuwa ni Logos. Kulikuwa na mwanazuoni moja aliyeitwa

Yustini Shahidi ambae aliweka mkazo kuwa Logos alikuwa ni Mungu wa pili.

Wanazuoni wengine waliweka mkazo katika umoja wa Yesu.Walikubali kwamba Logos

amefanyika kuwa mwili katika Yesu Kristo lakini alikuwa ni Mungu halisi, Mungu

mwana ndiye aliyefanyika mwili, si Mungu wa pili. Kulingana na mtazamo waYustini ni

dhahiri kwamba alikana ubinadamu wa Yesu. Yesu kama Logos alikuwa Kweli Mungu

na mwanadamu kweli.

Monarchianism. Dhana ya Mungu mmoja.

Kulikuwa na wanazuoni wengine waliopinga mafundisho ya kumhusisha Yesu na Logos

kwa sababu jambo hili lilielekea kupinga imani yakuwa Mungu ni mmoja. Wanazuoni

31

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!