21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kutokana na uzushi kutokea, kanisa ilibidi liwe na utambulisho au jina ambalo lingeli

tofautisha na makundi ya uzushi, hivyo kanisa lilianza kujiita Katoliki. Jina katoliki

linatokana na neno la kiingereza universal, lenye maana “ya popote au ya mahali

popote” Kanisa lilianza kutumia jina Katoliki kwa maana mbili, ambazo ni:

i. Kanisa lisilo na mipaka ya majimbo au ya nchi. Kanisa moja lililo katika nchi zote

ulimwenguni.

ii. Kanisa leye mafundisho sahihi.

G. SABABU ZA KANISA KUHITAJI UTAWALA WENYE NGUVU.

i. Kutokea kwa ukiri wa imani.(kanuni ya imani)

ii. Kutokea kwa Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.

iii. Kutokea kwa maaskofu waliopewa mamlaka ya kutunza mafundisho yaliyotokana na

mitume wa kwanza.

i. Ukiri Wa Imani.

Huu ulikuwa ni ushuhuda mfupi uliotumiwa katika kazi za kawaida sharikani kama vile

ubatizo. Ukiri wa imani ulieleza kwa kifupi kile kanisa linachoamini na ulitumika kama

kiapo kuwa mtu anakubaliana na taratibu za kanisa hilo hivyo anastaili kubatizwa na

kupokelewa katika kanisa.

ii. Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.

Kanuni ni kawaida inayotumiwa kupima usawa na usahihi wa kitu. Kanuni huelezea

vitabu vilivyokubaliwa na kupokelewa na kanisa kama maandiko Matakatifu. Kanisa

liliweka kanuni ili kubainisha kati ya vitabu vilivyokuwa ni neno la Mungu na vile

visivyokuwa Neno la Mungu. Mfano wa vitabu visivyokuwa neno la Mungu ni vile

vilivyoandikwa na wanosti. Makundi ya uzushi kama vile wanostika na Marsion

waliharakisha kutungwa kwa kanuni hii.

Mababa wa kanisa walitumia kanuni mbalimbali katika kuvibaini vitabu hivyo. Baadhi ya

njia hizo ni kumtambua mwandishi kama alikuwa ni mtume au la, Kupokelewa kwa kitabu

na watu walionadikwa kwa mara ya kwanza na matumizi ya kitabu hicho katika makanisa

mbalimbali na mamlaka ya kitabu chenyewe N.k

iii. Haja Ya Kutokea Kwa Viongozi Wenye Mamlaka.

Maaskofu walitokea kama watu wenye mamlaka ya kutafsili maandiko na kufundisha

wazi mafundisho ya mitume. Neno askofu maana yake ni mwangalizi/msimamizi. Neno

hili hapo awali lilitumiwa na watu wote na kulikuwa na maaskofu katika idara mbalimbali

za serikali, baadae matumizi ya istilahi hii yalibakia katika Kanisa tu.

Uaskofu ulisaidia kuleta utawala wenye nguvu na umoja katika kanisa kupitia mambo

mawili ambayo ni mafuatano ya mitume na ibada.

Mafuatano Ya Mitume

30

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!