You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Kutokana na uzushi kutokea, kanisa ilibidi liwe na utambulisho au jina ambalo lingeli
tofautisha na makundi ya uzushi, hivyo kanisa lilianza kujiita Katoliki. Jina katoliki
linatokana na neno la kiingereza universal, lenye maana “ya popote au ya mahali
popote” Kanisa lilianza kutumia jina Katoliki kwa maana mbili, ambazo ni:
i. Kanisa lisilo na mipaka ya majimbo au ya nchi. Kanisa moja lililo katika nchi zote
ulimwenguni.
ii. Kanisa leye mafundisho sahihi.
G. SABABU ZA KANISA KUHITAJI UTAWALA WENYE NGUVU.
i. Kutokea kwa ukiri wa imani.(kanuni ya imani)
ii. Kutokea kwa Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.
iii. Kutokea kwa maaskofu waliopewa mamlaka ya kutunza mafundisho yaliyotokana na
mitume wa kwanza.
i. Ukiri Wa Imani.
Huu ulikuwa ni ushuhuda mfupi uliotumiwa katika kazi za kawaida sharikani kama vile
ubatizo. Ukiri wa imani ulieleza kwa kifupi kile kanisa linachoamini na ulitumika kama
kiapo kuwa mtu anakubaliana na taratibu za kanisa hilo hivyo anastaili kubatizwa na
kupokelewa katika kanisa.
ii. Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.
Kanuni ni kawaida inayotumiwa kupima usawa na usahihi wa kitu. Kanuni huelezea
vitabu vilivyokubaliwa na kupokelewa na kanisa kama maandiko Matakatifu. Kanisa
liliweka kanuni ili kubainisha kati ya vitabu vilivyokuwa ni neno la Mungu na vile
visivyokuwa Neno la Mungu. Mfano wa vitabu visivyokuwa neno la Mungu ni vile
vilivyoandikwa na wanosti. Makundi ya uzushi kama vile wanostika na Marsion
waliharakisha kutungwa kwa kanuni hii.
Mababa wa kanisa walitumia kanuni mbalimbali katika kuvibaini vitabu hivyo. Baadhi ya
njia hizo ni kumtambua mwandishi kama alikuwa ni mtume au la, Kupokelewa kwa kitabu
na watu walionadikwa kwa mara ya kwanza na matumizi ya kitabu hicho katika makanisa
mbalimbali na mamlaka ya kitabu chenyewe N.k
iii. Haja Ya Kutokea Kwa Viongozi Wenye Mamlaka.
Maaskofu walitokea kama watu wenye mamlaka ya kutafsili maandiko na kufundisha
wazi mafundisho ya mitume. Neno askofu maana yake ni mwangalizi/msimamizi. Neno
hili hapo awali lilitumiwa na watu wote na kulikuwa na maaskofu katika idara mbalimbali
za serikali, baadae matumizi ya istilahi hii yalibakia katika Kanisa tu.
Uaskofu ulisaidia kuleta utawala wenye nguvu na umoja katika kanisa kupitia mambo
mawili ambayo ni mafuatano ya mitume na ibada.
Mafuatano Ya Mitume
30