21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

ix. Siku ya jumapili iliwekwa kuwa siku ya mapumziko kwa watumishi wa serikali.

x. Mfalme Kostantino Alisaidia kuunda umoja wa kanisa kupitia mikutano mbalimbali

aliyoiitisha, mfano mkutano wa Naikea mwaka 325 BK.

xi. Mfalme Kostantino alikusudia kuufanya ukristo ukubaliwe na serikali kama dini

zingine.

II. MATOKEO MABAYA.

i. Ilikuwa ni fahari kuwa mkristo, hivyo watu wengi walijiunga na ukristo kwa

maslahi binafsi.

ii. Watu walijiunga na ukristo ili waweze kupata vyeo katika kanisa na serikali.

iii.

iv.

Maadili ndani ya kanisa yalianza kumomonyoka.

Mambo ya kiroho yaliachwa kupewa kipaumbele na badala yake programu

mbalimbali zikapewa kipaumbele.

v. Sherehe na tamaduni za kipagani polepole zilihamia kanisani, kwa kubadilishwa

jina na malengo na badhi zilibadilishwa kuwa sikukuu za kikanisa, mfano

Krismasi.(Kuabudiwa kwa bikira Maria kuliasiliwa kutoka ibada za kipagani za

kuabudu miungu , Zeusi, mungu wa uzuri wa warumi na Diana mungu mwezi).

vi.

vii.

Katika jimbo la mashariki serikali ililitawala kanisa mpaka likapoteza nguvu na

maisha ya kiroho.

Katika jimbo la magharibi kanisa lilipata nguvu dhidi ya serikali.

D. WATAWALA WALIOFUATA BAADA KOSTANTINO

Kostantino hakutaka kutumia nguvu katika kuwafanya watu kuwa wakristo, alitaka jambo

hili lifanyike taratibu na kwa uchaguzi wa mtu mwenyewe, jambo hili halikufuatwa na

watawala waliofuata baada yake.

Baada ya utawala wa Kostantino watawala waliofuatia walikuwa wakali mno walipiga

marufuku ibada za kipagani na waabudu dini hizo walihukumiwa kifo na mali zao

zilitaifishwa. Walivunja mahekalu ya kipagani, watawala hawa(wakristo) kwa kutumia

jina la ukristo sasa walitumia njia zilezile mbaya zilizokuwa zimetumiwa na serikali

kulitesa kanisa.

E. AINA MBALIMBALI ZA MATESO.

i. Katika kipindi cha Efeso kanisa liliteswa na wayahudi.

ii. Katika kipindi cha Smirna kanisa liliteswa na dola ya Rumi.

iii. Katika kipindi cha Pergamo ugomvi ulizuka miongoni mwao wenyewe

(wakristo).

F. UMOJA NA UTAWALA WA KANISA.

Kanisa lililazimka kuwa na umoja kamili ili liweze kuwa na nguvu ya kukabiliana na

mateso yaliyoliandama na uzushi uliokuwa unajitokeza. Hivyo kanisa lilipambana na

maadui wakubwa wawili ambao ni mateso na mafundisho potofu.

29

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!