You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
MADA YA KWANZA.
UTANGULIZI JUU YA HISTORIA YA KANISA.
A.UTANGULIZI
Somo hili linaanza na kupaa kwa Yesu Mbinguni katika mlima wa mizeituni kama mwaka
wa 30 .AD na linaishia na kurudi kwa Yesu mara ya pili kupitia kwenye mlima wa
mizeituni katika kipindi cha mwisho {ufu 19-16-26, Zek 14:1-9}
Wanahistoria ya kanisa hawakubaliani katika namna ya ugawaji wa vipindi vya historia
ya kanisa .Baadhi hugawa vipindi kulingana na matukio muhimu kuhusu watu Fulani
maarufu, mfano kutawazwa kwa papa wa kwanza mnamo mwaka 590 A.D, au wakati wa
matengenezo ya Martin Luther, alipoandika andiko {Thesis} lake lenye hoja 95 na
kulibandika katika mlango wa kanisa huko Witenberg Ujerumani mwaka 1517 .
Baadhi pia hupenda kugawa vipindi katika historia ya kanisa kulingana na matukio
mbalimbali yaliyoleta athari katika kanisa, mfano kuongoka kwa Kiongozi mkuu wa Dola
ya Rumi Mfalme Kostantino mwaka 313 AD .Au patano la amani la Westphalia mwaka wa
1646.
Pia wataalamu wengine hugawa vipindi vya kanisa kwa kufuata mtindo wa kinabii kwa
kuzingatia orodha ya makanisa saba (7) kama yalivyoainishwa katika kitabu cha Ufunuo
wa Yohana sura ya pili na ya tatu.
Katika somo hili tutagawa vipindi vya historia ya kanisa kwa kufuata mhutasari wa
makanisa saba yanayopatikana katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana Sura ya pili na ya tatu
ambapo vipindi mbalimbali vya kanisa vimeorodheshwa kwa njia ya kinabii.
B. DHANA YA HISTORIA.
Historia kama somo inafafanuliwa kwamba ni somo linalohusu matukio mbalimali katika
vipindi mbalimbali vya maendeleo ya mwanadamu.
Baadhi ya wataalamu wanafafanua kwamba historia ni kumbukumbu za shughuli za
binadamu katika vipindi viliyopita mpaka sasa. Kwahiyo historia huhusika na kuainisha
matukio mbalimbali muhimu yaliyotokea katika vipindi mbalimbali katika jamii ya
mwanadamu.
C. MAANA YA HISTORIA YA KANISA
Historia ya Kanisa ni fani inayochunguza historia ya Ukristo na ya miundo yake
mbalimbali tangu Kanisa lilipoanzishwa na Yesu Kristo katika karne ya 1 hadi leo
Ni taaluma inayoelezea vipindi mbalimbali ambavyo kanisa limepitia tangu kuanzishwa
kwake mpaka Yesu kristo atakapokuja kulichukua kwenda mbinguni .
1