21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

MADA YA KWANZA.

UTANGULIZI JUU YA HISTORIA YA KANISA.

A.UTANGULIZI

Somo hili linaanza na kupaa kwa Yesu Mbinguni katika mlima wa mizeituni kama mwaka

wa 30 .AD na linaishia na kurudi kwa Yesu mara ya pili kupitia kwenye mlima wa

mizeituni katika kipindi cha mwisho {ufu 19-16-26, Zek 14:1-9}

Wanahistoria ya kanisa hawakubaliani katika namna ya ugawaji wa vipindi vya historia

ya kanisa .Baadhi hugawa vipindi kulingana na matukio muhimu kuhusu watu Fulani

maarufu, mfano kutawazwa kwa papa wa kwanza mnamo mwaka 590 A.D, au wakati wa

matengenezo ya Martin Luther, alipoandika andiko {Thesis} lake lenye hoja 95 na

kulibandika katika mlango wa kanisa huko Witenberg Ujerumani mwaka 1517 .

Baadhi pia hupenda kugawa vipindi katika historia ya kanisa kulingana na matukio

mbalimbali yaliyoleta athari katika kanisa, mfano kuongoka kwa Kiongozi mkuu wa Dola

ya Rumi Mfalme Kostantino mwaka 313 AD .Au patano la amani la Westphalia mwaka wa

1646.

Pia wataalamu wengine hugawa vipindi vya kanisa kwa kufuata mtindo wa kinabii kwa

kuzingatia orodha ya makanisa saba (7) kama yalivyoainishwa katika kitabu cha Ufunuo

wa Yohana sura ya pili na ya tatu.

Katika somo hili tutagawa vipindi vya historia ya kanisa kwa kufuata mhutasari wa

makanisa saba yanayopatikana katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana Sura ya pili na ya tatu

ambapo vipindi mbalimbali vya kanisa vimeorodheshwa kwa njia ya kinabii.

B. DHANA YA HISTORIA.

Historia kama somo inafafanuliwa kwamba ni somo linalohusu matukio mbalimali katika

vipindi mbalimbali vya maendeleo ya mwanadamu.

Baadhi ya wataalamu wanafafanua kwamba historia ni kumbukumbu za shughuli za

binadamu katika vipindi viliyopita mpaka sasa. Kwahiyo historia huhusika na kuainisha

matukio mbalimbali muhimu yaliyotokea katika vipindi mbalimbali katika jamii ya

mwanadamu.

C. MAANA YA HISTORIA YA KANISA

Historia ya Kanisa ni fani inayochunguza historia ya Ukristo na ya miundo yake

mbalimbali tangu Kanisa lilipoanzishwa na Yesu Kristo katika karne ya 1 hadi leo

Ni taaluma inayoelezea vipindi mbalimbali ambavyo kanisa limepitia tangu kuanzishwa

kwake mpaka Yesu kristo atakapokuja kulichukua kwenda mbinguni .

1

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!