Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
iv.
Kanisa lenye kusitawi {kukua}. Licha ya mateso yaliyolikumba kanisa, kanisa
liliendelea kukua kwa kasi. Kanisa lilikumbana na mateso makali chini ya
watawala mbalimbali wa Kirumi, lakini kanisa liliendelea kukabiliana na mateso
hayo na likawa tayari kuwapelekea watesi hao Injili ya uzima. Mateso
yalisababisha kanisa kukua na kuongezeka.
L. KUANDIKWA KWA AGANO JIPYA.
Hatuwezi kueleza kwa udhahiri au kikamilifu kwamba ni lini hili lilifanyika. Baadhi ya
vitabu kama vile nyaraka za Paulo zilikubaliwa kila mahali, wakati vingine kama vile
Waebrania, Yakobo na Ufunuo wa Yohana vilikubaliwa Mashariki peke yake na
kukataliwa Magharibi.
Kanisa la mashariki lilikubali baadhi ya vitabu ambavyo havipo katika Biblia. Baadhi ya
vitabu hivyo ni Waraka wa Balnaba, Mafundisho ya mitume kumi na wawali na Ufunuo
wa mtume Petro. Mabaraza yalikutana mara kwa mara ili kutambua ni vitabu gani
vilivyokuwa vimevuviwa na vipi havikuvuviwa. Inadhaniwa kwambaAgano jipya
halikutambuliwa rasmi mpaka baada ya mwaka 300AD.
MADA YA NNE
KIPINDI CHA PERGAMO
KANISA LA KIFAHARI/ KITAIFA.
A. UTANGULIZI.
KIPINDI: Toka tamko la amani la mfalme Kostantino (313 BK) hadi kuanguka kwa dola
ya Rumi mnamo mwaka 476 BK.
27