Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
katika kipindi cha mateso. Pia makundi haya yalijitenga baada ya kuona kwamba wakristo
wengi walikuwa wanaishi maisha machafu kama wapagani waliokuwa wanawazunguka.
I. UASI WA NOVATIANI.
Katika karne y tatu askofu wa Rumi aliyeitwa Kalisto alitangaza kwamba dhambi yoyote
inaweza kusamehewa ikiwa mkosaji anaonesha toba ya kweli. Fundisho hili lilienea
sana. Wakristo waliokuwa wameikana imani yao wakati wa mateso walitaka kurudi
kanisani na askofu Kalisto alikubali kuwapokea watu hao.
Kiongozi mmoja wa kanisa aliyeitwa Novatiani, hakukubaliana na jambo hilo na alilipinga
vikali na akaungwa mkono na wachungaji wengine ambao nao walikuwa kinyume na
maamuzi hayo ya askofu. Walijitenga na kanisa na kuanzisha ushirika wao. Novatiani
alichaguliwa kuwa kiongozi wao.
II. UASI WA DONATO.
Mmeguko wa kanisa chini ya uongozi wa Donato ulitokea Afrika ya kaskazini karne ya
nne baada ya utawala wa mfalme Deokletiani. Mfalme huyu katika kipindi cha utawala
wake alikuwa na mpango wa kufuta ukristo na kuchoma moto Biblia zote. Wakati
wakipindi cha mateso makali baadhi ya viongozi wa kanisa waliasi imani wakaamua kutoa
maandiko matakatifu (Biblia) yateketezwe ili kujinusuru na kifo.
Baada ya kipindi cha mateso kumalizika viongozi hao yaani wachungaji na maaskofu
walioasi walitaka kurudi kanisani. Kanisa katoliki lilikuwa limekubali kuwapokea. Kanisa
lilikubali kuwarudishaviongozi hao katika sharika zao. Katika mji wa Karthegi waamini
wengi sana walikataa kuongozwa na mtu aliyemkana Yesu na kutoa Biblia kwa
serikali ili ziteketezwe.
Donatuno alikuwa kiongozi wa mgomo huo na alipata wafuasi wengi. Watu hao
walijitenga na kanisa na kuanzisha huduma yao. Kulikuwa na ugomvi kati ya wakatoliki na
wadonato kwa kwa muda mrefu.
K. HALI YA KANISA KATIKA KIPINDI CHA MWISHO WA KARNE YA PILI:
i. Kanisa lililotakasika. Mateso yaliwaondolea mbali wale ambao hawakuwa
waaminifu katika imani yao. Wale ambao hawakuwa na imani kamilifu na
waliojiunga na kanisa kwa masilahi yao binafsi mateso yaliwatupa nje yya kanisa.
ii.
iii.
Mafundisho yenye mfumo mmoja. Japokuwa kanisa lilihusisha watu wa
tamaduni , rangi na jamii mbalimbali bado lilikuwa na umoja wa imani katika
kanisa lote. Walifuata mafundisho ya mtume Paulo, Petro na mitume wengine.
Mdo 2:42.
Kanisa lenye muundo: kazi iliyofanywa na Paulo ya kuweka viongozi wa Kanisa
katika kila mji ilileta ufanisi. Viongozi hao walikutana katika mikutano na
kujadili mambo mbalimbali muhimu kuhusu kanisa. Hii ilisababisha kutokea kwa
ushirikiano imara wa kimataifa. (International Fellowship) ambao umekuwepo
mpaka sasa.
26