21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

katika kipindi cha mateso. Pia makundi haya yalijitenga baada ya kuona kwamba wakristo

wengi walikuwa wanaishi maisha machafu kama wapagani waliokuwa wanawazunguka.

I. UASI WA NOVATIANI.

Katika karne y tatu askofu wa Rumi aliyeitwa Kalisto alitangaza kwamba dhambi yoyote

inaweza kusamehewa ikiwa mkosaji anaonesha toba ya kweli. Fundisho hili lilienea

sana. Wakristo waliokuwa wameikana imani yao wakati wa mateso walitaka kurudi

kanisani na askofu Kalisto alikubali kuwapokea watu hao.

Kiongozi mmoja wa kanisa aliyeitwa Novatiani, hakukubaliana na jambo hilo na alilipinga

vikali na akaungwa mkono na wachungaji wengine ambao nao walikuwa kinyume na

maamuzi hayo ya askofu. Walijitenga na kanisa na kuanzisha ushirika wao. Novatiani

alichaguliwa kuwa kiongozi wao.

II. UASI WA DONATO.

Mmeguko wa kanisa chini ya uongozi wa Donato ulitokea Afrika ya kaskazini karne ya

nne baada ya utawala wa mfalme Deokletiani. Mfalme huyu katika kipindi cha utawala

wake alikuwa na mpango wa kufuta ukristo na kuchoma moto Biblia zote. Wakati

wakipindi cha mateso makali baadhi ya viongozi wa kanisa waliasi imani wakaamua kutoa

maandiko matakatifu (Biblia) yateketezwe ili kujinusuru na kifo.

Baada ya kipindi cha mateso kumalizika viongozi hao yaani wachungaji na maaskofu

walioasi walitaka kurudi kanisani. Kanisa katoliki lilikuwa limekubali kuwapokea. Kanisa

lilikubali kuwarudishaviongozi hao katika sharika zao. Katika mji wa Karthegi waamini

wengi sana walikataa kuongozwa na mtu aliyemkana Yesu na kutoa Biblia kwa

serikali ili ziteketezwe.

Donatuno alikuwa kiongozi wa mgomo huo na alipata wafuasi wengi. Watu hao

walijitenga na kanisa na kuanzisha huduma yao. Kulikuwa na ugomvi kati ya wakatoliki na

wadonato kwa kwa muda mrefu.

K. HALI YA KANISA KATIKA KIPINDI CHA MWISHO WA KARNE YA PILI:

i. Kanisa lililotakasika. Mateso yaliwaondolea mbali wale ambao hawakuwa

waaminifu katika imani yao. Wale ambao hawakuwa na imani kamilifu na

waliojiunga na kanisa kwa masilahi yao binafsi mateso yaliwatupa nje yya kanisa.

ii.

iii.

Mafundisho yenye mfumo mmoja. Japokuwa kanisa lilihusisha watu wa

tamaduni , rangi na jamii mbalimbali bado lilikuwa na umoja wa imani katika

kanisa lote. Walifuata mafundisho ya mtume Paulo, Petro na mitume wengine.

Mdo 2:42.

Kanisa lenye muundo: kazi iliyofanywa na Paulo ya kuweka viongozi wa Kanisa

katika kila mji ilileta ufanisi. Viongozi hao walikutana katika mikutano na

kujadili mambo mbalimbali muhimu kuhusu kanisa. Hii ilisababisha kutokea kwa

ushirikiano imara wa kimataifa. (International Fellowship) ambao umekuwepo

mpaka sasa.

26

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!