21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Kwa kiasi kikubwa mafundisho yake yalifanana na mafundisho ya wanostiki.

i. Aliweka sharti la wafuasi wake (wanandoa) kutokutana kimwili na kwamba

walitakiwa kuachana na kuishi maisha ya upweke.

ii. Alikaza kwamba wokovu ni kwa watu wote. Wokovu hutegemea Injili ya Yesu

Kristo na si kwa kufunuliwa mafumbo kifalsafa.

iii. Injili ya upendo wa Mungu inahitaji kusikika zaidi katika kanisa.

iv. Kanisa limeichafua Injili kwa kuichanganya na mambo ya dini ya kiyahudi.

v. Mungu wa Agano la kale ni tofauti na baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa

sababu Mungu wa agano la kale alifurahia dhabihu za damu.

vi. Mungu aliyeumba ulimwengu na watu wake ni Mungu mwovu, Mungu mwingine

mwema alijificha hadi wakati wa Yesu Kristo.

4. UMONTANO.

Kilikuwa ni kikundi kilichoanzishwa na mtu mmoja aliyeitwa Montano mwenyeji wa

Frigia. Wafuasi wa kikundi hiki waliitwa wamontano. Kikundi hiki kilienea sana kuanzia

mwishoni mwa karne ya pili na kuendelea kwa karne mbili zaidi.

Wakati wa ubatizo wake Montano alinena kwa lugha nyingine na kutabiri na hivyo akajiita

kuwa ni kinywa cha Roho Mtakatifu aliyetabiriwa na Yohana. Alikuwa na wasaidizi

wawaili wanawake ambao nao pia walijitambulisha kuwa ni vyombo pekee vya Roho

Mtakatifu. Karama za kinabii zilijidhihirisha katika mlengo wa umontano. Kutokana na

mikazo yao wamontano walihukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa.

MAMBO MUHIMU YA MONTANO.

i. Walikaza kwamba wamefunuliwa juu ya mwisho wa dunia uliokuwa karibu sana

kutokea.

ii. Baadhi ya wafuasi wa umontano walikataa kulima kwa sababu Yesu angekuja kabla

ya msimu wa mavuno.

iii.

iv.

Baadhi ya wamontano walikataa ndoa kwa kuwa mwisho wa dunia ulikuwa karibu.

Kiongozi wao mmoja wa huko Pontusi aliwapeleka washirika wake porini kwenda

kumlaki Bwana Yesu wakati anarudi duniani kwa mara ya pili.

v. Kiongozi mwingine wa huko Shamu aliwakataza washirika wake wasilime kwa

sababu Yesu angerudi kabla ya msimu wa mavuno.

vi.

vii.

viii.

Montano alikataa hali ya kanisa kumezwa na ulimwengu.

Alidai kuwa kanisa lilikuwa limepoa na hivyo lisitarajie kurudi kwa Yesu.

Walipinga suala la uaskofu kuchukua mamlaka katika kanisa. Waliweka mkazo

katika huduma ya unabii na ukuhani wa waamini wote.

5. KUMEGEKA KWA KANISA CHINI YA UONGOZI WA NOVATIANO NA DONATO.

Katika karne ya tatu na ya nne kulitokea na kumegeka kwa kanisa. Mmeguko huo

uliongozwa na Novatiano katika karne ya tatu na Donato karne ya nne. Kugawanyika

huko kulitokana na kurejeshwa kwa viongozi na wamini waliokuwa wameikana imani

25

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!