21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

maandiko ya mtume Paulo kwa sababu yalipinga mafundisho yao. Kundi hili lilitoweka

katika karne ya pili BK.

2. UNOSTIKI

Unostiki ilikuwa ni falsafa iliyojaribu kutumia imani ya ukristo katika kuthibitisha

ukweli wake. Kundi hili waliamini kwamba Baada ya ngazi ya Mungu mkuu kulikuwa na

miungu wengine wengi ambao baadhi wakiwa wema na wengine waovu. Unosti ulikuwa

na elementi za falsafa za kiyunani na dini za kipagani. Hivyo kanisa lilipinga vikali mno

unosti likikana kwamba imani yake si falsafa na wokovu hautegemei falsafa na mafumbo

bali ufunuo wa Yesu kristo.

Wanostiki walipunguza thamani ya maisha na huduma ya Yesu Kristo. Habari nzima juu

ya maisha na huduma ya Yesu ilielezwa kwa njia ya mafumbo (allegory). Unostiki ulizuka

katika karne ya pili baada ya Kristo na ulishamiri katika karne ya tatu na ya nne.

Unostiki hata sasa unajidhihirisha katika karne hii ya ishirini na moja katika dini

mbalimbali hapa ulimwenguni. Hususani kupitia falsafa ya mpango mpya wa dunia (New

World order Philosophy)

MAFUNDISHO YA UNOSTIKI.

i. Maarifa ya pekee hufunuliwa kwa watu wachache tu.

ii. Wokovu si kwa watu wote, ni kwa watu wachache tu wenye kuyaelewa maarifa

yanayofunuliwa.

iii. Ulimwengu huu na vitu vilivyomo ndani yake vimeumbwa kwa nguvu isiyokamili na

hii ndio asili ya maovu yote katika ulimwengu.

iv. Yesu si mwanadamu, alikuwa na roho tu. Yesu alikuwa ni roho aliyejifanya aonekane

katika umbile la binadamu.

v. Waliamini kwamba mmoja wa miungu wadogo alikuwa ndani ya Yesu na ndio

aliyekuwa asili ya uungu wake.

3. MARSION

Huyu alikuwa ni mtoto wa askofu wa Pontus. Alikuja Rumi yapata mnamo mwaka

138AD. Alipofika Rumi alijulikana kwa haraka sana kutokana na jinsi alivyojitolea sana

katika kanisa kwa mali zake. Pia mafundisho yake yalimpa umaarufu na kumfanya

ajulikane sana. Kutokana na umaarufu huo Marsion alipata wafuasi wengi. Mafundisho

yake hayakukubaliwa na kanisa hivyo alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa

mnamo mwaka 144 BK.

Marsioni aliunda kikundi chake ambacho kiliwaunganisha wafuasi wake wote. Kikundi

chake hakikuongezeka kwa njia ya kuzaliana kwa sababu ya kukataa mambo ya ndoa.

Waliongezeka kwa njia ya wanachama wapya kujiunga. Marsion alikuwa ni mtu wa

kwanza kutunga kanuni ya maandiko. Alipogoapogoa baadhi ya vitabu na kutunga orodha

ya maandiko matakatifu aliyoakuwa anaiamini yeye.

MAFUNDISHO YA MARSION

24

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!