Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
maandiko ya mtume Paulo kwa sababu yalipinga mafundisho yao. Kundi hili lilitoweka
katika karne ya pili BK.
2. UNOSTIKI
Unostiki ilikuwa ni falsafa iliyojaribu kutumia imani ya ukristo katika kuthibitisha
ukweli wake. Kundi hili waliamini kwamba Baada ya ngazi ya Mungu mkuu kulikuwa na
miungu wengine wengi ambao baadhi wakiwa wema na wengine waovu. Unosti ulikuwa
na elementi za falsafa za kiyunani na dini za kipagani. Hivyo kanisa lilipinga vikali mno
unosti likikana kwamba imani yake si falsafa na wokovu hautegemei falsafa na mafumbo
bali ufunuo wa Yesu kristo.
Wanostiki walipunguza thamani ya maisha na huduma ya Yesu Kristo. Habari nzima juu
ya maisha na huduma ya Yesu ilielezwa kwa njia ya mafumbo (allegory). Unostiki ulizuka
katika karne ya pili baada ya Kristo na ulishamiri katika karne ya tatu na ya nne.
Unostiki hata sasa unajidhihirisha katika karne hii ya ishirini na moja katika dini
mbalimbali hapa ulimwenguni. Hususani kupitia falsafa ya mpango mpya wa dunia (New
World order Philosophy)
MAFUNDISHO YA UNOSTIKI.
i. Maarifa ya pekee hufunuliwa kwa watu wachache tu.
ii. Wokovu si kwa watu wote, ni kwa watu wachache tu wenye kuyaelewa maarifa
yanayofunuliwa.
iii. Ulimwengu huu na vitu vilivyomo ndani yake vimeumbwa kwa nguvu isiyokamili na
hii ndio asili ya maovu yote katika ulimwengu.
iv. Yesu si mwanadamu, alikuwa na roho tu. Yesu alikuwa ni roho aliyejifanya aonekane
katika umbile la binadamu.
v. Waliamini kwamba mmoja wa miungu wadogo alikuwa ndani ya Yesu na ndio
aliyekuwa asili ya uungu wake.
3. MARSION
Huyu alikuwa ni mtoto wa askofu wa Pontus. Alikuja Rumi yapata mnamo mwaka
138AD. Alipofika Rumi alijulikana kwa haraka sana kutokana na jinsi alivyojitolea sana
katika kanisa kwa mali zake. Pia mafundisho yake yalimpa umaarufu na kumfanya
ajulikane sana. Kutokana na umaarufu huo Marsion alipata wafuasi wengi. Mafundisho
yake hayakukubaliwa na kanisa hivyo alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa
mnamo mwaka 144 BK.
Marsioni aliunda kikundi chake ambacho kiliwaunganisha wafuasi wake wote. Kikundi
chake hakikuongezeka kwa njia ya kuzaliana kwa sababu ya kukataa mambo ya ndoa.
Waliongezeka kwa njia ya wanachama wapya kujiunga. Marsion alikuwa ni mtu wa
kwanza kutunga kanuni ya maandiko. Alipogoapogoa baadhi ya vitabu na kutunga orodha
ya maandiko matakatifu aliyoakuwa anaiamini yeye.
MAFUNDISHO YA MARSION
24