21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Ireneusi (130-202A.D) aliyezaliwa Smirna. Alipata elimu yake ya awali ya Biblia chini ya

Porikap. Kanisa la Asia ndogo lilimpeleka Ufaransa kama mmisionari. Aliuawa wakati wa

mateso ya Severusi mwaka wa 202 AD

Shule ya kathegi: Shule hii ilikuwa kaskazini mwa Afrika na ilifanya vizuri kuliko shule

zingine kubadili imani ya Kithiologia katika Ulaya. Watu wakuu katika shule hii

walikuwa ni Tetuliani na Sipriani. Tetuliani (160-200 A.D) Alikuwa ni mteteaji shujaa

wa imani ya kikristo dhidi ya dini ya kiyahudi na mafundisho potofu. Alijiunga na

umontano na alitumia kalamu na mahubiri kuthibitisha kile alichofikiri ni mambo ya

kidunia na mabishano katika kanisa.

Sipriani Askofu wa Kathegi (195-258 A.D) Alikuwa ni mtoto wa afisa wa ngazi ya juu

wa dola ya Kirumi. Alikuwa mkristo wakati wa ujana wake. Mambo matatu yaliyomvutia

mpaka kuwa mkristo ni Maandiko ya tetuliani, mafundisho ya Cellius toka Rumi na

Maandiko matakatifu (Biblia).

Mwaka mmoja baada ya kuwa mkristo alikuwa askofu na kiongozi mkuu wa makanisa ya

Afrika Kaskazini mwaka 248AD. Mnamo Mwaka 257AD Mfalme Valentine alimfungia

kufanya huduma na mwaka 258AD aliuawa.

Kanisa la karne ya pili lilipambana na mambo makuu mawili ambayo ni Mateso na

uzushi(Heresy) yaani mafundisho potofu. Mtume Paulo alitabiri ya kwamba:

“ Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali wataingia kwenu

wasilihurumie kundi. Tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu,

wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”Mdo20:29-30

I. UZUSHI NA MAFUNDISHO YA UONGO.

Mafundisho yasiyokubaliana na mafundisho rasmi ya kanisa yaliitwa uzushi na waamini

waliamriwa na kanisa kuyapinga na kutokuyapokea mafundisho hayo.

Kanisa katika historia yake lilitangaza kuwa baadhi ya mafundisho yaliyokuwa

yanaibuliwa na baadhi ya viongozi na waamini wa kanisa yalikuwa ni mafundisho potofu

na yakapewa jina UZUSHI (heresy) kutokana na kutokukubaliwa rasmi kwa mafundisho

hayo na uongozi wa kanisa kwa ujumla wake.

Si kila mafundisho waliyoyaita uzushi yalikuwa mabaya, kwani kile kilichoitwa

uzushi kilikubaliwa baadae na kanisa na kile ambacho kilionekana chema

kilikataliwa na kuitwa uzushi baadae. Hoja au mawazo yale waliyoyaita uzushi baadhi

yalikuwa na mambo mema ndani yake kama tutakavyotazama hapo baadae

Kanisa halikupambana na mateso tu bali pia na mafundisho ya uongo, sawsawa na unabii

uliotolewa

J. MAKUNDI YA UZUSHI.

1. UYAHUDISHAJI.

Hili lilikuwa ni kundi la wakristo wa kiyahudi lililojitokeza wakati kanisa linapanuka

katika miji ya wamataifa. Wayahudishaji hawa walifundisha kwamba wakristo wote

walitakiwa kuzifuata sheria za Musa na mapokeo ya dini ya kiyahudi. Waliyakataa

23

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!