Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Ireneusi (130-202A.D) aliyezaliwa Smirna. Alipata elimu yake ya awali ya Biblia chini ya
Porikap. Kanisa la Asia ndogo lilimpeleka Ufaransa kama mmisionari. Aliuawa wakati wa
mateso ya Severusi mwaka wa 202 AD
Shule ya kathegi: Shule hii ilikuwa kaskazini mwa Afrika na ilifanya vizuri kuliko shule
zingine kubadili imani ya Kithiologia katika Ulaya. Watu wakuu katika shule hii
walikuwa ni Tetuliani na Sipriani. Tetuliani (160-200 A.D) Alikuwa ni mteteaji shujaa
wa imani ya kikristo dhidi ya dini ya kiyahudi na mafundisho potofu. Alijiunga na
umontano na alitumia kalamu na mahubiri kuthibitisha kile alichofikiri ni mambo ya
kidunia na mabishano katika kanisa.
Sipriani Askofu wa Kathegi (195-258 A.D) Alikuwa ni mtoto wa afisa wa ngazi ya juu
wa dola ya Kirumi. Alikuwa mkristo wakati wa ujana wake. Mambo matatu yaliyomvutia
mpaka kuwa mkristo ni Maandiko ya tetuliani, mafundisho ya Cellius toka Rumi na
Maandiko matakatifu (Biblia).
Mwaka mmoja baada ya kuwa mkristo alikuwa askofu na kiongozi mkuu wa makanisa ya
Afrika Kaskazini mwaka 248AD. Mnamo Mwaka 257AD Mfalme Valentine alimfungia
kufanya huduma na mwaka 258AD aliuawa.
Kanisa la karne ya pili lilipambana na mambo makuu mawili ambayo ni Mateso na
uzushi(Heresy) yaani mafundisho potofu. Mtume Paulo alitabiri ya kwamba:
“ Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali wataingia kwenu
wasilihurumie kundi. Tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu,
wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”Mdo20:29-30
I. UZUSHI NA MAFUNDISHO YA UONGO.
Mafundisho yasiyokubaliana na mafundisho rasmi ya kanisa yaliitwa uzushi na waamini
waliamriwa na kanisa kuyapinga na kutokuyapokea mafundisho hayo.
Kanisa katika historia yake lilitangaza kuwa baadhi ya mafundisho yaliyokuwa
yanaibuliwa na baadhi ya viongozi na waamini wa kanisa yalikuwa ni mafundisho potofu
na yakapewa jina UZUSHI (heresy) kutokana na kutokukubaliwa rasmi kwa mafundisho
hayo na uongozi wa kanisa kwa ujumla wake.
Si kila mafundisho waliyoyaita uzushi yalikuwa mabaya, kwani kile kilichoitwa
uzushi kilikubaliwa baadae na kanisa na kile ambacho kilionekana chema
kilikataliwa na kuitwa uzushi baadae. Hoja au mawazo yale waliyoyaita uzushi baadhi
yalikuwa na mambo mema ndani yake kama tutakavyotazama hapo baadae
Kanisa halikupambana na mateso tu bali pia na mafundisho ya uongo, sawsawa na unabii
uliotolewa
J. MAKUNDI YA UZUSHI.
1. UYAHUDISHAJI.
Hili lilikuwa ni kundi la wakristo wa kiyahudi lililojitokeza wakati kanisa linapanuka
katika miji ya wamataifa. Wayahudishaji hawa walifundisha kwamba wakristo wote
walitakiwa kuzifuata sheria za Musa na mapokeo ya dini ya kiyahudi. Waliyakataa
23