You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Siku kumi za kujaribiwa zilizotajwa katika Ufunuo wa Yohana 2:10 zilifikia mwisho.
Baadae mfalme Deocletiani alipotambua kwamba yuko karibu na kufa alitubu dhambi zake
mbele ya askofu wa mji na mnamo mwka 337 A.D alibatizwa. Mtu aliyeamini kwamba
angeweza kuufuta ukristo alijikuta yeye mwenyewe anakuwa mkristo.
G. UONGOZI WA KANISA KATIKA KIPINDI HIKI.
Wakati mitume wakiwa hai uongozi ulionekana ni utumishi yaani kutumikia au
kuwajibika. Wakati Luka alipoandika kitabu cha Matendo na Paulo alipoandika nyaraka
zake tunakuta maneno askofu na wazee yakiwa na maana sawa yaani yakimaanisha ofisi
moja. Lakini katika miaka ya 125 tunakuta maaskofu wamekuwa watawala katika maeneo
yao. Katika baraza la Yerusalemu mwaka 48 A,D {Mdo 15} mitume wote na wazee
walihusika. Lakini katika baraza la mwaka 150 A.D waliohusika ni maaskofu pekee. Hii
inadhihirisha kwamba kanisa liliondoka taratibu kwenye mafundisho halisi ya mitume.
Huduma ya mitume ilizimwa na ikachukuliwa na maaskofu. Maaskofu walijifanya
watawala wa kanisa. Hii ndio sababu inayosababisha baadhi ya wanazuoni wa Kikristo
kuamini kwamba kipindi cha mitume kiliishia na kifo cha mtume Yohan, jambo ambalo si
kweli. Huduma za mitume, manabii, waalimu wachungaji na wainjilisti kama
zinavyoelezwa katika waefeso 4:11 ziliendelea kuwapo katika kipindi cha mitume na
vipindi vingine vyote vya kanisa, japokuwa zimekuwa zikikataliwa na katika vipindi
fulani ilionekana kama zimetoweka lakini kwa uhakika zimekuwapo na bado zimekuwa
zikifanya kazi katika kanisa hata sasa.
H. SHULE ZA THEOLOGIA.
Shule ya Alexandria. Ilianzishwa mwaka 180. A.D na Pantaenusi ambaye alikuwa ni
mwanafalsafa wa kigiriki na baadae akwa mkristo. Kisha alikwenda India, Irani na Saudi
Arabia katika huduma kama mmishenari. Alikufa mwaka 200 AD .
Klementi wa Alexandria alikuwa mwanafunzi wa Pantaenusi na alimsaidia katika
uendeshaji wa shule. Alikuwa ni mkuu wa shule hadi alipoondolewa kwenye wadhifa huo
katika kipindi cha mateso cha Septimus Severusi mwaka 2002AD, Baadhi ya vitabu vyake
mpaka sasa vipo.
Origeni (185-254 A.D). Alikuwa ni mwanatheologia mkuu. Alikuwa ni mtoto wa
Leonidasi. Baba yake aliuawa kutokana na imani yake katika Kristo chini ya utawala wa
mfalme Severus katika mwaka wa 2002 AD. Wakati huo Origeni alikuwa na umri wa
miaka 17. Origeni aliisaidia familia yake kwa kufundisha falsafa ya kigiriki pamoja na
fasihi. Aliianzisha shule ya Biblia kwa upya iliyokuwa imefungwa kutokana na kuondoka
kwa Klementi. Baadae alikuwa ni mwandishi wa vitabu vya Dogma na Thiologia. Baadae
alikwenda Kaisaria na alianzisha shule nyingine ya Biblia ambapo alikuwa ni kiongozi wa
shule hiyo kwa karibu zaidi ya miaka 20. Alifungwa jela chini ya mateso ya Deciani na
alikufa kutokana na kutendewa kinyama akiwa gerezani. alikufa akiwa na umri wa miaka
69 mnamo mwaka 254 AD.
Shule ya Asia ndogo. Shule hii haikuwa katika mji wowote ilikuwa ni shule ya masafa
(mobile Bible School). Ilihusisha waalimu wa thiolojia na waandishi. Baadhi yao ni
22