21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Siku kumi za kujaribiwa zilizotajwa katika Ufunuo wa Yohana 2:10 zilifikia mwisho.

Baadae mfalme Deocletiani alipotambua kwamba yuko karibu na kufa alitubu dhambi zake

mbele ya askofu wa mji na mnamo mwka 337 A.D alibatizwa. Mtu aliyeamini kwamba

angeweza kuufuta ukristo alijikuta yeye mwenyewe anakuwa mkristo.

G. UONGOZI WA KANISA KATIKA KIPINDI HIKI.

Wakati mitume wakiwa hai uongozi ulionekana ni utumishi yaani kutumikia au

kuwajibika. Wakati Luka alipoandika kitabu cha Matendo na Paulo alipoandika nyaraka

zake tunakuta maneno askofu na wazee yakiwa na maana sawa yaani yakimaanisha ofisi

moja. Lakini katika miaka ya 125 tunakuta maaskofu wamekuwa watawala katika maeneo

yao. Katika baraza la Yerusalemu mwaka 48 A,D {Mdo 15} mitume wote na wazee

walihusika. Lakini katika baraza la mwaka 150 A.D waliohusika ni maaskofu pekee. Hii

inadhihirisha kwamba kanisa liliondoka taratibu kwenye mafundisho halisi ya mitume.

Huduma ya mitume ilizimwa na ikachukuliwa na maaskofu. Maaskofu walijifanya

watawala wa kanisa. Hii ndio sababu inayosababisha baadhi ya wanazuoni wa Kikristo

kuamini kwamba kipindi cha mitume kiliishia na kifo cha mtume Yohan, jambo ambalo si

kweli. Huduma za mitume, manabii, waalimu wachungaji na wainjilisti kama

zinavyoelezwa katika waefeso 4:11 ziliendelea kuwapo katika kipindi cha mitume na

vipindi vingine vyote vya kanisa, japokuwa zimekuwa zikikataliwa na katika vipindi

fulani ilionekana kama zimetoweka lakini kwa uhakika zimekuwapo na bado zimekuwa

zikifanya kazi katika kanisa hata sasa.

H. SHULE ZA THEOLOGIA.

Shule ya Alexandria. Ilianzishwa mwaka 180. A.D na Pantaenusi ambaye alikuwa ni

mwanafalsafa wa kigiriki na baadae akwa mkristo. Kisha alikwenda India, Irani na Saudi

Arabia katika huduma kama mmishenari. Alikufa mwaka 200 AD .

Klementi wa Alexandria alikuwa mwanafunzi wa Pantaenusi na alimsaidia katika

uendeshaji wa shule. Alikuwa ni mkuu wa shule hadi alipoondolewa kwenye wadhifa huo

katika kipindi cha mateso cha Septimus Severusi mwaka 2002AD, Baadhi ya vitabu vyake

mpaka sasa vipo.

Origeni (185-254 A.D). Alikuwa ni mwanatheologia mkuu. Alikuwa ni mtoto wa

Leonidasi. Baba yake aliuawa kutokana na imani yake katika Kristo chini ya utawala wa

mfalme Severus katika mwaka wa 2002 AD. Wakati huo Origeni alikuwa na umri wa

miaka 17. Origeni aliisaidia familia yake kwa kufundisha falsafa ya kigiriki pamoja na

fasihi. Aliianzisha shule ya Biblia kwa upya iliyokuwa imefungwa kutokana na kuondoka

kwa Klementi. Baadae alikuwa ni mwandishi wa vitabu vya Dogma na Thiologia. Baadae

alikwenda Kaisaria na alianzisha shule nyingine ya Biblia ambapo alikuwa ni kiongozi wa

shule hiyo kwa karibu zaidi ya miaka 20. Alifungwa jela chini ya mateso ya Deciani na

alikufa kutokana na kutendewa kinyama akiwa gerezani. alikufa akiwa na umri wa miaka

69 mnamo mwaka 254 AD.

Shule ya Asia ndogo. Shule hii haikuwa katika mji wowote ilikuwa ni shule ya masafa

(mobile Bible School). Ilihusisha waalimu wa thiolojia na waandishi. Baadhi yao ni

22

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!