21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

manabii wa zamani wa Kiebrania. Aliandika maneno yafuatayo dhidi ya ukatili na mauaji

yaliyokuwa yanaendelea dhidi ya wakristo.

“wanatushitaki, wanatusulubisha kwenye misalaba na kutupa kwenye

viwanja vy wanyama wakali na kwenye moto. Lakini wanapofanya

mabaya zaidi juu yetu ndivyo idadi ya wakristo inaongezeka na kuwa

kubwa zaidi.

Mnamo mwaka 165 A.D alikamatwa na mfalme wa Rumi Marcus Aureliusi na

kuuawa.

KIPINDI CHA TANO CHA MATESO CHINI YA SEPTIMUS. 202-211. A.D.

Baada ya kifo cha Marcus Aurelius kanisa lilipata amani mpaka alipoinuka mtawala

mwingine aliyejulikana kwa jina la Septimus Severus. Mtawala huyu alimuua Leonidasi

baba wa Origeni mwanatheologia mkuu. Katika mji wa kathegi Perpetua na mtumwa wake

Felistas walitupwa katika viwanja vya wanyama poli wakali na wakauawa.

KIPINDI CHA SITA CHA MATESO CHINI YA THRAKA MAXIMUS 235-237

A.D. Baada ya kipindi cha amani Thraka alikalia kiti cha enzi cha Rumi. Alikua

mpiganaji na alikusudia kuonyesha huruma zake kwa dini za kipagani kwa kuwatesa

wakristo. Utawala wake ulikuwa mfupi kwa sababu ya kutawala kwake kwa njia ya

udikteta. Maadui zake walitengeneza kikundi ambacho kilifanikiwa kumuua.

KIPINDI CHA SABA CHA MATESO.CHINI YA DECIUS 250-253 A.D.

Katika kipindi cha utawala wake mateso makali yaliibuka tena na kwa bahati nzuri kipindi

chake cha utawala kilikuwa kifupi na kanisa lilipata raha na amani kwa miaka 40.

KIPINDI CHA NANE CHA MATESO CHINI YA VARELIANI. 257-260. A.D.

Askofu Sipriani wa Kathegi aliuawa pia askofu wa Rumi Sextus aliuawa.

KIPINDI CHA TISA CHA MATESO. CHINI YA AURELIUS. 270-275. A.D

Mfalme Aurelius alikuwa mwabudu jua japokuwa hakulitesa kanisa moja kwa moja

mwanzoni lakini hakuwapa uhuru wakristo. Hatimae aliamuru kwamba wakristo wateswa.

Mateso yalidumu kwa muda mfupi sana chini ya mtawala huyu aana aliuwawa na wafuasi

wake mwenyewe.

KIPINDI CHA KUMI CHA MATESO CHINI YA DEOCLETIAN 303- 3010. A.D

Mfalme Deocletiani na wasaidizi wake waliwafunga wakristo gerezani. Baadae sehemu ya

jengo hili lilibadilishwa na kuwa Kathedro ya Mtakatifu Petro. Deocletiani aliagiza

kuchomwa moto kwa kila nakala Biblia, makanisa kubomolewa na wakristo wenye

msimamo mkali kunyang’anywa uraia.

Akiwa na umri wamiaka 80 Deocletiani aliondoka kwenye kiti cha utawala, lakini wafuasi

wake Galarius na Kostantinusi waliendeleza mateso mpaka mfalme Kostantino mtoto wa

Kostantinus alipotoa tamko la amani kwa kanisa mwaka 313 A. Tamko hili la amani

lilisitisha mateso kwa kanisa kwa kipindi cha karne mbili

21

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!