You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
manabii wa zamani wa Kiebrania. Aliandika maneno yafuatayo dhidi ya ukatili na mauaji
yaliyokuwa yanaendelea dhidi ya wakristo.
“wanatushitaki, wanatusulubisha kwenye misalaba na kutupa kwenye
viwanja vy wanyama wakali na kwenye moto. Lakini wanapofanya
mabaya zaidi juu yetu ndivyo idadi ya wakristo inaongezeka na kuwa
kubwa zaidi.
Mnamo mwaka 165 A.D alikamatwa na mfalme wa Rumi Marcus Aureliusi na
kuuawa.
KIPINDI CHA TANO CHA MATESO CHINI YA SEPTIMUS. 202-211. A.D.
Baada ya kifo cha Marcus Aurelius kanisa lilipata amani mpaka alipoinuka mtawala
mwingine aliyejulikana kwa jina la Septimus Severus. Mtawala huyu alimuua Leonidasi
baba wa Origeni mwanatheologia mkuu. Katika mji wa kathegi Perpetua na mtumwa wake
Felistas walitupwa katika viwanja vya wanyama poli wakali na wakauawa.
KIPINDI CHA SITA CHA MATESO CHINI YA THRAKA MAXIMUS 235-237
A.D. Baada ya kipindi cha amani Thraka alikalia kiti cha enzi cha Rumi. Alikua
mpiganaji na alikusudia kuonyesha huruma zake kwa dini za kipagani kwa kuwatesa
wakristo. Utawala wake ulikuwa mfupi kwa sababu ya kutawala kwake kwa njia ya
udikteta. Maadui zake walitengeneza kikundi ambacho kilifanikiwa kumuua.
KIPINDI CHA SABA CHA MATESO.CHINI YA DECIUS 250-253 A.D.
Katika kipindi cha utawala wake mateso makali yaliibuka tena na kwa bahati nzuri kipindi
chake cha utawala kilikuwa kifupi na kanisa lilipata raha na amani kwa miaka 40.
KIPINDI CHA NANE CHA MATESO CHINI YA VARELIANI. 257-260. A.D.
Askofu Sipriani wa Kathegi aliuawa pia askofu wa Rumi Sextus aliuawa.
KIPINDI CHA TISA CHA MATESO. CHINI YA AURELIUS. 270-275. A.D
Mfalme Aurelius alikuwa mwabudu jua japokuwa hakulitesa kanisa moja kwa moja
mwanzoni lakini hakuwapa uhuru wakristo. Hatimae aliamuru kwamba wakristo wateswa.
Mateso yalidumu kwa muda mfupi sana chini ya mtawala huyu aana aliuwawa na wafuasi
wake mwenyewe.
KIPINDI CHA KUMI CHA MATESO CHINI YA DEOCLETIAN 303- 3010. A.D
Mfalme Deocletiani na wasaidizi wake waliwafunga wakristo gerezani. Baadae sehemu ya
jengo hili lilibadilishwa na kuwa Kathedro ya Mtakatifu Petro. Deocletiani aliagiza
kuchomwa moto kwa kila nakala Biblia, makanisa kubomolewa na wakristo wenye
msimamo mkali kunyang’anywa uraia.
Akiwa na umri wamiaka 80 Deocletiani aliondoka kwenye kiti cha utawala, lakini wafuasi
wake Galarius na Kostantinusi waliendeleza mateso mpaka mfalme Kostantino mtoto wa
Kostantinus alipotoa tamko la amani kwa kanisa mwaka 313 A. Tamko hili la amani
lilisitisha mateso kwa kanisa kwa kipindi cha karne mbili
21