Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Yohana uhamishoni kwenye kisiwa cha Patmo ambapo ndipo mahali alipopokea ufunuo
ambao sasa ni kitabu cha Ufunuo wa Yohana.
KIPINDI CHA TATU CHA MATESO CHINI YA TRAJANI 104-107 AD.
Trajani husemekana kuwa mtu muhimu sana miongoni mwa watawala wa Rumi. Alikuwa
mtawala mzuri kwa nchi yake lakini aliwaua wakristo. Mmoja wa mahakimu wake
aliyeitwa Plin the younger. Gavana wa Bethania alichunguza maisha ya wakristo na
mafundisho yao na kugundua kwamba mafundisho hayo hayakuwa na chochote chenye
kuleta uasi kwa serikali ya Rumi. Alileta ripoti yake mbele ya mfalme Trajani lakini
mfalme alijibu
“ Kama watu hawa walioletwa mbele yako wamepatikana na hatia kwa sababu ya kuwa
wakristo na wauawe lakini ikiwa wataikana imani yao ya kikristo na ikathibitika kwamba
wanaabudu miungu yetu na waachiwe huru. Katika kipindi hiki waliuawa wakristo
mbalimbali kama ifuatavyo.
‣ Simoni mdogo wa Bwana Yesu alisulubiwa katika mwaka wa 107 AD akiwa na
umri wa miaka 110. Alisulubiwa kwa amri ya mfalme wa Rumi {Trajani}.
‣ Askofu Ignatius wa Antiokia ambaye aliandika nyaraka mbalimbali kwa makanisa
mbalimbali ambazo baadhi yake zinapatikana katika kitabu kiitwacho “Mababa wa
Kitume”{Apostolic fathers}. Alikuwa tayari kuuawa kwaajili ya Bwana Yesu.
Aliandika barua za kuwafariji wakristo akiwa njiani kuelekea Rumi ambapo
alitupwa katika hifadhi ya wanyama wakali na akaliwa na wanyama wakali mnamo
mwaka 110.AD
‣ PORIKAP. {69-155 AD} Alikuwa mwanafunzi wa mtume Yohana na rafiki wa
Ignatius na mwalimu wa Ireniusi. Inadhaniwa kuwa Polikap aliteuliwa na mtume
Yohana kuwa askofu wa makanisa saba ya Asia. Alipoamriwa kumkana bwana Yesu
Kristo ili kuepukana na kuuawa yeye alijibu:
“Miaka 86 nimemtumikia Bwana wangu na hajatenda Jambo lolote baya
kwangu, nawezaje kunena vibaya juu ya Bwana wangu aliyeniokoa?
Alichomwa moto na akafa kifo cha kishujaa kwaajili ya Imani yake kwa Yesu Kristo.
Aliuawa chini ya utawala wa mfalme Antonius Pius mwaka 155 A.D.
KIPINDI CHA NNE CHA MATESO CHINI MARCUS
AURELIUS 161-180 A.D.
Marcus alijulikana kam mfalme bora wa nchi yake na mwandishi mwenye maadili.
Japokuwa alikuwa mtu mzuri kwa taifa lake alikuwa mtesi wa kanisa. Alifikiri kurejesha
maisha ya zamani ya kirumi na dini za zamani. Kwa wakati huo ukristo ulikuwa na
mashiko zaidi. Waamini wengi walikuwa tayari kufa kwa ajili ya imani yao na wala
hawakuogopa kifo. Walikikabili kifo kwa shangwe na ushindi mkuu. Katika kipindi hiki
waaminni wengi waliuawa na wengine walitupwa katika viwanja vya michezo vya
wanyama ili waliwe na wanyama wakali.
YUSTINI (JustineMarty) 100-165 A.D alizaliwa na alielimishwa vizuri mpaka kuwa
mwanafalsafa na aliendelea kufundisha hata baada ya kuwa mkristo. Alirejerea kwa
20