21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Yohana uhamishoni kwenye kisiwa cha Patmo ambapo ndipo mahali alipopokea ufunuo

ambao sasa ni kitabu cha Ufunuo wa Yohana.

KIPINDI CHA TATU CHA MATESO CHINI YA TRAJANI 104-107 AD.

Trajani husemekana kuwa mtu muhimu sana miongoni mwa watawala wa Rumi. Alikuwa

mtawala mzuri kwa nchi yake lakini aliwaua wakristo. Mmoja wa mahakimu wake

aliyeitwa Plin the younger. Gavana wa Bethania alichunguza maisha ya wakristo na

mafundisho yao na kugundua kwamba mafundisho hayo hayakuwa na chochote chenye

kuleta uasi kwa serikali ya Rumi. Alileta ripoti yake mbele ya mfalme Trajani lakini

mfalme alijibu

“ Kama watu hawa walioletwa mbele yako wamepatikana na hatia kwa sababu ya kuwa

wakristo na wauawe lakini ikiwa wataikana imani yao ya kikristo na ikathibitika kwamba

wanaabudu miungu yetu na waachiwe huru. Katika kipindi hiki waliuawa wakristo

mbalimbali kama ifuatavyo.

‣ Simoni mdogo wa Bwana Yesu alisulubiwa katika mwaka wa 107 AD akiwa na

umri wa miaka 110. Alisulubiwa kwa amri ya mfalme wa Rumi {Trajani}.

‣ Askofu Ignatius wa Antiokia ambaye aliandika nyaraka mbalimbali kwa makanisa

mbalimbali ambazo baadhi yake zinapatikana katika kitabu kiitwacho “Mababa wa

Kitume”{Apostolic fathers}. Alikuwa tayari kuuawa kwaajili ya Bwana Yesu.

Aliandika barua za kuwafariji wakristo akiwa njiani kuelekea Rumi ambapo

alitupwa katika hifadhi ya wanyama wakali na akaliwa na wanyama wakali mnamo

mwaka 110.AD

‣ PORIKAP. {69-155 AD} Alikuwa mwanafunzi wa mtume Yohana na rafiki wa

Ignatius na mwalimu wa Ireniusi. Inadhaniwa kuwa Polikap aliteuliwa na mtume

Yohana kuwa askofu wa makanisa saba ya Asia. Alipoamriwa kumkana bwana Yesu

Kristo ili kuepukana na kuuawa yeye alijibu:

“Miaka 86 nimemtumikia Bwana wangu na hajatenda Jambo lolote baya

kwangu, nawezaje kunena vibaya juu ya Bwana wangu aliyeniokoa?

Alichomwa moto na akafa kifo cha kishujaa kwaajili ya Imani yake kwa Yesu Kristo.

Aliuawa chini ya utawala wa mfalme Antonius Pius mwaka 155 A.D.

KIPINDI CHA NNE CHA MATESO CHINI MARCUS

AURELIUS 161-180 A.D.

Marcus alijulikana kam mfalme bora wa nchi yake na mwandishi mwenye maadili.

Japokuwa alikuwa mtu mzuri kwa taifa lake alikuwa mtesi wa kanisa. Alifikiri kurejesha

maisha ya zamani ya kirumi na dini za zamani. Kwa wakati huo ukristo ulikuwa na

mashiko zaidi. Waamini wengi walikuwa tayari kufa kwa ajili ya imani yao na wala

hawakuogopa kifo. Walikikabili kifo kwa shangwe na ushindi mkuu. Katika kipindi hiki

waaminni wengi waliuawa na wengine walitupwa katika viwanja vya michezo vya

wanyama ili waliwe na wanyama wakali.

YUSTINI (JustineMarty) 100-165 A.D alizaliwa na alielimishwa vizuri mpaka kuwa

mwanafalsafa na aliendelea kufundisha hata baada ya kuwa mkristo. Alirejerea kwa

20

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!