You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Mitume walifundisha kwamba sanamu si kitu na hazipaswi kuabudiwa anaepaswa
kuabudiwa ni Mungu muumba Mbingu na nchi pekee. Watu wengi waliacha kununua
sanamu hizo. Kitendo hicho kilisababisha biashara hiyo ya uuzaji sanamu kudolola.
Watengenezaji na wauzaji wa sanamu hizo walipata hasara na wakaamua kuja juu na
kuanzisha ghasia dhidi ya kanisa kwani walipoteza wateja wao.
E.HATUA ZA MATESO.
Kuna mwingiliano kati ya kipindi cha Efeso na Smirna. Kipindi cha Efeso kiliishia na kifo
cha mtume Yohana mwaka 100 B.K. Wakati kipindi cha Smirna kilianza wakati wa
mateso ya kitaifa.(dola) wakati mfalme Nero alipouchoma mji wa Rumi mwaka 64 B.K.
F. VIPINDI KUMI VYA MATESO YA KITAIFA.
MATESO YA KWANZA Chini ya Kaisari Nero.(54-68 B.K)
Klaudi Nero alikuwa na umri wa miaka 16 alipoingia katika utawala (ufalme) katika
mwaka 54 AD. Alikuwa mjukuu mkubwa wa Agustus aliyetoa amri ya watu wote
kuhesabiwa sensa (Lk 2). Nero alikuwa mfalme wa kwanza katika wafalme kumi
kuanzisha mateso dhidi ya kanisa.Alichoma mji wa Rumi mwaka 64 B.K .Theruthi mbili
ya mji wa Rumi iliteketea. Mfalme Nero aliwasingizia wakristo kwamba ndiyo
waliohusika na uharibifu huo. Hivyo kanisa lililazimika kuingia kwenye mateso makali.
Katika kipindi hiki mtume Petro alisulibiwa miguu juu kichwa chini mnamo mwaka 67
Pia mtume Paulo alikamatwa na kufungwa Rumi ambapo alihukumiwa kifo na kisha
akauawa kwa kukatwa kichwa mwaka 68 B.K Mjini Rumi.
Mfalme Nero alikuwa katili kuliko makaisari wote wa dola ya Rumi waliomtangulia na
waliomfuata. Kwani hajatokea kaisari katika dola ya Rumi aliyefanya mauaji kama Nero.
Mwaka 59 B.K . Mfalme Nero alimuua mama yake . pia alimuua mke wake wa kwanza
(Octavia)na kisha mkewe wa pili(Pompea) na baadae alimuua kaka yake na rafiki yake
mwalimu Seneka.
Mpaka mwaka wa 64. B.K Rumi ilikuwa katika ghasia kuu. Mfalme Nero alituhumiwa
kwamba yeye ndiye aliyehusika na kuuchoma moto mji wa Rumi. Lakini yeye alikanusha
na kuwashutumu wakristo kuwa ndiyo waliohusika na tukio hilo.
Kutokana na hilo kanisa liliingia katika kipindi cha mateso makali. Maelfu ya wakristo
waliuawa baadhi yao walitupiwa kwenye viwanja vya michezo vya wanyama poli ili
waliwe na wanyama wakali na baadhi yao walichomwa moto na mfalme akaendesha gari
lake juu yao katika bustani yake. Bustani ya mfalme ambako tukio hili lilifanyika leo ni
eneo la la jiji la Vatikani makao makuu ya papa na kania la mtakatifu Petro. Kaisari
Nero alijiua mwenyewe mwaka 68. B.K
KIPINDI CHA PILI CHA MATESO CHINI YA DOMITIAN. (90-96 B.K).
Baada ya Nero kujiua mwaka wa 68 B.K kanisa lilipata amani mpaka alipoinuka mtawala
mwingine ambaye ni Domitiani. Wakristo wengi waliuawa wakati huu .Baada ya juhudi
zote za kumuua mtume Yohana kushindikatiani Domitiani aliamua kumpeleka Mtume
19