You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Baadhi ya watu waliouawa katika kipindi hiki ni Fabiani askofu wa Rumi, Juliani
mwenyeji wa Cicil, (aliwekwa ndani ya ngozi ambayo ndani yake kulikuwa na nyoka
wengi na ng’e na kisha kutupwa baharini). Kijana mmoja aitwae Petro aliuawa baada
ya kukataa kutoa dhabihu kwa mungu wa kipagani Venasi, Nichomachus, binti Denisa.
Epimachus na Alexanda waliuawa kwa kuchomwa kwenye moto.
8. Vareliani (257-260 AD.) Idadi kubwa ya wakristo waliuawa pia katika kipindi hiki,
baadhi ya watu mashujaa walioifia imani yao katika kipindi hiki ni Rufina, Sekunda,
Stefano askofu wa Rumi, (alikatwa kichwa), Saturninus askofu wa Toulouse. Sektasi
askofu wa Rumi na Mashemasi sita waliuawa mnamo mwaka 258AD. Askofu Spriani
wa Kathegi aliuawa pia katika kipindi hiki.
9. Aureliani (270-275 B.K.) Badhi ya watu waliouawa chini ya utawala wa Aureliani ni
Agapetasi kijana aliyeuza shamba lake na kuwapa fedha maskini, Felix askofu wa
Rumi alikatwa kichwa katika kipindi chini ya utawala huu.
10. Deokretiani, Mtawala huyu aliimarisha na kuyakuza mateso katika dola yote ya
Rumi.Mateso yalienea kila eneo la himaya yake. Baadhi ya wafia dini waliouawa
katika kipindi hiki ni;- Sebastian,victor, Romanus,Susanna, Sipriani wa Antiokia,
Dorothea na wengine wengi, Mji wa frigia uliojulikana kama mji wa kikristo
ulichomwa moto na wakazi wake wote wakafa.
C. MATESO YA KITAIFA.
Tabia za msingi katika historia ya kanisa katika karne zote mbili yaani karne ya pili na ya
tatu ni kanisa au wakristo kuteswa na wafalme wa kirumi.
Mateso haya hayakuwa endelevu lakini yalitegemea mtazamo aliokuwa nao mfalme
aliyekuwa akitawala katika kipindi hicho.
Mateso ambayo yalikuwa yakijirudia katika kipindi hiki yalidumu kwa karibu miaka 200
mpaka mfalme Kostantino alipookoka na kutangaza tamko la amani.(Edict of Torelance)
katika mwaka wa 313 B.K
D. SABABU ZA KANISA KUTESWA.
1. Imani juu ya Mungu mmoja. Warumi walikuwa na miungu mbalimbali ambayo
walikuwa wakiiabudu pamoja na sanamu zao. Wakristo walitangaza kwamba kuna Mungu
mmoja tu. Mfalme wa Rumi alijenga hekalu ambalo lilipaswa kutumiwa na watu wote
kuabudu miungu yao.
Wakristo walilazimishwa kushiriki ibada hizo za kuabudu miungu. Kitendo cha Wakristo
kukataa kuabudu miungu hiyo kulisababisha mateso juu yao. Majanga ya aina yoyote
yalipotukia yalitazamwa kama ni matokeo ya muingu kukasirika hivyo basi watu wote
waliogoma kushiriki katika ibada hizo walihesabiwa kuwa ndiyo chanzo cha majanga
hayo hivyo kustahili adhabu.
2. Kukataa kumwabudu kaisari. Kama ilivyokwisha elezwa katika sura iliyopita
kwamba makaisari wa kirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai
17