21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Baadhi ya watu waliouawa katika kipindi hiki ni Fabiani askofu wa Rumi, Juliani

mwenyeji wa Cicil, (aliwekwa ndani ya ngozi ambayo ndani yake kulikuwa na nyoka

wengi na ng’e na kisha kutupwa baharini). Kijana mmoja aitwae Petro aliuawa baada

ya kukataa kutoa dhabihu kwa mungu wa kipagani Venasi, Nichomachus, binti Denisa.

Epimachus na Alexanda waliuawa kwa kuchomwa kwenye moto.

8. Vareliani (257-260 AD.) Idadi kubwa ya wakristo waliuawa pia katika kipindi hiki,

baadhi ya watu mashujaa walioifia imani yao katika kipindi hiki ni Rufina, Sekunda,

Stefano askofu wa Rumi, (alikatwa kichwa), Saturninus askofu wa Toulouse. Sektasi

askofu wa Rumi na Mashemasi sita waliuawa mnamo mwaka 258AD. Askofu Spriani

wa Kathegi aliuawa pia katika kipindi hiki.

9. Aureliani (270-275 B.K.) Badhi ya watu waliouawa chini ya utawala wa Aureliani ni

Agapetasi kijana aliyeuza shamba lake na kuwapa fedha maskini, Felix askofu wa

Rumi alikatwa kichwa katika kipindi chini ya utawala huu.

10. Deokretiani, Mtawala huyu aliimarisha na kuyakuza mateso katika dola yote ya

Rumi.Mateso yalienea kila eneo la himaya yake. Baadhi ya wafia dini waliouawa

katika kipindi hiki ni;- Sebastian,victor, Romanus,Susanna, Sipriani wa Antiokia,

Dorothea na wengine wengi, Mji wa frigia uliojulikana kama mji wa kikristo

ulichomwa moto na wakazi wake wote wakafa.

C. MATESO YA KITAIFA.

Tabia za msingi katika historia ya kanisa katika karne zote mbili yaani karne ya pili na ya

tatu ni kanisa au wakristo kuteswa na wafalme wa kirumi.

Mateso haya hayakuwa endelevu lakini yalitegemea mtazamo aliokuwa nao mfalme

aliyekuwa akitawala katika kipindi hicho.

Mateso ambayo yalikuwa yakijirudia katika kipindi hiki yalidumu kwa karibu miaka 200

mpaka mfalme Kostantino alipookoka na kutangaza tamko la amani.(Edict of Torelance)

katika mwaka wa 313 B.K

D. SABABU ZA KANISA KUTESWA.

1. Imani juu ya Mungu mmoja. Warumi walikuwa na miungu mbalimbali ambayo

walikuwa wakiiabudu pamoja na sanamu zao. Wakristo walitangaza kwamba kuna Mungu

mmoja tu. Mfalme wa Rumi alijenga hekalu ambalo lilipaswa kutumiwa na watu wote

kuabudu miungu yao.

Wakristo walilazimishwa kushiriki ibada hizo za kuabudu miungu. Kitendo cha Wakristo

kukataa kuabudu miungu hiyo kulisababisha mateso juu yao. Majanga ya aina yoyote

yalipotukia yalitazamwa kama ni matokeo ya muingu kukasirika hivyo basi watu wote

waliogoma kushiriki katika ibada hizo walihesabiwa kuwa ndiyo chanzo cha majanga

hayo hivyo kustahili adhabu.

2. Kukataa kumwabudu kaisari. Kama ilivyokwisha elezwa katika sura iliyopita

kwamba makaisari wa kirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai

17

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!