21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Simirna ni mji ambao ulikuwa umbali wa Km 65 Kaskazini mwa Efeso na ulijulikana

kama bandari ya salama kwa wakati ule. Ulikuwa katikati ya njia kuu kutoka Rumi

kwenda India na Persia (Irani)

Katika moja ya mitaa yake kulikuwa na hekalu la mungu wa kigiriki aliyejulikana kwa jina

la Zeus, Mungu mkuu na katika upande mwingine wa mji kulikuwa na hekalu la Cybele

{mama wa mungu}.

Mji wa Smirna pia ulikuwa ni kituo cha ibada ya kumwabudia kaisari. Kulikuwa na hekalu

la mfalme wa Rumi Teberio Kaisari

B. VIPINDI VYA MATESO

Historia ya kipindi cha Smirna. Inaaminika kwamba siku kumi za mateso yaliyotakiwa

kuja juu ya smirna huhusisha vipindi maalum kumi vya mateso chini ya watawala

mbalimbali wa kirumi ambao pia na wao watawala wangekuwa kumi.

Majina ya wafia dini mbalimali katika kipindi hiki cha Smirna chini ya wafalme

mbalimbali wa Rumi yanaorodheshwa hapa.

1. Klaudi Nero (64-68 B.K). Petro alisulubiwa katika kipindi cha utawala wa Nero.

Paulo alikatwa kichwa katika kipindi hiki.

2. Domitiani (90-95 B.K) alijaribu kumuua mtume Yohana kwa kumtumbukiza katika

mafuta yaliyokuwa yakichemka, lakini Yohana alitoka kwa muujiza bila kuungua.

Baada ya hapo akaamua kumpeleka uhamishoni katika kisiwa cha Patmo.Aliwaua

baadhi ya maseneta wa Rumi na kuamuru uzao wa Daudi wote kuuawa.

3. Trajani (104-117 B.K) Simoni ndugu wa Yesu aliuawa katika kipindi hiki

mwaka wa 107 B.K. Askofu Ignatius wa Antiokia aliuawa pia katika utawala wa

mfame huyu mwaka 110.B.K. Watu wengine waliouawa katika kipindi hiki ni

Polikap mwanafunzi wa Mtume Yohana (155 B.K),

4. Marcus Aurelius. (161-180 B.K). Yustini aliuawa katika utawala huu katika mwaka

165 B.K. Pia alifanya mauaji ya wakristo wengine wengi pia.

5. Septimus Severio. (200-211 B.K) alimuua Leonidasi baba wa Origeni,

mwanatheolojia mkuu, Victor askofu wa Rumi aliuawa katika kipindi hiki, pia

aliwaua Perpetua, Felistasi na Ireneusi mwaka 202 B.K

6. Thraker Maximus (235-237 B.K). kiongozi huyu alikuwa katili na asiye na huruma

kabisa. watu wengi sana waliuawa katika kipindi hiki baadhi yao ni, Pontianus

(askofu wa Rumi), Anterose, Maseneta wa Rumi na familia zao, Pamachius, Quirutus,

mwanamwali Martina na Hippolitus.

7. Desiusi. (250-253 B.K. ) katika kipndi cha utawala wake mateso yaliibuka tena juu

ya kanisa na kwa bahati nzuri utawala wake ulidumu kwa muda mfupi sana na baada

ya kuanguka kwa utawala wake kipindi kifupi cha amani kilikuja juu ya kanisa.

16

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!