Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Simirna ni mji ambao ulikuwa umbali wa Km 65 Kaskazini mwa Efeso na ulijulikana
kama bandari ya salama kwa wakati ule. Ulikuwa katikati ya njia kuu kutoka Rumi
kwenda India na Persia (Irani)
Katika moja ya mitaa yake kulikuwa na hekalu la mungu wa kigiriki aliyejulikana kwa jina
la Zeus, Mungu mkuu na katika upande mwingine wa mji kulikuwa na hekalu la Cybele
{mama wa mungu}.
Mji wa Smirna pia ulikuwa ni kituo cha ibada ya kumwabudia kaisari. Kulikuwa na hekalu
la mfalme wa Rumi Teberio Kaisari
B. VIPINDI VYA MATESO
Historia ya kipindi cha Smirna. Inaaminika kwamba siku kumi za mateso yaliyotakiwa
kuja juu ya smirna huhusisha vipindi maalum kumi vya mateso chini ya watawala
mbalimbali wa kirumi ambao pia na wao watawala wangekuwa kumi.
Majina ya wafia dini mbalimali katika kipindi hiki cha Smirna chini ya wafalme
mbalimbali wa Rumi yanaorodheshwa hapa.
1. Klaudi Nero (64-68 B.K). Petro alisulubiwa katika kipindi cha utawala wa Nero.
Paulo alikatwa kichwa katika kipindi hiki.
2. Domitiani (90-95 B.K) alijaribu kumuua mtume Yohana kwa kumtumbukiza katika
mafuta yaliyokuwa yakichemka, lakini Yohana alitoka kwa muujiza bila kuungua.
Baada ya hapo akaamua kumpeleka uhamishoni katika kisiwa cha Patmo.Aliwaua
baadhi ya maseneta wa Rumi na kuamuru uzao wa Daudi wote kuuawa.
3. Trajani (104-117 B.K) Simoni ndugu wa Yesu aliuawa katika kipindi hiki
mwaka wa 107 B.K. Askofu Ignatius wa Antiokia aliuawa pia katika utawala wa
mfame huyu mwaka 110.B.K. Watu wengine waliouawa katika kipindi hiki ni
Polikap mwanafunzi wa Mtume Yohana (155 B.K),
4. Marcus Aurelius. (161-180 B.K). Yustini aliuawa katika utawala huu katika mwaka
165 B.K. Pia alifanya mauaji ya wakristo wengine wengi pia.
5. Septimus Severio. (200-211 B.K) alimuua Leonidasi baba wa Origeni,
mwanatheolojia mkuu, Victor askofu wa Rumi aliuawa katika kipindi hiki, pia
aliwaua Perpetua, Felistasi na Ireneusi mwaka 202 B.K
6. Thraker Maximus (235-237 B.K). kiongozi huyu alikuwa katili na asiye na huruma
kabisa. watu wengi sana waliuawa katika kipindi hiki baadhi yao ni, Pontianus
(askofu wa Rumi), Anterose, Maseneta wa Rumi na familia zao, Pamachius, Quirutus,
mwanamwali Martina na Hippolitus.
7. Desiusi. (250-253 B.K. ) katika kipndi cha utawala wake mateso yaliibuka tena juu
ya kanisa na kwa bahati nzuri utawala wake ulidumu kwa muda mfupi sana na baada
ya kuanguka kwa utawala wake kipindi kifupi cha amani kilikuja juu ya kanisa.
16