21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Yudea, Siria, Rumi na Asia ndogo. Mtume Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa

chini miguu juu kwa ridhaa yake mwenyewe chini ya utawala wa Klaudi Nero.

2. Yakobo mwana wa Zebedayo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Bwana Yesu.

Baada ya kuitwa na Bwana Yesu aliacha kila kitu na kumfuata Yesu na alikuwa

mmojawapo wa wanafunzi watatu waliokuwa karibu sana na Yesu. Yakobo

alifanya huduma Yudea. Yakabo aliuawa kwa upanga kwa amri ya Herode

Antipa. Yakobo ni mtume pekee kati ya wale mitume waliouawa ambae kifo

chake kimeandikwa katika Biblia.

3. Yohana- alikuwa mvuvi wa samaki kabla ya kuitwa na Yesu. Baada ya kuitwa na

Yesu alikuwa mojawapo ya nguzo katika kanisa la Yerusalemu. Yohana

alifanya huduma Efeso, Patmo na Yudea. Yohana ni mtume pekee aliyekufa kifo

cha kawaida katika uzee mwema akiwa ameshiba siku. Inazaniwa kuwa yohana

alikufa kule efeso mnamo mwaka 100AD.

4. Andrea- Alikuwa mvuvi, alikuwa mwanafunzi wa Yohana mbatizaji na ni mtu wa

kwanza kumfuata Yesu na mwinjilisti wa kwanza. Aliitwa na Yesu kuwa mvuvi

wa watu. Inadhaniwa kwamba Andrea alifanya huduma katika maeneo ya

Ugiriki, Asia ndogo na Urusi. Mtume Andrea aliuawa kwa kusulubiwa katika

msalaba wenye umbo la X huko Ugiriki.

5. Filipo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Yesu. Mtume huyu alifanya huduma

katika maeneo ya alifanya huduma Frigia, Ukraine, Afrika Kaskazini, aliuawa

kwa kusulubiwa huko Hierapolis Uturuki

6. Batholomayo- ambaye anaitwa Nathanaeli, alikuwa mmisionari huko Asia.

Alimshuhudia Kristo katika maeneo ya Uturuki na akauwawa kwa sababu ya

kuhubiri injili huko Armenia, kw alichunwa ngozi akiwa hai mpaka akafa.

7. Thomaso. Mtume huyu kabla ya kuitwa na Yesu alikuwa ni fundi seremala na

fundi uashi. Mapokeo yanatuambia kuwa Thomaso alifanya huduma ya

umishenari katika nchi ya India. Mtume huyu aliuawa kwa kuchomwa

mkuki huko India.

8. Mathayo. Alikuwa ni afisa mapato (mtoza ushuru) katika Serikali ya Rumi katika

mji wa Kapernaum kabla ya kuitwa na Bwana Yesu. Mathayo alifanya huduma

katika nchi za Uajemi na Ethiopia. Mathayo aliuawa kwa kukatwa kichwa kwa

upanga baada ya kukataa kuikana imani.

9. Yakobo mwana wa Alfayo. Alifanya huduma katika nchi za Israeli, Misri na

Siriya. Mtume Yakobo wa Alfayo au Yakobo mdogo Alitupwa kutoka kwenywe

kinara cha hekalu na kisha kupigwa na rungu lenye misumari mpaka kufa huko

Yerusalem

14

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!