You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Yudea, Siria, Rumi na Asia ndogo. Mtume Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa
chini miguu juu kwa ridhaa yake mwenyewe chini ya utawala wa Klaudi Nero.
2. Yakobo mwana wa Zebedayo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Bwana Yesu.
Baada ya kuitwa na Bwana Yesu aliacha kila kitu na kumfuata Yesu na alikuwa
mmojawapo wa wanafunzi watatu waliokuwa karibu sana na Yesu. Yakobo
alifanya huduma Yudea. Yakabo aliuawa kwa upanga kwa amri ya Herode
Antipa. Yakobo ni mtume pekee kati ya wale mitume waliouawa ambae kifo
chake kimeandikwa katika Biblia.
3. Yohana- alikuwa mvuvi wa samaki kabla ya kuitwa na Yesu. Baada ya kuitwa na
Yesu alikuwa mojawapo ya nguzo katika kanisa la Yerusalemu. Yohana
alifanya huduma Efeso, Patmo na Yudea. Yohana ni mtume pekee aliyekufa kifo
cha kawaida katika uzee mwema akiwa ameshiba siku. Inazaniwa kuwa yohana
alikufa kule efeso mnamo mwaka 100AD.
4. Andrea- Alikuwa mvuvi, alikuwa mwanafunzi wa Yohana mbatizaji na ni mtu wa
kwanza kumfuata Yesu na mwinjilisti wa kwanza. Aliitwa na Yesu kuwa mvuvi
wa watu. Inadhaniwa kwamba Andrea alifanya huduma katika maeneo ya
Ugiriki, Asia ndogo na Urusi. Mtume Andrea aliuawa kwa kusulubiwa katika
msalaba wenye umbo la X huko Ugiriki.
5. Filipo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Yesu. Mtume huyu alifanya huduma
katika maeneo ya alifanya huduma Frigia, Ukraine, Afrika Kaskazini, aliuawa
kwa kusulubiwa huko Hierapolis Uturuki
6. Batholomayo- ambaye anaitwa Nathanaeli, alikuwa mmisionari huko Asia.
Alimshuhudia Kristo katika maeneo ya Uturuki na akauwawa kwa sababu ya
kuhubiri injili huko Armenia, kw alichunwa ngozi akiwa hai mpaka akafa.
7. Thomaso. Mtume huyu kabla ya kuitwa na Yesu alikuwa ni fundi seremala na
fundi uashi. Mapokeo yanatuambia kuwa Thomaso alifanya huduma ya
umishenari katika nchi ya India. Mtume huyu aliuawa kwa kuchomwa
mkuki huko India.
8. Mathayo. Alikuwa ni afisa mapato (mtoza ushuru) katika Serikali ya Rumi katika
mji wa Kapernaum kabla ya kuitwa na Bwana Yesu. Mathayo alifanya huduma
katika nchi za Uajemi na Ethiopia. Mathayo aliuawa kwa kukatwa kichwa kwa
upanga baada ya kukataa kuikana imani.
9. Yakobo mwana wa Alfayo. Alifanya huduma katika nchi za Israeli, Misri na
Siriya. Mtume Yakobo wa Alfayo au Yakobo mdogo Alitupwa kutoka kwenywe
kinara cha hekalu na kisha kupigwa na rungu lenye misumari mpaka kufa huko
Yerusalem
14