Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Kwa msaada wa Josephus (mwanahistoria) Tito ambaye hakutaka kuliangamiza taifa la
Wayahudi aliwasihi wayahudi kujisalimisha na kuweka silaha zao chini. Wayahudi
hawakuwa tayari.Hivyo basi hekalu lilichomwa moto na kubomolewa likiwa na watu
ndani ambao walikuwa wamekimbilia ndani ya hekalu ili kujinusuru na vita hiyo.
Liliongozwa na Tito lilifanikiwa kuiangusha Yerusalemu na kuchukua vitu vyote vya
thamani. Mambo yote yalitimia sawasawa na ilivyotabiliwa na Bwana wetu Yesu Kristo
katika Mathayo 24:1-2
1. Yes akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili
kumwonyesha majengo ya hekalu. 2 Naye akajibu akawaambia, Hamyaoni haya
yote ? Amin, nawaambieni, halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo
halitabomoshwa.
Ingawa wayahudi zaidi ya milioni waliuawa katika vita hiyo lakini ni wakristo
wachache tu waliopoteza maisha yao. Hii ni kwa sababu Bwana Yesu alikuwa amekwisha
kuwaonya tayari kabla ya maangamizi hayo kutokea. Tunajifunza kuwa ni muhimu sana
kufuata maelekezo ya Kimungu ili kuwa salama katika maisha na huduma kwa ujumla.
LUKA 21:20-24
20 Lakini, hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na mejeshi, ndipo jueni ya
kwamba uharibifu wake umekaribia.
21 Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie
nje, na walio katika mashamba wasiuingie.
22 Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.
Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida
nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili. 24Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao
watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na
mataifa, hata majira ya mataifa yatakapotimia.
Mahali lilipokuwepo hekalu umejengwa msikiti mkubwa sana na Wapalestina ambao ndio
mojawapo ya sababu za kutoisha kwa mgogoro wa mashariki ya kati. Israeli walianza
kurudi nchini kwao taratibu na hatimae taifa la Israeli liliundwa kwa upya mnamo mwaka
1948 chini ya Umoja wa mataifa. Umoja wa mataifa ulitangaza kuitambua Israeli kama
jamhuri yenye mamlaka kamili.
Mungu alilionya kanisa Ufunuo wa Yohana 2:4-5
4. Lakini nina neon juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.
5. Basi, kumbuka ni wapi ulipoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini
usipofanya hivyo, naja kwako name nitakiondoa kinara chako katika mahali
pake,usipotubu.
Q. VIFO VYA MITUME WA BWANA WETU YESU KRISTO NA MAENEO YAO YA HUDUMA
1. Petro- alikuwa mvuvi wa Samaki kabla ya kuitwa na Yesu na ndiye kiongozi wa
kwanza wa Kanisa. Petro alifanya huduma katika maeneo yafuatayo, Yerusalemu,
13