21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Kwa msaada wa Josephus (mwanahistoria) Tito ambaye hakutaka kuliangamiza taifa la

Wayahudi aliwasihi wayahudi kujisalimisha na kuweka silaha zao chini. Wayahudi

hawakuwa tayari.Hivyo basi hekalu lilichomwa moto na kubomolewa likiwa na watu

ndani ambao walikuwa wamekimbilia ndani ya hekalu ili kujinusuru na vita hiyo.

Liliongozwa na Tito lilifanikiwa kuiangusha Yerusalemu na kuchukua vitu vyote vya

thamani. Mambo yote yalitimia sawasawa na ilivyotabiliwa na Bwana wetu Yesu Kristo

katika Mathayo 24:1-2

1. Yes akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili

kumwonyesha majengo ya hekalu. 2 Naye akajibu akawaambia, Hamyaoni haya

yote ? Amin, nawaambieni, halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo

halitabomoshwa.

Ingawa wayahudi zaidi ya milioni waliuawa katika vita hiyo lakini ni wakristo

wachache tu waliopoteza maisha yao. Hii ni kwa sababu Bwana Yesu alikuwa amekwisha

kuwaonya tayari kabla ya maangamizi hayo kutokea. Tunajifunza kuwa ni muhimu sana

kufuata maelekezo ya Kimungu ili kuwa salama katika maisha na huduma kwa ujumla.

LUKA 21:20-24

20 Lakini, hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na mejeshi, ndipo jueni ya

kwamba uharibifu wake umekaribia.

21 Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie

nje, na walio katika mashamba wasiuingie.

22 Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.

Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida

nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili. 24Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao

watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na

mataifa, hata majira ya mataifa yatakapotimia.

Mahali lilipokuwepo hekalu umejengwa msikiti mkubwa sana na Wapalestina ambao ndio

mojawapo ya sababu za kutoisha kwa mgogoro wa mashariki ya kati. Israeli walianza

kurudi nchini kwao taratibu na hatimae taifa la Israeli liliundwa kwa upya mnamo mwaka

1948 chini ya Umoja wa mataifa. Umoja wa mataifa ulitangaza kuitambua Israeli kama

jamhuri yenye mamlaka kamili.

Mungu alilionya kanisa Ufunuo wa Yohana 2:4-5

4. Lakini nina neon juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.

5. Basi, kumbuka ni wapi ulipoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini

usipofanya hivyo, naja kwako name nitakiondoa kinara chako katika mahali

pake,usipotubu.

Q. VIFO VYA MITUME WA BWANA WETU YESU KRISTO NA MAENEO YAO YA HUDUMA

1. Petro- alikuwa mvuvi wa Samaki kabla ya kuitwa na Yesu na ndiye kiongozi wa

kwanza wa Kanisa. Petro alifanya huduma katika maeneo yafuatayo, Yerusalemu,

13

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!