You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
alikuwa mfungwa bado alileta athari kubwa katika kanisa huko Rumi. Moja ya mambo
makuu aliyofanya ni kuandika nyaraka kwa Waefeso, Wafilipi, Wakolosai na
Filemoni.
Inaaminika kwamba baada ya miaka miwili ya kukaa kifungoni mtume Paulo aliachiwa
huru (Mdo 28:30-31) lakini hakuna kumbukumbu kamili katika kipindi hiki isipokuwa
taarifa chache tu.
Mapokeo yanasema kwamba mtume Paulo alikamatwa Nikroporisi Kaskazini mwa
Ugiriki chini ya mtawala wa Rumi aliyeitwa Nero na akarudishwa Rumi katika kifungo
hiki cha pili aliandika nyaraka zifuatazo:- 1&2Timotheo, na Tito. Barua hizi zilikuwa ni
barua zake za mwisho mnamo mwaka 68. B.K. Mtume Paulo aliuawa kwa amri ya mfalme
Nero. Mtume huyu aliuawa kwa kukatwa kichwa.
N. UANDISHI WA MAANDIKO MATAKATIFU.
Inadhaniwa kwamba mpaka kipindi cha Mkutano Yerusalemu mnamo mwaka 48. B.K
hakuna hata kitabu kimoja cha Agano jipya kilichokuwa kimeandikwa, lakini karibu ya
mwaka 68.B.K idadi kubwa ya Maandiko ya Agano Jipya yalikuwa tayari yameandikwa,
hii ikijumlisha Injili ya Mathayo, marko, Luka, nyaraka za Paulo, Yakobo na 1Petro.
Katika kipindi cha miaka ya 68- 100.B.K vitabu vingine viliandikwa.Waraka kwa
Waebrania, 2Petro, Injili ya Yohana na nyaraka tatu za Yohana, yuda na Ufunuo wa
Yohana.
O. KIPINDI CHA UVULI
Tangu kukatwa kichwa mtume Paulo mwaka 68AD hadi kifo cha mtume Yohana 100 AD.
Kipindi hiki Kinaitwa kipindi cha uvuli kwa sababu wimbi la mateso lilikuwa limetanda
juu ya kanisa na kwamba ni mambo machache tu yanayofahamika kuhusu kipindi hiki.
Kipindi cha miaka 50 cha ukimya kinaelea juu ya kanisa baada ya kuuawa kwa mtume
Paulo. Kutoka mwaka 120AD tunapata maandiko ya mababa wa kwanza wa kanisa, lakini
pia tunakuta kanisa linatofautiana kwa namna nyingi na kanisa la siku za Petro na Paulo.
P. KUANGUKA KWA YERUSALEM
Mnamo mwaka 70AD kulitokea badiliko kubwa la kimahusiano kati ya Wakristo
Wayahudi. Mpaka kufikia kipindi hiki ni Wayahudi pekee waliokuwa wakiishi Israeli ndio
waliokuwa wakimpinga Kaisari. Wayahudi wa sehemu nyingine yote ya dola ya Rumi
walikuwa watii kwa Kaisari na hivyo waliishi kwa amani.
Wayahudi walitafsiri unabii katika Maandiko Matakatifu na kuamini kwamba walitakiwa
kuutawala ulimwengu wote kama ambavyo watafanya katika kipindi cha Milenia.
Mnamo mwaka 66AD wayahudi waliuasi utawala wa Rumi na mnamo mwaka 70AD
mfalme Vespasiani aliamua kuleta maangamizi juu ya taifa la Wayahudi.Alimtuma kijana
wake Tito na jeshi kubwa na imara kwenda kuishambulia Yerusalemu.
12