Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Inaonekena Wayahudi hao Walianzisha uvumi huo ili serikali iweze kushiriki katika zoezi
la kuwadhibiti mitume.
Kanisa katika Beroya. Injili ilikubaliwa kwa watu wote Wamataifa na Wayahudi. Wakati
Wayahudi wa Thesalonike waliposikia walikuja tena kufanya ghasia dhidi ya mitume
hivyo iliwalazimu Paulo na Sila kuondoka mjini hapo, lakini Neno la Mungu lilikuwa
tayari limehubiriwa.
Hakika mitume hawa waliishi sawasawa na Neno la Kristo “Watakapowafukuza katika mji
mmoja kimbilieni katika mji mwingine. (Mt 10:23)
Kanisa katika Athene. Hapa pia mitume hawa waliwaendea Wayahudi , lakini wayahudi
hao hawakulipokea Neno. Baadae mtume Paulo aligundua ya kwamba Mungu
aliwapofusha macho Waisraeli kwa muda kwa sababu walimsulubisa Kristo Yesu.
Wanafalsafa wa Kigiriki walimpa mtume paaulo changamoto japo kuwa si sana kwa
sababu walitaka kulisikia Neno, hawakutubu bali walivutiwa tu na mdahalo. Walipokuwa
hawajui chakujibu walidhihaki.
Kanisa katika Korintho. Pia mahali hapa kama ilivyokuwa kawaida yake mtume Paulo
alikwenda kwa Wayahudi kwanza. Alikaa na Wayahudi watengeneza mahema (Akila na
Prisila). Inadhaniwa kuwa alitengeneza nao mahema ili kujipatia pesa kwaajili ya kujikimu
ili aweze kuhubiri Injili pasipo kumlemea mtu yeyote.(Mdo 20:34). Japokuwa Paulo
alikuwa ni Rabi aliyeelimika na Mtume hakudharau kazi ndondogo kwaajili ya kueneza
Injili.
Maamuzi Thabiti. Wayahudi waliipinga Injili tena na hii ilileta mtazamo mpya kwa
huduma ya Injili ya Paulo. Mtume Paulo alisema
Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu mimi ni safi tangu sasa nitakwenda kwa watu wa
mataifa. (Mdo 18:6)
Paulo na Sila walikaa Korintho kwa muda wa miezi kumi na nane (18) wakiwafundisha
waamini. Kutoka Korintho mtume Paulo aliandika nyaraka mbili kwa Wathesalonike
Baada ya shambulio lingine lililofanywa na Wayahudi dhidi yake (Paulo) aliamua
kuondoka Korintho na kurejea Antiokia kwa kupitia Efeso na Kaisaria.
Safari ya tatu ya umisheni ya mtume Paulo (Mdo 18:23-22:17)
Katika awamu hii mtu aliyeambatana na mtume Paulo ni Timotheo aliyejiunga katika timu
yake katika safari ya pili ya umisheni huko Listra. (Mdo 1-3) na kwa muda mfupi idadi
kubwa ya wanatimu walikuwa pamojanae kabla hajamaliza safari hii. Mmojawapo wa
watu hao muhimu alikwa ni Dkt. Luka.
M. PAULO MTUME KATIKA MINYORORO (Mdo 22:23-28: 31)
Paulo alitumia miaka kadhaa akiwa gerezani lakini kamwe hakuacha kufanya kazi ya
umisheni. Mazingira hayakubadili kusudi lake. Baada ya safari ndefu Paulo alifika Rumi
jiji ambalo alitamini sana kuliona. Alikuwa na uhuru wa kuishi katika nyumba aliyokuwa
ameipanga mwenyewe huku akiwa chini ya uangalizi wa askari magereza, japokuwa
11