21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Inaonekena Wayahudi hao Walianzisha uvumi huo ili serikali iweze kushiriki katika zoezi

la kuwadhibiti mitume.

Kanisa katika Beroya. Injili ilikubaliwa kwa watu wote Wamataifa na Wayahudi. Wakati

Wayahudi wa Thesalonike waliposikia walikuja tena kufanya ghasia dhidi ya mitume

hivyo iliwalazimu Paulo na Sila kuondoka mjini hapo, lakini Neno la Mungu lilikuwa

tayari limehubiriwa.

Hakika mitume hawa waliishi sawasawa na Neno la Kristo “Watakapowafukuza katika mji

mmoja kimbilieni katika mji mwingine. (Mt 10:23)

Kanisa katika Athene. Hapa pia mitume hawa waliwaendea Wayahudi , lakini wayahudi

hao hawakulipokea Neno. Baadae mtume Paulo aligundua ya kwamba Mungu

aliwapofusha macho Waisraeli kwa muda kwa sababu walimsulubisa Kristo Yesu.

Wanafalsafa wa Kigiriki walimpa mtume paaulo changamoto japo kuwa si sana kwa

sababu walitaka kulisikia Neno, hawakutubu bali walivutiwa tu na mdahalo. Walipokuwa

hawajui chakujibu walidhihaki.

Kanisa katika Korintho. Pia mahali hapa kama ilivyokuwa kawaida yake mtume Paulo

alikwenda kwa Wayahudi kwanza. Alikaa na Wayahudi watengeneza mahema (Akila na

Prisila). Inadhaniwa kuwa alitengeneza nao mahema ili kujipatia pesa kwaajili ya kujikimu

ili aweze kuhubiri Injili pasipo kumlemea mtu yeyote.(Mdo 20:34). Japokuwa Paulo

alikuwa ni Rabi aliyeelimika na Mtume hakudharau kazi ndondogo kwaajili ya kueneza

Injili.

Maamuzi Thabiti. Wayahudi waliipinga Injili tena na hii ilileta mtazamo mpya kwa

huduma ya Injili ya Paulo. Mtume Paulo alisema

Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu mimi ni safi tangu sasa nitakwenda kwa watu wa

mataifa. (Mdo 18:6)

Paulo na Sila walikaa Korintho kwa muda wa miezi kumi na nane (18) wakiwafundisha

waamini. Kutoka Korintho mtume Paulo aliandika nyaraka mbili kwa Wathesalonike

Baada ya shambulio lingine lililofanywa na Wayahudi dhidi yake (Paulo) aliamua

kuondoka Korintho na kurejea Antiokia kwa kupitia Efeso na Kaisaria.

Safari ya tatu ya umisheni ya mtume Paulo (Mdo 18:23-22:17)

Katika awamu hii mtu aliyeambatana na mtume Paulo ni Timotheo aliyejiunga katika timu

yake katika safari ya pili ya umisheni huko Listra. (Mdo 1-3) na kwa muda mfupi idadi

kubwa ya wanatimu walikuwa pamojanae kabla hajamaliza safari hii. Mmojawapo wa

watu hao muhimu alikwa ni Dkt. Luka.

M. PAULO MTUME KATIKA MINYORORO (Mdo 22:23-28: 31)

Paulo alitumia miaka kadhaa akiwa gerezani lakini kamwe hakuacha kufanya kazi ya

umisheni. Mazingira hayakubadili kusudi lake. Baada ya safari ndefu Paulo alifika Rumi

jiji ambalo alitamini sana kuliona. Alikuwa na uhuru wa kuishi katika nyumba aliyokuwa

ameipanga mwenyewe huku akiwa chini ya uangalizi wa askari magereza, japokuwa

11

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!