You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
L. KANISA MIONGONI MWA MATAIFA.
Tangu mauaji ya Stefano (48 B.K) mpaka mauaji ya Paulo mtume mwaka 68 B.K
Katika kipindi hiki chote tunategemea kitabu cha Matendo ya Mitume, nyaraka za Paulo na
waraka wa kwanza wa Petro. Umisheni wa mtume Paulo na Watendakazi wenzake
ulifanyika katika dola yote ya Rumi. Wakati mitume wengine walikwenda nchi za
mbali zaidi. (hii ni kulingana na mapokeo).
Idadi ya waamini wa kimataifa ilikua kwa kasi sana wakati idadi ya waamini wa kiyahudi
iliendelea kushuka.Wayahudi walianza kukasirika na kufanya fitina dhidi ya kanisa na
walikuwa tayari kuanzisha mateso dhidi ya wakristo.
Safari Ya Pili Ya Mtume Paulo
Kwa sababu ya kupishana kwa Balnaba na Paulo, Balnaba alimchukua mpwa wake
Yohana (Marko) na kwenda katika nchi ya kwao Kipro, Paulo alimchukua nabii Sila katika
safari yake ya pili ya umisheni na kwenda kuyatembelea makanisa waliyokuwa
wameyafungua katika safari ya kwanza walipokuwa na Balnaba. Paulo alikusudia kwenda
Bithinia lakini Roho Mtakatifu akamkataza. Kisha walielekea Troa mji wa Kaskazini
Magharibi ya Asia ndogo.
Injili inakwenda Ulaya. (Wito wa Makedonia)
Usiku mmoja wakati Paulo na Sila wakiwa Troa mtu wa Makedonia alimtokea kwenye
maono akisema “Vuka uje Makedonia utusaidie” Mara Paulo na Sila walikwenda
Makedonia katika bara la Ulaya na wakaanzisha kanisa katika mji wa Filipi, Thesolanike,
Beroya, Athene na Korintho.
Tunakumbuka kwamba mwanzoni kila mahali Paulo alipokwenda , aliwaendea Wayahudi
kwanza. Wayahudi toka sehemu mbalimbali za dunia ya wakati ule walikuwepo katika
siku ya Pentekoste na walishuhudia kumiminwa kwa Roho Mtakatifu na ubatizo wa
waamini wapya 3,000. Wengi wao walitoka nchi za mbali kuja kusherehekea sikukuu ya
Pasaka katika mji wa Yesulasalemu na kurudi nchini kwao. Inawezekana baadhi yao
mtume Paulo alikutana nao, kwasababu baadhi yao walionekana kuwa na urafiki zaidi na
Paulo.
Wakati wayahudi wengi walipoikataa Injili ya Kristo kama mfufuka mwana wa Mungu,
Paulo aliwageukia watu wa mataifa.
Kanisa katika Filipi, Mwamini wa kwanza katika Ulaya alikuwa ni mwanamke aliyeitwa
Lidia muuzaji wa rangi za zambarau na mwenyeji wa Tiathira. Yeye na nyumba yake
walibatizwa na alifungua mlango wa nyumba yake kwaajili ya watumishi wa Mungu.
Kanisa katika Thesalonike. Pia katika mji huu mtume Paulo alikwenda kwa Wayahudi
kwanza kama ilvyokuwa desturi yake. Baadhi ya Wayahudi na Wayunani waliamini.
Wayahudi wasioamini walianzisha ghasia dhidi ya watumishi wa Mungu, yaani Paulo na
watendakazi wenzake. Kwa hakika washitaki hawa walijua nini cha kusema. Kama
mitume wangekamatwa kwa kuanzisha dini nyingine hakuna tatizo ambalo lingetokea kwa
watesi kwa sababu Ugiriki ilikuwa ina dini nyingi na walizikubali karibu zote.
Wao walikuja na uvumi mwingine kabisa kwa kusema kwamba
“Watu hawa wanadai kwamba kuna mfalme mwingine”.
10