Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
K. KUTENGANA KWA WAMISHENARI . Wakati mitume hao {Paulo na Balnaba}
walipokuwa wanajiandaa kwaajili ya safari yao ya pili ya umisheni walipishana. Kulitokea
kutokuelewana katika jambo moja. Balnaba alitaka kumchukua Marko{ ambae aliwaacha
katika safari ya kwanza ya umishenari na kurudi Yerusalemu} ili waende nae katika safari
ya pili ya umisheni, lakini Paulo alikataa kuambatana nae, hivyo kukatokea mgongano kati
yao na kisha wakaamua kutengana.
Hapa tunaona moyo wa kichungaji wa Balnaba, japokuwa Marko alishindwa katika
safari ya kwanza ya umishenari aliamua kumpa nafasi nyingine. tuna mwona Paulo
akiwa mtu wa kushikilia kanuni kuliko kumpendeza mtu yeyote. Mtu ambae yuko tayari
kuvunja mahusiano na Balnaba kuliko kukubaliana nae. Miaka ilipita na Mtume Paulo
akakomaa kiimani. Mtume Paulo ambae alisema katika uchanga wake : mimi si duni
kuliko hao mitume wakubwa {2Kor 11:5}. Baadae alisema ‘Mimi ni wa kwanza kwa
wenye dhambi {1Tim 1:16}. Paulo alifika mahali pakujitambua, kujisifu kulibadilishwa na
kujishusha na upendo ulichukua nafasi mahali pa chuki na kanuni.
Katika waraka wake wa pili kwa Wakorintho alisisitiza sana upendo na msamaha. Baadae
tunamwona Mtume Paulo akiwa katika upweke gerezani akisubiri kunyongwa.
Alimwagiza Timotheo kumleta Marko. Marko huyu huyu ndiye aliyemkataa wakati
wanafanya huduma na Balnaba.
Kutokana na hili tunajifunza ya kwamba tusimkatae mtu kutokana na makosa aliyoyafanya
kwa sababu twaweza kumhitaji tena baadae. Tuwasaidie wakosaji kwa upendo bila
kuwahukumu.
7. Mkutano wa Yerusalemu. {48.B.K}. Tatizo lilitokana na kuokoka kwa watu wa
wamataifa na kujiunga na kanisa. Wakristo wakiyahudi walikuwa na mitazamo tofauti
tofauti juu ya hili .Walikuwa na mitazamo ifuatayo:
1. Kundi lenye msimamo mkali. Kundi hili liliamini ya kwamba hakuna wokovu nje ya
Israeli . Kwa hiyo ingawa wamataifa wamempokea Yesu Kristo kama Masihi wao kwahiyo
walipaswa kutahiriwa na kushika Torati ya Musa {Sheria za Kiyahudi} Ili waweze
kuokolewa Bila kufanya hivyo wokovu wao ungekuwa ni batili.
Kundi la wenye mabadiliko.Hawa waliamini kwamba wokovu ni kwa njia ya imani katika
Yesu Kristo. Bila ya kushika sheria za kiyahudi. Wao waliamini kwamba sheria za
kiyahudi haziwahusu watu wa mataifa. Paulo na Balnaba walikuwa mojawapo wa watu
wenye mtazamo huu. Mkutano uliitishwa Yerusalemu ili kushughulikia jambo hili muhimu
la mafundisho kutokana na watu wa mataifa kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na
Mwokozi wao. Baada ya majadiliano marefu Mitume na Wazee walifikia hitimisho ambalo
lilithibitishwa na Roho mtakatifu kwamba Wamataifa hawakuwa chini ya Sheria za
kiyahudi na kwamba walichotakiwa kufanya ni kujiepusha na Ibada ya sanamu, kula
nyama iliyosongolewa na damu, kujiepusha na uasherati na uzinzi.
Mitume waliandika barua na ikapelekwa kwa kanisa la mataifa kwa mikono ya Paulo,
Balnaba, Yuda na Sila. Walipofika Antikoa walilikusanya kanisa na kuwapa ujumbe wa
kikao cha mitume na wazee kilichofanyika Yerusalemu kuhusu tatizo lao. Waamini hawa
walifurahi sana kupata ujumbe wenye kuwatia moyo {Mdo 15:30-31}
9