21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

K. KUTENGANA KWA WAMISHENARI . Wakati mitume hao {Paulo na Balnaba}

walipokuwa wanajiandaa kwaajili ya safari yao ya pili ya umisheni walipishana. Kulitokea

kutokuelewana katika jambo moja. Balnaba alitaka kumchukua Marko{ ambae aliwaacha

katika safari ya kwanza ya umishenari na kurudi Yerusalemu} ili waende nae katika safari

ya pili ya umisheni, lakini Paulo alikataa kuambatana nae, hivyo kukatokea mgongano kati

yao na kisha wakaamua kutengana.

Hapa tunaona moyo wa kichungaji wa Balnaba, japokuwa Marko alishindwa katika

safari ya kwanza ya umishenari aliamua kumpa nafasi nyingine. tuna mwona Paulo

akiwa mtu wa kushikilia kanuni kuliko kumpendeza mtu yeyote. Mtu ambae yuko tayari

kuvunja mahusiano na Balnaba kuliko kukubaliana nae. Miaka ilipita na Mtume Paulo

akakomaa kiimani. Mtume Paulo ambae alisema katika uchanga wake : mimi si duni

kuliko hao mitume wakubwa {2Kor 11:5}. Baadae alisema ‘Mimi ni wa kwanza kwa

wenye dhambi {1Tim 1:16}. Paulo alifika mahali pakujitambua, kujisifu kulibadilishwa na

kujishusha na upendo ulichukua nafasi mahali pa chuki na kanuni.

Katika waraka wake wa pili kwa Wakorintho alisisitiza sana upendo na msamaha. Baadae

tunamwona Mtume Paulo akiwa katika upweke gerezani akisubiri kunyongwa.

Alimwagiza Timotheo kumleta Marko. Marko huyu huyu ndiye aliyemkataa wakati

wanafanya huduma na Balnaba.

Kutokana na hili tunajifunza ya kwamba tusimkatae mtu kutokana na makosa aliyoyafanya

kwa sababu twaweza kumhitaji tena baadae. Tuwasaidie wakosaji kwa upendo bila

kuwahukumu.

7. Mkutano wa Yerusalemu. {48.B.K}. Tatizo lilitokana na kuokoka kwa watu wa

wamataifa na kujiunga na kanisa. Wakristo wakiyahudi walikuwa na mitazamo tofauti

tofauti juu ya hili .Walikuwa na mitazamo ifuatayo:

1. Kundi lenye msimamo mkali. Kundi hili liliamini ya kwamba hakuna wokovu nje ya

Israeli . Kwa hiyo ingawa wamataifa wamempokea Yesu Kristo kama Masihi wao kwahiyo

walipaswa kutahiriwa na kushika Torati ya Musa {Sheria za Kiyahudi} Ili waweze

kuokolewa Bila kufanya hivyo wokovu wao ungekuwa ni batili.

Kundi la wenye mabadiliko.Hawa waliamini kwamba wokovu ni kwa njia ya imani katika

Yesu Kristo. Bila ya kushika sheria za kiyahudi. Wao waliamini kwamba sheria za

kiyahudi haziwahusu watu wa mataifa. Paulo na Balnaba walikuwa mojawapo wa watu

wenye mtazamo huu. Mkutano uliitishwa Yerusalemu ili kushughulikia jambo hili muhimu

la mafundisho kutokana na watu wa mataifa kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na

Mwokozi wao. Baada ya majadiliano marefu Mitume na Wazee walifikia hitimisho ambalo

lilithibitishwa na Roho mtakatifu kwamba Wamataifa hawakuwa chini ya Sheria za

kiyahudi na kwamba walichotakiwa kufanya ni kujiepusha na Ibada ya sanamu, kula

nyama iliyosongolewa na damu, kujiepusha na uasherati na uzinzi.

Mitume waliandika barua na ikapelekwa kwa kanisa la mataifa kwa mikono ya Paulo,

Balnaba, Yuda na Sila. Walipofika Antikoa walilikusanya kanisa na kuwapa ujumbe wa

kikao cha mitume na wazee kilichofanyika Yerusalemu kuhusu tatizo lao. Waamini hawa

walifurahi sana kupata ujumbe wenye kuwatia moyo {Mdo 15:30-31}

9

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!