21.03.2020 Views

HISTORIA YA KANISA I DBT 2019 PRINT

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

ulitokea huka Samaria. Watu wa huko Samaria waliokoka na kubatizwa. Mitume

walipopata habari hii walikuja kuwaombea ujazo wa Roho Mtakatifu. Baada ya maombi

hayo Wasamaria walijazwa Roho Mtakatifu.

3. Injili inakwenda Afrika {Mdo 8 }. Roho mtakatifu alimtuma mwinjilisti Filipo kwenda

kumhubiri Neno Toashi wa Kushi {Waziri wa fedha wa Ethiopia}. Filipo alimwongoza

towashi huyu kwa Bwana na kisha akambatiza. Inaaminika kwamba toashi huyu alipeleka

Injili Afrika kwa sabau alikuwa ni mkazi wa Bara la Afrika katika nchi ya Ethiopia

J. MTESI WA KANISA ABADILI UPANGA {Mdo 9 }

Sauli wa Tarso ambae ndiye aliekuwa mtesi mkuu wa kanisa kwa kipindi hiki aliokoka

baada ya kukutana na Yesu Kristo alipokuwa safarini kuelekea Dameski kuwakamata na

kuwaua waamini {Mdo 9:20 }. Mara baada ya kuokoka alianza kuihubiri Injili {Kumhubiri

Kristo Yesu}. Paulo aliweka chini upanga wake wa mauaji na kuchukua upanga wa

Neno la mungu ambao hakuuacha mpaka kifo chake.{ 2Tim 4:7}.

Paulo alikwenda katika jangwa la Arabia kwa miaka Mitatu ambapo alipata mafunuo zaidi

toka kwa Mungu. Baada ya hapo alirudi Yerusalemu kuonana na mitume. Baada ya Sauli

kukutana na Ndugu alirudi tena Tarso. Kanisa lilipata raha baada ya kuokoka kwa Sauli wa

Tarso.{Gal 1:16-18, Mdo 9:20-31}.

5. Injili inakwenda kwa watu wa mataifa{Mdo 10 }. Mtume Petro alitumwa kwenda

kumhubiri Kornelio mtu wa Mataifa. Mtume Petro ndiye aliyefungu mlango wa Injili kwa

wayahudi na kwa Watu wa mataifa. Petro alihubiri Injili kwenye nyumba wote waliokuwa

wamekusanyika wakimsikiliza walishukiwa na Roho Mtakatifu na wakaanza kunena kwa

Lugha mpya, kisha Petro akawabatiza. Huu ulikuwa ni mwanzo wa Injili au kanisa

kuwafikia watu wa mataifa.

6. Injili inakwenda Asia Ndogo {Mdo 13} Katika sura hii tunaona wito wa wamishenari

wawili kwenda kuhubiri katika nchi ya kigeni. Wito huu na kutumwa huku kulifanyika

Antiokia mahali ambapo wanafunzi walipewa jina na kuitwa Wakristo kwa mara ya

kwanza {Mdo 11:26}.

Balnaba alikuwa ni mchungaji wakati Paulo alipokuja kutoka Dameski. Wanafunzi wote

walimwogopa Paulo, Balnaba alimpokea na kumtambulisha kwa kanisa {mitume

Yerusalemu} Mdo 9;26-29.

Japokuwa mitume walimtuma Balnaba Antiokia mahali ambapo kanisa lilikuwa na uamsho

mkubwa aliamua kufunga safari kutembea zaidi ya KM 150 kwa meli ili kwenda

kumtafuta Sauli wa Tarso .Alimpata na kisha akamchukua na kuja nae Antiokia bila kujua

kwamba miaka ya mbele sauti ya Bwana ingemwita kupitia njia ya unabii

‘Nitengeeni Balnaba na Sauli kwa kazi niliowaitia.{Mdo 13:1-5 }.

Balnaba na Paulo waliombewa na kanisa na kisha kwenda kwenye umisheni wao kuelekea

Asia ndogo mahali ambapo walianzisha makanisa mengi. Kama inavyoainishwa katika

Matendo ya Mitume 13 na 14. Baadae walirudi Antiokia mahali ambapo palikuwa ni kituo

chao cha umisheni.

8

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!