Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
ulitokea huka Samaria. Watu wa huko Samaria waliokoka na kubatizwa. Mitume
walipopata habari hii walikuja kuwaombea ujazo wa Roho Mtakatifu. Baada ya maombi
hayo Wasamaria walijazwa Roho Mtakatifu.
3. Injili inakwenda Afrika {Mdo 8 }. Roho mtakatifu alimtuma mwinjilisti Filipo kwenda
kumhubiri Neno Toashi wa Kushi {Waziri wa fedha wa Ethiopia}. Filipo alimwongoza
towashi huyu kwa Bwana na kisha akambatiza. Inaaminika kwamba toashi huyu alipeleka
Injili Afrika kwa sabau alikuwa ni mkazi wa Bara la Afrika katika nchi ya Ethiopia
J. MTESI WA KANISA ABADILI UPANGA {Mdo 9 }
Sauli wa Tarso ambae ndiye aliekuwa mtesi mkuu wa kanisa kwa kipindi hiki aliokoka
baada ya kukutana na Yesu Kristo alipokuwa safarini kuelekea Dameski kuwakamata na
kuwaua waamini {Mdo 9:20 }. Mara baada ya kuokoka alianza kuihubiri Injili {Kumhubiri
Kristo Yesu}. Paulo aliweka chini upanga wake wa mauaji na kuchukua upanga wa
Neno la mungu ambao hakuuacha mpaka kifo chake.{ 2Tim 4:7}.
Paulo alikwenda katika jangwa la Arabia kwa miaka Mitatu ambapo alipata mafunuo zaidi
toka kwa Mungu. Baada ya hapo alirudi Yerusalemu kuonana na mitume. Baada ya Sauli
kukutana na Ndugu alirudi tena Tarso. Kanisa lilipata raha baada ya kuokoka kwa Sauli wa
Tarso.{Gal 1:16-18, Mdo 9:20-31}.
5. Injili inakwenda kwa watu wa mataifa{Mdo 10 }. Mtume Petro alitumwa kwenda
kumhubiri Kornelio mtu wa Mataifa. Mtume Petro ndiye aliyefungu mlango wa Injili kwa
wayahudi na kwa Watu wa mataifa. Petro alihubiri Injili kwenye nyumba wote waliokuwa
wamekusanyika wakimsikiliza walishukiwa na Roho Mtakatifu na wakaanza kunena kwa
Lugha mpya, kisha Petro akawabatiza. Huu ulikuwa ni mwanzo wa Injili au kanisa
kuwafikia watu wa mataifa.
6. Injili inakwenda Asia Ndogo {Mdo 13} Katika sura hii tunaona wito wa wamishenari
wawili kwenda kuhubiri katika nchi ya kigeni. Wito huu na kutumwa huku kulifanyika
Antiokia mahali ambapo wanafunzi walipewa jina na kuitwa Wakristo kwa mara ya
kwanza {Mdo 11:26}.
Balnaba alikuwa ni mchungaji wakati Paulo alipokuja kutoka Dameski. Wanafunzi wote
walimwogopa Paulo, Balnaba alimpokea na kumtambulisha kwa kanisa {mitume
Yerusalemu} Mdo 9;26-29.
Japokuwa mitume walimtuma Balnaba Antiokia mahali ambapo kanisa lilikuwa na uamsho
mkubwa aliamua kufunga safari kutembea zaidi ya KM 150 kwa meli ili kwenda
kumtafuta Sauli wa Tarso .Alimpata na kisha akamchukua na kuja nae Antiokia bila kujua
kwamba miaka ya mbele sauti ya Bwana ingemwita kupitia njia ya unabii
‘Nitengeeni Balnaba na Sauli kwa kazi niliowaitia.{Mdo 13:1-5 }.
Balnaba na Paulo waliombewa na kanisa na kisha kwenda kwenye umisheni wao kuelekea
Asia ndogo mahali ambapo walianzisha makanisa mengi. Kama inavyoainishwa katika
Matendo ya Mitume 13 na 14. Baadae walirudi Antiokia mahali ambapo palikuwa ni kituo
chao cha umisheni.
8