You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
P.O.BOX 1917 MBEYA TANZANIA
Email: Elamseminary@gmail.com. Tel 0762532121
Kuwaandaa Watendakazi Kwaajili Ya Mavuno Ya Nyakati Za Mwisho
LUKA 10:2
By, Rev.Dr. Erick L, Mponzi (ThD)
Msingi wa Kujenga Watendakazi na Viongozi Watumishi
Wanaojizidisha na wenye Maono ya Kuigusa Dunia Nzima.
©Copyright, ECHASE 20014
MADA YA KWANZA.
UTANGULIZI JUU YA HISTORIA YA KANISA.
A.UTANGULIZI
Somo hili linaanza na kupaa kwa Yesu Mbinguni katika mlima wa mizeituni kama mwaka
wa 30 .AD na linaishia na kurudi kwa Yesu mara ya pili kupitia kwenye mlima wa
mizeituni katika kipindi cha mwisho {ufu 19-16-26, Zek 14:1-9}
Wanahistoria ya kanisa hawakubaliani katika namna ya ugawaji wa vipindi vya historia
ya kanisa .Baadhi hugawa vipindi kulingana na matukio muhimu kuhusu watu Fulani
maarufu, mfano kutawazwa kwa papa wa kwanza mnamo mwaka 590 A.D, au wakati wa
matengenezo ya Martin Luther, alipoandika andiko {Thesis} lake lenye hoja 95 na
kulibandika katika mlango wa kanisa huko Witenberg Ujerumani mwaka 1517 .
Baadhi pia hupenda kugawa vipindi katika historia ya kanisa kulingana na matukio
mbalimbali yaliyoleta athari katika kanisa, mfano kuongoka kwa Kiongozi mkuu wa Dola
ya Rumi Mfalme Kostantino mwaka 313 AD .Au patano la amani la Westphalia mwaka wa
1646.
Pia wataalamu wengine hugawa vipindi vya kanisa kwa kufuata mtindo wa kinabii kwa
kuzingatia orodha ya makanisa saba (7) kama yalivyoainishwa katika kitabu cha Ufunuo
wa Yohana sura ya pili na ya tatu.
Katika somo hili tutagawa vipindi vya historia ya kanisa kwa kufuata mhutasari wa
makanisa saba yanayopatikana katika kitabu cha Ufunuo wa Yohana Sura ya pili na ya tatu
ambapo vipindi mbalimbali vya kanisa vimeorodheshwa kwa njia ya kinabii.
B. DHANA YA HISTORIA.
Historia kama somo inafafanuliwa kwamba ni somo linalohusu matukio mbalimali katika
vipindi mbalimbali vya maendeleo ya mwanadamu.
Baadhi ya wataalamu wanafafanua kwamba historia ni kumbukumbu za shughuli za
binadamu katika vipindi viliyopita mpaka sasa. Kwahiyo historia huhusika na kuainisha
matukio mbalimbali muhimu yaliyotokea katika vipindi mbalimbali katika jamii ya
mwanadamu.
C. MAANA YA HISTORIA YA KANISA
Historia ya Kanisa ni fani inayochunguza historia ya Ukristo na ya miundo yake
mbalimbali tangu Kanisa lilipoanzishwa na Yesu Kristo katika karne ya 1 hadi leo
Ni taaluma inayoelezea vipindi mbalimbali ambavyo kanisa limepitia tangu kuanzishwa
kwake mpaka Yesu kristo atakapokuja kulichukua kwenda mbinguni .
1
D. SABABU ZA KUJIFUNZA HISTORIA YA KANISA
Kuna sababu nyingi ambazo zinatufanya tujifunze historia ya kanisa na kuifanya kuwa
mojawapo ya somo linalotakiwa kufundishwa katika shule za Biblia na vyuo vya thiolojia.
Baadhi ya sababu hizo ni:-
1. Historia ya kanisa inatusaidia kutambua jinsi kanisa lilivyoanza na jinsi
lilivyokabiliana na changamoto mbalimbali.
2. Inatusaidia kujifunza misimamo ya kiimani ya mababa wa kwanza wa kanisa na
kututia moyo sisi kuitetea imani kama wao walivyoitetea.
3. Inatusaidia kujua changamoto mbalimbali kanisa lilizopitia tangu kuanzishwa kwake
mpaka sasa, mfano changamoto ya mateso wakati wa watawala mbalimbali wa Dola
ya Rumi, kama vile kusulubiwa kwa mtume Petro, kukatwa kichwa mtume Paulo,
kuchunwa ngozi na kutumbukizwa kwenye mafuta yanayochemka motoni Mtume
Bathromayo.
4. Inatusaidia kujua jinsi wakristo waliotutangulia walivyoitetea imani kwa kuwa tayari
kufa bila kuisaliti imani mfano John Huss Martini Luther, Porykap, Klement Origen,
Urlich Zwingri. N.k
5. Inatusaidia kujua namna Mungu anavyotimiza Mpango wake wa milele hapa duniani
kupitia kanisa.
D.MAKANISA SABA YA ASIA NDOGO
Mfalme Domitiani alimpeleka mtume Yohana uhamishoni katika kisiwa cha Patmo kwa
sababu ya imani. Akiwa katika kisiwa hiki mtume Yohana alipokea jumbe toka kwa
Bwana Yesu Kristo kwa ajili ya makanisa saba yaliyokuwa katika Asia ndogo. Jumbe hizo
baadae ziliingizwa kwenye orodha ya kanuni ya Maandiko Mtakatifu na sasa ni kitabu
cha Ufunuo wa Yohana. Mtume Yohana alipokea jumbe hizi akiwa na umri wa kama
miaka 90.
Jumbe hizi zilikuwa na matuimizi ya aina nne ambayo ni
1. Zilikuwa ni jumbe maalum kwaaiili ya makanisa katika wakati wa mwandishi.
2. Zilidhihirisha na kufunua hali ya kiroho ya kila kanisa lililoandikiwa jinsi ilivokuwa.
3. Zilikuwa ni jumbe kwa waamini wote wa zama zote za kanisa.
4. Zilikuwa ni muhtasari wa kinabii wa historia ya kanisa.
F. MUHTASARI WA MPANGILIO WA MAKANISA SABA YA ASIA NDOGO.
KANISA KIPINDI MUDA
EFESO KIPINDI CHA MITUME (Kanisa la Mitume)
Tangu kupaa kwa Yesu Kristo Mbinguni mpaka kifo cha
Mtume Yohana.
SMIRNA
KIPINDI CHA MATESO (Kanisa la mateso).
Tangu kuchomwa moto mji wa Rumi mpaka kuongoka kwa
mfalme kostantino.
30 .BK- 100
B.K
64. B.K – 313
B.K
2
PERGAMO
THIATIRA
SARDI
FILADELFIA
LAODEKIA
KIPINDI CHA KIFAHARI (Kanisa la Kifahari)
Tangu kuongoka kwa mfalme Kostantino mpaka kuanguka
kwa dola ya Rumi.
KIPINDI CHA KIPAPA (Kanisa la Kipapa)
Tangu kuanguka kwa dola ya Rumi mpaka kuanguka kwa
Kostantinopali
KIPINDI CHA MATENGENEZO (Kanisa la Matengenezo)
Tangu kuanguka kwa Kostantinopali mpaka patano la
Westphalia
Kipindi cha umisheni au uinjilisti. (KANISA LA
UMISHENARI)
Tangu patano la Westphalia mpaka vita ya kwanza ya Dunia.
KIPINDI CHA UONGO (kanisa la uongo/vuguvugu)
Tangu vita ya kwanza ya dunia mpaka kipindi cha Milenia
mpya.
313 B.K -476.
B.K
476. B.K -
1453 .
1453.- 1648
1648-1914
1914…
3
MADA YA PILI
KIPINDI CHA EFESO.
{Kanisa la Mtume}
A. UTANGULIZI.
Kanisa la Efeso (ufunuo wa Yohana 2:1-7)
MUDA; Tangu kupaa kwa Yesu Kristo kama mwaka 30.AD.Mpaka kifo cha mtume
Yohana kama mwaka wa 100. B.K.
Efeso ulikuwa mji muhimu katika pwani ya Asia ndogo na ulipewa jina la heshima la
Nuru ya Asia. Waefeso waliabudu miungu ya kiasia ambayo ni Artemi, ambae pia aliitwa
Diana. Hekalu la artemi lilihesabiwa kuwa mojawapo ya maajabu ya dunia ya wakati ule.
Mahali pengine walipoabudia paliitwa Augusteum. Mahali hapo walitumia kumwabudu
mfalme . kiwango cha kiburudani za kidunia zilikuwa nyingi na inakadiliwa kuwa ukumbi
wa Efeso ulikuwa na uwezo wa kuchukua watu 25,000.
Kipindi hiki kinaitwa kipindi cha mitume kwa sababu karibia mitume wote12 wa
mwanakondoo {Yesu} waliishi katika kipndi hiki. Kipndi hiki kiliishia na kifo cha Mtume
Yohana ambae alikufa kifo cha kawaida akiwa mzee mwenye umri wa kama miaka 100.
Kuna walimu wa theologia wanaofundisha kwamba mitume na manabii waliishia katika
kipindi hiki. Jambo ambalo si kweli kabisa kwani huduma hizi zimekuwepo katika vipindi
vyote vya kanisa japokuwa katika vipindi fulani zilififia, lakini zimekuwepo katika zama
zote za kanisa.
B.ULIMWENGU WA WAKATI WA MITUME
Kanisa lilikutana na upinzani mara tu lilipoanza.Upinzani huo ulitokana na makundi
mbalimbali
1. Dini ya kiyahudi. Wayahudi walikuwa ni adui namba moja wa kanisa .walilivamia
kanisa wakati lingali changa kwa kushirikiana na mfalme wa kirumi walimsulibisha Yesu
Kristo. Ndani y dini ya kiyahudi kulikuwa na makundi/madhehebu mbalimbali ambayo
yalishiriki katika kulitesa kanisa. Baadhi ya makundi hayo ni:-
a).Mafarisayo. Hawa walianza katika kipindi cha Ezra na Nehemia waliporudi toka
uhamishoni Babeli wakati ukuhani mpya ulipoanzishwa. Mafarisayo Waliamini juu ya
‣ Ufufuo wa wafu
‣ adhabu kwa wenye dhambi
‣ Kutokufa kwa nafsi
‣ Uwepo wa malaika na huduma zao
‣ Kila kitu kinamtegemea Mungu.
‣ Mtazamo wao wa kisiasa ulikuwa ni wa kiyahudi na waliogopa kushirikiana na watu
wasiokuwa mafarisayo. Mfano Wasamaria, na Wamataifa na kwa namna zote
walizishika sheria za Musa na walifanya tohara.
4
b.Masadukayo, Hawa jina lao lilitoka kwa Sadoki kuhani mkuu wa wakati wa Daudi toka
uzao wa Haruni Kuhani Mkuu. Hivyo walikuwa ni uzao wa kikuhani.Wao hawakuamini
ufufuo wa wafu wala uwepo wa malaika.
2. Dola ya Kirumi,. Mwaka 63KK. mfalme wa Rumi Julius Kaizari aliivamia na
kuishinda Palestina na akaanzisha utawala wa kirumi katika nchi ya palestina . Huu
ulikuwa ni ufalme wanne uliokuwa umeishinda na kuitawala Israeli kulingana na unabii wa
Danieli . Israeli ilikuwa chini ya utawala wa dola ya Rumi Yesu Kristo alipozaliwa na
katika kipindi cha maisha yake hapa duniani.
a. Dini ya kipagani(Heathenism), hii ilikuwa ni dini ambayo mianzo yake ni mtawala
Nimrodi katika mnara wa Babeli na dini hii baadae ilisambaa katika maeneo mbalimbali
yaliyoizunguka Babeli mpaka Misri, Ugiriki na Rumi.Waliabudu miungu ya kigeni {Yer
2:25}. Ilikuwa ni miungu ya zamani sana ya Kibabeli, ilikuwa na majina mbalimbali katika
nchi mbalimbali, mfano A=`570rtemi, Diana, Osiris, Jupita Appolo Zeus. N.K
b. Ibada ya mfalme. Hii ilikuwani mojawapo ya tamaduni ya dola ya Rumi. Baadhi ya
wafalme wakirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai kwamba wananchi
wao wanatakiwa kuwaabudu.hivyo Ibada ya kuwaadudu wafalme {makaisari} ilianzishwa.
Kukataa kumwabudu Kaisari kungepelekea mtu kuhukumiwa adhabu ya kifo. Ibada
ya kumwabudi mfalme ilikuwa imerithiwa toka kipindi cha babeli. Kaisari Domitiani ni
mojawapo wa Makaisari waliosimamisha sanamu zao na kudai ibada zifanywe juu yao.
c. Wanafasalsafa wa Kigiriki. Kulizuka falsafa za kigiriki ambazo zilikuwa zinasisitiza
kwamba lengo la maisha ni furaha na anasa. Walisisitiza kwamba maarifa yanaweza
kupatikana kwa njia ya kufikiri {Logic}.Waliegemea katika vitu vinavyooneka tu
(materialism). Falsafa hizi ndizo ambazo zilikuwa zimeshikiliwa na watu mbalimbali
katika kipindi hiki.
Falsafa hizi zilisisitiza kwamba maisha ni kula na kunywa kwa sababu baada ya kufa
mwanadamu alikuwa anaoza na kwamba hakukuwa na maisha baada ya kufa.
C. KUANZA KWA KANISA.
Kanisa lilianza Yerusalemu siku aliposhuka Roho mtakatifu katika chumba cha juu katika
hekalu la Yerusalem. Baada ya Yesu Kristo kupaa Mbinguni wanafunzi walirudi toka
mlima wa Mizeituni mpaka hekaluni na kukaa katika chumba cha juu. Waliomba na
kusubiri kuvikwa nguvu. Baada ya siku kumi Roho Mtakatifu alishuka na wote
waliokuwemo kwenye chumba cha juu walijazwa Roho Mtakatifu na kuanza
kumwazimisha Mungu kwa Lugha zingine. Kazi ya uinjilisti ilianza papo hapo, mtume
Petro alihubiri na watu 3000 wakaokolewa na kubatizwa. Hii inahesabiwa kwamba ndio
mwanzo wa kanisa la agano jipya.
Matokeo ya kujazwa Roho Mtakaifu
5
1. Kutiwa nuru. Waamini walitiwa nuru katika akili na fahamu zao na wakapata
kuyaelewa maandiko matakatifu.
2. Kutiwa nguvu na ujasiri, wamini hawa walitiwa nguvu na ujasiri na kuwezeshwa
Kulihubiri Neno la Mungu kwa ujasiri.
3. Kutenda ishara na maajabu. Mitume waliwezeshwa kutenda miujiza sawasawa na
ahadi ya Yesu Kristo Mk 16:15-20.
D. WANACHAMA KTIK A KANISA.
Wanachama katika kanisa la mwanzo walikuwa ni wayahudi {proselytes} ambao twaweza
kuwagawanya katika makundi manne. ambayo ni ;
1. Waebrania . hawa walikuwa ni wayahudi ambao baba zao walikaa Palestina na
walikuwa ni uzao wa Kiebrania.
2. Hellenists, (Grecian Jews",) walikuwa ni wayahudi waliokuwa wanakaa katika nchi
zingine wengi wao walikaa Uyunani. Mdo 6:1
3. Proseliti (Proselytes).Walikuwa ni watu wamataifa waliokuwa wamefanyika kuwa raia
wa kiyahudi, walifuata sheria za kiyahudi na walijiunga na dini ya Kiyahudi. Pia
walitahiriwa kama wayahudi. Mfano Nikolasi {Mdo 6:5}
E. UONGOZI NA UTAWALA WA KANISA.
Kanisa la kwanza halikuwa na Mfumo wa uongozi wa kiutawala kama ilivyo sasa. Kila
kanisa la mahali pamoja lilikuwa na uongozi wake uliojitegemea. Hakukuwa uongozi
uliokuwa unasimamia makanisa yote. Mitume walikuwa ni waangalizi wa kanisa na
hawakujiweka kuwa watawala wa kanisa bali watumishi wa kanisa.
F. MAFUNDISHO YA KANISA LA KWANZA. Mafundisho ya kanisa la kwanza
yalikuwa rahisi, Agano jipya lilikua bado halijaandikwa. Ujumbe wao ulikuwa na maeneo
machache ambayo ni ;
i. Uungu wa Yesu Kristo. Yesu kristo wa nazareti ni mwana wa Mungu na ni nafsi
hai. Maelezo haya yalisababisha mateso katika kanisa .
ii. Ufufuo wa Yesu Kristo. Ufufuo wa Yesu kristo ulikuwa ni kiini cha mahubiri au
ujumbe wa kanisa la kwanza.
iii. Toba, Ubatizo wa maji na ubatizo wa Roho Mtakatifu. Waliweka mkazo juu ya
toba inayoleta ondoleo la dhambi na ubatizo wa maji na ujazo wa Roho mtakatifu .
iv. Kurudi kwa Yesu Kristo mara ya pili. Walihubiri kwamba Yesu Kristo atarudi
tena {Mdo 3:20-21, 1The 4;15-17}Hili lilikuwa ni tumaini la Baraka kwa waamini
wote.
G. KUSHINDWA KWA KANISA LA KWANZA.
Kanisa la kwanza lilishindwa kufikia kusudi kwa sababu zifuatazo.
Kukosa maono ya umisheni . Mungu aliliagiza kanisa kwenda kuhubiri Injili
ulimwenguni kote MT20:28, Mk 16:16} lakini kanisa la kwanza hawakufanya hivyo bali
walijihusisha na umisheni katika Yerusalemu.
6
Kujihusisha na shughuli za kijamii, Mitume walianza kujihusisha na mambo ya kijamii
{kiutawala} kwani shughuli zote za kanisa za kila siku zilifanywa na wao.Tunaona Petro
aliyekuwa mhubiri anaanza kujihusiha na mambo ya kiutwala.
Mitume walifika mahali wakagundua tatizo hilo na wakachagua wahudumu saba
waliotakiwa kushughulikia mambo ya kiutawala ili wao wadumu katika kulihubiri Neno
na Kuomba.
Bwana alilionya kanisa lake “Tubu na ukafanye mambo ya kwanza la sivyo nitakiondoa
kinara chako mahli pake. Mungu alitimiza Neno lake kama Tutakavyo ona hapo baadae.
H. KUENEA KWA KANISA LA KWANZA. Kupanuka kwa kanisa tangu mahubiri ya
Stefano {mwaka 35. AD} hadi mkutano wa Yerusalemu {mwka 48. AD}.Mambo ya
msingi katika kipindi hiki yalikuwa ni upandaji wa makanisa. Kipindi hiki kifupi kilikuwa
na umuhimu mkubwa kwa kanisa. Japokuwa kanisa mwanzo lilikuwa Yerusalemu tu sasa
lilipandwa katika maeneo mengine kama vile Siria na Asia ndogo na kuelekea Ulaya.
Waamini wa kwanza walikuwa ni Wayahudi lakini baada ya kipindi hiki kifupi waamini
wengi walikuwa ni wamataifa .
Mwanzoni Injili ilihubiriwa kwa kiebrani na kwa kiaramu lakini baadae iligundulika
kwamba ulimwengu mzima ungefikiwa na Injili kupitia lugha ya Kigiriki kwa sababu
kigiriki wakati huo kilikuwa ni lugha ya mawasiliano ya kimataifa kama ilivyo
kiingereza kwa dunia ya sasa.
I KUTESWA KWA KANISA NA VIONGOZI WA KIYAHUDI.
Yesu aliwaagiza mitume kwenda kuhubiri Injili duniani kote lakini wao walipenda kukaa
Yerusalemu .Mungu alikasirika na akaamua kuruhusu mateso katika kanisa .{Mdo 9}
1. Mahubiri ya Stefano {.Mdo 6:1-4, 7} Kwa sababu ya imani yake kwa Mungu Stefano
alihukumiwa kuuawa na kuwa mfia dini wa kwanza katika imani ya kikristo. Kijana
mmoja mfarisayo wa Tarso Sauli alishuhudia mauaji ya Stefano na Baadae kijana huyo
akawa kiongozi mkuu wa mauaji ya wakristo katika taifa la wayahudi.
Kutokana na tukio hili waamini wote walikimbia Yerusaelimu isipokuwa mitume {Mdo
8:1-4}.Waamini hao walisambaa maeneo mbalimbali na kila mahali walipokwenda
walilihubiri Neno . Kwa njia hii kwa muda mfupi Injili ilipata kuenea kwa haraka katika
maeneo yote yaliyoizunguka Yerusalemu.
2. Kanisa Linakwenda Samaria,{ Mdo 8}.Wasamaria walikuwa ni chotara ambao asili
yao ilikuwa ni Ashuru ambpo walihamishiwa katika eneo la Kaskazini mwa Israeli. Pale
waisraeli walipochukuliwa kwenda utumwani Ashuru {Irani}. Mchanganyiko wa wageni
hao na mabaki ya waisraeli ambao hawakwenda utumwani Ashuru yaliunda jamii ya
Wasamaria kwa njia ya kuzaliana, kutokana na kuoana kati ya wageni na mabaki ya
waisraeli. Watoto waliozaliwa walikuwa chotara na ndio kizazi cha Wasamaria .
Wasamaria Walikuwa na hekalu lao katika mlima Gelzimu na walivitumia vitabu vitano
vya Musa pekee kama Biblia yao. Kwahiyo Wayahudi hawakuchangamana nao.
Roho Mtakatifu alimwambia Shemasi Filipo kwenda kuhubiri Neno Samaria. Mungu
alimtumia kufanya ishara na maajabu kwa jina la Yesu huko Samaria. Uamsho mkuu
7
ulitokea huka Samaria. Watu wa huko Samaria waliokoka na kubatizwa. Mitume
walipopata habari hii walikuja kuwaombea ujazo wa Roho Mtakatifu. Baada ya maombi
hayo Wasamaria walijazwa Roho Mtakatifu.
3. Injili inakwenda Afrika {Mdo 8 }. Roho mtakatifu alimtuma mwinjilisti Filipo kwenda
kumhubiri Neno Toashi wa Kushi {Waziri wa fedha wa Ethiopia}. Filipo alimwongoza
towashi huyu kwa Bwana na kisha akambatiza. Inaaminika kwamba toashi huyu alipeleka
Injili Afrika kwa sabau alikuwa ni mkazi wa Bara la Afrika katika nchi ya Ethiopia
J. MTESI WA KANISA ABADILI UPANGA {Mdo 9 }
Sauli wa Tarso ambae ndiye aliekuwa mtesi mkuu wa kanisa kwa kipindi hiki aliokoka
baada ya kukutana na Yesu Kristo alipokuwa safarini kuelekea Dameski kuwakamata na
kuwaua waamini {Mdo 9:20 }. Mara baada ya kuokoka alianza kuihubiri Injili {Kumhubiri
Kristo Yesu}. Paulo aliweka chini upanga wake wa mauaji na kuchukua upanga wa
Neno la mungu ambao hakuuacha mpaka kifo chake.{ 2Tim 4:7}.
Paulo alikwenda katika jangwa la Arabia kwa miaka Mitatu ambapo alipata mafunuo zaidi
toka kwa Mungu. Baada ya hapo alirudi Yerusalemu kuonana na mitume. Baada ya Sauli
kukutana na Ndugu alirudi tena Tarso. Kanisa lilipata raha baada ya kuokoka kwa Sauli wa
Tarso.{Gal 1:16-18, Mdo 9:20-31}.
5. Injili inakwenda kwa watu wa mataifa{Mdo 10 }. Mtume Petro alitumwa kwenda
kumhubiri Kornelio mtu wa Mataifa. Mtume Petro ndiye aliyefungu mlango wa Injili kwa
wayahudi na kwa Watu wa mataifa. Petro alihubiri Injili kwenye nyumba wote waliokuwa
wamekusanyika wakimsikiliza walishukiwa na Roho Mtakatifu na wakaanza kunena kwa
Lugha mpya, kisha Petro akawabatiza. Huu ulikuwa ni mwanzo wa Injili au kanisa
kuwafikia watu wa mataifa.
6. Injili inakwenda Asia Ndogo {Mdo 13} Katika sura hii tunaona wito wa wamishenari
wawili kwenda kuhubiri katika nchi ya kigeni. Wito huu na kutumwa huku kulifanyika
Antiokia mahali ambapo wanafunzi walipewa jina na kuitwa Wakristo kwa mara ya
kwanza {Mdo 11:26}.
Balnaba alikuwa ni mchungaji wakati Paulo alipokuja kutoka Dameski. Wanafunzi wote
walimwogopa Paulo, Balnaba alimpokea na kumtambulisha kwa kanisa {mitume
Yerusalemu} Mdo 9;26-29.
Japokuwa mitume walimtuma Balnaba Antiokia mahali ambapo kanisa lilikuwa na uamsho
mkubwa aliamua kufunga safari kutembea zaidi ya KM 150 kwa meli ili kwenda
kumtafuta Sauli wa Tarso .Alimpata na kisha akamchukua na kuja nae Antiokia bila kujua
kwamba miaka ya mbele sauti ya Bwana ingemwita kupitia njia ya unabii
‘Nitengeeni Balnaba na Sauli kwa kazi niliowaitia.{Mdo 13:1-5 }.
Balnaba na Paulo waliombewa na kanisa na kisha kwenda kwenye umisheni wao kuelekea
Asia ndogo mahali ambapo walianzisha makanisa mengi. Kama inavyoainishwa katika
Matendo ya Mitume 13 na 14. Baadae walirudi Antiokia mahali ambapo palikuwa ni kituo
chao cha umisheni.
8
K. KUTENGANA KWA WAMISHENARI . Wakati mitume hao {Paulo na Balnaba}
walipokuwa wanajiandaa kwaajili ya safari yao ya pili ya umisheni walipishana. Kulitokea
kutokuelewana katika jambo moja. Balnaba alitaka kumchukua Marko{ ambae aliwaacha
katika safari ya kwanza ya umishenari na kurudi Yerusalemu} ili waende nae katika safari
ya pili ya umisheni, lakini Paulo alikataa kuambatana nae, hivyo kukatokea mgongano kati
yao na kisha wakaamua kutengana.
Hapa tunaona moyo wa kichungaji wa Balnaba, japokuwa Marko alishindwa katika
safari ya kwanza ya umishenari aliamua kumpa nafasi nyingine. tuna mwona Paulo
akiwa mtu wa kushikilia kanuni kuliko kumpendeza mtu yeyote. Mtu ambae yuko tayari
kuvunja mahusiano na Balnaba kuliko kukubaliana nae. Miaka ilipita na Mtume Paulo
akakomaa kiimani. Mtume Paulo ambae alisema katika uchanga wake : mimi si duni
kuliko hao mitume wakubwa {2Kor 11:5}. Baadae alisema ‘Mimi ni wa kwanza kwa
wenye dhambi {1Tim 1:16}. Paulo alifika mahali pakujitambua, kujisifu kulibadilishwa na
kujishusha na upendo ulichukua nafasi mahali pa chuki na kanuni.
Katika waraka wake wa pili kwa Wakorintho alisisitiza sana upendo na msamaha. Baadae
tunamwona Mtume Paulo akiwa katika upweke gerezani akisubiri kunyongwa.
Alimwagiza Timotheo kumleta Marko. Marko huyu huyu ndiye aliyemkataa wakati
wanafanya huduma na Balnaba.
Kutokana na hili tunajifunza ya kwamba tusimkatae mtu kutokana na makosa aliyoyafanya
kwa sababu twaweza kumhitaji tena baadae. Tuwasaidie wakosaji kwa upendo bila
kuwahukumu.
7. Mkutano wa Yerusalemu. {48.B.K}. Tatizo lilitokana na kuokoka kwa watu wa
wamataifa na kujiunga na kanisa. Wakristo wakiyahudi walikuwa na mitazamo tofauti
tofauti juu ya hili .Walikuwa na mitazamo ifuatayo:
1. Kundi lenye msimamo mkali. Kundi hili liliamini ya kwamba hakuna wokovu nje ya
Israeli . Kwa hiyo ingawa wamataifa wamempokea Yesu Kristo kama Masihi wao kwahiyo
walipaswa kutahiriwa na kushika Torati ya Musa {Sheria za Kiyahudi} Ili waweze
kuokolewa Bila kufanya hivyo wokovu wao ungekuwa ni batili.
Kundi la wenye mabadiliko.Hawa waliamini kwamba wokovu ni kwa njia ya imani katika
Yesu Kristo. Bila ya kushika sheria za kiyahudi. Wao waliamini kwamba sheria za
kiyahudi haziwahusu watu wa mataifa. Paulo na Balnaba walikuwa mojawapo wa watu
wenye mtazamo huu. Mkutano uliitishwa Yerusalemu ili kushughulikia jambo hili muhimu
la mafundisho kutokana na watu wa mataifa kumpokea Yesu Kristo kama Bwana na
Mwokozi wao. Baada ya majadiliano marefu Mitume na Wazee walifikia hitimisho ambalo
lilithibitishwa na Roho mtakatifu kwamba Wamataifa hawakuwa chini ya Sheria za
kiyahudi na kwamba walichotakiwa kufanya ni kujiepusha na Ibada ya sanamu, kula
nyama iliyosongolewa na damu, kujiepusha na uasherati na uzinzi.
Mitume waliandika barua na ikapelekwa kwa kanisa la mataifa kwa mikono ya Paulo,
Balnaba, Yuda na Sila. Walipofika Antikoa walilikusanya kanisa na kuwapa ujumbe wa
kikao cha mitume na wazee kilichofanyika Yerusalemu kuhusu tatizo lao. Waamini hawa
walifurahi sana kupata ujumbe wenye kuwatia moyo {Mdo 15:30-31}
9
L. KANISA MIONGONI MWA MATAIFA.
Tangu mauaji ya Stefano (48 B.K) mpaka mauaji ya Paulo mtume mwaka 68 B.K
Katika kipindi hiki chote tunategemea kitabu cha Matendo ya Mitume, nyaraka za Paulo na
waraka wa kwanza wa Petro. Umisheni wa mtume Paulo na Watendakazi wenzake
ulifanyika katika dola yote ya Rumi. Wakati mitume wengine walikwenda nchi za
mbali zaidi. (hii ni kulingana na mapokeo).
Idadi ya waamini wa kimataifa ilikua kwa kasi sana wakati idadi ya waamini wa kiyahudi
iliendelea kushuka.Wayahudi walianza kukasirika na kufanya fitina dhidi ya kanisa na
walikuwa tayari kuanzisha mateso dhidi ya wakristo.
Safari Ya Pili Ya Mtume Paulo
Kwa sababu ya kupishana kwa Balnaba na Paulo, Balnaba alimchukua mpwa wake
Yohana (Marko) na kwenda katika nchi ya kwao Kipro, Paulo alimchukua nabii Sila katika
safari yake ya pili ya umisheni na kwenda kuyatembelea makanisa waliyokuwa
wameyafungua katika safari ya kwanza walipokuwa na Balnaba. Paulo alikusudia kwenda
Bithinia lakini Roho Mtakatifu akamkataza. Kisha walielekea Troa mji wa Kaskazini
Magharibi ya Asia ndogo.
Injili inakwenda Ulaya. (Wito wa Makedonia)
Usiku mmoja wakati Paulo na Sila wakiwa Troa mtu wa Makedonia alimtokea kwenye
maono akisema “Vuka uje Makedonia utusaidie” Mara Paulo na Sila walikwenda
Makedonia katika bara la Ulaya na wakaanzisha kanisa katika mji wa Filipi, Thesolanike,
Beroya, Athene na Korintho.
Tunakumbuka kwamba mwanzoni kila mahali Paulo alipokwenda , aliwaendea Wayahudi
kwanza. Wayahudi toka sehemu mbalimbali za dunia ya wakati ule walikuwepo katika
siku ya Pentekoste na walishuhudia kumiminwa kwa Roho Mtakatifu na ubatizo wa
waamini wapya 3,000. Wengi wao walitoka nchi za mbali kuja kusherehekea sikukuu ya
Pasaka katika mji wa Yesulasalemu na kurudi nchini kwao. Inawezekana baadhi yao
mtume Paulo alikutana nao, kwasababu baadhi yao walionekana kuwa na urafiki zaidi na
Paulo.
Wakati wayahudi wengi walipoikataa Injili ya Kristo kama mfufuka mwana wa Mungu,
Paulo aliwageukia watu wa mataifa.
Kanisa katika Filipi, Mwamini wa kwanza katika Ulaya alikuwa ni mwanamke aliyeitwa
Lidia muuzaji wa rangi za zambarau na mwenyeji wa Tiathira. Yeye na nyumba yake
walibatizwa na alifungua mlango wa nyumba yake kwaajili ya watumishi wa Mungu.
Kanisa katika Thesalonike. Pia katika mji huu mtume Paulo alikwenda kwa Wayahudi
kwanza kama ilvyokuwa desturi yake. Baadhi ya Wayahudi na Wayunani waliamini.
Wayahudi wasioamini walianzisha ghasia dhidi ya watumishi wa Mungu, yaani Paulo na
watendakazi wenzake. Kwa hakika washitaki hawa walijua nini cha kusema. Kama
mitume wangekamatwa kwa kuanzisha dini nyingine hakuna tatizo ambalo lingetokea kwa
watesi kwa sababu Ugiriki ilikuwa ina dini nyingi na walizikubali karibu zote.
Wao walikuja na uvumi mwingine kabisa kwa kusema kwamba
“Watu hawa wanadai kwamba kuna mfalme mwingine”.
10
Inaonekena Wayahudi hao Walianzisha uvumi huo ili serikali iweze kushiriki katika zoezi
la kuwadhibiti mitume.
Kanisa katika Beroya. Injili ilikubaliwa kwa watu wote Wamataifa na Wayahudi. Wakati
Wayahudi wa Thesalonike waliposikia walikuja tena kufanya ghasia dhidi ya mitume
hivyo iliwalazimu Paulo na Sila kuondoka mjini hapo, lakini Neno la Mungu lilikuwa
tayari limehubiriwa.
Hakika mitume hawa waliishi sawasawa na Neno la Kristo “Watakapowafukuza katika mji
mmoja kimbilieni katika mji mwingine. (Mt 10:23)
Kanisa katika Athene. Hapa pia mitume hawa waliwaendea Wayahudi , lakini wayahudi
hao hawakulipokea Neno. Baadae mtume Paulo aligundua ya kwamba Mungu
aliwapofusha macho Waisraeli kwa muda kwa sababu walimsulubisa Kristo Yesu.
Wanafalsafa wa Kigiriki walimpa mtume paaulo changamoto japo kuwa si sana kwa
sababu walitaka kulisikia Neno, hawakutubu bali walivutiwa tu na mdahalo. Walipokuwa
hawajui chakujibu walidhihaki.
Kanisa katika Korintho. Pia mahali hapa kama ilivyokuwa kawaida yake mtume Paulo
alikwenda kwa Wayahudi kwanza. Alikaa na Wayahudi watengeneza mahema (Akila na
Prisila). Inadhaniwa kuwa alitengeneza nao mahema ili kujipatia pesa kwaajili ya kujikimu
ili aweze kuhubiri Injili pasipo kumlemea mtu yeyote.(Mdo 20:34). Japokuwa Paulo
alikuwa ni Rabi aliyeelimika na Mtume hakudharau kazi ndondogo kwaajili ya kueneza
Injili.
Maamuzi Thabiti. Wayahudi waliipinga Injili tena na hii ilileta mtazamo mpya kwa
huduma ya Injili ya Paulo. Mtume Paulo alisema
Damu yenu na iwe juu ya vichwa vyenu mimi ni safi tangu sasa nitakwenda kwa watu wa
mataifa. (Mdo 18:6)
Paulo na Sila walikaa Korintho kwa muda wa miezi kumi na nane (18) wakiwafundisha
waamini. Kutoka Korintho mtume Paulo aliandika nyaraka mbili kwa Wathesalonike
Baada ya shambulio lingine lililofanywa na Wayahudi dhidi yake (Paulo) aliamua
kuondoka Korintho na kurejea Antiokia kwa kupitia Efeso na Kaisaria.
Safari ya tatu ya umisheni ya mtume Paulo (Mdo 18:23-22:17)
Katika awamu hii mtu aliyeambatana na mtume Paulo ni Timotheo aliyejiunga katika timu
yake katika safari ya pili ya umisheni huko Listra. (Mdo 1-3) na kwa muda mfupi idadi
kubwa ya wanatimu walikuwa pamojanae kabla hajamaliza safari hii. Mmojawapo wa
watu hao muhimu alikwa ni Dkt. Luka.
M. PAULO MTUME KATIKA MINYORORO (Mdo 22:23-28: 31)
Paulo alitumia miaka kadhaa akiwa gerezani lakini kamwe hakuacha kufanya kazi ya
umisheni. Mazingira hayakubadili kusudi lake. Baada ya safari ndefu Paulo alifika Rumi
jiji ambalo alitamini sana kuliona. Alikuwa na uhuru wa kuishi katika nyumba aliyokuwa
ameipanga mwenyewe huku akiwa chini ya uangalizi wa askari magereza, japokuwa
11
alikuwa mfungwa bado alileta athari kubwa katika kanisa huko Rumi. Moja ya mambo
makuu aliyofanya ni kuandika nyaraka kwa Waefeso, Wafilipi, Wakolosai na
Filemoni.
Inaaminika kwamba baada ya miaka miwili ya kukaa kifungoni mtume Paulo aliachiwa
huru (Mdo 28:30-31) lakini hakuna kumbukumbu kamili katika kipindi hiki isipokuwa
taarifa chache tu.
Mapokeo yanasema kwamba mtume Paulo alikamatwa Nikroporisi Kaskazini mwa
Ugiriki chini ya mtawala wa Rumi aliyeitwa Nero na akarudishwa Rumi katika kifungo
hiki cha pili aliandika nyaraka zifuatazo:- 1&2Timotheo, na Tito. Barua hizi zilikuwa ni
barua zake za mwisho mnamo mwaka 68. B.K. Mtume Paulo aliuawa kwa amri ya mfalme
Nero. Mtume huyu aliuawa kwa kukatwa kichwa.
N. UANDISHI WA MAANDIKO MATAKATIFU.
Inadhaniwa kwamba mpaka kipindi cha Mkutano Yerusalemu mnamo mwaka 48. B.K
hakuna hata kitabu kimoja cha Agano jipya kilichokuwa kimeandikwa, lakini karibu ya
mwaka 68.B.K idadi kubwa ya Maandiko ya Agano Jipya yalikuwa tayari yameandikwa,
hii ikijumlisha Injili ya Mathayo, marko, Luka, nyaraka za Paulo, Yakobo na 1Petro.
Katika kipindi cha miaka ya 68- 100.B.K vitabu vingine viliandikwa.Waraka kwa
Waebrania, 2Petro, Injili ya Yohana na nyaraka tatu za Yohana, yuda na Ufunuo wa
Yohana.
O. KIPINDI CHA UVULI
Tangu kukatwa kichwa mtume Paulo mwaka 68AD hadi kifo cha mtume Yohana 100 AD.
Kipindi hiki Kinaitwa kipindi cha uvuli kwa sababu wimbi la mateso lilikuwa limetanda
juu ya kanisa na kwamba ni mambo machache tu yanayofahamika kuhusu kipindi hiki.
Kipindi cha miaka 50 cha ukimya kinaelea juu ya kanisa baada ya kuuawa kwa mtume
Paulo. Kutoka mwaka 120AD tunapata maandiko ya mababa wa kwanza wa kanisa, lakini
pia tunakuta kanisa linatofautiana kwa namna nyingi na kanisa la siku za Petro na Paulo.
P. KUANGUKA KWA YERUSALEM
Mnamo mwaka 70AD kulitokea badiliko kubwa la kimahusiano kati ya Wakristo
Wayahudi. Mpaka kufikia kipindi hiki ni Wayahudi pekee waliokuwa wakiishi Israeli ndio
waliokuwa wakimpinga Kaisari. Wayahudi wa sehemu nyingine yote ya dola ya Rumi
walikuwa watii kwa Kaisari na hivyo waliishi kwa amani.
Wayahudi walitafsiri unabii katika Maandiko Matakatifu na kuamini kwamba walitakiwa
kuutawala ulimwengu wote kama ambavyo watafanya katika kipindi cha Milenia.
Mnamo mwaka 66AD wayahudi waliuasi utawala wa Rumi na mnamo mwaka 70AD
mfalme Vespasiani aliamua kuleta maangamizi juu ya taifa la Wayahudi.Alimtuma kijana
wake Tito na jeshi kubwa na imara kwenda kuishambulia Yerusalemu.
12
Kwa msaada wa Josephus (mwanahistoria) Tito ambaye hakutaka kuliangamiza taifa la
Wayahudi aliwasihi wayahudi kujisalimisha na kuweka silaha zao chini. Wayahudi
hawakuwa tayari.Hivyo basi hekalu lilichomwa moto na kubomolewa likiwa na watu
ndani ambao walikuwa wamekimbilia ndani ya hekalu ili kujinusuru na vita hiyo.
Liliongozwa na Tito lilifanikiwa kuiangusha Yerusalemu na kuchukua vitu vyote vya
thamani. Mambo yote yalitimia sawasawa na ilivyotabiliwa na Bwana wetu Yesu Kristo
katika Mathayo 24:1-2
1. Yes akaenda zake, akatoka hekaluni; wanafunzi wake wakamwendea ili
kumwonyesha majengo ya hekalu. 2 Naye akajibu akawaambia, Hamyaoni haya
yote ? Amin, nawaambieni, halitasalia hapa jiwe juu ya jiwe ambalo
halitabomoshwa.
Ingawa wayahudi zaidi ya milioni waliuawa katika vita hiyo lakini ni wakristo
wachache tu waliopoteza maisha yao. Hii ni kwa sababu Bwana Yesu alikuwa amekwisha
kuwaonya tayari kabla ya maangamizi hayo kutokea. Tunajifunza kuwa ni muhimu sana
kufuata maelekezo ya Kimungu ili kuwa salama katika maisha na huduma kwa ujumla.
LUKA 21:20-24
20 Lakini, hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na mejeshi, ndipo jueni ya
kwamba uharibifu wake umekaribia.
21 Ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani, na walio katikati yake wakimbilie
nje, na walio katika mashamba wasiuingie.
22 Kwa kuwa siku hizo ndizo za mapatilizo, ili yatimizwe yote yaliyoandikwa.
Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida
nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili. 24Wataanguka kwa ukali wa upanga, nao
watatekwa nyara na kuchukuliwa katika mataifa yote; na Yerusalemu utakanyagwa na
mataifa, hata majira ya mataifa yatakapotimia.
Mahali lilipokuwepo hekalu umejengwa msikiti mkubwa sana na Wapalestina ambao ndio
mojawapo ya sababu za kutoisha kwa mgogoro wa mashariki ya kati. Israeli walianza
kurudi nchini kwao taratibu na hatimae taifa la Israeli liliundwa kwa upya mnamo mwaka
1948 chini ya Umoja wa mataifa. Umoja wa mataifa ulitangaza kuitambua Israeli kama
jamhuri yenye mamlaka kamili.
Mungu alilionya kanisa Ufunuo wa Yohana 2:4-5
4. Lakini nina neon juu yako, ya kwamba umeuacha upendo wako wa kwanza.
5. Basi, kumbuka ni wapi ulipoanguka; ukatubu, ukayafanye matendo ya kwanza. Lakini
usipofanya hivyo, naja kwako name nitakiondoa kinara chako katika mahali
pake,usipotubu.
Q. VIFO VYA MITUME WA BWANA WETU YESU KRISTO NA MAENEO YAO YA HUDUMA
1. Petro- alikuwa mvuvi wa Samaki kabla ya kuitwa na Yesu na ndiye kiongozi wa
kwanza wa Kanisa. Petro alifanya huduma katika maeneo yafuatayo, Yerusalemu,
13
Yudea, Siria, Rumi na Asia ndogo. Mtume Petro aliuawa kwa kusulubiwa kichwa
chini miguu juu kwa ridhaa yake mwenyewe chini ya utawala wa Klaudi Nero.
2. Yakobo mwana wa Zebedayo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Bwana Yesu.
Baada ya kuitwa na Bwana Yesu aliacha kila kitu na kumfuata Yesu na alikuwa
mmojawapo wa wanafunzi watatu waliokuwa karibu sana na Yesu. Yakobo
alifanya huduma Yudea. Yakabo aliuawa kwa upanga kwa amri ya Herode
Antipa. Yakobo ni mtume pekee kati ya wale mitume waliouawa ambae kifo
chake kimeandikwa katika Biblia.
3. Yohana- alikuwa mvuvi wa samaki kabla ya kuitwa na Yesu. Baada ya kuitwa na
Yesu alikuwa mojawapo ya nguzo katika kanisa la Yerusalemu. Yohana
alifanya huduma Efeso, Patmo na Yudea. Yohana ni mtume pekee aliyekufa kifo
cha kawaida katika uzee mwema akiwa ameshiba siku. Inazaniwa kuwa yohana
alikufa kule efeso mnamo mwaka 100AD.
4. Andrea- Alikuwa mvuvi, alikuwa mwanafunzi wa Yohana mbatizaji na ni mtu wa
kwanza kumfuata Yesu na mwinjilisti wa kwanza. Aliitwa na Yesu kuwa mvuvi
wa watu. Inadhaniwa kwamba Andrea alifanya huduma katika maeneo ya
Ugiriki, Asia ndogo na Urusi. Mtume Andrea aliuawa kwa kusulubiwa katika
msalaba wenye umbo la X huko Ugiriki.
5. Filipo- alikuwa mvuvi kabla ya kuitwa na Yesu. Mtume huyu alifanya huduma
katika maeneo ya alifanya huduma Frigia, Ukraine, Afrika Kaskazini, aliuawa
kwa kusulubiwa huko Hierapolis Uturuki
6. Batholomayo- ambaye anaitwa Nathanaeli, alikuwa mmisionari huko Asia.
Alimshuhudia Kristo katika maeneo ya Uturuki na akauwawa kwa sababu ya
kuhubiri injili huko Armenia, kw alichunwa ngozi akiwa hai mpaka akafa.
7. Thomaso. Mtume huyu kabla ya kuitwa na Yesu alikuwa ni fundi seremala na
fundi uashi. Mapokeo yanatuambia kuwa Thomaso alifanya huduma ya
umishenari katika nchi ya India. Mtume huyu aliuawa kwa kuchomwa
mkuki huko India.
8. Mathayo. Alikuwa ni afisa mapato (mtoza ushuru) katika Serikali ya Rumi katika
mji wa Kapernaum kabla ya kuitwa na Bwana Yesu. Mathayo alifanya huduma
katika nchi za Uajemi na Ethiopia. Mathayo aliuawa kwa kukatwa kichwa kwa
upanga baada ya kukataa kuikana imani.
9. Yakobo mwana wa Alfayo. Alifanya huduma katika nchi za Israeli, Misri na
Siriya. Mtume Yakobo wa Alfayo au Yakobo mdogo Alitupwa kutoka kwenywe
kinara cha hekalu na kisha kupigwa na rungu lenye misumari mpaka kufa huko
Yerusalem
14
10. Yuda/Thadeo- mtume huyu alifanya huduma huko Uturuki, Iraq, Kuwait,
Syria, Iran, na Lebanon. Mtume huyu Aliuawa kwa kupigwa na mshale ubavuni.
11. Simon Mzerote-huyu alikuwa ni mmojawapo wa askari waasi waliokuwa
wanajitayarisha kwaajili ya kuipindua dola ya Rumi. Baada ya kukutana na
Yesu aliacha kazi ya uaskari na kuwa mwanafunzi wa Yesu. Simon mzerote
alifanya huduma katika nchi za Misri, Israel, Siria, Afrika Kaskazini Libya na
Uingereza. Simoni aliuawa kwa kusulubiwa baada ya kukataa kutoa dhabibu
kwa mungu jua.
1 2.Yuda Iskariote- alikuwa ni mtunza Hazina wa Huduma ya Yesu. Yuda
alimsaliti Yesu na kisha kujinyonga.
MADA YA TATU
KANISA LA SMIRNA (KIPINDI CHA MATESO)
KIPINDI CHA SMIRNA
A. UTANGULIZI.
15
Simirna ni mji ambao ulikuwa umbali wa Km 65 Kaskazini mwa Efeso na ulijulikana
kama bandari ya salama kwa wakati ule. Ulikuwa katikati ya njia kuu kutoka Rumi
kwenda India na Persia (Irani)
Katika moja ya mitaa yake kulikuwa na hekalu la mungu wa kigiriki aliyejulikana kwa jina
la Zeus, Mungu mkuu na katika upande mwingine wa mji kulikuwa na hekalu la Cybele
{mama wa mungu}.
Mji wa Smirna pia ulikuwa ni kituo cha ibada ya kumwabudia kaisari. Kulikuwa na hekalu
la mfalme wa Rumi Teberio Kaisari
B. VIPINDI VYA MATESO
Historia ya kipindi cha Smirna. Inaaminika kwamba siku kumi za mateso yaliyotakiwa
kuja juu ya smirna huhusisha vipindi maalum kumi vya mateso chini ya watawala
mbalimbali wa kirumi ambao pia na wao watawala wangekuwa kumi.
Majina ya wafia dini mbalimali katika kipindi hiki cha Smirna chini ya wafalme
mbalimbali wa Rumi yanaorodheshwa hapa.
1. Klaudi Nero (64-68 B.K). Petro alisulubiwa katika kipindi cha utawala wa Nero.
Paulo alikatwa kichwa katika kipindi hiki.
2. Domitiani (90-95 B.K) alijaribu kumuua mtume Yohana kwa kumtumbukiza katika
mafuta yaliyokuwa yakichemka, lakini Yohana alitoka kwa muujiza bila kuungua.
Baada ya hapo akaamua kumpeleka uhamishoni katika kisiwa cha Patmo.Aliwaua
baadhi ya maseneta wa Rumi na kuamuru uzao wa Daudi wote kuuawa.
3. Trajani (104-117 B.K) Simoni ndugu wa Yesu aliuawa katika kipindi hiki
mwaka wa 107 B.K. Askofu Ignatius wa Antiokia aliuawa pia katika utawala wa
mfame huyu mwaka 110.B.K. Watu wengine waliouawa katika kipindi hiki ni
Polikap mwanafunzi wa Mtume Yohana (155 B.K),
4. Marcus Aurelius. (161-180 B.K). Yustini aliuawa katika utawala huu katika mwaka
165 B.K. Pia alifanya mauaji ya wakristo wengine wengi pia.
5. Septimus Severio. (200-211 B.K) alimuua Leonidasi baba wa Origeni,
mwanatheolojia mkuu, Victor askofu wa Rumi aliuawa katika kipindi hiki, pia
aliwaua Perpetua, Felistasi na Ireneusi mwaka 202 B.K
6. Thraker Maximus (235-237 B.K). kiongozi huyu alikuwa katili na asiye na huruma
kabisa. watu wengi sana waliuawa katika kipindi hiki baadhi yao ni, Pontianus
(askofu wa Rumi), Anterose, Maseneta wa Rumi na familia zao, Pamachius, Quirutus,
mwanamwali Martina na Hippolitus.
7. Desiusi. (250-253 B.K. ) katika kipndi cha utawala wake mateso yaliibuka tena juu
ya kanisa na kwa bahati nzuri utawala wake ulidumu kwa muda mfupi sana na baada
ya kuanguka kwa utawala wake kipindi kifupi cha amani kilikuja juu ya kanisa.
16
Baadhi ya watu waliouawa katika kipindi hiki ni Fabiani askofu wa Rumi, Juliani
mwenyeji wa Cicil, (aliwekwa ndani ya ngozi ambayo ndani yake kulikuwa na nyoka
wengi na ng’e na kisha kutupwa baharini). Kijana mmoja aitwae Petro aliuawa baada
ya kukataa kutoa dhabihu kwa mungu wa kipagani Venasi, Nichomachus, binti Denisa.
Epimachus na Alexanda waliuawa kwa kuchomwa kwenye moto.
8. Vareliani (257-260 AD.) Idadi kubwa ya wakristo waliuawa pia katika kipindi hiki,
baadhi ya watu mashujaa walioifia imani yao katika kipindi hiki ni Rufina, Sekunda,
Stefano askofu wa Rumi, (alikatwa kichwa), Saturninus askofu wa Toulouse. Sektasi
askofu wa Rumi na Mashemasi sita waliuawa mnamo mwaka 258AD. Askofu Spriani
wa Kathegi aliuawa pia katika kipindi hiki.
9. Aureliani (270-275 B.K.) Badhi ya watu waliouawa chini ya utawala wa Aureliani ni
Agapetasi kijana aliyeuza shamba lake na kuwapa fedha maskini, Felix askofu wa
Rumi alikatwa kichwa katika kipindi chini ya utawala huu.
10. Deokretiani, Mtawala huyu aliimarisha na kuyakuza mateso katika dola yote ya
Rumi.Mateso yalienea kila eneo la himaya yake. Baadhi ya wafia dini waliouawa
katika kipindi hiki ni;- Sebastian,victor, Romanus,Susanna, Sipriani wa Antiokia,
Dorothea na wengine wengi, Mji wa frigia uliojulikana kama mji wa kikristo
ulichomwa moto na wakazi wake wote wakafa.
C. MATESO YA KITAIFA.
Tabia za msingi katika historia ya kanisa katika karne zote mbili yaani karne ya pili na ya
tatu ni kanisa au wakristo kuteswa na wafalme wa kirumi.
Mateso haya hayakuwa endelevu lakini yalitegemea mtazamo aliokuwa nao mfalme
aliyekuwa akitawala katika kipindi hicho.
Mateso ambayo yalikuwa yakijirudia katika kipindi hiki yalidumu kwa karibu miaka 200
mpaka mfalme Kostantino alipookoka na kutangaza tamko la amani.(Edict of Torelance)
katika mwaka wa 313 B.K
D. SABABU ZA KANISA KUTESWA.
1. Imani juu ya Mungu mmoja. Warumi walikuwa na miungu mbalimbali ambayo
walikuwa wakiiabudu pamoja na sanamu zao. Wakristo walitangaza kwamba kuna Mungu
mmoja tu. Mfalme wa Rumi alijenga hekalu ambalo lilipaswa kutumiwa na watu wote
kuabudu miungu yao.
Wakristo walilazimishwa kushiriki ibada hizo za kuabudu miungu. Kitendo cha Wakristo
kukataa kuabudu miungu hiyo kulisababisha mateso juu yao. Majanga ya aina yoyote
yalipotukia yalitazamwa kama ni matokeo ya muingu kukasirika hivyo basi watu wote
waliogoma kushiriki katika ibada hizo walihesabiwa kuwa ndiyo chanzo cha majanga
hayo hivyo kustahili adhabu.
2. Kukataa kumwabudu kaisari. Kama ilivyokwisha elezwa katika sura iliyopita
kwamba makaisari wa kirumi walijitangaza kwamba wao ni miungu na wakadai
17
waabudiwe na wananchi au raia wao. Makaisari hao walisimamisha sanamu zao na
wananchi wakaziabudu na kutoa sadaka.
Hivyo raia wote wa dola ya Rumi walilazimika kushiriki ibada ya kumwabudu kaisari.
Mahekalu ya ibada za kaisari yalijengwa kila mahali na sanamu za makaisari zikawekwa
na watu wakalazimishwa kumwabudu kaisari na kutoa dhabihu mbele ya sanamu za
kaisari. Hii ilikuwa mojawapo ya ibada za kitaifa katika dola ya Rumi.
Wakristo walipinga vikali ibada hizo na hawakuwa tayari kushiriki ibada hizo wala kutoa
dhabihu mbele ya sanamu za kaisari. Kutokana na sababu hiyo wakristo walihesabiwa
kuwa waasi dhidi ya kaisari na dola kwa ujumla na hivyo walipaswa kuhukumiwa kifo.
Wakristo walianza kuteswa na dola ya Rumi kwa sababu ya kukataa kumwabudu kaisari na
kumwita Yesu Mfalme (Kurious).
3. Kutojihusisha kwenye ibada za sanamu. Ibada hizi za sanamu zilikuwa sehemu ya
maisha ya kila siku katika dola ya Rumi. Sanamu hizo zilisimamishwa katika kila nyumba
na ziliabudiwa katika kila sherehe. Dhabihu za vinywaji zilitolewa kwa sanamu hizo.
Hivyo wakristo walikataa kujihusisha katika shughuli za kila siku za kijamii zilizohusiusha
ibada za sanamu(mfano sherehe mbalimbali). Wakristo walipokataa kujihusisha na hayo
mambo walionekana wako kinyume na jamii nzima.Kwa sababu hiyo jamii iliwahesabu
kama maadui.
4. Kutambuliwa rasmi kwa dini ya kiyahudi: Dini ya kiyahudi ilitambuliwa rasmi na
dola ya Rumi kama dini ya kitaifa. Mwanzoni kanisa wakati linaanza lilitambuliwa kama
kikundi tu ndani ya dini ya kiyahudi chenye msimamo mkali na hivyo kanisa lilipata
upendeleo wa serikali kwa namna fulani. Lakini mara baada ya kuanguka kwa Yerusalemu
na kubomolewa kwa hekalu katika mwaka wa 70 B.K, kanisa au ukristo ulisimama peke
yake na dini ya kiyahudi walikuwa tayari kushirikiana na serikali kulitesa kanisa.
5. Kanisa kufanya mikutano ya faragha. Kutokana na mateso kanisa lilianza kukutana
katika maeneo ya siri na hasa wakati wa usiku. Hii ilipelekea kanisa kuhisiwa vibaya na
serikali kwamba lilikuwa linafanya njama ya kupindua serikali au kufanya maasi kwa
sababu serikali ya Rumi ilipiga marufuku mikutano yote isiyo halali, pia mikutano ya usiku
ilipigwa marufuku kwa kuogopa kwamba mikutano yote iliyokuwa haina kibali cha
serikali na iliyofanyika vifichoni haikuwa na nia njema kwa dola ya Rumi. Kwa sababu
hiyo wakristo walitazamwa na dola kama waasi. Watu wanopanga njama na maadui wenye
kuleta vurugu na maasi ndani ya dola na hivyo dola ilianzisha mateso juu ya kanisa.
6. Usawa katika kanisa. Kanisa liliwaona watu wote kuwa sawa. Hakukuwa na matabaka
katika kanisa. Waliwaona watu wote kuwa sawa na hawakumwogopa mtu yeyote na wala
hawakuogopa cheo cha mtu. Kutokana na sababu hiyo kanisa lilionekana kuwa na dharau,
lisilo na heshima na hivyo kanisa lilifanyika adui wa dola.
7. Kudolola kwa biashara za sanamu.: Kulikuwa na biashara iliyokuwa inafanywa
ndani ya dola ya Rumi. Biashara hiyo ilikuwa ni ya uuzaji wa sanamu. Watu wengi
walijipatia faida kutokana na biashara hiyo. Mitume walipohubiri Injili watu waliokoka
na kuachana na ibada za sanamu .
18
Mitume walifundisha kwamba sanamu si kitu na hazipaswi kuabudiwa anaepaswa
kuabudiwa ni Mungu muumba Mbingu na nchi pekee. Watu wengi waliacha kununua
sanamu hizo. Kitendo hicho kilisababisha biashara hiyo ya uuzaji sanamu kudolola.
Watengenezaji na wauzaji wa sanamu hizo walipata hasara na wakaamua kuja juu na
kuanzisha ghasia dhidi ya kanisa kwani walipoteza wateja wao.
E.HATUA ZA MATESO.
Kuna mwingiliano kati ya kipindi cha Efeso na Smirna. Kipindi cha Efeso kiliishia na kifo
cha mtume Yohana mwaka 100 B.K. Wakati kipindi cha Smirna kilianza wakati wa
mateso ya kitaifa.(dola) wakati mfalme Nero alipouchoma mji wa Rumi mwaka 64 B.K.
F. VIPINDI KUMI VYA MATESO YA KITAIFA.
MATESO YA KWANZA Chini ya Kaisari Nero.(54-68 B.K)
Klaudi Nero alikuwa na umri wa miaka 16 alipoingia katika utawala (ufalme) katika
mwaka 54 AD. Alikuwa mjukuu mkubwa wa Agustus aliyetoa amri ya watu wote
kuhesabiwa sensa (Lk 2). Nero alikuwa mfalme wa kwanza katika wafalme kumi
kuanzisha mateso dhidi ya kanisa.Alichoma mji wa Rumi mwaka 64 B.K .Theruthi mbili
ya mji wa Rumi iliteketea. Mfalme Nero aliwasingizia wakristo kwamba ndiyo
waliohusika na uharibifu huo. Hivyo kanisa lililazimika kuingia kwenye mateso makali.
Katika kipindi hiki mtume Petro alisulibiwa miguu juu kichwa chini mnamo mwaka 67
Pia mtume Paulo alikamatwa na kufungwa Rumi ambapo alihukumiwa kifo na kisha
akauawa kwa kukatwa kichwa mwaka 68 B.K Mjini Rumi.
Mfalme Nero alikuwa katili kuliko makaisari wote wa dola ya Rumi waliomtangulia na
waliomfuata. Kwani hajatokea kaisari katika dola ya Rumi aliyefanya mauaji kama Nero.
Mwaka 59 B.K . Mfalme Nero alimuua mama yake . pia alimuua mke wake wa kwanza
(Octavia)na kisha mkewe wa pili(Pompea) na baadae alimuua kaka yake na rafiki yake
mwalimu Seneka.
Mpaka mwaka wa 64. B.K Rumi ilikuwa katika ghasia kuu. Mfalme Nero alituhumiwa
kwamba yeye ndiye aliyehusika na kuuchoma moto mji wa Rumi. Lakini yeye alikanusha
na kuwashutumu wakristo kuwa ndiyo waliohusika na tukio hilo.
Kutokana na hilo kanisa liliingia katika kipindi cha mateso makali. Maelfu ya wakristo
waliuawa baadhi yao walitupiwa kwenye viwanja vya michezo vya wanyama poli ili
waliwe na wanyama wakali na baadhi yao walichomwa moto na mfalme akaendesha gari
lake juu yao katika bustani yake. Bustani ya mfalme ambako tukio hili lilifanyika leo ni
eneo la la jiji la Vatikani makao makuu ya papa na kania la mtakatifu Petro. Kaisari
Nero alijiua mwenyewe mwaka 68. B.K
KIPINDI CHA PILI CHA MATESO CHINI YA DOMITIAN. (90-96 B.K).
Baada ya Nero kujiua mwaka wa 68 B.K kanisa lilipata amani mpaka alipoinuka mtawala
mwingine ambaye ni Domitiani. Wakristo wengi waliuawa wakati huu .Baada ya juhudi
zote za kumuua mtume Yohana kushindikatiani Domitiani aliamua kumpeleka Mtume
19
Yohana uhamishoni kwenye kisiwa cha Patmo ambapo ndipo mahali alipopokea ufunuo
ambao sasa ni kitabu cha Ufunuo wa Yohana.
KIPINDI CHA TATU CHA MATESO CHINI YA TRAJANI 104-107 AD.
Trajani husemekana kuwa mtu muhimu sana miongoni mwa watawala wa Rumi. Alikuwa
mtawala mzuri kwa nchi yake lakini aliwaua wakristo. Mmoja wa mahakimu wake
aliyeitwa Plin the younger. Gavana wa Bethania alichunguza maisha ya wakristo na
mafundisho yao na kugundua kwamba mafundisho hayo hayakuwa na chochote chenye
kuleta uasi kwa serikali ya Rumi. Alileta ripoti yake mbele ya mfalme Trajani lakini
mfalme alijibu
“ Kama watu hawa walioletwa mbele yako wamepatikana na hatia kwa sababu ya kuwa
wakristo na wauawe lakini ikiwa wataikana imani yao ya kikristo na ikathibitika kwamba
wanaabudu miungu yetu na waachiwe huru. Katika kipindi hiki waliuawa wakristo
mbalimbali kama ifuatavyo.
‣ Simoni mdogo wa Bwana Yesu alisulubiwa katika mwaka wa 107 AD akiwa na
umri wa miaka 110. Alisulubiwa kwa amri ya mfalme wa Rumi {Trajani}.
‣ Askofu Ignatius wa Antiokia ambaye aliandika nyaraka mbalimbali kwa makanisa
mbalimbali ambazo baadhi yake zinapatikana katika kitabu kiitwacho “Mababa wa
Kitume”{Apostolic fathers}. Alikuwa tayari kuuawa kwaajili ya Bwana Yesu.
Aliandika barua za kuwafariji wakristo akiwa njiani kuelekea Rumi ambapo
alitupwa katika hifadhi ya wanyama wakali na akaliwa na wanyama wakali mnamo
mwaka 110.AD
‣ PORIKAP. {69-155 AD} Alikuwa mwanafunzi wa mtume Yohana na rafiki wa
Ignatius na mwalimu wa Ireniusi. Inadhaniwa kuwa Polikap aliteuliwa na mtume
Yohana kuwa askofu wa makanisa saba ya Asia. Alipoamriwa kumkana bwana Yesu
Kristo ili kuepukana na kuuawa yeye alijibu:
“Miaka 86 nimemtumikia Bwana wangu na hajatenda Jambo lolote baya
kwangu, nawezaje kunena vibaya juu ya Bwana wangu aliyeniokoa?
Alichomwa moto na akafa kifo cha kishujaa kwaajili ya Imani yake kwa Yesu Kristo.
Aliuawa chini ya utawala wa mfalme Antonius Pius mwaka 155 A.D.
KIPINDI CHA NNE CHA MATESO CHINI MARCUS
AURELIUS 161-180 A.D.
Marcus alijulikana kam mfalme bora wa nchi yake na mwandishi mwenye maadili.
Japokuwa alikuwa mtu mzuri kwa taifa lake alikuwa mtesi wa kanisa. Alifikiri kurejesha
maisha ya zamani ya kirumi na dini za zamani. Kwa wakati huo ukristo ulikuwa na
mashiko zaidi. Waamini wengi walikuwa tayari kufa kwa ajili ya imani yao na wala
hawakuogopa kifo. Walikikabili kifo kwa shangwe na ushindi mkuu. Katika kipindi hiki
waaminni wengi waliuawa na wengine walitupwa katika viwanja vya michezo vya
wanyama ili waliwe na wanyama wakali.
YUSTINI (JustineMarty) 100-165 A.D alizaliwa na alielimishwa vizuri mpaka kuwa
mwanafalsafa na aliendelea kufundisha hata baada ya kuwa mkristo. Alirejerea kwa
20
manabii wa zamani wa Kiebrania. Aliandika maneno yafuatayo dhidi ya ukatili na mauaji
yaliyokuwa yanaendelea dhidi ya wakristo.
“wanatushitaki, wanatusulubisha kwenye misalaba na kutupa kwenye
viwanja vy wanyama wakali na kwenye moto. Lakini wanapofanya
mabaya zaidi juu yetu ndivyo idadi ya wakristo inaongezeka na kuwa
kubwa zaidi.
Mnamo mwaka 165 A.D alikamatwa na mfalme wa Rumi Marcus Aureliusi na
kuuawa.
KIPINDI CHA TANO CHA MATESO CHINI YA SEPTIMUS. 202-211. A.D.
Baada ya kifo cha Marcus Aurelius kanisa lilipata amani mpaka alipoinuka mtawala
mwingine aliyejulikana kwa jina la Septimus Severus. Mtawala huyu alimuua Leonidasi
baba wa Origeni mwanatheologia mkuu. Katika mji wa kathegi Perpetua na mtumwa wake
Felistas walitupwa katika viwanja vya wanyama poli wakali na wakauawa.
KIPINDI CHA SITA CHA MATESO CHINI YA THRAKA MAXIMUS 235-237
A.D. Baada ya kipindi cha amani Thraka alikalia kiti cha enzi cha Rumi. Alikua
mpiganaji na alikusudia kuonyesha huruma zake kwa dini za kipagani kwa kuwatesa
wakristo. Utawala wake ulikuwa mfupi kwa sababu ya kutawala kwake kwa njia ya
udikteta. Maadui zake walitengeneza kikundi ambacho kilifanikiwa kumuua.
KIPINDI CHA SABA CHA MATESO.CHINI YA DECIUS 250-253 A.D.
Katika kipindi cha utawala wake mateso makali yaliibuka tena na kwa bahati nzuri kipindi
chake cha utawala kilikuwa kifupi na kanisa lilipata raha na amani kwa miaka 40.
KIPINDI CHA NANE CHA MATESO CHINI YA VARELIANI. 257-260. A.D.
Askofu Sipriani wa Kathegi aliuawa pia askofu wa Rumi Sextus aliuawa.
KIPINDI CHA TISA CHA MATESO. CHINI YA AURELIUS. 270-275. A.D
Mfalme Aurelius alikuwa mwabudu jua japokuwa hakulitesa kanisa moja kwa moja
mwanzoni lakini hakuwapa uhuru wakristo. Hatimae aliamuru kwamba wakristo wateswa.
Mateso yalidumu kwa muda mfupi sana chini ya mtawala huyu aana aliuwawa na wafuasi
wake mwenyewe.
KIPINDI CHA KUMI CHA MATESO CHINI YA DEOCLETIAN 303- 3010. A.D
Mfalme Deocletiani na wasaidizi wake waliwafunga wakristo gerezani. Baadae sehemu ya
jengo hili lilibadilishwa na kuwa Kathedro ya Mtakatifu Petro. Deocletiani aliagiza
kuchomwa moto kwa kila nakala Biblia, makanisa kubomolewa na wakristo wenye
msimamo mkali kunyang’anywa uraia.
Akiwa na umri wamiaka 80 Deocletiani aliondoka kwenye kiti cha utawala, lakini wafuasi
wake Galarius na Kostantinusi waliendeleza mateso mpaka mfalme Kostantino mtoto wa
Kostantinus alipotoa tamko la amani kwa kanisa mwaka 313 A. Tamko hili la amani
lilisitisha mateso kwa kanisa kwa kipindi cha karne mbili
21
Siku kumi za kujaribiwa zilizotajwa katika Ufunuo wa Yohana 2:10 zilifikia mwisho.
Baadae mfalme Deocletiani alipotambua kwamba yuko karibu na kufa alitubu dhambi zake
mbele ya askofu wa mji na mnamo mwka 337 A.D alibatizwa. Mtu aliyeamini kwamba
angeweza kuufuta ukristo alijikuta yeye mwenyewe anakuwa mkristo.
G. UONGOZI WA KANISA KATIKA KIPINDI HIKI.
Wakati mitume wakiwa hai uongozi ulionekana ni utumishi yaani kutumikia au
kuwajibika. Wakati Luka alipoandika kitabu cha Matendo na Paulo alipoandika nyaraka
zake tunakuta maneno askofu na wazee yakiwa na maana sawa yaani yakimaanisha ofisi
moja. Lakini katika miaka ya 125 tunakuta maaskofu wamekuwa watawala katika maeneo
yao. Katika baraza la Yerusalemu mwaka 48 A,D {Mdo 15} mitume wote na wazee
walihusika. Lakini katika baraza la mwaka 150 A.D waliohusika ni maaskofu pekee. Hii
inadhihirisha kwamba kanisa liliondoka taratibu kwenye mafundisho halisi ya mitume.
Huduma ya mitume ilizimwa na ikachukuliwa na maaskofu. Maaskofu walijifanya
watawala wa kanisa. Hii ndio sababu inayosababisha baadhi ya wanazuoni wa Kikristo
kuamini kwamba kipindi cha mitume kiliishia na kifo cha mtume Yohan, jambo ambalo si
kweli. Huduma za mitume, manabii, waalimu wachungaji na wainjilisti kama
zinavyoelezwa katika waefeso 4:11 ziliendelea kuwapo katika kipindi cha mitume na
vipindi vingine vyote vya kanisa, japokuwa zimekuwa zikikataliwa na katika vipindi
fulani ilionekana kama zimetoweka lakini kwa uhakika zimekuwapo na bado zimekuwa
zikifanya kazi katika kanisa hata sasa.
H. SHULE ZA THEOLOGIA.
Shule ya Alexandria. Ilianzishwa mwaka 180. A.D na Pantaenusi ambaye alikuwa ni
mwanafalsafa wa kigiriki na baadae akwa mkristo. Kisha alikwenda India, Irani na Saudi
Arabia katika huduma kama mmishenari. Alikufa mwaka 200 AD .
Klementi wa Alexandria alikuwa mwanafunzi wa Pantaenusi na alimsaidia katika
uendeshaji wa shule. Alikuwa ni mkuu wa shule hadi alipoondolewa kwenye wadhifa huo
katika kipindi cha mateso cha Septimus Severusi mwaka 2002AD, Baadhi ya vitabu vyake
mpaka sasa vipo.
Origeni (185-254 A.D). Alikuwa ni mwanatheologia mkuu. Alikuwa ni mtoto wa
Leonidasi. Baba yake aliuawa kutokana na imani yake katika Kristo chini ya utawala wa
mfalme Severus katika mwaka wa 2002 AD. Wakati huo Origeni alikuwa na umri wa
miaka 17. Origeni aliisaidia familia yake kwa kufundisha falsafa ya kigiriki pamoja na
fasihi. Aliianzisha shule ya Biblia kwa upya iliyokuwa imefungwa kutokana na kuondoka
kwa Klementi. Baadae alikuwa ni mwandishi wa vitabu vya Dogma na Thiologia. Baadae
alikwenda Kaisaria na alianzisha shule nyingine ya Biblia ambapo alikuwa ni kiongozi wa
shule hiyo kwa karibu zaidi ya miaka 20. Alifungwa jela chini ya mateso ya Deciani na
alikufa kutokana na kutendewa kinyama akiwa gerezani. alikufa akiwa na umri wa miaka
69 mnamo mwaka 254 AD.
Shule ya Asia ndogo. Shule hii haikuwa katika mji wowote ilikuwa ni shule ya masafa
(mobile Bible School). Ilihusisha waalimu wa thiolojia na waandishi. Baadhi yao ni
22
Ireneusi (130-202A.D) aliyezaliwa Smirna. Alipata elimu yake ya awali ya Biblia chini ya
Porikap. Kanisa la Asia ndogo lilimpeleka Ufaransa kama mmisionari. Aliuawa wakati wa
mateso ya Severusi mwaka wa 202 AD
Shule ya kathegi: Shule hii ilikuwa kaskazini mwa Afrika na ilifanya vizuri kuliko shule
zingine kubadili imani ya Kithiologia katika Ulaya. Watu wakuu katika shule hii
walikuwa ni Tetuliani na Sipriani. Tetuliani (160-200 A.D) Alikuwa ni mteteaji shujaa
wa imani ya kikristo dhidi ya dini ya kiyahudi na mafundisho potofu. Alijiunga na
umontano na alitumia kalamu na mahubiri kuthibitisha kile alichofikiri ni mambo ya
kidunia na mabishano katika kanisa.
Sipriani Askofu wa Kathegi (195-258 A.D) Alikuwa ni mtoto wa afisa wa ngazi ya juu
wa dola ya Kirumi. Alikuwa mkristo wakati wa ujana wake. Mambo matatu yaliyomvutia
mpaka kuwa mkristo ni Maandiko ya tetuliani, mafundisho ya Cellius toka Rumi na
Maandiko matakatifu (Biblia).
Mwaka mmoja baada ya kuwa mkristo alikuwa askofu na kiongozi mkuu wa makanisa ya
Afrika Kaskazini mwaka 248AD. Mnamo Mwaka 257AD Mfalme Valentine alimfungia
kufanya huduma na mwaka 258AD aliuawa.
Kanisa la karne ya pili lilipambana na mambo makuu mawili ambayo ni Mateso na
uzushi(Heresy) yaani mafundisho potofu. Mtume Paulo alitabiri ya kwamba:
“ Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa mwitu wakali wataingia kwenu
wasilihurumie kundi. Tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu,
wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao”Mdo20:29-30
I. UZUSHI NA MAFUNDISHO YA UONGO.
Mafundisho yasiyokubaliana na mafundisho rasmi ya kanisa yaliitwa uzushi na waamini
waliamriwa na kanisa kuyapinga na kutokuyapokea mafundisho hayo.
Kanisa katika historia yake lilitangaza kuwa baadhi ya mafundisho yaliyokuwa
yanaibuliwa na baadhi ya viongozi na waamini wa kanisa yalikuwa ni mafundisho potofu
na yakapewa jina UZUSHI (heresy) kutokana na kutokukubaliwa rasmi kwa mafundisho
hayo na uongozi wa kanisa kwa ujumla wake.
Si kila mafundisho waliyoyaita uzushi yalikuwa mabaya, kwani kile kilichoitwa
uzushi kilikubaliwa baadae na kanisa na kile ambacho kilionekana chema
kilikataliwa na kuitwa uzushi baadae. Hoja au mawazo yale waliyoyaita uzushi baadhi
yalikuwa na mambo mema ndani yake kama tutakavyotazama hapo baadae
Kanisa halikupambana na mateso tu bali pia na mafundisho ya uongo, sawsawa na unabii
uliotolewa
J. MAKUNDI YA UZUSHI.
1. UYAHUDISHAJI.
Hili lilikuwa ni kundi la wakristo wa kiyahudi lililojitokeza wakati kanisa linapanuka
katika miji ya wamataifa. Wayahudishaji hawa walifundisha kwamba wakristo wote
walitakiwa kuzifuata sheria za Musa na mapokeo ya dini ya kiyahudi. Waliyakataa
23
maandiko ya mtume Paulo kwa sababu yalipinga mafundisho yao. Kundi hili lilitoweka
katika karne ya pili BK.
2. UNOSTIKI
Unostiki ilikuwa ni falsafa iliyojaribu kutumia imani ya ukristo katika kuthibitisha
ukweli wake. Kundi hili waliamini kwamba Baada ya ngazi ya Mungu mkuu kulikuwa na
miungu wengine wengi ambao baadhi wakiwa wema na wengine waovu. Unosti ulikuwa
na elementi za falsafa za kiyunani na dini za kipagani. Hivyo kanisa lilipinga vikali mno
unosti likikana kwamba imani yake si falsafa na wokovu hautegemei falsafa na mafumbo
bali ufunuo wa Yesu kristo.
Wanostiki walipunguza thamani ya maisha na huduma ya Yesu Kristo. Habari nzima juu
ya maisha na huduma ya Yesu ilielezwa kwa njia ya mafumbo (allegory). Unostiki ulizuka
katika karne ya pili baada ya Kristo na ulishamiri katika karne ya tatu na ya nne.
Unostiki hata sasa unajidhihirisha katika karne hii ya ishirini na moja katika dini
mbalimbali hapa ulimwenguni. Hususani kupitia falsafa ya mpango mpya wa dunia (New
World order Philosophy)
MAFUNDISHO YA UNOSTIKI.
i. Maarifa ya pekee hufunuliwa kwa watu wachache tu.
ii. Wokovu si kwa watu wote, ni kwa watu wachache tu wenye kuyaelewa maarifa
yanayofunuliwa.
iii. Ulimwengu huu na vitu vilivyomo ndani yake vimeumbwa kwa nguvu isiyokamili na
hii ndio asili ya maovu yote katika ulimwengu.
iv. Yesu si mwanadamu, alikuwa na roho tu. Yesu alikuwa ni roho aliyejifanya aonekane
katika umbile la binadamu.
v. Waliamini kwamba mmoja wa miungu wadogo alikuwa ndani ya Yesu na ndio
aliyekuwa asili ya uungu wake.
3. MARSION
Huyu alikuwa ni mtoto wa askofu wa Pontus. Alikuja Rumi yapata mnamo mwaka
138AD. Alipofika Rumi alijulikana kwa haraka sana kutokana na jinsi alivyojitolea sana
katika kanisa kwa mali zake. Pia mafundisho yake yalimpa umaarufu na kumfanya
ajulikane sana. Kutokana na umaarufu huo Marsion alipata wafuasi wengi. Mafundisho
yake hayakukubaliwa na kanisa hivyo alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa
mnamo mwaka 144 BK.
Marsioni aliunda kikundi chake ambacho kiliwaunganisha wafuasi wake wote. Kikundi
chake hakikuongezeka kwa njia ya kuzaliana kwa sababu ya kukataa mambo ya ndoa.
Waliongezeka kwa njia ya wanachama wapya kujiunga. Marsion alikuwa ni mtu wa
kwanza kutunga kanuni ya maandiko. Alipogoapogoa baadhi ya vitabu na kutunga orodha
ya maandiko matakatifu aliyoakuwa anaiamini yeye.
MAFUNDISHO YA MARSION
24
Kwa kiasi kikubwa mafundisho yake yalifanana na mafundisho ya wanostiki.
i. Aliweka sharti la wafuasi wake (wanandoa) kutokutana kimwili na kwamba
walitakiwa kuachana na kuishi maisha ya upweke.
ii. Alikaza kwamba wokovu ni kwa watu wote. Wokovu hutegemea Injili ya Yesu
Kristo na si kwa kufunuliwa mafumbo kifalsafa.
iii. Injili ya upendo wa Mungu inahitaji kusikika zaidi katika kanisa.
iv. Kanisa limeichafua Injili kwa kuichanganya na mambo ya dini ya kiyahudi.
v. Mungu wa Agano la kale ni tofauti na baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Kwa
sababu Mungu wa agano la kale alifurahia dhabihu za damu.
vi. Mungu aliyeumba ulimwengu na watu wake ni Mungu mwovu, Mungu mwingine
mwema alijificha hadi wakati wa Yesu Kristo.
4. UMONTANO.
Kilikuwa ni kikundi kilichoanzishwa na mtu mmoja aliyeitwa Montano mwenyeji wa
Frigia. Wafuasi wa kikundi hiki waliitwa wamontano. Kikundi hiki kilienea sana kuanzia
mwishoni mwa karne ya pili na kuendelea kwa karne mbili zaidi.
Wakati wa ubatizo wake Montano alinena kwa lugha nyingine na kutabiri na hivyo akajiita
kuwa ni kinywa cha Roho Mtakatifu aliyetabiriwa na Yohana. Alikuwa na wasaidizi
wawaili wanawake ambao nao pia walijitambulisha kuwa ni vyombo pekee vya Roho
Mtakatifu. Karama za kinabii zilijidhihirisha katika mlengo wa umontano. Kutokana na
mikazo yao wamontano walihukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa.
MAMBO MUHIMU YA MONTANO.
i. Walikaza kwamba wamefunuliwa juu ya mwisho wa dunia uliokuwa karibu sana
kutokea.
ii. Baadhi ya wafuasi wa umontano walikataa kulima kwa sababu Yesu angekuja kabla
ya msimu wa mavuno.
iii.
iv.
Baadhi ya wamontano walikataa ndoa kwa kuwa mwisho wa dunia ulikuwa karibu.
Kiongozi wao mmoja wa huko Pontusi aliwapeleka washirika wake porini kwenda
kumlaki Bwana Yesu wakati anarudi duniani kwa mara ya pili.
v. Kiongozi mwingine wa huko Shamu aliwakataza washirika wake wasilime kwa
sababu Yesu angerudi kabla ya msimu wa mavuno.
vi.
vii.
viii.
Montano alikataa hali ya kanisa kumezwa na ulimwengu.
Alidai kuwa kanisa lilikuwa limepoa na hivyo lisitarajie kurudi kwa Yesu.
Walipinga suala la uaskofu kuchukua mamlaka katika kanisa. Waliweka mkazo
katika huduma ya unabii na ukuhani wa waamini wote.
5. KUMEGEKA KWA KANISA CHINI YA UONGOZI WA NOVATIANO NA DONATO.
Katika karne ya tatu na ya nne kulitokea na kumegeka kwa kanisa. Mmeguko huo
uliongozwa na Novatiano katika karne ya tatu na Donato karne ya nne. Kugawanyika
huko kulitokana na kurejeshwa kwa viongozi na wamini waliokuwa wameikana imani
25
katika kipindi cha mateso. Pia makundi haya yalijitenga baada ya kuona kwamba wakristo
wengi walikuwa wanaishi maisha machafu kama wapagani waliokuwa wanawazunguka.
I. UASI WA NOVATIANI.
Katika karne y tatu askofu wa Rumi aliyeitwa Kalisto alitangaza kwamba dhambi yoyote
inaweza kusamehewa ikiwa mkosaji anaonesha toba ya kweli. Fundisho hili lilienea
sana. Wakristo waliokuwa wameikana imani yao wakati wa mateso walitaka kurudi
kanisani na askofu Kalisto alikubali kuwapokea watu hao.
Kiongozi mmoja wa kanisa aliyeitwa Novatiani, hakukubaliana na jambo hilo na alilipinga
vikali na akaungwa mkono na wachungaji wengine ambao nao walikuwa kinyume na
maamuzi hayo ya askofu. Walijitenga na kanisa na kuanzisha ushirika wao. Novatiani
alichaguliwa kuwa kiongozi wao.
II. UASI WA DONATO.
Mmeguko wa kanisa chini ya uongozi wa Donato ulitokea Afrika ya kaskazini karne ya
nne baada ya utawala wa mfalme Deokletiani. Mfalme huyu katika kipindi cha utawala
wake alikuwa na mpango wa kufuta ukristo na kuchoma moto Biblia zote. Wakati
wakipindi cha mateso makali baadhi ya viongozi wa kanisa waliasi imani wakaamua kutoa
maandiko matakatifu (Biblia) yateketezwe ili kujinusuru na kifo.
Baada ya kipindi cha mateso kumalizika viongozi hao yaani wachungaji na maaskofu
walioasi walitaka kurudi kanisani. Kanisa katoliki lilikuwa limekubali kuwapokea. Kanisa
lilikubali kuwarudishaviongozi hao katika sharika zao. Katika mji wa Karthegi waamini
wengi sana walikataa kuongozwa na mtu aliyemkana Yesu na kutoa Biblia kwa
serikali ili ziteketezwe.
Donatuno alikuwa kiongozi wa mgomo huo na alipata wafuasi wengi. Watu hao
walijitenga na kanisa na kuanzisha huduma yao. Kulikuwa na ugomvi kati ya wakatoliki na
wadonato kwa kwa muda mrefu.
K. HALI YA KANISA KATIKA KIPINDI CHA MWISHO WA KARNE YA PILI:
i. Kanisa lililotakasika. Mateso yaliwaondolea mbali wale ambao hawakuwa
waaminifu katika imani yao. Wale ambao hawakuwa na imani kamilifu na
waliojiunga na kanisa kwa masilahi yao binafsi mateso yaliwatupa nje yya kanisa.
ii.
iii.
Mafundisho yenye mfumo mmoja. Japokuwa kanisa lilihusisha watu wa
tamaduni , rangi na jamii mbalimbali bado lilikuwa na umoja wa imani katika
kanisa lote. Walifuata mafundisho ya mtume Paulo, Petro na mitume wengine.
Mdo 2:42.
Kanisa lenye muundo: kazi iliyofanywa na Paulo ya kuweka viongozi wa Kanisa
katika kila mji ilileta ufanisi. Viongozi hao walikutana katika mikutano na
kujadili mambo mbalimbali muhimu kuhusu kanisa. Hii ilisababisha kutokea kwa
ushirikiano imara wa kimataifa. (International Fellowship) ambao umekuwepo
mpaka sasa.
26
iv.
Kanisa lenye kusitawi {kukua}. Licha ya mateso yaliyolikumba kanisa, kanisa
liliendelea kukua kwa kasi. Kanisa lilikumbana na mateso makali chini ya
watawala mbalimbali wa Kirumi, lakini kanisa liliendelea kukabiliana na mateso
hayo na likawa tayari kuwapelekea watesi hao Injili ya uzima. Mateso
yalisababisha kanisa kukua na kuongezeka.
L. KUANDIKWA KWA AGANO JIPYA.
Hatuwezi kueleza kwa udhahiri au kikamilifu kwamba ni lini hili lilifanyika. Baadhi ya
vitabu kama vile nyaraka za Paulo zilikubaliwa kila mahali, wakati vingine kama vile
Waebrania, Yakobo na Ufunuo wa Yohana vilikubaliwa Mashariki peke yake na
kukataliwa Magharibi.
Kanisa la mashariki lilikubali baadhi ya vitabu ambavyo havipo katika Biblia. Baadhi ya
vitabu hivyo ni Waraka wa Balnaba, Mafundisho ya mitume kumi na wawali na Ufunuo
wa mtume Petro. Mabaraza yalikutana mara kwa mara ili kutambua ni vitabu gani
vilivyokuwa vimevuviwa na vipi havikuvuviwa. Inadhaniwa kwambaAgano jipya
halikutambuliwa rasmi mpaka baada ya mwaka 300AD.
MADA YA NNE
KIPINDI CHA PERGAMO
KANISA LA KIFAHARI/ KITAIFA.
A. UTANGULIZI.
KIPINDI: Toka tamko la amani la mfalme Kostantino (313 BK) hadi kuanguka kwa dola
ya Rumi mnamo mwaka 476 BK.
27
B. USHINDI WA WAKRISTO
Baada ya miaka miambili ya mateso kanisa liliishinda dola ya Rumi na kupata amani.
Mfalme Deokletiani katika utawala wake aliweka watawala wasaidizi katika majimbo
yake kutokana na ukubwa wa dola ya Rumi. Baba wa Kostantino alikuwa ni mmoja wa
watawala wasaidizi, aliongoza majimbo ya Galia, Uingereza na Hispania, Baada ya kufa
kwa watawala wasaidizi kulitokea na kugombea madaraka baina ya watoto wao.
Baba wa Kostantino alipofariki Kostantino alitangazwa kuwa mtawala badala ya baba
yake, na hivyo watoto wa watawala wengine waliamua kuanzisha mapigano ili kuuchukua
utawala huo. Miongoni mwao hao aliyekuwa na nguvu ni Maksentio, huyu alikuwa ni mtu
aliyeshabikia mauaji ya wakristo. Walianzisha mapigano huko Italia maili kumi kutoka
Rumi mnamo 28.10. 312 BK
Wakiwa katika eneo la mapigano kabla ya vita kuanza Kostantino aliona alama ya msalaba
angani ikiwa imeandikwa maneno yafuatayo, “Kwa alama hii utashinda”. Kostantino
aliitikia kwa sala na akaifanya alama ya msalaba kuwa nembo ya Jeshi lake na walipokuwa
vitani Kostantino aliwashinda kabisa maadui zake, adui yake mkuu Maksentio alikufa
katika vita hiyo, hivyo Kostantino akawa mshindi.
Kostantino alitambua kwamba msalaba ilikuwa ni alama ya wakristo na hivyo Mungu wa
wakristo ndio aliyekuwa amemsaidia katika vita hiyo. Mwaka uliofuata Kostantino
alitangaza PATANO LA AMANI na Wakristo, (Edict of Torelant). Patano hili
lilikomesha mateso juu ya wakristo katika dola yote ya Rumi.
Patano hili lililowaletea amani wakristo katika dola ya Rumi lilikuwa na matokeo chanya
na hasi katika kanisa.
C. MATOKEO YA TAMKO LA AMANI
Matokeo ya patano la amani yanaweza kuainishwa katika pande mbili ambazo ni matokeo
mazuri na matokeo mabaya kama ifuatavyo;
I. MATOKEO MAZURI,
i. Mateso juu ya wakristo yalikomeshwa.
ii. Makanisa yaliyokuwa yamebomolewa wakati wa mateso yalijengwa tena kwa fedha ya
serikali.
iii. Maaskofu na wachungaji walisamehewa kodi.
iv. Watumishi wa kanisa walianza kufadhiliwa na serikali na hawakutakiwa kuhukumiwa
kwa sheria za kawaida.
v. Wakristo waliruhusiwa kujenga makanisa mahali popote katika dola ya Rumi.
vi. Dhabihu za kipagani zilikomeshwa.
vii. Kostantino alijenga makanisa makubwa katika miji ya Yerusalemu, Bethlehemu na
katika mji wa Kostantinapali ambapo ndio uliokuwa makao makuu mapya ya serikali
yake.
viii. Watumwa waliachiwa huru.
28
ix. Siku ya jumapili iliwekwa kuwa siku ya mapumziko kwa watumishi wa serikali.
x. Mfalme Kostantino Alisaidia kuunda umoja wa kanisa kupitia mikutano mbalimbali
aliyoiitisha, mfano mkutano wa Naikea mwaka 325 BK.
xi. Mfalme Kostantino alikusudia kuufanya ukristo ukubaliwe na serikali kama dini
zingine.
II. MATOKEO MABAYA.
i. Ilikuwa ni fahari kuwa mkristo, hivyo watu wengi walijiunga na ukristo kwa
maslahi binafsi.
ii. Watu walijiunga na ukristo ili waweze kupata vyeo katika kanisa na serikali.
iii.
iv.
Maadili ndani ya kanisa yalianza kumomonyoka.
Mambo ya kiroho yaliachwa kupewa kipaumbele na badala yake programu
mbalimbali zikapewa kipaumbele.
v. Sherehe na tamaduni za kipagani polepole zilihamia kanisani, kwa kubadilishwa
jina na malengo na badhi zilibadilishwa kuwa sikukuu za kikanisa, mfano
Krismasi.(Kuabudiwa kwa bikira Maria kuliasiliwa kutoka ibada za kipagani za
kuabudu miungu , Zeusi, mungu wa uzuri wa warumi na Diana mungu mwezi).
vi.
vii.
Katika jimbo la mashariki serikali ililitawala kanisa mpaka likapoteza nguvu na
maisha ya kiroho.
Katika jimbo la magharibi kanisa lilipata nguvu dhidi ya serikali.
D. WATAWALA WALIOFUATA BAADA KOSTANTINO
Kostantino hakutaka kutumia nguvu katika kuwafanya watu kuwa wakristo, alitaka jambo
hili lifanyike taratibu na kwa uchaguzi wa mtu mwenyewe, jambo hili halikufuatwa na
watawala waliofuata baada yake.
Baada ya utawala wa Kostantino watawala waliofuatia walikuwa wakali mno walipiga
marufuku ibada za kipagani na waabudu dini hizo walihukumiwa kifo na mali zao
zilitaifishwa. Walivunja mahekalu ya kipagani, watawala hawa(wakristo) kwa kutumia
jina la ukristo sasa walitumia njia zilezile mbaya zilizokuwa zimetumiwa na serikali
kulitesa kanisa.
E. AINA MBALIMBALI ZA MATESO.
i. Katika kipindi cha Efeso kanisa liliteswa na wayahudi.
ii. Katika kipindi cha Smirna kanisa liliteswa na dola ya Rumi.
iii. Katika kipindi cha Pergamo ugomvi ulizuka miongoni mwao wenyewe
(wakristo).
F. UMOJA NA UTAWALA WA KANISA.
Kanisa lililazimka kuwa na umoja kamili ili liweze kuwa na nguvu ya kukabiliana na
mateso yaliyoliandama na uzushi uliokuwa unajitokeza. Hivyo kanisa lilipambana na
maadui wakubwa wawili ambao ni mateso na mafundisho potofu.
29
Kutokana na uzushi kutokea, kanisa ilibidi liwe na utambulisho au jina ambalo lingeli
tofautisha na makundi ya uzushi, hivyo kanisa lilianza kujiita Katoliki. Jina katoliki
linatokana na neno la kiingereza universal, lenye maana “ya popote au ya mahali
popote” Kanisa lilianza kutumia jina Katoliki kwa maana mbili, ambazo ni:
i. Kanisa lisilo na mipaka ya majimbo au ya nchi. Kanisa moja lililo katika nchi zote
ulimwenguni.
ii. Kanisa leye mafundisho sahihi.
G. SABABU ZA KANISA KUHITAJI UTAWALA WENYE NGUVU.
i. Kutokea kwa ukiri wa imani.(kanuni ya imani)
ii. Kutokea kwa Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.
iii. Kutokea kwa maaskofu waliopewa mamlaka ya kutunza mafundisho yaliyotokana na
mitume wa kwanza.
i. Ukiri Wa Imani.
Huu ulikuwa ni ushuhuda mfupi uliotumiwa katika kazi za kawaida sharikani kama vile
ubatizo. Ukiri wa imani ulieleza kwa kifupi kile kanisa linachoamini na ulitumika kama
kiapo kuwa mtu anakubaliana na taratibu za kanisa hilo hivyo anastaili kubatizwa na
kupokelewa katika kanisa.
ii. Kanuni Ya Maandiko Matakatifu.
Kanuni ni kawaida inayotumiwa kupima usawa na usahihi wa kitu. Kanuni huelezea
vitabu vilivyokubaliwa na kupokelewa na kanisa kama maandiko Matakatifu. Kanisa
liliweka kanuni ili kubainisha kati ya vitabu vilivyokuwa ni neno la Mungu na vile
visivyokuwa Neno la Mungu. Mfano wa vitabu visivyokuwa neno la Mungu ni vile
vilivyoandikwa na wanosti. Makundi ya uzushi kama vile wanostika na Marsion
waliharakisha kutungwa kwa kanuni hii.
Mababa wa kanisa walitumia kanuni mbalimbali katika kuvibaini vitabu hivyo. Baadhi ya
njia hizo ni kumtambua mwandishi kama alikuwa ni mtume au la, Kupokelewa kwa kitabu
na watu walionadikwa kwa mara ya kwanza na matumizi ya kitabu hicho katika makanisa
mbalimbali na mamlaka ya kitabu chenyewe N.k
iii. Haja Ya Kutokea Kwa Viongozi Wenye Mamlaka.
Maaskofu walitokea kama watu wenye mamlaka ya kutafsili maandiko na kufundisha
wazi mafundisho ya mitume. Neno askofu maana yake ni mwangalizi/msimamizi. Neno
hili hapo awali lilitumiwa na watu wote na kulikuwa na maaskofu katika idara mbalimbali
za serikali, baadae matumizi ya istilahi hii yalibakia katika Kanisa tu.
Uaskofu ulisaidia kuleta utawala wenye nguvu na umoja katika kanisa kupitia mambo
mawili ambayo ni mafuatano ya mitume na ibada.
Mafuatano Ya Mitume
30
Ilidaiwa kwamba maaskofu walikuwa badala ya mitume. Kwa namna fulani uaskofu
ulitokana na mitume, yaani maaskofu waliwekwa na mitume kuwa watawala katika kanisa
na mamlaka ya utawala wao ilihusisha kuhubiri na kuitetea Injili.
Umoja Wa Ibada
Ibada mbalimbali zilizokuwa zikifanywa na kanisa kwa pamoja zilisaidia kukuza umoja wa
kanisa na kutokea kwa viongozi wenye mamlaka. Kulikuwa na ibada mbalimbali ambazo
zilifanywa na kanisa, baadhi ya ibada hizo ni ibada ya ubatizo na ibada ya meza ya
Bwana. Pia kanisa liliadhimisha sikukuu mbalimbali ambazo pia kwa namna fulani
zilichangia kukuza umoja wa kanisa.
H. MABISHANO YA KITHIOLOJIA.
Mabishano ya kitheolojia yalikuwa ni majadiliano ya mafundisho na mitazamo mbalimbali
ya kitheolojia na kiuongozi iliyokuwa ikiibuliwa na baadhi ya viongozi wa kanisa.
Kutokana na kutofautiana mitazamo juu ya hoja Fulani za kitheolojia mababa wa kanisa
walibishana na kuitisha mikutano ili kuweza kutoa suluhu juu ya tofauti hizo za
kimafundisho na kitheolojia. Kundi la walioshindwa katika mikutano hiyo lilihukumiwa na
kuitwa wazushi na kisha kutengwa na kanisa.
Mabishano ya kithiolojia yalisababishwa na mitazamo mbalimbali ambayo wakristo
walikuwa nayo juu ya Yesu Kristo. Baadhi ya mitazamo hiyo ni .
Uungu wa Yesu Kristo.
Wakristo wa awali walimpa Yesu heshima kwa kumwita majina mbalimbali kama vile
Masihi, Kurios, Kritos na Logos.
Jina la Logosi lilitokana na falsafa za kigiriki, Kutokana na falsafa hizo Logos ilikuwa ni
njia ya Mungu kufanyika mwili na kukaa na watu hapa duniani. Hivyo wakristo wa awali
walimtambua Yesu kama Mungu.
Kristo kama Logosi.
Katika kipindi cha karne ya pili na ya tatu karibu wanazuoni wote wa kikiristo
walifundisha kwamba Kristo alikuwa ni Logos. Kulikuwa na mwanazuoni moja aliyeitwa
Yustini Shahidi ambae aliweka mkazo kuwa Logos alikuwa ni Mungu wa pili.
Wanazuoni wengine waliweka mkazo katika umoja wa Yesu.Walikubali kwamba Logos
amefanyika kuwa mwili katika Yesu Kristo lakini alikuwa ni Mungu halisi, Mungu
mwana ndiye aliyefanyika mwili, si Mungu wa pili. Kulingana na mtazamo waYustini ni
dhahiri kwamba alikana ubinadamu wa Yesu. Yesu kama Logos alikuwa Kweli Mungu
na mwanadamu kweli.
Monarchianism. Dhana ya Mungu mmoja.
Kulikuwa na wanazuoni wengine waliopinga mafundisho ya kumhusisha Yesu na Logos
kwa sababu jambo hili lilielekea kupinga imani yakuwa Mungu ni mmoja. Wanazuoni
31
hao waliona kwamba dhana ya utatu wa Mungu ilielekea kuwa ni uzushi wa kuwa na
miumngu mingi.
Wamonarchianism waligawanyika katika makundi mawili ambayo ni;
1. Wamonarchianism wa kimabadiliko, hawa walikuwa na mtazamo wenye kumwona
Yesu kama mwanadamu pekee tu, ambae hakuwa Mungu aliyefanyika mwili. Kundi hili
liliongozwa na Askofu Paulo Samosota wa Antiokia.
2. Wamonarchianism wa kimfano. Hawa waliona kuwa hakuna tofauti kati ya baba na
mwana. Baba ndiye aliyevaa mwili. Kwa hiyo majina haya baba, mwana na Roho
mtakatifu yalitumika kuonesha kwetu njia au hali tatu Mungu alizotumia
kujidhihirisha. Hivyo hakuna nafsi tatu bali ni nafsi moja. Kundi hili liliongozwa na
Sabelio.
Baada ya mateso kukoma katika kanisa kulitokea mgogoro mwingine ndani ya kanisa
uliohusisha mgongano wa kimafundisho (doctrinal controversals).
Baadhi ya viongozi wa kanisa walianza kuibuka na mafundisho yaliyoonekana kuwa
mageni katika kanisa na hivyo walihukumiwa uzushi na kutengwa na kanisa.
Wakristo walitumia muda mwingi kujadiliana wao kwa wao badala ya kuipeleka
Injili mbele. Katika moduli hii tutajadili badhi tu ya mabishano ya kithiolojia yaliyotokea
ndani ya kanisa.
1. Mabishano Baina Ya Mchungaji Ario Na Askofu Alexander.
Ario alimshutumu askofu wake kuwa alikuwa anaweka mkazo sana juu ya uungu wa Yesu
katika mafundisho yake. Alexander alifundisha kwamba mwana ni wa milele sawa na
baba. Ario alipinga fundisho hilo yeye alidai kwamba baba ni wa milele lakini mwana
alikuwa na mwanzo wake. Kuna kipindi ambapo mwana hakuwapo. Askofu Alexander
aliitisha mkutano wa sinodi huko Iskanderia ili kujadili suala hilo na hatimae Ario
alitangazwa kuwa mzushi na alitengwa na kanisa.
Ario aliungana na Askofu Euzebio wa Nikomedia na wakaandika nyaraka mbalimbli
ambazo zilitetea fundisho lao na wakazisambaza maeneo mbalimbali ili ziendelee
kusomwa na wakristo mbalimbali.
Mkutano Wa Naikea.
Baada ya nyaraka hizo kusomwa majadiliano miongoni wa viongozi wa kanisa yalipamba
moto na kuleta mgawanyiko ndani ya kanisa. Mfalme Kostantino hakupendezwa na
mgogoro huo ulioleta mgawanyiko miongoni mwa wakristo hivyo aliwaomba viongozi hao
wapatane na iliposhindikana kupatana kwa viongozi hao, mfalme akitumia nguvu ya dola
aliamua kuitisha mkutano wa viongozi wote wa kanisa toka sehemu mbalimbali ili aweze
kuwapatanisha. Mkutano huo ulifanyika mwaka 325BK katika mji wa Naikea na
kutambulikana kama mkutano wa kwanza wa kanisa zima, kwa sababu ulihusisha viongozi
mbalimbali toka sehehemu mbalimbali.
Katika mkutano huo Askofu alexender alishinda kwa hoja na hatimae Ario alitangazwa
kuwa mzushi na akatengwa na kanisa. Katika kipindi hiki kanisa lilitunga ukiri wa imani
32
ambao ulipaswa kutumiwa na makanisa yote. Ukiri huo uliweka mkazo katika uungu wa
Yesu kuwa Yesu ni sawa na baba.
Mkutano wa Naikea haukuweza kumaliza majadiliano na badala yake uliyachochea
kwani majadiliano hayo yaliendelea kwa muda wa miaka 35 baada ya mkutano wa Naikea.
Baadhi ya viongozi wa kanisa walitilia mashaka ukiri wa Naikea kwasababu hawakuuzoea.
Mkutano Wa Kostantinopali
Kutokana na majadiliano hayo ya muda mrefu na makali kulikuwepo na haja ya kuitisha
mkutano mwingine wa kanisa zima. Mkutano hu uliitishwa katika mji wa Kostantinopali
mnamo mwaka wa 381 BK. Katika mkutano huu walifanya marekebisho kidogo ya
ukiri wa imani wa Naikea.
Mkutano Wa Efeso. (Mabishano kati ya Sirilo na Nestori)
Baada ya Apolinari kuhukumiwa uzushi, kuliendelea mabishano makali katika kanisa.
Baadhi ya mabishano hayo yalikuwa baina ya askofu Sirilo wa Iskandelia na askofu
Nestori wa Kostantinopali.
Sirio alipinga fundisho la Apolinari. Aliona kwamba uungu na ubinadamu wa Yesu
kuwa ni hali mbili zisizoweza kutenganishwa . Alipokuwa anataka kueleza uungu wa
Yesu alianza kwa kumwita bikira Maria ‘Theotokos’ yaani mama wa Mungu.
Askofu Nestori alibaini uzushi katika maelezo ya Sirilo, yeye alipendekeza Mariamu aitwe
mama wa Kristo. Maaskofu hao walishambuliana vikali sana kwa maandishi. Shauli hilo
lilipelekwa kwa askofu wa Rumi ili aweze kutoa uamuzi. Askofu wa Rumi alimpa ushindi
Sirilo na kumtangaza Nestori kuwa mzushi.Hayo yalifanyika katika mkutano wa tatu wa
kanisa uliofanyika katika mji wa Efeso mnamo mwaka 433 BK.
2. Majadiliano Ya Apolinari.
Apolinari alikuwa ni askofu wa Laodikia. Askofu huyu alijaribu kueleza uhusiano uliopo
baina ya hali mbili tofauti alizo nazo Yesu. Yaani hali ya uungu na hali ya ubinadamu.
Yeye alikuwa na mtazamo wa kwamba mwili wa Yesu ni ubinadamu na akili na roho
yake ni Logosi aliyefanyika mwili. Katika kueleza fundisho hilo askofu huyu alikaza
uugu wa Yesu uliokana ubinadamu wake. Kutokana na fundisho hili Apolinari
alitangazwa kuwa mzushi katika mkutano wa Kostantinopali mnamo mwaka 381BK.
3. Mabishano Ya Pelegio.
Pelegio alikuwa ni mmonaki, mwingereza aliyekuja Afrika Kaskazini kwajili ya kuhubiri
Neno la Mungu katika kanisa la Afrika ya Kaskazini.
Peregio alifundisha kwamba mtu harithi dhambi toka kwa Adamu, lakini kila mtu ni
lazima afanye uchaguzi yeye mwenyewe.
Pelegio alipingwa vikali na Agustino mkuu kwa mafundisho yake. Agustino alifundisha
kwamba Adamu alipotenda dhambi alikiwakilisha kizazi chote cha binadamu na
33
kwamba mtu hawezi kuokolewa kwa uchaguzi wake mwenyewe, bali ni kwa mapenzi ya
Mungu na kwamba neema ya Mungu haiwezi kukataliwa na wanadamu.
Mafundisho ya pelegio yalipingwa vikali na kanisa na kuonekana ni uzushi. Kanisa
lilikubali mafundisho ya Agustino mkuu ambayo pia yalijengewa hoja na
wanamatengenzo ya kanisa katika kipindi cha matengenezo katika karne ya 16 1
I. KUZUKA KWA UMONAKI.
Utawa au umonaki ulianza katika karne ya tatu BK. Kabla ya kipindi hicho wakristo
waliishi katika jamii na familia. Mara baada ya ukristo kushamiri mambo ya dunia yalianza
kuingia kanisani, baadhi ya wacha Mungu hawakuridhika na hali hiyo hivyo waliamua
kujitenga na kukaa peke yao nje ya mji katika mapango au katika nyumba walizokuwa
wamejenga. Nyumba hizo zilijulikana kama nyumba za watawa maarufu kama Monastery.
Baadhi ya mambo yaliyochochea kuanzishwa kwa utawa ni
i. Mvuto wa Injili, Injili ya Yesu alipomwambia Yule kijana tajiri kuuza kila kitu na
kuwapa maskini kasha kumfuata Yesu.
ii. Maovu kukithirikatika kanisa. Kutokana na mmonyoko wa maadili na kuhalalishwa
kwa dhambi ndani ya kanisa.s
iii. Falsafa ya uovu wa mwili. Imani ya kuwa mwili ni muovu na hivyo unapaswa
kuteswa vikali ili kuudhibiti.
Kutokana na mikazo juu ya mambo yaliyotajwa hapo juu, kulikuwa na watu ambao
waliuza kila kitu walichokuwanacho wakawagawia maskini na kisha wakajitenga na
kuamua kuishi maisha ya kimasikini mbali na jamii yao. Baadhi ya watu hao ni;
Antoni Mtawa Wa Kwanza.
Mtu huyu alikuwa ni mwenyeji wa Misri na ndiye mwanzilishi wa utawa. Antoni aliuza
kila kitu alichokuwa nacho na kuwagawia maskini mali zake na kisha akaishi nje ya mji
akilima na kuwapatia maskini chakula alicholima. Baada ya muda alijitenga na kuishi
peke yake pangoni mlimani. Watu mbalimbali walimwendea huko pangoni ili kujifunza na
kisha alifanikiwa kupata wafuasi ambao nao waliamua kuungana nae kuishi maisha ya
utawa. Alipat wafuasi karibuni 2000
Pokomeo Mwanzilishi Wa Nyumba Za Utawa.
Huyu alikuwa mdogo wa Antoni na ndie aliyeanzisha nyumba za utawa. Yeye alijenga
boma kubwa ambalo wafuasi wake waliishi ndani wakijitenga na mambo ya ulimwengu.
Watawa hawa walijishughulisha na ibada na kazi, utawa huu ulikaza ushirika na
ulipendwa na watu wengi.
Jerome (Hironimo)
34
Utawa ulienea sana sehemu ya magharibi kwa njia ya Jerome. Mtu huyu alikuwa na uwezo
mkubwa wa kufasiri Maandiko na alifanywa kuwa katibu wa Papa wa Rumi kwa kipindi
kirefu. Aliishi maisha ya kujikana. Alisema “ Mtu asieoa hujipatia sifa ya pekee mbele ya
Mungu. Alikiri kwa wazi kabisa kwamba “ Maisha ya utawa hayawezi kuondoa majaribu
yote” Alidai kwamba alipokaa katika boma la utawa huko mlimani bado aliwaza juu ya
wasichana wa Rumi.
Jerome alikuwa fundi wa Maandiko na elimu. Alitafsiri Biblia kwa lugha ya Kilatini
iliyojulikana kwa jina la Vulgate. Tafsiri inayopendwa sana na wakatoliki wa Rumi mpaka
sasa.
Yeye alishirikiana na wanawake watawa kutunza yatima Huko Bethrehemu na Palestina.
Walikuwa na nyumba mbili za watawa, moja ikiwa ya watawa wa kiume na nyingine ya
watawa wa kike.
Benedikto Mwanzilishi wa Kanuni Za Utawa.
Benedikto wa Nusia alianzisha shirika la utawa huko Monte Kasino Italia. Yeye aliweka
mkazo katika umoja. Aliweka uongozi uliosimamia nyumba zote za utawa. Aliona kuwa
kila nyumba ya utawa ni jeshi la Yesu waliotayari kumtumikia wakati wowote.
Kiongozi wa kila nyumba ya utawa aliitwa Aboot, na watawa wote walipaswa kumtii.
Aliweka mpangilio mzuri wa saa za ibada, sala na kusoma. Nyumba za kanuni za
Benedikto zilikuwa mahali pakuu pa elimu na kilimo.
Umonaki katika nchi za Ulaya
Umonaki uienea taratibu katika nchi za Ulaya ikilinganishwa na Afrika na Asia. Badala ya
kila mtu kuishi peke yake, umonaki wa ulaya ulipangiliwa na kusimamiwa vizuri. Kazi na
sala ziliunganishwa pamoja.
Faida Za Utawa.
1. Ulifanyika kuwa vituo vya wakimbizi.
2. Walitoa msaada kwa watu wenye mahitaji , mfano kusaidia maskini na wasiojiweza.
3. Walileta mchango mkubwa katika kuinua kilimo.
4. Walikuza elimu kwani watawa walitumia muda mwingi katika kusoma na kuandika
maandiko mbalimbali.
5. Walipeleka wamishenari katika mataifa mbalimbali kueneza Injili.
6. Walitoa viongozi bora katika jamii na katika kanisa.
7. Walitafsiri Maandiko katika lugha mbalimbali.
Madhaifu Ya Utawa.
1. Mkazo wa juu ya kuishi maisha ya useja.waliwakataza wafuasi wao wasioe wala
kuolewa.
2. Walikuwa omba omba kwa watu waliowatembelea
35
3. Upendeleo na anasa. Baada ya utawa kupata umaarufu, walianza kuishi maisha ya
anasa na kukwepa kulipa kodi.
4. Utawa haukuwa na msingi ki-Biblia
5. Watawa waliielewa visivyo Injili ya Yesu kristo waliyoitumia kuhalalisha utawa.
J. KUANGUKA KWA DOLA YA RUMI
Mfalme Kostantino mara baada ya kuingia katika utawala alihamishia makao makuu ya
dola ya Rumi katika mji wa Kostantinopali. Tutatazama namna Rumi ilivyokuwa makao
makuu ya kanisa. Wakati kanisa la Orthodox la mashariki lilikuwa likitawaliwa na serikali,
Patriaki wa Rumi alidai kuwa na mamlaka katika kanisa lote la ulimwengu wa magharibi,
ambao ulikuwa kupitia kanisa la Katoliki la Rumi. Hii iliwezekana kwa sababu kadhaa,
badhi zikiwa ni;
Kufanana kiutawala. Kulikuwa na mazoea kuongoza kanisa kwa mfumo wa kiserikali
ambapo kunakuwa na kiongozi mkuu mmoja anaetakiwa kusikilizwa . wakati huu
kulikuwa na maaskofu karibu kila mji, ambao katika miji mikubwa waliitwa Patriaki
(patriarch) yaani baba mkubwa. Kulikuwa na mapatriaki katika miji ya Yerusalemu,
Antiokia, Iskanderia, Rumi na Kostantinopali.
Kulikuwa na mashindano ya kugombea ukuu miongoni mwa mapatriaki. Swali lilikuwa
nani angekuwa kiongozi mkuu wa kanisa lote ulimwenguni. Rumi ikiwa imetengeneza njia
ya kuwa makao makuu ya kanisa ilikuwa na viongozi bora.
Kwa muda mrefu kanisa la Rumi lilikuwa imara. Lilisimama kidete kupinga mafundisho
potofu. Kanisa la Rumi liliihudumia Jamii kiroho na kimwili kwa kuanzisha kazi za kijamii
dunia nzima. Nyumba za utawa, shule na hospitali zilianzishwa katika maeneo
mbalimbali, jambo hili lililipa umaarufu kanisa la Rumi. Wamishenari walitumwa katika
ulimwengu mzima wa wakati ule kueneza Neno la Mungu.
Wakati nguvu ya kanisa ilikuwa inakua, nguvu ya dola iliendelea kuzorota, nguvu ya
kisiasa ya Rumi ilizidi kuporomoka.
Kwa muda mrefu wa utawala wake dola ya Rumi ilikuwa imetajirika sana. Maadui zake
waliokuwa wanaishi jirani nae waliutamani utajiri wake. Maadui hao waliivamia Rumi
ambayo sasa haikuwa na uzoefu wa kivita. Baadhi ya maadui walioivamia Rumi na
kuishambulia ni wavisigothi, wasaksoni, wavandali, , wahuni, wabarigandiana na
wafranka. Uvamizi wa mataifa haya ulipunguza nguvu ya dola ya Rumi.
Janga lingine lilikuwa ni vita ya wenyewe kwa wenyewe, baina ya wanachama wa seneti
kugombania kiti cha utawala. Kabila la kijerumani lililojulikana kama Herulisi liliivamia
na kuishinda dola ya Rumi mnamo mwaka 476 BK.
36
MADA YA TANO
KIPINDI CHA THIATIRA; KANISA LA NYAKATI ZA GIZA.
KIPINDI. Tangu kuanguka kwa dola ya Rumi hadi kuanguka kwa Kostantinopali.
A. UTANGULIZI
37
Katika kipindi cha Pergamo tuliona jinsi Patriaki wa Rumi alivyochukua mamlaka ya
uongozi wa kanisa na kuinuka kwa Rumi kuwa makao makuu ya kanisa. Tuliona jinsi
mafundisho potofu pamoja mambo ya kipagani yalivyoingia kanisani
Haikutosha kwa Patriaki wa Rumi kuwa Askofu mkuu wa kanisa lote duniani na kuwa na
mji wa Rumi kama makao makuu ya kanisa lote duniani, baada ya hapo alijitangaza kuwa
kiongozi wa mataifa kwa njia ya kukuza upapa katika karne kumi za kipindi cha giza.
Kipindi cha giza kilikuwa na hatua tatu ambazo ni, kukua, kusitawi na kuanguka.
1. Kukua.
Gregori I alipokuwa kijana aliteuliwa kuwa msimamizi wa majengo na vyakula katika Mji
wa Rumi. Baada ya kifo cha baba yake aliamua kutoa kwa kanisa mirathi ya babaye.
Mnamo mwaka 578 BK Gregori I aliteuliwa na papa kuwa balozi wake katika mji wa
Kostantinopali. Mwaka 585 hadi 590 BK alikuwa msaidizi wa papa huko Rumi na
kiongozi mkuu wa Monastery(nyumba za utawa). Baada ya papa Pelegio II kufariki dunia
kwa ugonjwa wa tauni mwaka 590 BK, Grogori I aliteuliwa na umati wa watu huko Rumi
kuwa Askofu badala ya Peregio II.
Kukua kwa nguvu ya upapa kulianza baada ya Gregori I kushika wadhifa wa upapa
katika mwaka wa 590 BK. Mfumo wa kubadilisha majina mtu alipokuwa anaingia
katika nafasi ya upapa ulianza katika kipindi hiki. Gregori aliitwa mkuu kwa sababu ya
mafanikio yake ambayo baadhi ni,
i. Alitumia uwezo wa kikanisa katika kuwasaidia watu, (kuwapa chakula na nguo).
ii. Serikali ilipolega aliimarisha ulinzi katika mji wa Rumi.
iii. Alimtambua papa wa Rumi kuwa na mamlaka juu ya viongozi wengine wote wa
kanisa.
iv. Alilipatia kanisa nguvu ya kisiasa na kidini.
v. Alitengeneza dogma ya kanisa.
vi. Kutokana na misaada ya kijamii iliyokuwa ikitolewa na papa Gregori I wananchi wa
Rumi walianza kumheshimu na kumhesabu kama kiongozi wao. Hivyo basi Gregori
Mkuu aliimarisha nguvu ya upapa katika mambo ya kidini na kisiasa pia.
Sababu za kukua kwa upapa
Mbali na mchango wa Gregori Mkuu katika kukuza nguvu ya upapa kulikuwa mambo
mengine kadhaa yaliyopelekea kukua kwa upapa katika kipindi hiki. Baadhi ya sababu
hizo ni:
1. Nguvu ya haki, kanisa liliwatetea raia dhidi ya watawala dhalimu hivyo likapendwa na
watu wengi.
Kuzolota kwa serikali, Wakati serikali inazolota kanisa lilizidi kujiimarisha, kiuchumi na
kijeshi hivyo viongozi dhaifu walihitaji msaada wa kanisa katika kupambana na adui zao
hivyo kanisa likazidi kuwa na mamlaka na nguvu ya ushawishi.
2. Ulaghai, Kanisa lilitumia kigezo cha ujinga wa watu kujipatia mamlaka. Kanisa
lilitengeneza nyaraka mbalimbali zenye kulipa mamlaka ya kiutawala na kudai kwamba
38
nyaraka hizo ziliandikwa na wahusika walioandikwa kumbe sivyo. Zifuatazo ni baadhi ya
nyaraka hizo
Waraka wa mfalme Kostantino kwa askofu Silvesta (314-335 BK). Huu ulikuwa ni waraka
uliogushiwa na viongozi wa kanisa kwamba uliandikwa na Kostantino kumpa askofu wa
Rumi (Silvesta) mamlaka ya kiutawala juu ya wafalme wote wa Ulaya na Ulaya nzima.
Tamko la uongo la Isodore(850 BK). Kulikuwa na maandiko yaliyokuwa yanadai
kwamba askofu wa Rumi alikuwa amepokea waraka toka kwa mitume uliokuwa
unamtangaza askofu wa Rumi kuwa askofu wa kanisa dunia nzima na kwamba kanisa
lilitangazwa kuwa huru (yaani kanisa kutokuwa chini ya serikali).
2 KUSITAWI KWA UPAPA (1073- 1216 )
Nguvu ya upapa ilifikia kilele chake katika utawala wa Gegori VII ambaye pia alijulikana
kama Hildebrand. Katika kipindi hiki upapa ulikuwa na nguvu kamili kikanisa na
kiserikali katika mataifa yote ya kule Ulaya.
i. Papa Gregori VII alifanya matengenezo ya ukreli na kukataza ndoa kwa wakreli.
ii. Aliliondoa kanisa chini ya utawala wa serikali, kanisa likaanza kujitawala, alifuta suala
la maaskofu kuteuliwa na watawala wa serikali (wafalme).
iii. Alilifanya kanisa kuwa juu ya selikali.
Papa Innocent III (1198 -1216).
Huyu alikuwa ni papa mwingine mwenye nguvu kubwa. Katika siku yake ya kutawazwa
kuwa papa alitoa usemi wenye maneno yafuatayo.
“ Mahalifa wa mtakatifu Petro wako katikati ya Mungu na watu; wadogo kuliko
Mungu lakini wakubwa kuliko watu, wenye uwezo wa kuwahukumu watu wote lakini
wasioweza kuhukumiwa na yeyote”
Katika barua yake ya kiofisi aliandika
“ papa hajapewa mamlaka kwa kanisa pekee bali kwa ulimwengu mzima. Akiwa na
haki ya kuwaondoa na kuwaweka watawala katika uongozi”
Papa innocent III alijitwalia mamlaka ya serikali ya mji wa Rumi akijifanya yeye
mwenyewe kuwa bwana kwa kuanzisha nchi ndani ya nchi ijulikanayo kama nchi ya
Vatikani. Hivyo papa akawa kiongozi wa kidini na kiserikali.
3 KUANGUKA KWA UPAPA.
Kuanguka kwa upapa kulianza wakati wa papa Bonifasi VIII katika mwaka 1303. Jambo
hili lilisababishwa na kuanza kuibuka kwa roho ya utaifa miongoni mwa nchi mbalimbali.
Jambo hili lilileta mtikisiko dhidi ya Bonifasi VIII. Watu walianza kuwaheshimu viongozi
wa nchi zao kuliko kumheshimu papa. Amri na maagizo mbalimbali ya papa yalipuuzwa
na viongozi wa nchi. Baada ya mfalme wa ufaransa kukata kutii maagizo ya papa, papa
39
Alianzisha vita na mfalme wa ufaransa na hatimae Bonifasi VII akashindwa vita hiyo na
kuwekwa kizuizini mpaka mauti ilipomfika.
B. KUINUKA KWA UISLAMU
Kanisa lilipata mashambulizi makuu katika karne ya saba kutoka kwa waislamu. Dini ya
Uislamu ilianzishwa na kijana mmoja aliyeitwa Mohamed. Kijana huyo alizaliwa mnamo
mwaka 570 BK katika mji wa Maka. Alianza kazi yake kama nabii na mwana
matengenezo kwa kuanzisha dini yake mnamo mwak 610 BK katika mji aliozaliwa.
Kutokana na kutokukubaliwa na watu wa mji huo aliamua kuhamia katika mji wa Madina
katika mwaka wa 622 BK. Kipindi hicho kinaitwa Hajira. Kalenda ya Waislamu inaanza
wakati huo wa kuhama kwa Mohamed toka Maka kwenda Madina.
Ndani ya kipndi cha miaka miambili waislamu walikuwa wameisha zishinda sehemu
mbalimbali za dunia na kuanzisha dini yao ya uislamu, Uanzishaji wa dini hiyo ulienda
sambamba na uanzishaji wa dola ya Kiislamu katika maeneo yoyote waliyoyashinda.
Baadhi ya maeneo waliyokuwa wameyashinda na kuanzisha utawala wao ni nchi za
Mashariki ya kati, Afrika ya Kaskazini na Asia ndogo. Mohamedi na wafuasi wake
walieneza dini yao kwa kutumia upanga, mahali popote watu walipokataa kuipokea dini
hiyo walilazimika kutumia vita na nguvu ya kijeshi.
Maeneo yoyote waliyofanikiwa kuyateka hatua ya kwanza ilikuwa ni kufuta dini zingine
zote zilizokuwa maeneo hayo na kuwalazimisha raia wote kujiunga na dini hiyo.
Kuinuka kwa dini ya Uislamu kulichangia katika kuanguka kwa upapa na kuzoofisha
nguvu ya kanisa kwa ujumla. Kwa mfano Afrika kaskazini kanisa lilidhoofika na hatimae
likafifia kabisa.
C. KUTENGANA KWA KANISA KATOLIKI.
Kanisa la katoliki la mashariki na lile la magharibi yalitengana rasmi mwaka 1054 BK,
japokuwa kihuduma yalitengana tangu zamani. Daima kulikuwa na kushindania madaraka
ya kwamba ni nani aliyekuwa mkuu kati ya papa wa Rumi na Patriaki wa Kostantinopali.
Hatimae katika mwaka 1054 BK makanisa haya yalitengana ramsi.
SABABU ZA KUTENGANA
Kutofautiana kimafundisho, Kuhusu asili ya Roho mtakatifu. Kanisa la magharibi lilidai
kwamba Roho mtakatifu alitoka kwa baba na kwa mwana wakati lile la mashariki lilidai
kwamba Roho mtkatifu alitoka kwa baba pekee.
Ndoa kwa makuhani. Kanisa la magharibi lilikataza makuhani kuoa wakati kanisa la
mashariki liliruhusu makuhani kuoa.
Sababu ya kisiasa, Baada ya kuanguka kwa dola ya Rumi mataifa ya magharibi yalitaka
kuwa chini ya Kostantinopali.
Kuabudu sanamu. Kanisa la magharibi lilianzisha matumizi ya sanamu katika ibada
wakati kanisa la mashariki lilipinga matumizi ya sanamu.
40
Kugombea ukuu, Madai ya kanisa la mashariki ya kuwa ni kanisa la kitawala.
D. KUSITAWI KWA UTAWA.
Mashirika mbalimbali ya kitawa yalisitawi katika kipindi hiki na yakajitolea kusaidia jamii
katika maeneo mbalimbali. Baadhi ya mashrika hayo ni :
Wabenedectino walianza mwaka 529 BK
Wasisteri mwaka 1098.
Wafransiska mwaka 1209.
Wadomenica mwaka 1215.
Kipindi cha karne za katikati kilichangia sana katika ustaarabu wa ulimwengu, hasa katika
mambo ya elimu, maandiko, na mambo ya ufundi, katika kipindi hiki zilijengwa kathedro
kubwa . kuna baadhi ya vyuo vikuu vikubwa vilivyojengwa wakati huu, mfano wa vyuo
vikuu hivyo ni Chuo kikuu cha Parisi huko Ufarasnsa, Chuo Kikuu cha Kambridge,
Chuo Kikuu cha Oxford, na vyote viwili vikiwa huko Uingereza. Kuanzishwa kwa vyuo
vikuu hivi kulipelekea elimu kukua na kuleta mtazamo mpya katika jamii kama
tutakavyoangalia baadae katika kipindi kitakachofuata.
E. WATANGULIZI WA MATENGENEZO YA KANISA.
Katika mwaka wa 1229 kanisa la Rumi lilikataza waumini wa kawaida wasisiome Biblia
isipokuwa makuhani tu. Lugha ya kilatini iliteuliwa kuwa lugha takatifu na hivyo mtu
yeyote asiyejua kilatini alizuiliwa kuhubiri.
1. PITA WALDO.
Katika miaka ya 1170 alitokea mfanya biashara mmoja aliyeitwa Pita waldo mwenyeji
wa Loyona Ufaransa. Mtu huyu alipenda kujua mambo yaliyo katka Biblia lakini
hakuweza kwa sababu hakufahamu kilatini hivyo aliwaajiri mapadri wawili wamtafsirie
Biblia katika lugha ya kifaransa. Baada ya kusoma neno la Mungu alivutiwa nalo sana
hivyo akauza kila kitu alichokuwa nacho na akala kiapo cha umaskini, akajitoa kikamilifu
kuhubiri neno la Mungu.
Pita Waldo Alianzisha timu iliyoitwa watu maskini. walianza kuhubiri, lakni walipingwa
na papa. Mwaka 1184 walijitenga na kanisa kwa sababu hawakukubali kitendo cha wao
kuzuiwa kuhubiri,
Waldo alipinga baadhi ya mafundisho ya kanisa Katoliki. Baadhi ya mambo aliyoyapinga
ni
Mafundisho kuhusu toharani,
Misa kwaajili ya wafu
Kumwabudu Mariamu mama wa Yesu.
Kanisa kuwa na mamlaka juu ya Biblia
Kuifanya lugha ya kilatini kuwa lugha takatifu
41
Watu hawa waliamini kwamba kila mtu alitakiwa kuwa na Biblia katika lugha yake ya asili
na ya kwamba Biblia ilitakiwa kuwa mamlaka ya mwisho na iliyokuu katika mambo
ya imani na maisha. Kanisa lilianzisha mateso dhidi ya wawadeni yaani wafuasi wa
Waldo.Watu hawa Kadili walivyoteswa ndivyo walivyokuwa wakiongozeka. Mnamo
mwaka 1211 wawadeni 80 walichomwa moto huko Ujerumani. Pita waldo alisaidia kuleta
matengenezo ya kanisa kwani alisaidia kupatikana kwa Biblia katika Lugha zingine na
kuhamasisha kila mtu kusoma Biblia. Waldo anajulikan kama mmoja wa wanamatengezo
ya kanisa watangulizi.
2. JOHN WIKRIF
Huyu alikuwa mwalimu wa Chuo kikuu cha Oxford. Mnamo mwaka 1378 Wikrif alitaka
kuleta matengenezo katika kanisa kwa kuwaondoa watumishi wa kanisa waliokuwa
dhalimu,na kuwanyang’anya mali ambazo aliamini kwamba ndizo zilizokuwa chanzo cha
watumishi hao kuwa dhalimu. Alichapisha andiko lililoeleza maadili wanayotakiwa
kuwa nayo watumishi wa kanisa.
Alifundisha kwamba wakati viongozi wa kanisa wanapokuwa mafisadi serikali ilitakiwa
kuchukua mali zao na kuwapa watu wengine wenye nia ya kumtumikia Mungu. Katika
mwaka wa 1379 alianza kupinga dogma ya kanisa kwa kutoa madai yafuatayo;
Yesu pekee ndiye aliyekuwa kiongozi mkuu wa kanisa na si papa.
Biblia pekee ndio yenye mamlaka kuu na ya mwisho kwa waamini na si kanisa wala
papa.
Kanisa lilitakiwa kuiga mfano wa kanisa la agano jipya.
Kwa msaada wa tajiri Lord Cobham John Wikrif alitafsiri Biblia katika lugha ya
kiingereza na kuisambaza katika maeneo mbalimbali . Alianzisha chama cha Wahubiri
maskini na wakaanza kuzunguka katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo wakihubiri neno
la Mungu watu
Mwaka 1382 alipinga fundisho la mageuzo ya maumbo ya mwili na damu ya Yesu
linalojulikana kama transubstan-tiation. Mawazo yake yalipingwa vikali na kanisa na
serikali na akafukuzwa ukufunzi. Mwaka 1402 Bunge La Uingereza lilipitisha sheria ya
hukumu ya kifo kwa watu wanohubiri mafundisho kinyume na yale yaliyokubaliwa na
kanisa. Wahubiri maskini waliteswa vikali sana, baadhi walifungwa na kuchomwa moto
na kufukuzwa nchini. Viongozi wa kanisa walijaribu kuchoma moto Biblia zote za
Kiingereza. Wikrif alifariki mnamo mwaka 1384.
Shujaa huyu anakumbukwa sana katika historia ya kanisa kwa mchango wake wa kutafsiri
Biblia katika Lugha ya kiingereza. Wikrif ndiye mtu wa kwanza kutafsiri Biblia kwa lugha
ya kingereza.
3. JOHN HUS
Huyu alikuwa ni mkuu wa chuo kikuu cha Plague huko Bohemia, mtawa na padre wa
kanisa katoliki. Mwaka 1401 John Hus alipata upadrisho. Padre huyu alipendezwa na
42
maandiko ya John Wikrif na hivyo alianza kuhubiri mafundisho ya mtangulizi wake
Wikrif.
Alipinga mafundisho mbalimbali yasiyo ya ki-Biblia ya kanisa la Romani katoliki na
akasisitiza watu kuishi maisha matakatifu. Alisisitiza kwamba Biblia ndiyo mamlaka ya
mwisho kwa mwamini na katika huduma za kanisa.
Katika kitabu chake alichoandika juu ya kanisa, alifasili kwamba kanisa ni mwili wa
Kristo, na Yesu Kristo pekee akiwa kiongozi wake mkuu. Alitetea nafasi ya ukuhani na
kudai kwamba Mungu pekee ndiye aliyekuwa na uwezo wa kusamehe dhambi. Alieleza
kwamba hakuna mamlaka ya kanisa inayoruhusiwa kuanzisha mafundisho (doctrine)
yaliyo kinyume na Biblia na kwamba Waamini hawatakiwi kutii maagizo yasiyo ya
kimaandiko.
John Hus Alipinga baadhi ya mambo yafuatayo,
Udhalimu wa mapadre
kuuzwa kwa vyeti vya msamaha,
kuondolewa kikombe cha divai kwa walei.
Kanisa kuwa na mamlaka juu ya Biblia
Uwezo wa Makuhani kusamehe dhambi
Ukuhani wa wachache (crerism)
Baada ya mashambulizi hayo mazito dhidi ya mafundisho ya kanisa Hus alifukuzwa
upadre na akaambiwa abadilishe msimamo wake kwa kufuta kauli, jambo ambalo Hus
hakukubaliana nalo. Hatimae Hus alihukumiwa kifo na akachomwa moto. Hus akiwa
anachomwa moto alitoa unabii kwa kusema “leo mnaniua mimi lakini miaka miamoja
ijayo Mungu atamwinua mtu mwingine ambaye matengenezo yake hayataweza
kuzimwa” Kweli baada ya kipindi hicho Mungu alimwinua Martin Luther mwana
matengenezo mkuu kama tutakavyoona hapo baadae.
4. JEROME SAVANAROLA.
Alizaliwa Ferrara Italia mnamo mwaka 1452, alikuwa ni mtawa wa shiriki la wadominico.
Mtu huyu alijaribu kuleta matengenezo katika kanisa na serikali. Alipinga uovu uliokuwa
unafanywa na mapapa. Alisomea mambo ya ubinadamu na utabibu. Kufikia mwaka 1491
alikuwa mhubiri maarufu kule Frolence.
Alitabiri kwamba papa na mfalme wa Naples wangekufa siku moja, jambo ambalo
lilitokea kama alivyotabiri. Katika mahubiri yake alitabiri hukumu kubwa ambayo
ingekuja juu ya mji ikifuatiwa na kipindi chema ambapo Frolence ingewaunganisha watu
wote wa Itali. Utimilizo wa unabii huu ulionekana kuwa ni kuvamiwa kwa Itali na mfalme
Charles VIII. Ambaye mwaka 1494 aliuondoa utawala dhalimu wa Frolence.
Baada ya kuanzishwa kwa serikali mpya Saravano alipata umaarufu sana pale Frolence
kupitia mahubiri yake na alileta mabadiliko mengi katika jamii. Alianzisha matengenezo
ya kodi, Kusaidia maskini na matengenezo katika mahakama. Aliubadilisha mji kutoka
katika maisha ya kimwili na kuishi maisha ya kiroho.
Kutokana na mabadiliko hayo kila mtu katika mji alikwenda kanisani na matajiri waliwapa
misaada masikini.Wafanya biashara walirudisha vitu walivyokuwa wamewatapeli wateja
wao. Waimbaji waliacha kuimba nyimbo za kidunia na kuanza kuimba nyimbo za kumsifu
Mungu. Waliachana na maisha maovu, walichoma moto mawigi, vinyago, vitabu vya
43
kipagani, picha za ngono na kila kitu walichodhani kuwa ni kiovu. Hakika uamsho mkuu
ulitokea kama alivyokuwa ametabiri.
Jerome alitabiri kwamba angehubiri kwa miaka nane tu pale Florence na kisha angeuawa.
Katika mwaka 1498 Jerome alimshutumu papa Alexander VI kwa kutangaza hadharani
maovu aliyokuwa anayafanya yeye na wasaidizi wake. Baada ya mkasa huo Alexander VI
aliamua kumwekea vikwazo na kisha baadaye akamnyonga na kuuchoma moto mwili
wake mnamo mwaka huohuo wa 1498. Maneno yake ya mwisho akiwa anauawa alisema
“ Bwana Aliteseka sana kwaajili yangu”. Mapambano yake dhidi ya papa yalimfanya
kuwa shujaa na kuwa mtangulizi wa matengenezo ya kanisa. Alikuwa tayari kuitetea
imani kwa gharama yoyote.
Wanamatengenzo watangulizi walionyesha ushujaa katika kuitetea imani. Hawakukubali
kusalimu amri kwa uongozi wa kanisa au serikali na hawakuwa tayari kunyamaza kimya
na kuacha hali mbaya kuendelea kulitafuna kanisa, walikubali kulipa gharama katika
kuitetea imani na kupinga uovu. Walitengeneza njia ambayo ilifuatwa na
wanamatengenezo wakuu baadae kidogo katika kipindi cha kanisa la Sardi yaani kanisa la
matengezo.
Kuna mengi ambayo twaweza kujifunza kwa watu hao kutokana na vile kila mmoja
alivyosimamia kusudi lake kwa ujasiri na imani kuu. Kama tutajifunza na kutetea imani kama
wao tunaweza kuleta matengenezo katika kanisa vuguvugu la wakati huu wa mwisho
F. KUANGUKA KWA KOSTANTINOPALI.
Wanahistoria wengi wana tazama kuanguka kwa Kostantinopali kama mpaka wa kipindi
cha karne za katikati na nyakati hizi zetu. Waislamu toka Uturuki waliivamia
Kostantinopali na kuishinda mnamo mwaka 1453. Hekalu zuri liliojengwa na mfalme
Kostantino lililojulikana kama Saint Sophia liligeuzwa na kuwa msikiti. Huu ndio
uliokuwa mwisho wa kipindi cha giza au mediaval Period.
MADA YA SITA
KIPINDI CHA SARDI KANISA LA MATENGENEZO
KIPINDI : Tangu kuanguka kwa Kostantinopali hadi Patano la Amani la Westpharia.
A. SABABU ZA KUZUKA KWA MATENGENEZO YA KANISA.
Kitendo cha Kanisa la Rumi kutokuwa tayari kupokea mabadiliko yaliyokuwa
yanapendekezwa na watu wema kama vile, Wikrif na Hus, viongozi wa baraza la
44
matengenezo na mengine mengi kulipeleka kuanza kwa nguvu wimbi kubwa la
matengenezo.
Hadi kufikia miaka 1500 misingi ya jamii ya kipindi cha giza ilikuwa inabadilika
kutokana na mabadiliko ya kielimu, kisiasa, kidini na kiuchumi. Kanisa la ulimwengu
lilianza kupoteza nguvu na kanisa la kitaifa likaanza kuchukua nafasi
Kupanuka kijiografia kulileta mabadiliko mengi katika kufikiri. Kwa kifupi kulikuwa na
sababu mbalimbali zilizopelekea wimbi la matengenezo ya kanisa kutokea, baadhi ya
sababu hizo ni;
1. Kukua kwa utaifa(nationalism).
Kila nchi ilianza kuweka mkazo kujijenga yenyewe, hivyo nchi mbalimbali zilianza
kujitenga na ushirikiano wa kimataifa, Hii ilipelekea kanisa la ulimwengu kokosa nguvu
kwani utaifa ulisababisha kuanza kwa kanisa la kitaifa kila mahali.
Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.(Utumwa wa Babeli. Kugombania madaraka
yaupapa.)(Great Schism)
2. Kuvumbuliwa kwa mashine za uchapishaji.
Johann Guthenberg alivumbua mashine ya uchapaji mwaka 1456. Mpaka wakati huu
vitabu vyote viliandkwa na kunakiliwa kwa mkono. Kuvumbuliwa kwa mashine hii
kulisababisha Biblia na maandiko mengine kuchapwa na kusambazwa katika maeneo
mbalimbali. Kusambazwa kwa maandiko hayo kulipelekea kuamsha akili za watu na
kutambua hitaji la kuwepo kwa mabadiliko katika maeneo mbalimbali ikiwemo Kanisa.
3. Kuzuka kwa mwamko wa kujifunza. (Renaissence)
Hiki kilikuwa ni kipindi ambacho ulizuka mwamko mkubwa
wa kujifunza . Kipindi hiki kilianza huko Ulaya Italia karne ya 14 na kuendelea hadi
karne ya 17. Wasomi wengi waliibuka katika kipindi hiki. Watu walianza kufikiri mambo
kwa upya kutokana na elimu waliyokuwa wamepata. Kutokana na elimu hiyo watu
walihitaji mabadiliko katika maeneo mbalimbali ili kuweza kuleta maendeleo. Hivyo
kanisa nalo likajikuta linahitaji mabadiliko japo kuwa halikuwa tayari kwaajili ya
mabadiliko hayo. Tunaweza kufupisha sababu zilizopelekea matengenezo ya kanisa kwa
kuziorodhesha hapa chini kama ifuatavyo:-
Mgogoro wa kanisa katika karne ya 14 na 15.( Great Schism)
Rushwa.
Kanisa kutojali maisha ya kiroho ya watu na kujikita katika mambo ya kiuchumi.
Kuuzwa kwa vyeti vya msamaha
Upendeleo. (Mtu mmoja kuwa na vyeo vingi kwa wakati mmoja)
Mapapa kukosa maadili.
Mapadri kuwa na elimu duni.
Kuzuka kwa falsafa ya Mantiki.
45
B. VIONGOZI WA MATENGENEZO YA KANISA.
Katika kipengele hiki tutawatalii baadhi ya wanamatengenezo ya kanisa, yaani
tutawachunguza watu ambao Mungu aliwatumia kuleta kweli ya neno la Mungu katika
kanisa lililokuwa limepotoka na lisilokubali matengenezo kwa hiali. Tutawatalii
wanamatengenezo wafuatao, Martn Luther, John Calvin, Ulrich Zwingli na John
Knox.
1. ULRICH ZWINGLY
Alikuwa ni mwanamatengenezo wa kanisa wa kiswisi asiyejulikana sana kama Martn
Luther na John Calvin lakini aliye na mchango mkubwa katika mategenezo ya kanisa.
Alizaliwa mwaka 1484, na kuelimishwa katika Chuo kikuu cha Basel na Vienna
akisomea fani ya ubinadamu (humanism). Alifanya kazi kama Padre wa Parish Huko
Glarus Uswisi mwaka 1512. Katika mwaka wa 1515 Ulrich alianza kuyatilia shaka
mafundisho ya Kanisa Katoliki na alianzisha kile kilichoitwa matengenezo ya Zurich.
Alihubiri jumbe za ki-Biblia na kufanikiwa kulibadilisha baraza la mji kuwa na mtazamo
kama wa kwake.
Baraza hili liliufanya mji kuwa ngome ya Uprotestant. Hoja 67 za Zwingli
ziliasiliwa(adopted) na kufanywa Mafundisho rasmi ya mji na mji uliweza kubadilika kwa
haraka sana. Mahubiri na mafundisho yalifanywa mara kwa mara, sanamu ziliondolewa ,
mapadre waliruhusiwa kuoa, Watawa walihamasishwa kutoka katika makao yao
yaliyowatenga na jamii na kuja kuishi na jamii. Nyumba za kitawa zilivunjika na
wakatumia mali zao katika kufadhili elimu na misaada kwa maskini.
Mwaka 1525 Zwingly alijitenga na kanisa katoliki, na akaanzisha mlengo wake. Mnamo
mwaka 1450 baada ya kuongoka Zwingly alianza kuwakusanya wanafunzi waliopenda
kujifunza kigiriki, baadhi ya wanafunzi hawa waliongoka na wakavutiwa sana na Biblia.
Katika mdahalo wa mji uliofanyika katika ukumbi wa mji, Zwingly aliwasilisha hoja 67
Mnamo Februari1523 ambamo aliambatisha mamlaka ya Kanisa la Romani Katoliki.
Mamlaka ya papa, kuwabudu watakatifu, wokovu kwa matendo mema, mifungo, sikukuu,
hija, vikundi (order) vya watawa, useja kwa mapadre, Uuuzaji wa vyeti vya msamaha,
adhabu na toharani. Viongozi wa mji walivutiwa sana na hoja za Zwingli.
Katika mdahalo mwingine wa Oktoba 1523 Zwingli alishambulia matumizi ya sanamu na
akataka kuiondoa Krismas. Viongozi wa mji hawakukubaliana na jambo hili na hivyo
zwingly alikaa kimya. Zwingry aliwaogopa watawala. Kulitokea kutoridhishwa kwa
wanafunzi wake Zwinngry
Baadhi ya wanafunzi wake waliokuwa wamemsaidia katika kuhitimisha hoja zake zote
mbili walijisikia kwamba wamesalitiwa na Zwingli. Kwa kuacha kushughulikia swala la
Sakramenti, kwa kuwapendeza watawala. Walikuwa wamefundishwa na yeye mwenyewe
kufuata mafundisho ya Biblia hivyo wakatambua kwamba Zwingly hakuwa anawaongoza
katika mwelekeo sahihi. Hivyo wakaamua kuanza kujisimamia wenyewe.
Vijana hawa walikuwa ni Conrad Grebel na Felix Manz. Conrad alikuwa ni mwanazuoni
wa kigiriki na Felix alikuwa ni mwanazuoni wa kiebrania. Kwa pamoja vijana hawa
46
waliongoza kikundi cha watu katika kujifunza kikamilifu mafundisho ya Biblia juu ya
ubatizo.
Mwaka 1524 walihitimisha kwamba ubatizo usifanywe kwa watoto wadogo. Walifundisha
kwamba watu waliompokea Yesu kama Bwana na mwokozi wao ndio wanaostahili
kubatizwa. Pia walitengeneza mawazo mapya kuhusu kanisa wakiamini kwamba kanisa la
kweli lilikuwa linahusisha watu wale walibatizwa baada ya kukiri.
Vijana hawa walijaribu kumshawishi mlezi wao wa zamani akubaliane na mawazo haya,
kwa kiasi fulani Zwingli alikubaliana na mawazo haya, japo shauku yake ya kuwapendeza
watawala ilisababisha kuwakataa na kupinga mawazo ya hawa wanafunzi wake wa
zamani.
Katika mdahalo wa Januari 18-19 – 1525 vijana hawa walibishana na Zwingli kuhusu
suala la ubatizo wa watoto, Kiongozi wa mji alimtangaza Zwingly kuwa mshindi wa
mdahalo huo na akatangaza ya kwamba yeyote ambaye hangefanya ubatizo wa watoto
wadogo au angebatiza ubatizo wa waamini alitakiwa ama kutubu au kuondoka Zurich
ndani ya siku nane.
Kuanzishwa kwa kanisa huru la kwanza.
Katika nyumba ya Conrad Grebel walikusanyika watu wachache ili kujadili nini
walitakiwa kufanya. Baada ya majadiliano hayo walifikia uamuzi wa kwamba wanatakiwa
kubatizwa upya kwa kwa sababu wote walibatizwa wakiwa watoto katika kanisa Katoliki.
Conrad alimbatiza George Blaurock kwa sababu mtu huyu alikuwa ni padre. Hivyo baada
ya kubatizwa kwake alipewa jukumu la kuwabatiza wengine. Kwa sababu hii walianza
kuitwa wanabatisti, maana yake ikiwa ni wabatizwa upya.
Hii ilikuwa ni moja ya mapinduzi ya matengenezo. Mapinduzi haya yalianzisha kanisa
jipya. Watu hawa walianza kukutana kwaajili ya ibada na wakaanza kueneza kanisa lao
katika maeneo mbalimbali.Kikundi hiki pia kiliitwa undugu wa uswisi.
Baada ya mlengo huu kukua na kuenea, ulishambuliwa na kupingwa sana karibu katika
Ulaya nzima. Kanisa la Romani Katoliki, pamoja na wanamatengenezo yaani Martin
Luther pamoja na John Calvin walihusika katika kuwaua Wanabatisti. Zaidi ya wanabatisti
4000 walinyongwa.
Mnamo mwaka 1529 wanamatengenezo walikutana katika mji wa Marbag ili kuweza
kuimarisha umoja wao. Wanamatengezo hao walikubaliana katika mambo kadhaa, lakini
kulitokea kutokukubaliana katika jambo moja ambalo ni meza ya Bwana. Zwingli alisema
kwamba mkate na divai ni kielelezo tu cha ukumbusho wa mauti ya Yesu, wakati Luther
alikaza kwamba kwa namna fulani Yesu alikuwa katika mkate na divai kwa njia ya fumbo.
Jambo hili lilileta utengano mkubwa baina ya wanamatengenezo hawa.
Kulizuka vita baina ya Kanisa la Romani katoliki na Waprotestant, katika vita hiyo
Zwingly aliuawa, hii ilikuwa mwaka 1531.
2. MARTIN LUTHER.
Martin Luther alizaliwa mnamo mwaka 1483. Baba yake aliitwa Hans na mama yake
aliitwa magareth. Alizaliwa katika familia ya kimsikini, baba yake alikuwa mfanyakazi
katika mgodi wa madini. Martin Luther alisoma Theolojia katika vyuo vikuu vya Erfurt
na Edburg. Mnamo mwaka 1505 alitunukiwa shahada ya kwanza katika falsafa na katika
47
mwaka 15012 alipata shahada ya pili ya udaktari katika Theolojia. Baada ya masomo yake
alianza kufundisha Biblia katika Vyuo Vikuu vya Erfurt na Witternberg Mnamo mwaka
1507 alipata ubarikio na kuwa padre.
Mnamo mwaka 1510, Martin Luther na mmonaki mwingine mmoja walisafiri kwenda
Rumi kwaajili ya shughuli za Chama chao cha umonaki. Akiwa Rumi alishangaa kuona
udhalimu uliokuwa ukifanywa na mapdre huko Rumi. Martin akiwa mmonaki alipata
mabishano makubwa moyoni mwake, na alijiuliza namna gani ambavyo angeweza
kupata rehema za Mungu. Alijipiga, Alifunga na kujitesa kwa muda mrefu ili aweze
kusamehewa dhambi zake. Alipata majibu ya maswali yake yote baada ya kusoma Waraka
kwa Warumi 1:16-17. Ukiwa na maneno mwenye haki ataishi kwa imani.
Wakati huo huo papa Leo X aliwatuma wawakilishi wake katika nchi mbalimbali
kukusanya fedha kwajili ya ujenzi wa kanisa la Mt Petro. Walikusanya fedha hivyo kwa
njia ya kuuza vyeti vya msamaha. Wakristo waliweza kununua vyeti kwajili yao wenyewe
na kwaajili ya ndugu zao waliokwisha kufariki ili waweze kupata msamaha.
Luther alipinga vikali jambo hili pamoja na mambo mengine ambayo yalikuwa kinyume
na Maandiko matakatifu kwa kuandika hoja 95 na kuzibandika katika mlango wa kanisa
Huko Wittenberg. Rafiki zake Luther walipiga kopi hoja hizo na kuzisambaza katika
maeneo mbalimbali ya nchi ya ujerumani ili ziweze kusomwa na watu wote. Kwa muda
mfupi nakala hizo ziliweza kuenea na mafundisho ya Luther yakaenea katika maeneo
mbalimbali.
Baada ya hoja hizo kuenea Luther aliitwa na Kardinali, Cajetan katika mji wa Dusgbarg (
1518). Kardinari huyo alimtaka Luther kukiri makosa yake lakini Luther alipinga swala
hilo.
Papa Leo X alimwandikia Luther barua ya kumtishia kumtenga na kanisa iwapo hangekiri
makosa yake. Baada ya Luther kuipata barua hii aliichoma moto hadharani mbele ya
kadamnasi
Mnamo mwaka 1521. Luther alitengwa rasmi na kanisa Katoliki. Luther aliitwa katika
mkutano uliofanyika katika mji wa worms ulioitishwa na kaisari Charles V, ili aweze
kusikilizwa na kumaliza mgogoro. Katika mkutano huo Luther alitakwa kukiri makosa
yake kuhusu vitabu alivyokuwa ameviandika na kuvisambaza. Luther alikataa kubadili
msimamo wake, kuyakana maandishi yake, na hatimaye kaisari na wafalme wake
walitangaza hukumu ya kifo dhidi ya Luther. Katika mkutano huo kulitokea fujo na
hatimae Luther alitoroka na kuokolewa na mfalme Fredrick wa Saksoni na kupelekwa
katika boma lake la Wartburg. Akiwa huko alijificha kama mfungwa na alibadilishwa jina
na kuitwa Jorg na kupelekewa nguo zingine. Alibadili sura yake kwa kufuga ndevu.
Akiwa katika boma hilo alianza kazi ya kutafsiri Biblia katika lugha ya kijerumani.
Katika muda huu wa kukaa mafichoni Luther alifanya kazi kubwa ya matengenzo kuliko
wakati mwingine wote kwake.
Mnamo mwaka 1529 Wafalme walibadili msimamo wao wakaamua kupigana dhidi ya
wanamatengenezo. Wafalme 19 walipinga uamuzi huu, na hivyo wakaitwa waprotestanti.
48
Hivyo neno hilo wakapewa watu wale waliokubali matengenezo ya kanisa. Martin Luther
alifariki dunia mnamo mwaka 17, Februari, 1546.
3. JOHN CALVIN
John Calvin Kwa kifarnsa Jean Cauvin alizaliwa mnamo Julai 10, 1509 katika mji wa
Nayoni jimbo la Picard Ufaransa. Baba yake aliitwa Gerard Cauvin, Mama yake aliitwa
Jeahn Lefrenc. Katika familia yao walizaliwa watoto watano, wakiume watatu na wakike
wawili ambapo mtoto wa kiume wa tatu alifariki angali mchanga siku chache tu baada ya
kuzaliwa. John Calvin alikuwa mtoto wa pili kuzaliwa katika familia ya baba yake. Gerard
Cauvin alikuwa Mwanasheria na msajiri katika ofisi ya Askofu wa Nayon.Gerard Cauvini
alitaka watoto wake wapate elimu bora kulingana na nafasi yake aliyokuwa nayo katika
kanisa. John alikuwa mtoto mwenye akili sana, akiwa na umri wa miaka 12 alipata kazi
katika ofisi ya askofu wa mji. Baba yake alipenda mtoto wake awe kuhani (padre) hivyo
basi John alijiunga na chuo kikuu cha Paris kusomea clasics.
Kabla ya kendelea na masomo zaidi kulitokea mgongano kati ya baba yake na askofu wa
Nayon, jambo ambalo lilimfanya baba yake kumsitisha John kuendelea na masomo katika
chuo kikuu cha Parisi ili asiendelee na matayarisho ya upadri badala yake John Calvin
alijiunga na chuo cha Orleans kusomea sheria.
Katika mwaka wa 1531 Gerard Cauvin alifariki dunia na hapo John Calvin akawa huru
kuchagua kusomea taaluma aliyoihitaji mwenyewe. John Calvin alirudi Paris tena
japokuwa baadae kidogo tena alirejea katika chuo ch Orleans kumalizia masomo yake ya
sheria.
Akiwa Paris alichapisha kitabu chake kimoja alichokiita Ufafanuzi wa kitabu na Seneka
(A commentary of a book by Seneca) mwandishi aliyeishi wakati wa dola ya zamani ya
Rumi.
Kwa wakati huu John Calvin alivutiwa sana na mafundisho ya wanamatenegenzo wa
Ujerumani. Moyo wake ulijazwa na upendo kwa Mungu na kwa watu wake. Inaamininka
kuwa kati ya wanamatengenezo wote wa Kanisa hakuna aliyetoa mchango mkubwa
katika kanisa kama John Calvin. Kwa kuwa hakuna kati yao aliyechunguza Neno la
Mungu kwa kina zaidi na kwa maombi zaidi kama John Calvin.
Wakati Waprotestanti wakiwindwa na kuteswa, john Calvin kwa wazi kabisa aliamua
kuwa upande wao. Aliwatembelea na kuwa tia moyo kwa kadli alivyoweza. Rafiki yake
aliyeitwa Nicholas Cop aliteuliwa kuwa mkuu wa chuo (rector ) chuo kikuu cha mji na
ilionekana kuwa john Calvin alimsaidia kuandaa hotuba yake ya Ufunguzi ambayo katika
hotuba hiyo Nicholas alilishambulia sana kanisa la Roman katoliki na kusisitiza
kufanyika kwa matengenezo. Baada ya hotuba hiyo Nicholas alishambuliwa na wanazuoni
wenzake na viongozi wengine na kuitwa mzushi na akalazimika kukimbia na kwenda
kuishi na wakimbizi kule Uswis Basel ili kuokoa uhai wake.
Baadae john Calvin alihusishwa kwamba alishirikiana na Nicholas Cop hivyo mwaka
uliofuta nayeye alilazimika kukimbia kwaajili ya usalama wake na kwenda Basel Uswisi
Mji wa Basel ulielezwa kuwa mji wa Uhuru na wa makimbilio kwa miaka mingi.
49
Baada ya kukaa Basel kwa mwaka mmoja john Calvin alimaua kwenda Straburg. Lakini
ilikuwa vigumu kwa yeye kuendelea kuwepo kule kutokana na vita ilyokuwepo kati ya
mfalme Francis I na Mfalme Charles V. hivyo basi John Calvin aliamua kuelekea kusini
na akaamua kutumia usiku mmoja pale Jiniva. Baada ya taarifa za ujio wa John Calvin
kumfikia William ferali mwanamatengenezo ya kanisa wa ufaransa pale Jiniva
alimkaribisha john Calvin na kumuomba kukaa pamoja nae na kuendeleza kazi ya
matengenzo ya kanisa pamoja. Hivi ndivyo john Calvin alivyoingia rasmi katika kazi ya
matengenezo ya Kanisa. Inasadikiwa kuwa john Calvin aliokoka mnamo mwaka 1530.
Ferali aliandika rasimu ya ukiri wa Imani na Calvin aliandika andiko lake la Uhuisho wa
Muundo wa Kanisa jiniva (Reorganization). Mnamo Januari, 16, 1537 Waliwasilisha
Rasimu yao mbele ya baraza la mji. Mwaka huohuo baraza lilikubali na kupitisha rasimu
hiyo.
Kadli miaka ivyozidi kwenda uhusiano baina ya baraza na wanamatengenzo hao ulianza
kuteteleka.Baraza lilisita kusimamia mapendekezo ya rasimu yao kwasababu wananchi
wengi walionekana kutokukubaliana na mapendekezo ya rasimu hiyo. Novemba 26
mwaka hu huo wanamatengenezo hao walifanya mdahalo na baraza kuhusu rasimu yao.
Kulitokea kutokuelewana katika mdahalo huo.
Mgongano mkubwa ulitokea pale ambapo viongozi wa mji wa Bern uliokuwa umeungana
na Jiniva katika matengenezo ya makanisa ya Uswisi ulipotoa mapendekezo ya
kuanzishwa kwa mfumo mmoja unaofanana (unifoymity) wa uendeshaji wa misa. Moja
ya mapendekezo hayo ilikuwa ni kutumika kwa mkate usiotiwa chachu katika sakramenti
ya Ekaristi Takatifu. Wanamatengenezo hao hawakuwa tayari kufuata wala kutekeleza.
Hawakuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakisubiri mkutano wa sinodi kule Zurich
ambao ndio ungepaswa kutoa maamuzi ya mwisho Baraza liliwaamuru wanamatengenezo
hao kuendesha misa ya sakramenti ya ekaristi wakati wa pasaka. Wanamatengenezo hao
walikataa kuongoza misa wakati wa ibada ya pasaka. Jambo hili lilisababisha vurugu
katika ibada na siku iliyofuata baraza liliwaamuru Wanamatengenezo hao kuondoka mjini
hapo.
Wanamatengenezo hao wawili walipeleka kesi yao kule Zurich na Bern. Sinodi ilipoketi
iliwalaumu sana wanamatengenezo kwa kutokuwa watii kwaajili ya watu wa jiniva. Sinodi
iliwaomba Bern kufanya suruhu kwa lengo la kuwarudisha wanamatengenezo hao.
Baraza la Jiniva lilikataa kuwarudisha wanamatengenezo.
Ferali alipata mwaliko wa kwenda kuongoza kanisa Neuchâtel, John Calvin alipata
mwaliko wa kwenda Strasburg kuongoza kanisa la wakimbizi (refugees) John Calvin
alikutana na wanamatengenezo wa kanisa katika mji huu ambao ni Martin Bucer,
Wolfgang Capito. Miezi michache baadae John Calvin alipewa uraia katika mji huu.
Katika kipindi hiki John Calvin hakuambatana na kanisa moja tu bali bali alifanya kazi
katika makanisa kadhaa yakiwemo St. Nicholas na Kanisa la Dominika. Aliwahudumua
waamini 400-500 katika ibada moja.
50
Rafiki zake walimshauri John Calvin kuoa lakini yeye alikataa lakini baada ya muda kupita
alikubali na akamuoa mjane mmoja wa watoto wawili aliyeitwa Idelete Burry Walizaa
mtoto mmoja wa kiume aliefariki siku chache tu baada ya kuzaliwa kwake. Mkewe John
Calvin alifariki baada ya miaka tisa tu tangu kuoana kwao.
John Calvin alikaa kwa muda wa miaka mitatu hivi Strasburgy, wakati huu kanisa Katoliki
lilitaka kuurudisha mji wa Jiniva mikononi mwao. Kwa bahati rafiki zake Calvin
walifanikiwa kuchukua nafasi za uongozi katika baraza la mji wa Jiniva na wakaamua
kumwita John Calvin kurejea tena Jiniva. Mwanzoni Calvin hakuwa tayari kurejea Jiniva
kwa sababu hakuwa na uhakika kama alikuwa mtu sahihi kwa kazi ile. Hatimae mwaka
1541 aliamua kurudi Jiniva.
John Calvin alipokelewa kwa furaha mno pale jiniva na akapewa jukumu la kurejesha
mfumo wa maisha ya kijamii na kidini kulingana na neno la Mungu. Calvin alianza kazi
ya kuhuburi Neno la Mungu kwa mara ya pili pale Jiniva. Kutokana na kanuni
zilizowekwa watu wote kwa pamoja walikuja kusikiliza neno la Mungu. Jiniva
iligawanywa katika sharika (parish) tano zikiwa na wahudumu watatu na wahudumu
wasaidizi wawili. Ilikuwa ni lazima kuhudhuria ibada, faini iliwekwa kwa yeyote
asiyehudhuria
Kufikia katikati ya karne ya 16 John Calvin alikuwa kiongozi maarufu sana wa
matengenezo ya kanisa. Baada ya kifo cha Martin Luther mwaka 1546 watu wengi
waliotilia mashaka mafundisho ya Kanisa Katoliki walimwendea John Calvin kwaajili ya
ushauri na maelekezo.
Afya ya John Calvin ilianza kuzorota, mwili wake ulianza kuwa dhaifu kutokana na
kusoma na mifungo (Fasting). Calvin aliweza kupitisha siku kadhaa bila kula wala kupata
usingizi. Miaka mitatu kabla ya kifo chake afya yake ilizidi kuwa mbaya zaidi. Rafiki zake
walimshauri kupunguza kazi lakini yeye alikataa akawajibu mnataka Bwana anikute
sijamaliza kazi yake ?
Watu wengi waliokimbia mateso kutoka maeneo mbalimbali walipokelewa Jiniva. Mmoja
wa wakimbizi hao alikuwa ni John Knox wa Skotilandi. Vijana wengi walikwenda Jiniva
kuandaliwa kwaajili ya kazi ya huduma ya Injili Ulaya ya kati na ulaya Magharibi.
Mvuto mkubwa wa Calvin ulitokana na mafundisho na mihadhara yake. Vijana wengi
waliokuja kuandaliwa kwaajili ya huduma waliporudi kwao walibeba Kweli ya Neno la
Mungu katika mioyo na akili zao. Walieneza Nuru ya Injili katika maeneo yote.
John Calvin alikuwa anabebwa na kupelekwa kwenye mikutano aliyokuwa anahitaji
kuhudhuria. Mwaka 1564 alipelekwa kwenye ukumbi wa mji kuhudhuria mkutano wa
baraza na aliwashukuru sana kwa yote waliyofanya kwaajili yake. Siku chache viongozi
wa kanisa walimtenbelea akiwa kitandani, Calvin alisalimiana nao na kuwaaga.
Mwanamatengenezo huyu alifariki mnamo Mei 27, 1564 na alizikwa katika kaburi la
51
Cemetri ambalo halikuwekwa alama yoyote. Hadi sasa kaburi la John Calvin halijulikani
lilipo.
4. JOHN KNOX
John Knox alizaliwa katika miaka ya 1513 katika Haddington, mji mdogo kaskazini mwa
Edinburg, Scotland. Maisha yake ya awali yalimwezesha kukutana na watu wengi, na
elimu yake ya juu ilimwezesha kuwafikia watu wa hali ya juu katika jamii. Alipoteza
wazazi wake akiwa bado mtoto. Knox alijifunza kilatini shuleni Haddington. Mwaka 1529,
alianza masomo ya Theolojia katika chuo cha mtakatifu Andrews. Aliwekewa mikono ya
ukuhani mwaka 1536 ila hakuajiriwa katika nafasi hiyo kutokana na Scotland kuwa na
makuhani wengi.
Mwaka 1540, utawala wa Scotland ulianza kuwatesa wahubiri wa Neno la Mungu. George
Wishart hakuogopa muda wa majaribu na akasafiri kutoka kijiji kimoja hadi kijiji kingine
kuhubiri ukweli wa Biblia. Knox, kwa kushawishika na ujumbe wa Wishart, aliamua
kumsindikiza kama mlinzi wake, akiwa na mapanga mawili kumkinga mhubiri huyu dhidi
ya vitisho vya watesi. Kwa wiki tano, alimsindikiza Wishart katika kuhubiri kwake mpaka
mamlaka yaliamua kunyamazisha sauti ya mheshimiwa huyu kwa kumfunga gerezani.
John Knox Aliamua kujiunga nae na kumuunga mkono, lakini Wishart alimsihi arudi
nyumbani, akisema: “Hapana, rudi kwa watoto wako, na Mungu akubariki. Mmoja
anatosha kuwa kafara. Knox alirudi.
Henry Balnaves, mmoja ya waheshimiwa, alifurahishwa na kipaji chaa ufundishaji wa
wanamatengenezo na kuungana na mhubiri John Rough kwa kumwalika Knox kuwa mkuu
wa kanisa na mchungaji wa kanisa la nyumba ya mtakatifu Andrews. Knox alikataa
mwaliko huo, nakusema hawakuwa na mamlaka ya kutoa wito huo na kurudi chumbani
mwake
. Wiki chache baade, alihudhuria ibada ambayo mhudumu alitetea kanisa la kikatoliki
kuwa mke wa Kristo. Knox alishindwa kunyamaza na kuzungumza kwamba kanisa la
kikatoliki sio mke wa Kristo bali ni kahaba. Kanisa waliomba maneno yake yachunguzwe
jumapili iliyofuata. Baada ya siku saba, alihubiri Danieli 7, akilinganisha upapa na mpinga
Kristo, Knox alitambua maandiko kuwa mamlaka pekee kwa kutunga mafundisho ya dini
na kuthibitisha umhimu wa haki kwa imani pekee, mambo yaliounda msingi wa mahubiri
yake hadi mwisho wa uhai wake.
Siku kadhaa baadae, John Knox alitoa maandishi ya mafundisho yanayopinga utaratibu wa
misa, pugatori, na maombi kwa wafu. Ndipo palianza kazi ya John Knox, aliyetokea kuwa
mmoja wa wahubiri wa kupinga mafundisho potofu ya kanisa.
Kutoka utumwani kuwa mkuu wa Kanisa katika huduma kwa mfalme
Kundi la waheshimiwa kumi na sita, wafuasi wa mfia dini Wishart, waliokuwa
wamekasirishwa na padre David Beaton kwa kuuwa mhubiri huyo, waliuwa padre huo
52
nyumbani kwake miezi miwili baadae na kuhamia kwenye nyumba ya mfalme ya
Mtakatifu Andrews, ambako Knox alikuja kuisha mwaka mmoja baadae.
Kutokana na uasi huo, malkia wa kikatoliki Maria wa Gise aliamua kutafuta msaada
wa mfalme Henry II, mfalme wa Ufaransa, alietuma jeshi la meli na kushambulia nyumba
ya kifalme ya mtakatifu Andrews. Mweli Julai, 1547, wanamatengezo waliokuwa ndani ya
ngome hiyo walijisalimisha kwa jeshi la majini la Ufaransa wakachukuliwa mateka. Kati
yao alikuwepo pia na John Knox, ambae alifungwa pingu kwenye viti vya meli akiwa hana
nafasi ya kubadirisha mkao wake. Pamoja na wafungwa wengine wa vita na waharibifu
wengine , Knox alilazimishwa kusaidia kusukuma meli, afisa mmoja akiwa upande mmoja
kusubiri kuwapiga wafungwa ambao hawakuwa tayari kufuata maagizo katika kufanya
kazi ngumu.
Ndani ya meli, wafungwa walilazimishwa kushiriki misa na kutoa ishara ya kumheshimu
bikira Maria, au wateswe. Knox alikataa. Pale picha ya bikira Maria iliposukumizwa usoni
mwake ili aibusu, aliichukua nakuitupia baharini akisema, “Acha mama yetu ajiokoe; yeye
ni mwepesi sana; acha ajifunze kuogelea.”
Baada ya miezi kadhaa na kwa kuwa katika kipindi kikali cha msimu wa baridi kwenye
meli, afya ya Knox ilidhoofu sana. Pamoja nakuumwa bado alifariji wenzake katika
mateso, akiwa na uhakika ya kwamba wataachiwa huru na kuendeleza kazi yake ya
kutangaza ukweli wa Biblia. Miezi kumi na tisa ya mateso makali, majaribu na maumivu
makali. Inadhaniwa kuwa kwa ombi la mfalme wa Uingereza Edward VI John Knox
aliachiwa huru mwezi Februari 1549.
April 7, 1549, Knox aliitwa kutumika kama mhubiri katika mji wa Berwick-upon-Tweed,
chini ya Kanisa la Uingereza. Mwishoni mwa 1550, alihamishwa kama mhubiri wa kanisa
la Mtakatifu Nikolasi, mji wa Newcastle sehemu ya Taini; na 1551, aliwekwa kuwa
msimamizi mkuu wa dini wa Mfalme pamoja na wengine watano, ikimpa nafasi ya
kuhubiria ufalme. Kwa kipindi hiki, alipinga taratibu ya kupokea meza ya bwana kwa
kupiga magoti na pia mafundisho ya kwamba mwili halisi wa Kristo upo kwenye
Sakramenti
Knox alikutana na Elizabeth Bowes, mahiri na msomi wa maandiko, ambae alikuja
kumtambua kama mwelekezaji wake kwa mambo ya kiroho, na Margery Bowes, mmoja
wa binti zake Elizabeth, ambae alimchumbia mwaka 1553 na kuoa muda mfupi baadae.
Mwaka mmoja baadae alikuwa Geneva, Uswisi, akiwa ametoroka Uingereza alipoingia
Mary Tudor kwenye utawala na kurudisha uKatoliki nchini Uingereza. Knox alichapisha
kipeperushi akimshambulia malkia huyo kwa msimamo wake wa kikatoliki pamoja na
maaskofu waliomsaidia kuingia kwenye utawala, na pia kiongozi wa kirumi, Charles V,
akimtaja kuwa “Adui wa Kristo kama Nero
Kuhubiri Frankfurt
Muda mfupi baada ya kufika Uswisi, Knox alipokea barua ya mwaliko kuwa mchungaji
wa kanisa la wakimbizi wa Uingereza wanaoishi mji wa Frankfurt, Ujerumani na
53
akakubali. Kule Frankfurt tatizo lingine liliibuka: Taratibu za ibada. Mawazo
yaligawanyika na ujio wa wakimbizi wapya. Wengine waliunga utaratibu mpya uliokuwa
ukipendekezwa na Knox na wengine kuzitingatia kwa umakini sana kama ilivyo kwenye
kitabu cha taratibu za ibada za kanisa la katoliki. Kupitia ushauri wa Calvin, Knox
alifanikiwa kufikia makubaliano; ila na ujio wa wakimbizi wengi zaidi, msukumo ulizidi
kiasi ya kwamba waliokuwa wakipinga walishitaki kwa utawala wa Frankfurt, na
akaombwa aondoke. Hata hivo Knox alirudi Geneva.
Jaribio Jipya Scotland
Ndani ya Scotland, pamoja na nguvu ya kirumi, baadhi ya waheshimiwa waliamua
kusimamisha neno la Mungu kama msingi wa makanisa yao, walipinga mafundisho potofu
yaliyokuwa yakitolewa na kanisa. Baadhi yao walimwalika Knox kurudi Scotland ili
kusimamia maengenezo ya Kanisa. Kwa miezi tisa Knox alijitoa sana kuhubiri
mafundisho ya matengenezo na taratibu mpya za ibada katika makanisa mbali mbali ya
Scotland.
Kurudi kwake Scotland na umarufu wake kulishangaza makuhani wa Katoliki, waliomuita
ajitokeze mjini Ediburg mwezi Mei 15, 1556, wakimchukulia kuwa tishio kwa mamlaka ya
kanisa. Alisindikizwa kwenye hicho kikao na waheshimiwa wengi wenye ushawishi, na
maaskofu waliomshitaki waliamua kufuta mashtaka. Knox alikuwa huru kuhubiri wazi
misingi ya uprotestanti.
Kazi ya tatu Geneva
Gafla Knox aliamua kurudi Uswisi, na alifika Uswisi mwezi Septemba 13, 1556, pamoja
na mke wake, Margery Bowes, na mama mkwe wake, Elizabeth Bowes. Hii ilikuwa miaka
ya Knox ya furaha zaidi, licha ya kazi yake ngumu kama mchunganji katika kanisa la
kiingereza la Geneva, ambalo lilikusanyika kwenye Eglise de Notre Dame la Neuve,
ambalo kwa sasa linajulikana kama Ukumbi wa Calvin. Akiwa Geneva, watoto wake
wawili wakiume walizaliwa, Nathaniel na Eleazar.
Knox alishauri Geneva kwa marafiki zake wote Uingereza kuwa sehemu bora zaidi ya
kimbilio. Katika moja wa barua zake aliandika: “Sina hofu wala aibu kusema, (Geneva) ni
shule ya kristo iliyokamilika zaidi kutokea duniani tangu siku za mitume. Katika baadhi ya
sehemu na shuhudia Kristo kuhubiriwa kiukweli; ila tabia na dini yenye matengenezo ya
dhati sijawahi kuona katika sehemu nyingine.
Mwaka 1558 Knox aliandika akiwa Geneva mmoja wa vipeperushi vyake maarufu
kiitwacho “Sauti ya kwanza ya tarumbeta dhidi ya utawala wa kinyama wa wanawake.”
Knox alimaanisha Maria I wa Uingereza na Maria wa Gise wa Scotland kwa kutesa wa
protestanti na kusema wanapaswa kuondolewa katika utawala. Jarida hilo lilichapishwa
kisiri bila ushauri wa Calvin. Lilipigwa marufuku nchini Uingereza na hata Geneva na
Calvin, alilikataa kabisa. Knox mwenyewe alikubali kwamba jarida hili lilikamilisha
kufarakana kwake na marafiki zake wa Uingereza. Elizabeth Tudour, aliyekuja kuwa
malkia miezi michache baadae, alikwazika sana na jarida hilo na hakumsamehe Knox.
54
Kufunguka kwa matengenezo ya kiprotestanti Scotland
Pale malkia aliependelea uprotestanti, Elizabeth Tudor, alipoingia madarakani Uingereza,
wakambizi waliokuwa Ujerimani waliamua kurudi nchini kwao. Knox aliamua kurudi
Scotland. Kabla hajaondoka, utawala wa Geneva ulimtaja kwa heshima kwa mchango
wake kwa uprotestanti. Nchini Scotland, hali ilikuwa tete kati ya malkia Maria wa Gise na
kuandamana kwa waprotestanti.
Baada ya siku chache kufika Scotland, Knox alihubiri mahubiri ya kuvutia katika mji wa
Perth kupinga kuabudu sanamu kwa wa katoliki. Mara baada ya kumaliza tu, maandamano
yaliibuka dhidi ya kanisa la Katoliki, na kusababisha kuharibiwa kwa sanamu,
madhabahu, na hekalu na mji wa Perth uliozungushwa na ukuta kuchimbwa chimbwa.
Maria wa Gise alituma jeshi kuzingira huo mji. Mazungumzo yalifikia makubaliano na
jeshi la waprotestanti ili kusitokee vita na jeshi la Ufaransa waliounganika na Malkia Maria
wa Gise. Lakini baada ya kuingia kwenye huo mji, malkia aliujaza na jeshi la wa Scot kwa
kudhaminiwa na Ufaransa. Jambo hili lilichukuliwa kama usaliti kwa upande wa baadhi ya
waheshimiwa waliounga mkono makubaliano kati ya waprotestanti na wanaomuunga
mkono Mary wa Gise, hivo waliamua kubadili msimamo wao na kuunga mkono
matengenezo ya uprotestanti
Kutokana na matatizo ya Perth, Knox alienda katika kanisa la mtakatifu Andrews, huko
alihubiri ujumbe wa moto uliosababisha athari kama kule Perth - maandamano na
kuvunjwa kwa mali ya kanisa. Jeshi la waprotestanti waliweza kuvamia miji kadhaa
Scotland, wakiungwa mkono na mahubiri ya Knox yenye nguvu. Waheshimiwa wa
kiprotestant, wakisaidiwa na jeshi, pia walivamia Edinburgh, mji mkuu wa Scotland.
Mwezi Julai 25, 1559, baada ya viongozi wa kiprotestant, waitwao mabwana wa
kusanyiko, kujitoa katika mji Edinburgh, na malkia waScotland, Maria wa Gise, kuahidi
uhuru wa dhamira.
Ila malkia alikuwa na mpango mwingine. Aliomba msaada kutoka jeshi la ufaransa.
Walipotua Leith, waprotestanti waliuvamia na kuuchukua tena mji Edinburgh na kumvua
cheo Maria wa Gise kwenye kuongoza Scotland. Baadhi ya waheshimiwa waliweza
kushawishi Uingereza kutuma wanajeshi kusaidia waprotestanti.
Kifo cha malkia kiongozi Maria wa Gise mwezi Juni 10, 1560, kilitengeneza njia ya
muafaka wenye amani. Julai 6 mwaka huo, makubaliano ya Edinburgh yalitiwa sahihi,
ambapo jeshi la majini la Ufaransa na jeshi la Uingereza walipaswa kuondoka Scotland,
hivyo kuimarisha mwendelezo wa kiprotestant. Julai 19, Knox aliongoza ibada ya shukrani
kwa ngazi ya taifa kwenye kanisa la mtakatifu Gilles mjini Edinburgh. Kuanzia Agosti, 1,
1560, bunge lilikutana kutoa mwongozo mpya juu ya dini inayotambulika kitaifa. Knox,
pamoja na wachungaji wengine, waliandaa mwongozo mpya wa imani ambao bunge
lilipitisha na rasmi kuanzisha matengenezo ya kiprotestant nchini humo. Baadhi ya mambo
yaliyokataliwa na waprotestanti ni:-
‣ Mamlaka ya papa nchini Scotland yaliondolewa
‣ Mafundisho na matendo yote yalio kinyume na uprotestanti yalikataliwa
‣ Kuabudu Maria kulikataliwa
55
‣ Misa kwa lugha ya kilatini kuliondolewa
‣ Siku kuu za kikatoliki zilifutwa
‣ Maombi ya wafu yalipigwa marufuku
‣ Imani ya kwamba wafu wapo toharani ilikataliwa
‣ Misalaba ilikataliwa
‣ Sherehe za misa zilikataliwa
‣ Ilidhibitishwa kwamba mkate kuwa mwili wa Yesu ni mfano tu na sio kwamba mkate ni
mwili wake halisi.
Pamoja na hayo, bunge liliwaagiza Knox na wachungaji wengine kuandaa kuundwa upya
kwa kanisa la matengenezo nchini Scotland na taratibu mpya za ibada zilihamisha
msisitizo kutoka kweye kutazama makuhani na kuuweka kwenye kushirikiana kwa
waumini wote, na masomo ya Biblia, mahubiri, maombi, kusoma Zaburi na kuimba kwa
kusanyiko lote.
Magumu mapya
Disemba 1560, Knox alipokea pigo kubwa pale mke wake Margery alipofariki, akiachwa
na watoto wawili wadogo wakuwatunza, Muda usio mrefu sana baada ya hapo, Agosti 19,
1561, sauti ya mabomu ilisikika kwenye bandari ya Leith, ikitambulisha ujio wa Malkia
mdogo Maria, mtoto wa Maria Gise, aliyekuwa amekimbilia Ufaransa. Ilitangazwa
kwamba hakutakuwa na mabadiriko yoyote juu ya maswala ya dini na hakuna
kinachopaswa kusumbua wafanyakazi wake wakikatoliki.
Baadhi ya waheshimiwa, waliopendelea siasa, waliamua kumuunga mkono malkia mpya,
na si John Knox. Knox alipaza suti, akihubiri kupinga msimamo wa malkia kuhusu
mambo ya dini. Malkia Mary alimuita Knox wiki mbili baada ya kufika Scotland,
akimtuhumu kwa uasi wake na kuandika kupinga mamlaka yake.
"Baada yakuletwa uso kwa uso na malkia wa Scotland, mahali ambapo udhahiri wa
viongozi wakiprotestanti ulikosa nguvu, John knox alisimama bila kutikisika kushuhudia
ukweli. Hakukubali kununuliwa na maneno matamu, hakuwa na hofu kwa kutishwa.
Malkia alimshtaki kwa mafundisho potofu. Alikuwa amefundisha watu kupokea dini
iliokataliwa na taifa, alisema, hiyo ni kuvunja amri ya Mungu kwamba watu watii walio
juu yao.
Knox aliitwa Mara kadhaa na malkia kujibu mashtaka, lakini mwanamatengenezo huyu
alijibu kila wakati kwa msimamo na kuweza kubaki huru kutokana na ushawishi wake
mkubwa na kuungwa mkono na waheshimiwa wakiprotestanti. Malkia alimkumbusha
kwamba anapaswa kuishi kulingana na sheria za Scotland na kwamba misa ilikatazwa.
Mwezi Machi 26, 1564, Knox, akiwa hana mke, akiwa na miaka 50, aliamua kuoa tena, na
alimuoa Margaret wa Stewart, ambae alizaa nae watoto wakike watatu ambao ni Martha,
Margaret, na Elizabeth.
Knox hakunyamaza, Mwaka 1565, alihubiri, kama siku zote, kwa ujasiri, akipinga ndoa ya
malkia na Henry Stuart. Ndoa hiyo haikudumu, Stuart aliuwawa. Malkia Maria aliolewa
tena, . Kutokana na hayo, mamlaka ya Scotland ilimlazimisha Malkia Maria ajiuzuru
56
wadhifa wake, alifungwa jela kwenye nyumba ya kifalme ya Loch Leven lakini alifanikiwa
kutoroka Mei 2, 1568.
Miaka ya mwisho ya John Knox
Scotland ilijikuta ikiwa kwenye vita ya wenyewe kwa wenyewe kati ya wale waliomuunga
mkono malkia aliyeondolewa na waprotestanti.1571, msimamizi wa nyumba ya kifalme ya
Edinburgh, nae alimuunga mkono malkia, alifukuza waprotestanti wote kwenye jiji hilo.
Knox alistaafu kwenye nyumba ya kifalme ya mtakatifu Andrew lakini akarudi tena
mwaka 1572, tayari akiwa dhaifu kimwili kutokana na umri wake lakini, kama siku zote,
akiwa imara katika misingi yake ya kusambaza neno kwenye kanisa la mtakatifu Gilles,
akimtambulisha mrithi wake, mchungaji Lawson Aberdeen. Knox alirudi nyumbani kwake
kwa mara ya mwisho na kufariki Novemba 24, 1572, mke wake akimfariji na akiwa
amezungukwa na waprotestanti wenye vyeo vya heshima. Ombi lake la mwisho
lilikuwa kusomewa neno la Mungu. Mwili wake ulizikwa ndani ya kanisa la mtakatifu
Gilles
Mwanamatengenezo huyu hakuogopa sura ya mwanadamu. Moto wa Injili ya kweli
uliwaka ndani yake daima na alikuwa tayari kuitetea kweli ya Neno kwa gharama yoyote
ile.
Knox aliishi kwa imani. Alibaki kuwa mkweli kwa kazi yake na kwa ukweli wa Mungu,
akipigania vita ya Bwana hadi Scotland ilipata wa uhuru. Kanisa la Presbyterian lina
mtambua Knox kuwa mmoja wa waanzilishi wake.
Hitimisho
" Tunapaswa kuwa na shauku kama aliyokuwa nayo John Knox alipoomba mbele ya
Mungu kwa ajili ya Scotland. Alilia, "Nipe Scotland, Bwana, au nitakufa. Hakika shujaa
huyu alipewa Scotland kama alivyoomba na akawa tayari kufa kupona kuhakikisha nuru ya
matengenezo inang’aa Scotland.
Kwa hakika Wanamatengenezo walisimama kidete kuitetea kweli ya Mungu. Bado leo
Mungu anahitaji na anainua wanamatengezo katika kanisa la sasa. Kazi ya matengenezo
ya kanisa haijamalizika. Mungu analiandaa kanisa lake kwaajili ya unyakuo . Kazi ya
matengenezo ya kanisa itakwisha pale kanisa litakapokuwa limenyakuliwa kwenda
mbinguni.
Kanisa la leo limekengeuka. Ulimwengu umeingia kanisani na karibu kila mtu katika
dunia ya sasa anajiita ameokoka. Wanahitajika wanamatengenezo wa kizazi hiki
watakaosimama na kupaza sauti zao ili kulirudisha kanisa katika nafasi yake.
Kama mtumishi wa Mungu unapaswa kusimama katika zamu yako. Usimezwe na dunia
na anasa zake. Hubiri kweli ya neno la Mungu. Usikubali kuhalalisha baadhi ya mambo ili
kujipatia kundi kubwa au kujijengea umaarufu. Simama na Bwana katika utumishi
aliokwitia bila kuyumbishwa na mtu yeyote.
57
Ni matumaini yangu kuwa mambo yote uliyojifunza katika kozi hii yatakuwa chachu ya
kukufanya usimame katika nafasi yako ya kiutumishi na kumtumikia Bwana Yesu sawa
sawa na agizo lake.
Mungu anamtaka kila kiongozi asimame kwa miguu yake mwenyewe katika utumishi
Bwana aliomuitia.
Ezekieli 2:1 Akaniambia, mwanadamu simama kwa miguu yako, name nitasema nawe.
Kumbuka kuwa utumishi huu hatuufanyi kwa nguvu zetu wenyewe bali kwa kuwezeshwa
na Mungu mwenyewe.
(Zekaria 4:6) “Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana
wa majeshi.”
1Wakoritho 2:4 Na neno langu na kuhubiri kwangu hakukuwa kwa maneno ya hekima
yenye kushawishi akili za watu, bali kwa dalili za Roho na nguvu, ili imani yenu
isiwe katika hekima ya wanadamu, bali katika nguvu ya Mungu.
Simama katika kweli ya Mungu na acha Mungu akutumie mwenyewe kama apendavyo.
PICHA ZA BAADHI YA WANAMATENGENEZO MAARUFU WA KANISA
Ulrich Zwingli Dr. Martin Luther John Carvin John Knox
58