SHUJAAZ TANZANIA TOLEO 54
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
2
3
4
Mambo vipi? Tumepokea meseji nyingi sana kutoka<br />
kwenu na kama kawaida mimi na Jay tutajibu baadhi.<br />
#VEE mimi nina ndoto ya uchoraji wa ramani za nyumba.<br />
Nifanye nini ili ndoto yangu ikamilike? - Malugu<br />
Sijajua una kiwango gani cha elimu lakini nakushauri<br />
usomee masomo ya Usanifu majengo (Architecture)<br />
ya kiwango cha chuo kwa kuwa kipaji pekee hakitoshi<br />
kufanikisha ndoto zako. Ujenzi ni jambo linalohusisha<br />
sanaa na sayansi hivyo uelewa wa yote mawili unahusika<br />
sana. Isitoshe, ili kazi zako ikubalike, unahitaji vibali kutoka<br />
serikalini na vibali hivi hupewa watu waliokidhi vigezo.<br />
#Vee mimi ni mvulana nina miaka 27, nina mpenzi ambaye<br />
nipo naye kwenye uchumba kwa miaka mitatu sasa. Kila<br />
nikimwambia tuanze maisha anakataa, nifanyaje kwa sasa?<br />
Ndoa ni maamuzi makubwa na hufanywa mara moja hivyo<br />
mtu kupatwa na wasiwasi wa kuingia kwenye ndoa ni jambo la<br />
kawaida. Jaribu kuongea naye kuhusu sababu zinazompelekea<br />
kukataa, labda anaweza akawa na mipango ya kimaisha ambayo<br />
angependa kuikamilisha kabla hajaingia kwenye ndoa kama<br />
masomo,kazi au biashara au labda bado hajajiridhisha kwamba<br />
wewe ni mtu sahihi kwake. Muondoe wasiwasi na mhakikishie<br />
kuwa utamsapoti kwenye masomo au mishe zake hata baada<br />
ya ndoa na kuwa wewe ndiye mtu sahihi kwake.<br />
#VEE, kuna umuhimu wowote wa kuwa na boyfriend ukiwa shule?<br />
Sijawahi kusikia mtu amefaulu kwa kuwa na mpenzi bora shuleni<br />
kwa kuwa ulichokifuata pale ni elimu na si kingine. Hakuna ulazima<br />
wa kuwa na mpenzi ukiwa shuleni kwa kuwa wanafunzi wengi<br />
hujiingiza kwenye mahusiano si kwa mapenzi ila ni kwa kufuata<br />
mkumbo na mihemko inayotokana na ukuaji. Huna haja ya kufuata<br />
wengine, kuwa wewe kwa kuwa dunia nzima ina wewe mmoja na<br />
imejaa watu wengine.<br />
1<br />
2<br />
Vee, mimi ni msichana wa miaka 20 na kuna kaka ananipenda sana na mimi nampenda<br />
lakini nasikia kuwa ni mume wa mtu. Nikimuuliza anakataa na nikimwambia tuachane<br />
hataki, nifanyeje?<br />
Kuna mambo matatu muhimu ya kuzingatia:<br />
Wanaume wako wengi sana, huna haja ya kuwa na mume wa mtu na kuvunja ndoa za watu.<br />
Bado una umri mdogo, una nafasi ya kupata mtu mwingine atakayekufaa hapo mbeleni<br />
hivyo usiogope kuachana naye. Huna haja ya kumuomba kuachana naye, ni kitendo cha<br />
kumpa taarifa tu na kuendelea na maisha yako. Hakuna mtu anayemiliki maisha ya<br />
mwingine hivyo chukua umiliki wa maisha yako.
Vee mimi ni kijana wa miaka 24, nina mchumba ananipenda nami nampenda, tatizo<br />
anapenda hela! Nikimwambia sina ananiambia mimi mwanaume gani sina hela?<br />
Naomba ushauri - Fadhili<br />
Wanaume huvutiwa na uzuri wa wanamke na wanawake huvutiwa na wanaume wazuri na<br />
wenye mafanikio hivyo ni muhimu kuhakikisha unafanikiwa au unaonesha jitihada na una<br />
mipango ya kuleta mafanikio ili kuendeleza mahusiano yako. Lakini kama huyo msichana<br />
anakupenda kipindi una pesa na kukudharau kipindi huna basi kuna uwezekano mkubwa<br />
kuwa anapenda pesa zako zaidi ya kukupenda wewe. Endelea naye lakini akiendelea<br />
kukudharau haina haja ya kuendelea naye.<br />
#Vee je, ukitumia njia za uzazi wa mpango unaweza kupata madhara? - Asha<br />
Njia za uzazi wa mpango zipo nyingi, kuna vidonge, kitanzi, sindano,<br />
kijiti, mipira ya kike na ya kiume, pachi na kadhalika. Zote hizi hufanya<br />
kazi tofauti tofauti na kutokea kwa madhara kutategemea na mwili<br />
wako uta-react vipi na njia hizo hivyo, ni muhimu kupata ushauri wa<br />
daktari kuhusu njia sahihi na itakayokufaa kabla ya kuanza kutumia.<br />
Kama ikishindikana kupata daktari basi tumia mipira ya kike au ya kiume.<br />
#Vee nataka kufuga kuku lakini sijui nitatoa wapi<br />
mkopo wa kuanzisha biashara hii, naomba ushauri.<br />
Kuna mifumo rasmi na isiyo rasmi ya kupata mikopo. Njia<br />
rasmi ni pamoja benki, vikoba, SACCOSS, serikali za mitaa<br />
kupitia mifuko ya maendeleo ya vijana, mitandao ya simu<br />
na kadhalika, huku njia zisizo rasmi ni pamoja na vikundi vya<br />
kuwezeshana (mchezo), mikopo kutoka kwa ndugu, jamaa na<br />
marafiki, taasisi za kidini na kadhalika. Kwa njia zilizo rasmi,<br />
kuna mahitaji utatakiwa kuwasilisha kulingana na ukubwa wa<br />
mkopo au mifumo wanayotumia kwa mfano dhamana, rekodi<br />
zako za kibenki na kadhalika wakati njia zisizo rasmi mara nyingi<br />
huwa na masharti machache na kiwango kidogo cha pesa.<br />
Unaweza kujaribu njia yoyote kati ya hizi kulingana na mahitaji<br />
yako. Nakushauri uanze kidogo kidogo, usichukue mkopo<br />
mkubwa halafu biashara ikafanya vibaya na ukashindwa<br />
kurudisha pesa za watu.<br />
# Vee, kuna msichana nampenda sana ila ana V.V.U, nifanyaje?<br />
Kumpenda mtu mwenye V.V.U hakuna ubaya wowote kwa kuwa<br />
siku hizi V.V.U ni ugonjwa unaoweza kuudhibiti kama umeupata<br />
na unaweza kujizuia kuupata kama bado. Cha muhimu ni kwenda<br />
kwa muelimisha rika ili kupata ushauri zaidi na kujua jinsi gani ya<br />
kuishi pamoja bila ya mmoja kumuambukiza mwenzake, mtoto na<br />
kadhalika.<br />
Tuma maswali kwenda 0784551616 nasi tutayajibu. Kumbuka, anza na #Vee.<br />
Kwa maswali yanayohusiana na unyanyasaji unaweza kupiga 116 ili kuongea na<br />
mtaalam. Kwa maswali ya elimu ya afya ya uzazi piga 0800753333.
8
9
15