26.07.2019 Views

SHUJAAZ TANZANIA TOLEO 54

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

2


3


4


Mambo vipi? Tumepokea meseji nyingi sana kutoka<br />

kwenu na kama kawaida mimi na Jay tutajibu baadhi.<br />

#VEE mimi nina ndoto ya uchoraji wa ramani za nyumba.<br />

Nifanye nini ili ndoto yangu ikamilike? - Malugu<br />

Sijajua una kiwango gani cha elimu lakini nakushauri<br />

usomee masomo ya Usanifu majengo (Architecture)<br />

ya kiwango cha chuo kwa kuwa kipaji pekee hakitoshi<br />

kufanikisha ndoto zako. Ujenzi ni jambo linalohusisha<br />

sanaa na sayansi hivyo uelewa wa yote mawili unahusika<br />

sana. Isitoshe, ili kazi zako ikubalike, unahitaji vibali kutoka<br />

serikalini na vibali hivi hupewa watu waliokidhi vigezo.<br />

#Vee mimi ni mvulana nina miaka 27, nina mpenzi ambaye<br />

nipo naye kwenye uchumba kwa miaka mitatu sasa. Kila<br />

nikimwambia tuanze maisha anakataa, nifanyaje kwa sasa?<br />

Ndoa ni maamuzi makubwa na hufanywa mara moja hivyo<br />

mtu kupatwa na wasiwasi wa kuingia kwenye ndoa ni jambo la<br />

kawaida. Jaribu kuongea naye kuhusu sababu zinazompelekea<br />

kukataa, labda anaweza akawa na mipango ya kimaisha ambayo<br />

angependa kuikamilisha kabla hajaingia kwenye ndoa kama<br />

masomo,kazi au biashara au labda bado hajajiridhisha kwamba<br />

wewe ni mtu sahihi kwake. Muondoe wasiwasi na mhakikishie<br />

kuwa utamsapoti kwenye masomo au mishe zake hata baada<br />

ya ndoa na kuwa wewe ndiye mtu sahihi kwake.<br />

#VEE, kuna umuhimu wowote wa kuwa na boyfriend ukiwa shule?<br />

Sijawahi kusikia mtu amefaulu kwa kuwa na mpenzi bora shuleni<br />

kwa kuwa ulichokifuata pale ni elimu na si kingine. Hakuna ulazima<br />

wa kuwa na mpenzi ukiwa shuleni kwa kuwa wanafunzi wengi<br />

hujiingiza kwenye mahusiano si kwa mapenzi ila ni kwa kufuata<br />

mkumbo na mihemko inayotokana na ukuaji. Huna haja ya kufuata<br />

wengine, kuwa wewe kwa kuwa dunia nzima ina wewe mmoja na<br />

imejaa watu wengine.<br />

1<br />

2<br />

Vee, mimi ni msichana wa miaka 20 na kuna kaka ananipenda sana na mimi nampenda<br />

lakini nasikia kuwa ni mume wa mtu. Nikimuuliza anakataa na nikimwambia tuachane<br />

hataki, nifanyeje?<br />

Kuna mambo matatu muhimu ya kuzingatia:<br />

Wanaume wako wengi sana, huna haja ya kuwa na mume wa mtu na kuvunja ndoa za watu.<br />

Bado una umri mdogo, una nafasi ya kupata mtu mwingine atakayekufaa hapo mbeleni<br />

hivyo usiogope kuachana naye. Huna haja ya kumuomba kuachana naye, ni kitendo cha<br />

kumpa taarifa tu na kuendelea na maisha yako. Hakuna mtu anayemiliki maisha ya<br />

mwingine hivyo chukua umiliki wa maisha yako.


Vee mimi ni kijana wa miaka 24, nina mchumba ananipenda nami nampenda, tatizo<br />

anapenda hela! Nikimwambia sina ananiambia mimi mwanaume gani sina hela?<br />

Naomba ushauri - Fadhili<br />

Wanaume huvutiwa na uzuri wa wanamke na wanawake huvutiwa na wanaume wazuri na<br />

wenye mafanikio hivyo ni muhimu kuhakikisha unafanikiwa au unaonesha jitihada na una<br />

mipango ya kuleta mafanikio ili kuendeleza mahusiano yako. Lakini kama huyo msichana<br />

anakupenda kipindi una pesa na kukudharau kipindi huna basi kuna uwezekano mkubwa<br />

kuwa anapenda pesa zako zaidi ya kukupenda wewe. Endelea naye lakini akiendelea<br />

kukudharau haina haja ya kuendelea naye.<br />

#Vee je, ukitumia njia za uzazi wa mpango unaweza kupata madhara? - Asha<br />

Njia za uzazi wa mpango zipo nyingi, kuna vidonge, kitanzi, sindano,<br />

kijiti, mipira ya kike na ya kiume, pachi na kadhalika. Zote hizi hufanya<br />

kazi tofauti tofauti na kutokea kwa madhara kutategemea na mwili<br />

wako uta-react vipi na njia hizo hivyo, ni muhimu kupata ushauri wa<br />

daktari kuhusu njia sahihi na itakayokufaa kabla ya kuanza kutumia.<br />

Kama ikishindikana kupata daktari basi tumia mipira ya kike au ya kiume.<br />

#Vee nataka kufuga kuku lakini sijui nitatoa wapi<br />

mkopo wa kuanzisha biashara hii, naomba ushauri.<br />

Kuna mifumo rasmi na isiyo rasmi ya kupata mikopo. Njia<br />

rasmi ni pamoja benki, vikoba, SACCOSS, serikali za mitaa<br />

kupitia mifuko ya maendeleo ya vijana, mitandao ya simu<br />

na kadhalika, huku njia zisizo rasmi ni pamoja na vikundi vya<br />

kuwezeshana (mchezo), mikopo kutoka kwa ndugu, jamaa na<br />

marafiki, taasisi za kidini na kadhalika. Kwa njia zilizo rasmi,<br />

kuna mahitaji utatakiwa kuwasilisha kulingana na ukubwa wa<br />

mkopo au mifumo wanayotumia kwa mfano dhamana, rekodi<br />

zako za kibenki na kadhalika wakati njia zisizo rasmi mara nyingi<br />

huwa na masharti machache na kiwango kidogo cha pesa.<br />

Unaweza kujaribu njia yoyote kati ya hizi kulingana na mahitaji<br />

yako. Nakushauri uanze kidogo kidogo, usichukue mkopo<br />

mkubwa halafu biashara ikafanya vibaya na ukashindwa<br />

kurudisha pesa za watu.<br />

# Vee, kuna msichana nampenda sana ila ana V.V.U, nifanyaje?<br />

Kumpenda mtu mwenye V.V.U hakuna ubaya wowote kwa kuwa<br />

siku hizi V.V.U ni ugonjwa unaoweza kuudhibiti kama umeupata<br />

na unaweza kujizuia kuupata kama bado. Cha muhimu ni kwenda<br />

kwa muelimisha rika ili kupata ushauri zaidi na kujua jinsi gani ya<br />

kuishi pamoja bila ya mmoja kumuambukiza mwenzake, mtoto na<br />

kadhalika.<br />

Tuma maswali kwenda 0784551616 nasi tutayajibu. Kumbuka, anza na #Vee.<br />

Kwa maswali yanayohusiana na unyanyasaji unaweza kupiga 116 ili kuongea na<br />

mtaalam. Kwa maswali ya elimu ya afya ya uzazi piga 0800753333.


8


9


15

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!