27.12.2015 Views

MCHANGO WA MOFOLOJIA KATIKA ISIMU

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Chuo Kikuu cha Katoliki Afrika Mashariki<br />

Bewa la Langata<br />

Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Kijamii;<br />

Kitivo cha Elimu<br />

Idara ya Kiswahili<br />

Kozi: Kis 300; Mofolojia ya Kiswahili<br />

Kazi ya Muhula: Mchango wa mofolojia katika taaluma nzima ya isimu.<br />

Mwanafunzi wa shahada ya kwanza;<br />

1024584 Chaka Jumaa Ngombeko<br />

@jumaachaka<br />

Chaka Jumaa Nazarety<br />

Agosti-Disemba; 2015<br />

1


UTANGULIZI.<br />

Isimu hushughulikia uchunguzi wa lugha mbalimbali kwa kutumia misingi ya kisayansi.<br />

Matawi ya isimu kama fonetiki, fonolojia, semantiki, mofolojia na sintaksia ndiyo huifanya<br />

isimu kuonekana kuwa sayansi ya lugha kulingana na majukumu mbalimbali yanayofanywa<br />

na matawi haya katika lugha.<br />

Fonetiki huchunguza sauti za lugha ya binadamu; nayo fonolojia huchunguza jinsi sauti hizo<br />

huweza kuunganisha na kuunda maneno yenye maana na baadaye mofolojia huangalia maneno<br />

yaliyoundwa miundo yake na kuzalisha maneno zaidi.<br />

Mofolojia ni taaluma ya isimu ambayo ina jukumu la kuchunguza maneno ili kuelewa maumbo<br />

yake yalivyo (Mgullu, 1999).<br />

<strong>MCHANGO</strong> <strong>WA</strong> <strong>MOFOLOJIA</strong> <strong>KATIKA</strong> TAALUMA NZIMA YA <strong>ISIMU</strong>.<br />

Matthews (1991, Uk3) Mofolojia ni tawi la isimu linaloshughulika na ustadi wa maumbo ya<br />

maneno na jinsi maumbo hayo yanavyotumika katika miktadha mbalimbali ya matumizi ya<br />

lugha. Jukumu la neno husika katika sentensi hubainika vyema kulingana na uhusiano baina<br />

ya maneno mengine katiaka tungo. Kwa mfano: Jumaa amefika chuoni. Jumaa ni kiima kwani<br />

ndilo neno linalohusika na utendaji ilhali amefika chuoni ni kiarifu kwani sehemu hii inatoa<br />

maelezo juu ya kiima.<br />

Maneno ni maumbo katika lugha yanayojisimamia. Maneno yenye maumbo sahili huwa na<br />

mofu moja tu; hayawezi kukatwakatwa na kutoa mofu zingine. Mofu hizi ni mofu huru. Kwa<br />

mfano baba, mama. Kwa upande mwingine maneno yenye maumbo changamani huwa na<br />

mofu zaidi ya moja; yaani kiambishi awali, mzizi na kiambishi tamati. Kwa mfano;<br />

Mtangazaji {M+tangaz+a+ji}<br />

{M}-kiambishi awali cha kunominisha;<br />

{-tangaz-} mzizi wa nomino<br />

{-a-} kiambishi tamati endelezi<br />

{-ji} kiambishi tamati cha kunominisha<br />

Bauer Laurie (2003, Uk 91), taaluma ya mofolojia imegawanywa katika matawi mawili;<br />

mofolojia ya minyambuliko ya maneno na mofolojia ya uundaji wa maneno. Mofolojia ya<br />

minyambuliko ya maneno husaidia kupatikana kwa maumbo mbalimbali ya leksimu ilhali<br />

mofolojia ya uundaji wa maneno husaidia kupatikana kwa leksimu mpya. Maneno<br />

yanapoundwa husaidia katika kuboresha mawasiliano baina ya binadamu. Watumiaji wa lugha<br />

2


hutafuta njia mbalimbali ili kupata maneno yanayotosheleza mawasiliano yao. Hivyo basi<br />

mofolojia imejenga isimu-jamii.<br />

Matthews (1991, Uk9) mofolojia ni tawi la kisarufi linalochunguza maumbo ya ndani ya<br />

maneno. Mofolojia hutilia maanani sarufi ambayo ndiyo sehemu muhimu ya kila lugha. Sarufi<br />

ndiyo uti wa mgongo wa kila lugha hapa duniani. Bila sarufi lugha haiwezi kuwa na muundo<br />

sanifu unaokubalika na wenye kueleweka na watumiaji wake. Mofolojia huangalia hijai.<br />

Mofolojia huhakikisha maneno yameendelezwa vizuri. Ni sehemu hii ndiyo inaonyesha jinsi<br />

mofolojia huchunguza muundo wa maneno ambayo yameundwa kwa kutegemea taaluma ya<br />

fonolojia.<br />

Matthews (1991, Uk 63) mofolojia pia huonyesha mifanyiko mbalimbali ya maneno katika<br />

lugha. Kwa mfano nomino huweza kuundwa kutokana na vitenzi, kiwakilishi, vivumishi,<br />

kielezi. Katika lugha ya Kiingereza maumbo ya nomino hutokana na maumbo ya vitenzi<br />

yanapoongezewa mofu –ion-. Kwa mfano:generate-generation.<br />

Katika lugha ya Kiswahili aina ya neno huweza kubadilika linapoambishwa au kunyambuliwa.<br />

Kwa mfano: nomino msomi inaweza kuzalisha maneno kama kisomo, masomo, somea, someka,<br />

kusomeka.<br />

Mofolojia huhusika na utambuzi wa mofu, mofimu, shina, mzizi na alomofu katika neno.<br />

Dhana hizi ambazo zilizalishwa na taaluma ya mofolojia husaidia katika taaluma nzima ya<br />

isimu ambapo dhana hizi huleta maana katika maneno ya lugha. Maana inayopatikana katika<br />

maneno ya lugha ndiyo semantiki.<br />

Mgullu (1999), mofu ni umbo la neno ambalo huwakilisha mofimu na ambalo hudhihirika<br />

kifonolojia. Mofu ni sehemu halisi ya neno ambayo ina maana.<br />

Mtangazaji (M+tangaz+a+ji)<br />

{M} kiambishi awali cha kunominisha;<br />

{-tangaz-} mzizi wa nomino<br />

{-a-} kiambishi tamati endelezi mofimu<br />

{-ji} kiambishi tamati cha kunominisha<br />

Kumekuwa na swala la kuainisha lugha hasa katika karne ya Ishirini. Hapo mwanzo kulikuwa<br />

na haja ya kuelewa lugha ya kilatini na Kigiriki. Uelewa wa lugha zingine uliendelea kukua<br />

pia; ndipo lugha zikaanza kuainishwa kifamilia. Katika taaluma ya mofolojia lugha<br />

zinaainishwa kulingana na muundo wa maneno ya lugha hizo. Kigezo hiki cha kimofolojia<br />

kinatupatia lugha ambishi na tenganishi (Matthews, 1991 uk3-4). Hii husaidia kutofautisha<br />

miundo ya maneno ya lugha mbalimbali. Hivyo basi mofolojia inasaidia kuelewa miundo ya<br />

3


maneno ya lugha. Pia wanaohitaji kujifunza lugha za kigeni huweza kujifunza kwa urahisi<br />

wanapoelewa muundo wa maneno ya lugha hiyo.<br />

Mgullu (1999, Uk 12), lugha ambishi ni ile lugha ambayo maneno yake huambishwa viambishi<br />

mbalimbali ambavyo huwakilisha maana mbalimbali; kwa mfano lugha ya Kiswahili- Neno:<br />

PIGA<br />

Anapiga<br />

Atapiga<br />

Alipigia<br />

Alipigiwa<br />

Matthews (1991, Uk 20) Lugha tenganishi ni ile aina ya lugha ambayo maumbo ya maneno<br />

yake huonekana tu kama mofu moja moja. Mfano ni Kituruki, Kichina na Kiingereza.<br />

Maumbo ya maneno ya lugha tenganishi hayaambishwi wala kunyambuliwa. (Mgullu, 1999<br />

Uk 12). Kwa mfano katika lugha ya Kiingereza;<br />

With,<br />

Rice.<br />

Matthews (1991, Uk 19), mofolojia imeleta mchango mkubwa katika isimu nzima. Mofolojia<br />

ni kiungo muhimu katika isimu. Mofolojia imeweka wazi masuala muhimu kuhusu maumbo<br />

ya maneno katika lugha zote duniani. Mofolojia imeweza kusaidia wanaisimu kutambua mofu,<br />

mofimu, na alomofu katika kuchunguza miundo ya maneno katika lugha.<br />

Kwa mfano; viambishi katika lugha ya Kiingereza hupatikana mwishoni mwa mzizi wa neno<br />

kwa sababu mara nyingi huonyesha dhana ya wingi; kama –s, ies, ren, (child-children). Katika<br />

lugha ya Kiswahili mara nyingi mzizi wa neno hutanguliwa na mofu ambayo ni kiambishi<br />

awali na kisha kufuatiwa na kiambishi tamati. Haya ni yale maneno ambayo yana mofu<br />

tegemezi. Kwa mfano:<br />

-endnaenda<br />

Siendi<br />

Endea<br />

Endeleza<br />

Hivyo basi mofolojia imesaidia kujua maumbo ya maneno ya lugha mbalimbali.<br />

Matthews (1991, Uk 19-20) mofolojia inaeleza jinsi maneno katika lugha yanavyobadilika hasa<br />

kimaendelezo jinsi muda unavyosonga. Hapa mofoloia hujikita kuangalia mabadiliko ya<br />

maneno katika lugha husika kwa kuzingatia vipindi vya kihistoria. Mahitaji ya kimatumizi ya<br />

maneno husika katika lugha ndiyo husukuma wanajamii kubadili dhana za kimatumizi ya<br />

4


maneno fulani kulingana na wakati huo. Kwa mfano; neno girl (gyrle) hapo kale lilikuwa<br />

linamaanisha mtoto wa kiume au wa kike lakini likafinyika kimaana na leo hii linarejelea tu<br />

mtoto wa kike. (http://www.etymonline.com/index.php?term=girl).<br />

Katika lugha ya Kiingereza kipashio –pter- kiliazimwa kutoka lugha ya Kigiriki kikiwa<br />

kinamaanisha unyoya feather au ubawa wing. Kipashio hiki kimetumika kuunda neno<br />

helicopter ambapo kifaa hiki kina tabia sawa na dhana ya kipashio hicho (Katamba na<br />

Stonham, 2006 Uk.22) Hivyo basi mofolojia imesaidia kueleza historia ya maneno katika<br />

lugha.<br />

Matthews (1991, Uk 37) mofolojia husaidia katika kupeana njia mbalimbali za uundaji wa<br />

maneno katika lugha. Hii ni kwa sababu kila lugha inakua kulingana na mahitaji ya jamii yake.<br />

Kila lugha inahitaji maneno mapya yaundwe kila siku kwa sababu jamii mbalimbali<br />

hutagusana kila siku. Ili kurahisisha mawasiliano lazima kuwe na maneno yanayoweza<br />

kusaidia kurahisisha mawasiliano ya watu wa jamii hizo tofauti. Pia maneno yanaweza<br />

kuundwa ili kupeana majina vitu vigeni; yaani vitu vinavyovumbuliwa kila siku kupitia<br />

teknolojia. Kuna njia kama mwambatano, kukopa, kubuni, akronimu. Maumbo ya maneno<br />

yanayoundwa hutegemea mazingira ya jamii na sheria inayothibiti uundaji wa maneno katika<br />

lugha hiyo. Hivyo basi mofolojia husaidia kuchagua njia mwafaka ya uundaji wa maneno<br />

kulingana na mazingira husika.<br />

(Katamba na Stonham, 2006 Uk. 78-79), mofolojia pia inadhihirisha uhusiano uliopo baina ya<br />

lugha moja na nyingine. Lugha nyingi duniani zinategemeana katika mawasiliano. Wenyeji wa<br />

lugha mbalimbali hulazimika kukopa maneno ya lugha za kigeni ili kusaidia katika<br />

mawasiliano. Mofu za kigeni zinapoingizwa katika lugha fulani husahihishwa na kufuata<br />

muundo wa maneno ya lugha husika kulingana na sheria ya uundaji wa maneno wa lugha hiyo.<br />

Hivyo basi mofolojia imesaidia lugha nyingi kuingiza mofu za kigeni na kukuza lugha hizo na<br />

kurahisisha mawasiliano.<br />

Taaluma ya mofolojia hueleza ni kwa nini majina mengine huwa na maumbo yale yale katika<br />

dhana ya umoja na wingi. Majina kama maziwa, mchanga, maji hubaki vivyo hivyo<br />

kimaandishi katika umoja na wingi. Mofolojia imerahisisha kueleweka kwa hali hii kwani<br />

majina mengine huwa tu na dhana ya wingi au umoja katika akili za wazungumzaji. Mofolojia<br />

hutumia mofu kapa kuonyesha umoja au wingi wa majina kama hayo.<br />

5


Kwa mfano:<br />

Wingi<br />

Maziwa<br />

umoja<br />

Ømaziwa<br />

Mofolojia ndiyo chanzo cha kujifunza msamiati. Wanafunzi hutumia elimu ya mofolijia ili<br />

kutambua maana ya maneno yanayoibuka kila wakati. Mofolojia huwa na sharia ambazo<br />

humwongoza msemaji kuongeza umilisi katika lugha.<br />

Mofolojia humhamasisha mwanafunzi kuhusu uandishi na usomaji bora katika lugha.<br />

Mwanafunzi huweza kujua namna ya kuandika maneno na maumbo yake mbalimbali.<br />

Msomaji anapotambua sheria ya uundaji wa maneno katika lugha na jinsi ya kuandika na<br />

kusoma maneno humrahisishia kusoma matini mbalimbali na kuzielewa vizuri. Mofolojia<br />

husaidia kujua maana ya maneno inayonuiwa katika mawasiliano ndani ya lugha. Maana ya<br />

maneno huenda yakabadilika kutegemea mazingira yalimowekwa. Maneno yanapowekwa<br />

pamoja na maneno mengine katika tungo huweza kuwa na maana. Hivyo basi mofolojia<br />

imejenga semantiki na sintaksia na kuifanya isimu nzima ikue (Nagy, Carlisle & Goodwin<br />

(2013).<br />

Maneno huweza kuwekwa katika makundi yaani ngeli. Nomino hugawanywa na kuainishwa<br />

kimakundi kulingana na sarufi; kila kundi likiwa na mabadiliko ya aina moja ya viambishi vya<br />

umoja na wingi (Kihore na wenzake, 2003).Mofolojia ndiyo imechangia kuainisha ngeli<br />

kisintaksia kwani maana ya maneno yanayofafanuliwa na taaluma ya mofolojia ndiyo<br />

huongoza uanishaji wa majina kisintaksia.<br />

6


Marejeleo:<br />

Bauer Laurie (2003), Introducing Linguistic Morphology: 2 nd Edition. Edinburgh. Edinburgh<br />

University Press.<br />

Katamba Francis and Stonham John (2006), Modern Linguistics Morphology: New York.<br />

PALGRAVE MACMILLAN.<br />

Kihore na wenzake (2003), Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: TUKI<br />

Matthews P. H (1991), Morphology (Second Edition): United Kingdom. Cambridge University<br />

Press.<br />

Mgullu R. S. (1999), Mtalaa wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Nairobi.<br />

Longhorn Kenya Ltd.<br />

Nagy, W. E., Carlisle, J. F, & Goodwin, A. P. (2013). Morphological Knowledge and Literacy<br />

Acquisition. Journal of Learning Disabilities, 47(1) 3–12. DOI: 10.1177/0022219413509967.<br />

7

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!