MCHANGO WA MOFOLOJIA KATIKA ISIMU
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
Chuo Kikuu cha Katoliki Afrika Mashariki<br />
Bewa la Langata<br />
Kitivo cha Sanaa na Sayansi za Kijamii;<br />
Kitivo cha Elimu<br />
Idara ya Kiswahili<br />
Kozi: Kis 300; Mofolojia ya Kiswahili<br />
Kazi ya Muhula: Mchango wa mofolojia katika taaluma nzima ya isimu.<br />
Mwanafunzi wa shahada ya kwanza;<br />
1024584 Chaka Jumaa Ngombeko<br />
@jumaachaka<br />
Chaka Jumaa Nazarety<br />
Agosti-Disemba; 2015<br />
1
UTANGULIZI.<br />
Isimu hushughulikia uchunguzi wa lugha mbalimbali kwa kutumia misingi ya kisayansi.<br />
Matawi ya isimu kama fonetiki, fonolojia, semantiki, mofolojia na sintaksia ndiyo huifanya<br />
isimu kuonekana kuwa sayansi ya lugha kulingana na majukumu mbalimbali yanayofanywa<br />
na matawi haya katika lugha.<br />
Fonetiki huchunguza sauti za lugha ya binadamu; nayo fonolojia huchunguza jinsi sauti hizo<br />
huweza kuunganisha na kuunda maneno yenye maana na baadaye mofolojia huangalia maneno<br />
yaliyoundwa miundo yake na kuzalisha maneno zaidi.<br />
Mofolojia ni taaluma ya isimu ambayo ina jukumu la kuchunguza maneno ili kuelewa maumbo<br />
yake yalivyo (Mgullu, 1999).<br />
<strong>MCHANGO</strong> <strong>WA</strong> <strong>MOFOLOJIA</strong> <strong>KATIKA</strong> TAALUMA NZIMA YA <strong>ISIMU</strong>.<br />
Matthews (1991, Uk3) Mofolojia ni tawi la isimu linaloshughulika na ustadi wa maumbo ya<br />
maneno na jinsi maumbo hayo yanavyotumika katika miktadha mbalimbali ya matumizi ya<br />
lugha. Jukumu la neno husika katika sentensi hubainika vyema kulingana na uhusiano baina<br />
ya maneno mengine katiaka tungo. Kwa mfano: Jumaa amefika chuoni. Jumaa ni kiima kwani<br />
ndilo neno linalohusika na utendaji ilhali amefika chuoni ni kiarifu kwani sehemu hii inatoa<br />
maelezo juu ya kiima.<br />
Maneno ni maumbo katika lugha yanayojisimamia. Maneno yenye maumbo sahili huwa na<br />
mofu moja tu; hayawezi kukatwakatwa na kutoa mofu zingine. Mofu hizi ni mofu huru. Kwa<br />
mfano baba, mama. Kwa upande mwingine maneno yenye maumbo changamani huwa na<br />
mofu zaidi ya moja; yaani kiambishi awali, mzizi na kiambishi tamati. Kwa mfano;<br />
Mtangazaji {M+tangaz+a+ji}<br />
{M}-kiambishi awali cha kunominisha;<br />
{-tangaz-} mzizi wa nomino<br />
{-a-} kiambishi tamati endelezi<br />
{-ji} kiambishi tamati cha kunominisha<br />
Bauer Laurie (2003, Uk 91), taaluma ya mofolojia imegawanywa katika matawi mawili;<br />
mofolojia ya minyambuliko ya maneno na mofolojia ya uundaji wa maneno. Mofolojia ya<br />
minyambuliko ya maneno husaidia kupatikana kwa maumbo mbalimbali ya leksimu ilhali<br />
mofolojia ya uundaji wa maneno husaidia kupatikana kwa leksimu mpya. Maneno<br />
yanapoundwa husaidia katika kuboresha mawasiliano baina ya binadamu. Watumiaji wa lugha<br />
2
hutafuta njia mbalimbali ili kupata maneno yanayotosheleza mawasiliano yao. Hivyo basi<br />
mofolojia imejenga isimu-jamii.<br />
Matthews (1991, Uk9) mofolojia ni tawi la kisarufi linalochunguza maumbo ya ndani ya<br />
maneno. Mofolojia hutilia maanani sarufi ambayo ndiyo sehemu muhimu ya kila lugha. Sarufi<br />
ndiyo uti wa mgongo wa kila lugha hapa duniani. Bila sarufi lugha haiwezi kuwa na muundo<br />
sanifu unaokubalika na wenye kueleweka na watumiaji wake. Mofolojia huangalia hijai.<br />
Mofolojia huhakikisha maneno yameendelezwa vizuri. Ni sehemu hii ndiyo inaonyesha jinsi<br />
mofolojia huchunguza muundo wa maneno ambayo yameundwa kwa kutegemea taaluma ya<br />
fonolojia.<br />
Matthews (1991, Uk 63) mofolojia pia huonyesha mifanyiko mbalimbali ya maneno katika<br />
lugha. Kwa mfano nomino huweza kuundwa kutokana na vitenzi, kiwakilishi, vivumishi,<br />
kielezi. Katika lugha ya Kiingereza maumbo ya nomino hutokana na maumbo ya vitenzi<br />
yanapoongezewa mofu –ion-. Kwa mfano:generate-generation.<br />
Katika lugha ya Kiswahili aina ya neno huweza kubadilika linapoambishwa au kunyambuliwa.<br />
Kwa mfano: nomino msomi inaweza kuzalisha maneno kama kisomo, masomo, somea, someka,<br />
kusomeka.<br />
Mofolojia huhusika na utambuzi wa mofu, mofimu, shina, mzizi na alomofu katika neno.<br />
Dhana hizi ambazo zilizalishwa na taaluma ya mofolojia husaidia katika taaluma nzima ya<br />
isimu ambapo dhana hizi huleta maana katika maneno ya lugha. Maana inayopatikana katika<br />
maneno ya lugha ndiyo semantiki.<br />
Mgullu (1999), mofu ni umbo la neno ambalo huwakilisha mofimu na ambalo hudhihirika<br />
kifonolojia. Mofu ni sehemu halisi ya neno ambayo ina maana.<br />
Mtangazaji (M+tangaz+a+ji)<br />
{M} kiambishi awali cha kunominisha;<br />
{-tangaz-} mzizi wa nomino<br />
{-a-} kiambishi tamati endelezi mofimu<br />
{-ji} kiambishi tamati cha kunominisha<br />
Kumekuwa na swala la kuainisha lugha hasa katika karne ya Ishirini. Hapo mwanzo kulikuwa<br />
na haja ya kuelewa lugha ya kilatini na Kigiriki. Uelewa wa lugha zingine uliendelea kukua<br />
pia; ndipo lugha zikaanza kuainishwa kifamilia. Katika taaluma ya mofolojia lugha<br />
zinaainishwa kulingana na muundo wa maneno ya lugha hizo. Kigezo hiki cha kimofolojia<br />
kinatupatia lugha ambishi na tenganishi (Matthews, 1991 uk3-4). Hii husaidia kutofautisha<br />
miundo ya maneno ya lugha mbalimbali. Hivyo basi mofolojia inasaidia kuelewa miundo ya<br />
3
maneno ya lugha. Pia wanaohitaji kujifunza lugha za kigeni huweza kujifunza kwa urahisi<br />
wanapoelewa muundo wa maneno ya lugha hiyo.<br />
Mgullu (1999, Uk 12), lugha ambishi ni ile lugha ambayo maneno yake huambishwa viambishi<br />
mbalimbali ambavyo huwakilisha maana mbalimbali; kwa mfano lugha ya Kiswahili- Neno:<br />
PIGA<br />
Anapiga<br />
Atapiga<br />
Alipigia<br />
Alipigiwa<br />
Matthews (1991, Uk 20) Lugha tenganishi ni ile aina ya lugha ambayo maumbo ya maneno<br />
yake huonekana tu kama mofu moja moja. Mfano ni Kituruki, Kichina na Kiingereza.<br />
Maumbo ya maneno ya lugha tenganishi hayaambishwi wala kunyambuliwa. (Mgullu, 1999<br />
Uk 12). Kwa mfano katika lugha ya Kiingereza;<br />
With,<br />
Rice.<br />
Matthews (1991, Uk 19), mofolojia imeleta mchango mkubwa katika isimu nzima. Mofolojia<br />
ni kiungo muhimu katika isimu. Mofolojia imeweka wazi masuala muhimu kuhusu maumbo<br />
ya maneno katika lugha zote duniani. Mofolojia imeweza kusaidia wanaisimu kutambua mofu,<br />
mofimu, na alomofu katika kuchunguza miundo ya maneno katika lugha.<br />
Kwa mfano; viambishi katika lugha ya Kiingereza hupatikana mwishoni mwa mzizi wa neno<br />
kwa sababu mara nyingi huonyesha dhana ya wingi; kama –s, ies, ren, (child-children). Katika<br />
lugha ya Kiswahili mara nyingi mzizi wa neno hutanguliwa na mofu ambayo ni kiambishi<br />
awali na kisha kufuatiwa na kiambishi tamati. Haya ni yale maneno ambayo yana mofu<br />
tegemezi. Kwa mfano:<br />
-endnaenda<br />
Siendi<br />
Endea<br />
Endeleza<br />
Hivyo basi mofolojia imesaidia kujua maumbo ya maneno ya lugha mbalimbali.<br />
Matthews (1991, Uk 19-20) mofolojia inaeleza jinsi maneno katika lugha yanavyobadilika hasa<br />
kimaendelezo jinsi muda unavyosonga. Hapa mofoloia hujikita kuangalia mabadiliko ya<br />
maneno katika lugha husika kwa kuzingatia vipindi vya kihistoria. Mahitaji ya kimatumizi ya<br />
maneno husika katika lugha ndiyo husukuma wanajamii kubadili dhana za kimatumizi ya<br />
4
maneno fulani kulingana na wakati huo. Kwa mfano; neno girl (gyrle) hapo kale lilikuwa<br />
linamaanisha mtoto wa kiume au wa kike lakini likafinyika kimaana na leo hii linarejelea tu<br />
mtoto wa kike. (http://www.etymonline.com/index.php?term=girl).<br />
Katika lugha ya Kiingereza kipashio –pter- kiliazimwa kutoka lugha ya Kigiriki kikiwa<br />
kinamaanisha unyoya feather au ubawa wing. Kipashio hiki kimetumika kuunda neno<br />
helicopter ambapo kifaa hiki kina tabia sawa na dhana ya kipashio hicho (Katamba na<br />
Stonham, 2006 Uk.22) Hivyo basi mofolojia imesaidia kueleza historia ya maneno katika<br />
lugha.<br />
Matthews (1991, Uk 37) mofolojia husaidia katika kupeana njia mbalimbali za uundaji wa<br />
maneno katika lugha. Hii ni kwa sababu kila lugha inakua kulingana na mahitaji ya jamii yake.<br />
Kila lugha inahitaji maneno mapya yaundwe kila siku kwa sababu jamii mbalimbali<br />
hutagusana kila siku. Ili kurahisisha mawasiliano lazima kuwe na maneno yanayoweza<br />
kusaidia kurahisisha mawasiliano ya watu wa jamii hizo tofauti. Pia maneno yanaweza<br />
kuundwa ili kupeana majina vitu vigeni; yaani vitu vinavyovumbuliwa kila siku kupitia<br />
teknolojia. Kuna njia kama mwambatano, kukopa, kubuni, akronimu. Maumbo ya maneno<br />
yanayoundwa hutegemea mazingira ya jamii na sheria inayothibiti uundaji wa maneno katika<br />
lugha hiyo. Hivyo basi mofolojia husaidia kuchagua njia mwafaka ya uundaji wa maneno<br />
kulingana na mazingira husika.<br />
(Katamba na Stonham, 2006 Uk. 78-79), mofolojia pia inadhihirisha uhusiano uliopo baina ya<br />
lugha moja na nyingine. Lugha nyingi duniani zinategemeana katika mawasiliano. Wenyeji wa<br />
lugha mbalimbali hulazimika kukopa maneno ya lugha za kigeni ili kusaidia katika<br />
mawasiliano. Mofu za kigeni zinapoingizwa katika lugha fulani husahihishwa na kufuata<br />
muundo wa maneno ya lugha husika kulingana na sheria ya uundaji wa maneno wa lugha hiyo.<br />
Hivyo basi mofolojia imesaidia lugha nyingi kuingiza mofu za kigeni na kukuza lugha hizo na<br />
kurahisisha mawasiliano.<br />
Taaluma ya mofolojia hueleza ni kwa nini majina mengine huwa na maumbo yale yale katika<br />
dhana ya umoja na wingi. Majina kama maziwa, mchanga, maji hubaki vivyo hivyo<br />
kimaandishi katika umoja na wingi. Mofolojia imerahisisha kueleweka kwa hali hii kwani<br />
majina mengine huwa tu na dhana ya wingi au umoja katika akili za wazungumzaji. Mofolojia<br />
hutumia mofu kapa kuonyesha umoja au wingi wa majina kama hayo.<br />
5
Kwa mfano:<br />
Wingi<br />
Maziwa<br />
umoja<br />
Ømaziwa<br />
Mofolojia ndiyo chanzo cha kujifunza msamiati. Wanafunzi hutumia elimu ya mofolijia ili<br />
kutambua maana ya maneno yanayoibuka kila wakati. Mofolojia huwa na sharia ambazo<br />
humwongoza msemaji kuongeza umilisi katika lugha.<br />
Mofolojia humhamasisha mwanafunzi kuhusu uandishi na usomaji bora katika lugha.<br />
Mwanafunzi huweza kujua namna ya kuandika maneno na maumbo yake mbalimbali.<br />
Msomaji anapotambua sheria ya uundaji wa maneno katika lugha na jinsi ya kuandika na<br />
kusoma maneno humrahisishia kusoma matini mbalimbali na kuzielewa vizuri. Mofolojia<br />
husaidia kujua maana ya maneno inayonuiwa katika mawasiliano ndani ya lugha. Maana ya<br />
maneno huenda yakabadilika kutegemea mazingira yalimowekwa. Maneno yanapowekwa<br />
pamoja na maneno mengine katika tungo huweza kuwa na maana. Hivyo basi mofolojia<br />
imejenga semantiki na sintaksia na kuifanya isimu nzima ikue (Nagy, Carlisle & Goodwin<br />
(2013).<br />
Maneno huweza kuwekwa katika makundi yaani ngeli. Nomino hugawanywa na kuainishwa<br />
kimakundi kulingana na sarufi; kila kundi likiwa na mabadiliko ya aina moja ya viambishi vya<br />
umoja na wingi (Kihore na wenzake, 2003).Mofolojia ndiyo imechangia kuainisha ngeli<br />
kisintaksia kwani maana ya maneno yanayofafanuliwa na taaluma ya mofolojia ndiyo<br />
huongoza uanishaji wa majina kisintaksia.<br />
6
Marejeleo:<br />
Bauer Laurie (2003), Introducing Linguistic Morphology: 2 nd Edition. Edinburgh. Edinburgh<br />
University Press.<br />
Katamba Francis and Stonham John (2006), Modern Linguistics Morphology: New York.<br />
PALGRAVE MACMILLAN.<br />
Kihore na wenzake (2003), Sarufi Maumbo ya Kiswahili Sanifu. Dar es Salaam: TUKI<br />
Matthews P. H (1991), Morphology (Second Edition): United Kingdom. Cambridge University<br />
Press.<br />
Mgullu R. S. (1999), Mtalaa wa Isimu: Fonetiki, Fonolojia na Mofolojia ya Kiswahili. Nairobi.<br />
Longhorn Kenya Ltd.<br />
Nagy, W. E., Carlisle, J. F, & Goodwin, A. P. (2013). Morphological Knowledge and Literacy<br />
Acquisition. Journal of Learning Disabilities, 47(1) 3–12. DOI: 10.1177/0022219413509967.<br />
7