You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
TAASISI YA ELIMU TANZANIA<br />
``<br />
KUSOMA NA KUANDIKA<br />
KITABU CHA MWALIMU DARASA LA KWANZA<br />
USER<br />
2014<br />
T E T . S . L . P 35094 - D A R ES S A L A A M
2014<br />
Yaliyom0<br />
Ukurasa<br />
SHUKURANI…………………………………………………………………………<br />
UTANGULIZI………………………………………………………………………..<br />
SURA<br />
KWANZA……………………………………………………………………<br />
YA<br />
2
KUSALIMIANA NA KUAGANA………………………………<br />
Somo la 1: Tusalimiane asubuhi…………………………………………………..<br />
Somo la 2: Tusalimiane mchana………………………………………………….<br />
Somo la 3: Tuagane………………………………………………………………………<br />
SURA YA PILI……………………………………………………………………………<br />
TUJITAMBULISHE…………………………………………………………………………<br />
Somo la 4: Tujitambulishe kwa majina…………………………………………<br />
Somo la 5: Tutambulishane………………………………………………………….<br />
SURA YA TATU…………………………………………………………………………<br />
TUTAJE MAJINA YA VITU MBALIMBALI………………………………………..<br />
Somo la 6: Tutaje vitu vilivyo karibu……………………………………………<br />
Somo la 7: Tutaje vitu vilivyo mbali…………………………………………….<br />
SURA YA NNE…………………………………………………………………………<br />
TUHESABU VITU………………………………………………………………………..<br />
Somo La 8: Tutaje vitu vinavyohesabika……………………………………..<br />
Somo la 9: Tutaje vitu visivyohesabika……………………………………….<br />
SURA YA TANO………………………………………………………………………<br />
TUOMBE KITU AU HUDUMA………………………………………………………<br />
Somo la 10: Tuombe kwa adabu………………………………………………..<br />
Somo la 11: Tukubali kwa adabu………………………………………………..<br />
Somo la 12: Tukatae kwa adabu…………………………………………<br />
Somo la 13: Tushukuru kwa adabu……………………………………<br />
Somo la 14: Tuombe radhi…………………………………………………<br />
SURA YA SITA…………………………………………………………………<br />
KUSOMA KWA UTAMBUZI NA KUANDIKA……………………………<br />
3
Herufi na silabi……………………………………………………………….<br />
Somo la 15: Irabu a ……………………………………………………………<br />
Somo la 16: Irabu e…………………………………………<br />
Somo la 17: Irabu i………………………………………….<br />
Somo la 18: Irabu o…………………………………………<br />
Somo la 19: Irabu u…………………………………………<br />
Somo la 20: Herufi b …………………………………………………………<br />
Somo la 21: Herufi ch ………………………<br />
Somo la 22: Herufi d……………………………………….<br />
Somo la 23: Herufi f………………………………………..<br />
Somo la 24: Herufi g………………………<br />
Somo la 25: Herufi h………………………………<br />
Somo la 26: Herufi j………………………………………..<br />
Somo la 27: Herufi k……………………………………….<br />
Somo la 28: Herufi l…………………………………………<br />
Somo la 29: Herufi m……………………………………….<br />
Somo la 30: Herufi n………………………………………..<br />
Somo la 31: Herufi p…………………………………………<br />
Somo la 32: Herufi r…………………………………………<br />
Somo la 33: Herufi s…………………………………………<br />
Somo la 34: Herufi t…………………………………………<br />
Somo la 35: Herufi v………………………………………..<br />
Somo la 36: Herufi w……………………………………….<br />
Somo la 37: Herufi y………………………………………..<br />
Somo la 38: Herufi z……………………………………….<br />
Herufi Mwambatano…………………………………………………….<br />
Somo la 39: Herufi bw………………………………………………………<br />
4
Somo la 40: Herufi chw……………………………………<br />
Somo la 41: Herufi dh……………………………………..<br />
Somo la 42: Herufi fy………………………………………<br />
Somo la 43: Herufi gw………………………………………………………<br />
Somo la 44: Herufi kw………………………………………………………<br />
Somo la 45: Herufi mb……………………………………..<br />
Somo la 46: Herufi mf………………………………………<br />
Somo la 47: Herufi mk………………………………………<br />
Somo la 48: Herufi ml……………………………………….<br />
Somo la 49: Herufi mp………………………………………<br />
Somo la 50: Herufi mt……………………………………….<br />
Somo la 51: Herufi mv………………………………………<br />
Somo la 52: Herufi mw……………………………………<br />
Somo la 53: Herufi mz…………………………………….<br />
Somo la 54: Herufi nd…………………………………….<br />
Somo la 55: Herufi ng…………………………………….<br />
Somo la 56: Herufi ng’……………………………………<br />
Somo la 57: Herufi ny…………………………………….<br />
Somo la 58: Herufi py…………………………………….<br />
Somo la 59: Herufi pw……………………………………<br />
Somo la 60: Herufi sh…………………………………….<br />
Somo la 61: Herufi sk…………………………………….<br />
Somo la 62: Herufi st……………………………………..<br />
Somo la 63: Herufi sw……………………………………<br />
Somo la 64: Herufi th…………………………………….<br />
Somo la 65: Herufi tw…………………………………….<br />
Somo la 66: Herufi vy…………………………………….<br />
5
Somo la 67: Herufi chw………………………………….<br />
Somo la 68: Herufi mbw…………………………………<br />
Somo la 69: Herufi ngw………………………………….<br />
Somo la 70: Herufi mpw…………………………………<br />
Somo la 71: Herufi nyw………………………………….<br />
KUSOMA NA KUANDIKA NAMBA<br />
Somo la 72: Kusoma na kuandika namba 0, 1, 2 …………………………………<br />
Somo la 73: Kusoma na kuandika namba 3, 4, 5……………………<br />
Somo la 74: Kusoma na kuandika namba 6, 7, 8, 9…………………<br />
Herufi kubwa na ndogo…………………………………….<br />
Somo la 75: Aa……………………………………………………….<br />
Somo la 76: Bb………………………………………………………..<br />
Somo la 77: Cc………………………………………………………..<br />
Somo la 78: Dd………………………………………………………..<br />
Somo la 79: Ee………………………………………………………..<br />
Somo la 80: Ff…………………………………………………………<br />
Somo la 81: Gg………………………………………………………..<br />
Somo la 82: Hh………………………………………………………..<br />
Somo la 83: Ii………………………………………………………….<br />
Somo la 84: Jj…………………………………………………………<br />
Somo la 85: Kk………………………………………………………..<br />
Somo la 86: Ll…………………………………………………………<br />
Somo la 87: Mm………………………………………………………<br />
Somo la 88: Nn………………………………………………………..<br />
Somo la 89: Oo……………………………………………………….<br />
Somo la 90: Pp…………………………………………………………<br />
6
Somo la 91: Rr…………………………………………………………<br />
Somo la 92: Ss………………………………………………….<br />
Somo la 93: Tt…………………………………………………..<br />
Somo la 94: Uu…………………………………………………<br />
Somo la 95: Vv…………………………………………………<br />
Somo la 96: Ww………………………………………………..<br />
Somo la 97: Yy…………………………………………………<br />
Somo la 98: Zz…………………………………………………<br />
SURA YA SABA……………………………………………..<br />
TUTOE NA TUTEKELEZE AMRI……………………….<br />
Somo la 99: Tutii amri………………………………………..<br />
SURA YA NANE………………………………………………………………….<br />
TUSIMULIE MATUKIO………………………………..<br />
Somo la 100: Matukio ya wakati uliopo……………………….<br />
Somo la 101: Matukio ya wakati uliopita……………………..<br />
SURA YA TISA………………………………………………………………………<br />
TUTAMBUE RANGI………………………………………………………………….<br />
Somo la 102: Tuzijue rangi…………………………………………………….<br />
Somo la 103: Tutumie rangi……………………………………………………<br />
SURA YA KUMI…………………………………………………………………….<br />
UFAHAMU………………………………………………………………………………<br />
Somo la 104: Kusoma kwa ufahamu………………………………………<br />
Somo la 105: Kusoma kwa burudani…………………………………….<br />
SURA YA KUMI NA MOJA<br />
TUJIELEZA KWA LUGHA YA KIFASIHI………………………………………………<br />
Somo la 106: Vitendawili……………………………………………………………….<br />
7
SHUKURANI<br />
Taasisi ya Elimu inawashukuru wafuatao kwa juhudi zao katika kuandaa kitabu hiki:<br />
Waandishi:<br />
Adelgot J.B. Mapunda…….Mkuza Mitaala, Taasisi ya Elimu Tanzania<br />
Safarani A. M. Kalole........Afisa Mitihani, Baraza la Mitihani Tanzania<br />
Theobald A. Mvungi……….Mkuza Mitaala Mstaafu, DSM<br />
Mhazili:<br />
Gladness M. Samiji<br />
Wasanii:<br />
Godwin Chipenya<br />
Idd Marumba<br />
Wapiga chapa……..?<br />
8
UTANGULIZI<br />
Madhumuni ya Kitabu hiki cha Kwanza cha Mwalimu ni kuwasaidia walimu na wakufunzi wa<br />
vyuo vya ualimu waweze kuwaongoza wanafunzi wao wapate maarifa na stadi za kusoma na<br />
kuandika. Stadi hizo ni muhimu katika ufundishaji wa lugha.<br />
Kimsingi mwanafunzi wa darasa la kwanza siku za awali inambidi aanze kwa kuyazoea<br />
mazingira ya shule. Katika sura ya kwanza mwalimu atawaongoza watoto katika matendo<br />
yafuatayo: Kusalimiana na kuagana, kujitambulisha na kutambulishana pia kuonesha vitu<br />
vilivyo karibu na vile vilivyo mbali. Baada ya hapo uandishi wa alfabeti na michoro utafuata na<br />
jinsi ya kuandika herufi ndogo na kubwa za alfabeti. Hatimaye wanafunzi watajifunza mambo<br />
mbalimbali kama ya hadithi na habari zinazoweza kuwajengea watoto maadili katika jamii yetu<br />
ya kitanzania.<br />
Mambo muhimu ya kuzingatia<br />
1. Mwongozo huu unakusudiwa kumsaidia mwalimu kufundisha kusoma na kuandika.<br />
Unampa mwalimu mbinu za kusoma na kuandika kwa kufuata hati ya wima yenye<br />
vikonyo. Mifano ya herufi hizo imeoneshwa kitabuni humu. Mwongozo huu unafuata<br />
mpangilio wa kufundisha kwa herufi moja moja za alfabeti. Herufi hutumika kama<br />
matofali ya kujengea nyumba. Tofali likiwa imara ndio na nyumba itakavyokuwa imara.<br />
Kwa hiyo lengo ni kumfundisha mwanafunzi amudu kutambua herufi na namba na<br />
kuziandika kwa hatua zilizooneshwa. Kila baada ya kufundisha herufi ya konsonanti,<br />
mwalimu unashauriwa ufundishe silabi zinazoendana nayo kwa kutumia irabu zote tano.<br />
2. Matumizi ya nomino za pekee yameelezwa kwa kuhusisha herufi kubwa. Ni muhimu<br />
mwalimu usisitize mambo haya.<br />
9
3. Mwanafunzi anatakiwa akae vizuri kitini ili aweze kuandika hati nzuri. Utaratibu huu<br />
hulinda afya yake pia. Pia mwanafunzi aelekezwe namna nzuri ya kushika kalamu. Ni<br />
muhimu sana mwanafunzi awe na vifaa hivi na umwelekeze jinsi ya kuvitumia: dawati,<br />
vibao vya kuandikia, daftari na kalamu.<br />
4. Ni lazima sana wanafunzi wapate mazoezi mengi ya kusoma na kuandika. Mazoezi haya<br />
yanaweza kuwa ya aina anuai. Kwa mfano kupanga herufi ili kupata maneno, kupanga<br />
sentensi ili kupata kifungu cha habari, kunakili kutoka ubaoni, imla, utungaji wa picha,<br />
kujibu maswali, kutunga sentensi, kuandika hadithi na nyinginezo. Ni muhimu uzingatie<br />
kuwa mazoezi yawe mafupi na yanayofurahisha wanafunzi.<br />
5. Katika sehemu ya Kusoma kwa ufahamu na Kusoma kwa burudani ni muhimu mwalimu<br />
uzingatie matumizi sahihi ya vituo ili kumjengea mwanafunzi matamshi na lafudhi<br />
sahihi ya Kiswahili.<br />
Kusalimiana na Kuagana<br />
Somo la 1: Tusalimiane asubuhi<br />
Sura ya Kwanza<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa usahihi katika muktadha wa kusalimiana na watu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kujieleza katika muktaha wa kusalimiana na watu<br />
mbalimbali wakati wa asubuhi.<br />
Muda: Vipindi 5<br />
Zana/vifaa: Picha za kusalimiana za watu mbalimbali<br />
Hatua:<br />
1. Wapange wanafunzi kwenye mduara kisha uwaelekeze waimbe wimbo wa<br />
“Tuamkapo asubuhi tuwasalimu wazazi, shikamoo baba, shikamoo mama. Hiyo<br />
ndiyo tabia njema.<br />
2. Wachague baadhi yao waeleze jinsi wanavyowaamkia wazazi wao asubuhi.<br />
Pia baadhi yao waeleze jinsi wanavyosalimiana wenyewe kwa wenyewe.<br />
3. Waongoze wanafunzi kutazama picha za kusalimiana zilizo kwenye kitabu chao.<br />
4. Waongoze wanafunzi waigize kusalimiana kama ilivyoonyeshwa katika kitabu chao<br />
zoezi A.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi zaidi ya kusalimiana bila ya kuangalia vitabu<br />
vyao.<br />
Tafakuri: Waongoze wanafunzi wajibu maswali haya ya tafakuri:<br />
1. Kusalimiana kuna faida gani?<br />
2. Wewe umefaidikaje na somo hili?<br />
10
Somo la 2: Tusalimiane mchana<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa usahihi katika muktadha wa kusalimiana na watu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kujieleza katika muktaha wa kusalimiana na watu<br />
mbalimbali wakati wa mchana.<br />
Muda: Vipindi 5<br />
Zana/vifaa: Picha za watu wa umri mbalimbali wakisalimiana.<br />
Hatua:<br />
2. Wasalimie wanafunzi kwa kusema: Habari za Mchana? Waelekeze wajibu. Ni nzuri,<br />
Shikamoo mwalimu.<br />
3. Itikia salamu kwa kusema Marahaba.<br />
4. Waongoze wanafunzi wasalimiane kwa kusema Habari za Mchana na kuitikia: Ni<br />
nzuri<br />
5. Waongoze wanafunzi watazame picha za kusalimiana wakati wa mchana zilizopo<br />
kwenye kitabu chao<br />
6. Waongoze wanafunzi waigize kusalimiana kama ilivyooneshwa katika kitabu chao zoezi<br />
B.<br />
7. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi zaidi ya kusalimiana mchana bila ya kuangalia<br />
vitabu vyao.<br />
Tafakuri: Katika somo lililopita tulijifunza kusalimiana asubuhi. Je, kuna tofauti gani na<br />
kusalimiana mchana?<br />
Somo la 3: Tusalimiane jioni<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika muktadha wa kusalimiana na watu.<br />
Muda: Vipindi 5.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kujieleza katika muktaha wa kusalimiana na watu<br />
mbalimbali wakati wa jioni.<br />
Zana/vifaa: Picha za watu mbalimbali wanaosalimiana.<br />
Hatua:<br />
1. Wasalimie wanafunzi kwa kusema: Habari za jioni? Waelekeze Wajibu. Ni nzuri,<br />
Shikamoo mwalimu.<br />
2. Itikia salamu kwa kusema Marahaba.<br />
3. Waongoze wanafunzi wasalimiane kwa kusema Habari za jioni na kuitikia: Ni nzuri<br />
4. Waongoze wanafunzi watazame picha za kusalimiana wakati wa jioni zilizopo kwenye<br />
kitabu chao zoezi C<br />
5. Waongoze wanafunzi waigize kusalimiana kama ilivyooneshwa katika kitabu chao zoezi<br />
C.<br />
6. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi zaidi ya kusalimiana wakati wa jioni bila ya<br />
kuangalia vitabu vyao.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Unafikiria tendo la kusalimiana jioni linaanza<br />
muda gani?<br />
Somo la 4: Tuagane<br />
11
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kuagana na watu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kujieleza katika kuaga.<br />
Kujieleza katika kuitikia anapoagwa.<br />
Muda: Vipindi 5<br />
Zana/vifaa: Picha za watu wanaoagana.<br />
Hatua:<br />
1. Wapange wanafunzi kwenye mduara kisha uwaelekeze waimbe wimbo wa<br />
“Kwaheri Mwalimu. Sasa ni saa ya kwenda kwetu………”<br />
2. Wachague baadhi yao waeleze jinsi wanavyowaaga wazazi wao.<br />
Pia baadhi yao waeleze jinsi wanavyoagana wenyewe kwa wenyewe.<br />
3. Waongoze wanafunzi watazame picha za kuagana zilizo kwenye kitabu chao.<br />
4. Waongoze wanafunzi waigize kuagana kama ilivyooneshwa katika kitabu chao<br />
zoezi D.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi zaidi ya kuagana bila ya kuangalia vitabu<br />
vyao.<br />
6. Fanya marudio na wanafunzi wako namna ya kusalimiana asubuhi, mchana, jioni<br />
na kisha kuagana kulingana na picha zilizooneshwa katika kitabu cha<br />
Mwanafunzi zoezi A, B, C na D. Wanafunzi wafanye marudio kwa kuonesha<br />
Vitendo.<br />
Waongoze wanafunzi watumie maneno haya katika kusalimiana<br />
Habari<br />
za<br />
asubuhi<br />
Shikamoo<br />
Umeshindaje Habari<br />
za<br />
mchana<br />
Habari<br />
za jioni<br />
Habari<br />
za usiku<br />
Umeamkaje<br />
Waongoze wanafunzi watumie maneno haya katika kuagana<br />
asubuhi<br />
njema,<br />
mchana<br />
mwema<br />
kazi<br />
njema<br />
jioni<br />
njema,<br />
kwaheri,<br />
usiku<br />
mwema<br />
lala<br />
salama,.<br />
usingizi<br />
mwema<br />
7. Wapime wanafunzi uelewa wao katika sura hii kwa kuwauliza maswali<br />
yafuatayo:<br />
a). Ni nani wanaoamkiwa shikamoo?<br />
b). Wazazi wanawasalimiaje watoto wao?<br />
c).Unamsalimiaje kaka asubuhi?<br />
d). Mwalimu anasalimiwaje?<br />
e). Unamsalimiaje rafiki yako mchana?<br />
f). mnamsalimiaje baba jioni?<br />
g). Unamuagaje mwalimu baada ya masomo?<br />
h). Unamuagaje baba yako mchana?<br />
i). Unamuagaje baba yako jioni?<br />
j). Kwa nini tunawasalimu wazazi wetu?<br />
12
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Unafikiri kwa nini watu wanaagana?<br />
13
Sura ya pili<br />
TUJITAMBULISHE<br />
Somo la 1: Tujitambulishe kwa majina<br />
Ujuzi: Kujitambulisha kwa ufasaha.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kujitambulisha mwenyewe kwa mtu/ watu wengine.<br />
Muda: Vipindi 7<br />
Zana/vifaa: Picha za watu wanaotambulishana.<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi waimbe wimbo wa: “Mwenzetu unaitwa nani? Naitwa<br />
Neema. Rafiki unaitwa nani? Ninaitwa Mapunda”.<br />
2. Wapange wanafunzi katika jozi kisha wajitambulishe kwa majina na sehemu<br />
wanazotoka..<br />
3.<br />
4. Rudia kuwaongoza hivyo mara nyingi hadi kila mwanafunzi aweze kujitambulisha<br />
kwa ufasaha na kwa kujiamini.<br />
5. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya pili, na waigize<br />
matendo ya kujitambulisha yaliyopo katika picha hizo.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Kuna faida gani ya kujiambulisha?<br />
Somo la 2: Tutambulishane<br />
Ujuzi: Kuwatambulisha watu wengine kwa ufasaha na kwa kujiamini<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kumtambulisha mtu kwa watu wengine kwa ufasaha.<br />
Muda: Vipindi 7<br />
Zana/vifaa: Picha za watu wanaotambulishana.<br />
Hatua:<br />
1. Wapange wanafunzi katika jozi kisha kila mmoja amtambulishe mwenzake kwa jina.<br />
2. Waongoze baadhi ya wanafunzi waende mbele ya darasa na kujipanga katika<br />
makundi matatu ya wanafunzi watano watano.<br />
3. Waongoze wanafunzi mmoja mmoja kwa kila kundi awatambulishe wenzake kwa<br />
mwalimu akitaja jina.<br />
4. Rudia kuwaongoza hivyo mara nyingi hadi kila mwanafunzi aweze kuwatambulisha<br />
wengine kwa ufasaha na kwa kujiamini.<br />
5. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya pili, na waigize<br />
matendo ya kuwatambulisha wengine yaliopo katika picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi ya kutambulishana zaidi darasani. Wafanye<br />
kama mchezo ufuatao:<br />
14
Juma: Yule nani?<br />
Maria: John<br />
8. Mwalimu wapime wanafunzi uelewa wao katika somo hili kwa kuwauliza<br />
maswali kwa mfano:<br />
1. Mwalimu wenu anaitwa nani?<br />
2. Rafiki yako anaitwa nani?<br />
3. Wewe unaitwa nani?<br />
4. Unayekaa karibu naye darasani anaitwa nani?<br />
5. Dada yako anaitwa nani?<br />
6. Kaka yako anaitwa nani?<br />
Tafakuri: Mwalimu waongoze wanafunzi watafakari waliyojifunza katika somo hili kwa<br />
kuwauliza maswali. Kwa mfano, kuna faida gani kujua jina la mwenzako?<br />
15
Sura ya tatu<br />
TUTAJE MAJINA YA VITU MBALIMBALI<br />
Somo la 1: Tutaje vitu vilivyo karibu<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa kutaja majina ya vitu villivyo karibu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kutambua vitu vilivyo karibu katika umoja na wingi.<br />
Muda: Vipindi 7<br />
Zana/vifaa: viti, meza, madawati, kalamu, chaki na ubao<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi waoneshe vitu vilivyo karibu nao. Waongoze wavitaje vitu<br />
hivyo katika umoja na wingi.<br />
2. Waongoze wanafunzi wachache waende mbele ya darasa na kujipanga katika<br />
makundi ya wanafunzi watano watano. Kisha waongoze kila mwanakikundi ataje<br />
vitu vilivyo nyumbani kwao.<br />
3. Waongoze wanafunzi waangalie picha katika vitabu vyao sura ya tatu zoezi A<br />
kuhusu vitu vilivyo karibu.<br />
4. Wanafunzi wajibu kwa mdomo maswali yaliyo chini ya picha hizo.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi ya marudio ya kutaja vitu vilivyo karibu<br />
darasani mwao. Vitu hivyo ni kama; vitabu, madawati, rula, chaki na ubao wa<br />
mwalimu.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Je, unafurahia kujua majina ya vitu mbalimbali?<br />
Somo la 2: Tutaje vitu vilivyo mbali<br />
Ujuzi: Kujieleza katika umoja na wingi kwa vitu vilivyo karibu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kutambua vitu vilivyo mbali katika umoja na wingi.<br />
Muda: Vipindi 7<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha vitu vilivyo mbali nje ya darasa<br />
kama miti, milima, barabara, mawe, ua na maua.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe kisha waongoze wanafunzi wataje majina ya vitu mbalimbali<br />
vilivyochorwa katika kadi.<br />
2. Wapange wanafunzi katika makundi ya watano watano kisha watoke nje ya darasa na<br />
kuangalia vitu mbalimbali kama miti, majani, maua na kadhalika.wazunguke<br />
walivyoona. .<br />
3.<br />
3. 3.Baada ya kurudi darasani mwanafunzi mmoja baada ya mwingine aoneshe kitu<br />
kimoja anachokiona nje ya darasa, Kwa mfano zile ni kamba, ile ni miti.<br />
16
4. 4. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao, sura ya tatu zoezi B<br />
kuhusu vitu vilivyo mbali.<br />
5. 5.Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya tatu zoezi A na B kisha wajibu<br />
kwa mdomo maswali yafuatayo.<br />
a. Kitabu hiki kina rangi gani?<br />
b. Kisu kina kazi gani?<br />
c. Lile gari lina rangi gani?<br />
d. Mbele ya Mlima Kilimanjaro kuna nini?<br />
e. Vile vitunguu ni vingapi?<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Ni nini kilichokufurahisha katika somo hili?<br />
17
TUHESABU VITU<br />
Somo la 1: Tutaje vitu vinavyohesabika<br />
sura ya NNE<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kueleza vitu<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze: a). Kutaja vitu mbalimbali vinavyohesabika.<br />
b). Kuhesabu kwa usahihi vitu mbalimbali.<br />
Muda: Vipindi 12<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonyesha vitu vinavyohesabika kama vile<br />
kalamu, karatasi, kikombe, mayai, shati, gauni, daftari, dawati na kadhalika<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi wataje majina ya vitu mbalimbali vinavyohesabika<br />
vilivyochorwa katika kadi.<br />
2. Waoneshe wanafunzi vitu kama kalamu, karatasi, kikombe, mayai, shati, gauni,<br />
daftari, dawati kisha waulize kama vinaweza kuhesabika kwa mfano Je, tunaweza<br />
kuhesabu kalamu?<br />
3. Muite mwanafunzi mmoja mmoja apite mbele ya darasa na kuhesabu vitu hivyo.<br />
4. Waongoze wanafunzi mmoja baada ya mwingine aoneshe kitu kimoja anachokiona<br />
ndani ya darasa ambacho kinahesabika.<br />
5. Rudia kuwaongoza wanafunzi kutaja vitu vinavyohesabika hadi mwanafunzi wote<br />
waweze kuvitaja kwa usahihi na kwa kujiamini.<br />
6. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya nne zoezi A kuhusu<br />
vitu vinavyohesabika.<br />
7. Wanafunzi wajibu kwa mdomo maswali yaliyo chini ya picha za zoezi A.Wanafunzi<br />
warudie kufanya mazoezi katika kujibu maswali hayo mpaka kila mmoja wao<br />
ayamudu vizuri.<br />
18
8. Warejeshe wanafunzi katika mazungumzo mafupi yaliyo katika vitabu vyao sura ya<br />
nne zoezi A la vitu vinavyohesabika. Waongoze wanafunzi wayaigize.<br />
9. Waongoze wanafunzi wajibu maswali yafuatayo wakizingatia vitabu vyao sura ya<br />
nne zoezi A sehemu za vitu vinavyohesabika.<br />
Tafakuri: Waongoze wanafunzi watafakari walichojifunza katika somo hili kwa<br />
kuwauliza maswali. Kwa mfano,ukijua kuhesabu vitu unapata faida gani?<br />
Somo la 2: Tutaje vitu visivyohesabika<br />
Ujuzi: Kujieleza katika kutaja vitu visivyohesabika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kutaja majina ya vitu visivyohesabika.<br />
Muda: Vipindi 13<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha vitu visivyohesabika:<br />
maji, maziwa, sukari, mchanga, wino, unga na kadhalika<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi zilizochorwa vitu visivyohesabika kisha wataje majina ya<br />
vitu hivyo.<br />
2. Waongoze wanafunzi wataje vitu vingine visivyohesabika vilivyopo katika mazingira<br />
ya shuleni na nyumbani.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya nne zoezi B kuhusu<br />
vitu visivyohesabika.<br />
4. Kisha waongoze wajibu kwa mdomo maswali yaliyo chini ya picha hizo.Wanafunzi<br />
warudie kufanya mazoezi katika kujibu maswali hayo mpaka kila mmoja wao<br />
ayamudu vizuri.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi yafuatayo kwa ukizingatia picha zilizo<br />
katika kitabu cha mwanafunzu sura ya nne zoezi A na B kuhusu vitu vinavyohesabika<br />
na visivyohesabika.<br />
a. Darasani kwenu kuna madawati mangapi?<br />
b.<br />
c. Unaweza kula samaki wangapi?<br />
d.<br />
e. Una madaftari mangapi?<br />
f. Una kalamu ngapi?<br />
g. Darasani kwenu kuna mbao ngapi za kuandikia?<br />
h. Pale sokoni kwenu kuna maduka mangapi?<br />
i. Unapenda kunywa vikombe vingapi vya chai?<br />
Tafakuri: Mwalimu waulize wanafunzi swali hili. Je, umelifurahia somo hili? Kitu<br />
gani kimekufurahisha? Sehemu gani hukuilewa vizuri?.<br />
19
Sura ya tano<br />
Tuombe kitu au huduma<br />
Somo la 1: Tuombe kwa adabu<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kuomba kitu kwa adamu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuomba kitu kwa adabu.<br />
Muda: Vipindi 6<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonyesha matendo mbalimbali ya<br />
wanafunzi wakiomba vitu kwa adabu. Matendo hayo ni kama:<br />
Msichana anamwomba chakula mama yake.<br />
Mvulana anamwomba baba yake amnunulie kitabu.<br />
Hatua:<br />
1. Waulize wanafunzi, unapotaka kuomba kalamu, kitabu au chakula unasemaje?<br />
2. Wapange wanafunzi kutika jozi kisha waigize namna ya kuombana vitu mbalimbali<br />
kwa adabu.<br />
3. .<br />
4.<br />
3. Wabadilishe wanafunzi katika jozi ili waunde jozi nyingine kisha waendelee na zoezi<br />
hilo la kuombana vitu au huduma mbalimbali kwa adabu. Mwanafunzi mmoja<br />
amwombe mwenzake amuokotee kalamu au<br />
amchane nywele<br />
4.<br />
4.Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya tano zoezi A<br />
kuhusu kuomba vitu au huduma kwa adabu.<br />
5. Waongoze wanafunzi waigize matendo yaliyopo katika picha hizo.Wanafunzi<br />
warudie kufanya matendo ya kuigiza mpaka kila mmoja wao ayamudu vizuri.<br />
6. Waongoze wanafunzi watazame kadi zinazoonesha matendo mbalimbali ya<br />
wanafunzi wakiomba vitu kwa adabu<br />
7.<br />
Tafakuri: Mwalimu waulize wanafunzi swali hili.Kwa nini tunaomba kitu kwa adabu?<br />
Somo la 2: Tukubali kwa adabu<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kukubali kitu kwa adamu<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kukubali kitu au huduma kwa adabu.<br />
Muda: Vipindi 6<br />
Zana: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha matendo ya kukubali kwa adabu. Kadi<br />
ioneshe matendo kama hivi: Juma akipokea kitabu kwa adabu kutoka kwa mwalimu.<br />
Roza akipokea zawadi kwa adabu.kutoka kwa<br />
shangazi<br />
20
Hatua:<br />
1. Waulize wanafunzi, unapopewa zawadi na kukubali kuipokea unafanyaje?<br />
2. Wapange wanafunzi katika jozi.<br />
3. Waongoze wanafunzi waigize kukubali kitu au huduma kwa adabu.<br />
4. Wapange wanafunzi katika jozi kisha waigize namna ya kukubali kitu au huduma kwa adabu.<br />
4. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya tano kuhusu zoezi B<br />
kuhusu kukubali vitu au huduma kwa adabu.<br />
5. Waongoze wanafunzi waigize matendo yaliyomo katika picha za zoezi B .<br />
6. Wanafunzi warudie kufanya matendo ya kuigiza mpaka kila mmoja wao ayamudu vizuri.<br />
7. Waongoze wanafunzi watazame kadi zinazoonesha matendo ya kukubali kwa adabu kisha<br />
waigize matendo yaliyo katika kadi hizo.<br />
8.<br />
9.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili Je unafurahia mtu akikubali kitu kwa adabu?<br />
Somo la 3: Tukatae kwa adabu<br />
Somo la 3: Tukataa kwa adabu<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kukataa kitu au huduma kwa adamu<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kukataa kitu au huduma kwa adabu.<br />
Muda: Vipindi 6<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha matendo ya kukataa kwa adabu.<br />
Matendo kama: Mvulana anakataa kupokea sahani ya matunda kwa kuonesha<br />
viganja. Msichana anakaribishwa soda na mvulana lakini anaikataa kwa adabu.<br />
Hatua:<br />
1. Waulize wanafunzi, unapokataa kitu unasemaje?<br />
2. Wapange wanafunzi kwa jozi darasani<br />
3. Waongoze wanafunzi katika jozi wachunguze picha zilizo kwenye kadikisha waigize<br />
matendo yatokanayo na kadi hizo wakitumia maneno kama samahani, sihitaji, nimetosheka,<br />
nimeshahudumiwa na kadhalika.<br />
4. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya tano zoezi C kuhusu<br />
kukataa vitu au huduma kwa adabu kisha waigize matendo ya picha hizo.<br />
5. .Wanafunzi warudie kufanya matendo ya kuigiza mpaka kila mmoja wao ayamudu vizuri.<br />
6. Mwalimu tunga wimbo au dayolojia inayohusu kukataa kwa adabu kisha wanafunzi<br />
waimbe au kuigiza<br />
Tafakuri: Mwalimu waulize wanafunzi Je, unaweza kukataa kwa adabu? Onesha namna<br />
21
unavyoweza kukataa kwa adabu?<br />
Somo la 4: Tushukuru kwa adabu<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kushukuru kwa adamu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kushukuru kwa adabu.<br />
Muda: Vipindi 6<br />
Zana/vifaa: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha matendo ya kushukuru kwa<br />
adabu. Matendo hayo ni kama; mtoto anamshukuru mama yake baada ya kula. Babu<br />
anamshukuru mjukuu kwa kumpa fedha.<br />
Hatua:<br />
1. Waulize wanafunzi, unapopewa zawadi unasemaje?<br />
2. Wapange wanafunzi katika jozi kisha wachunguze picha zilizo kwenye kadi na waigize<br />
matendo yatokanayo na kadi hizo wakitumia maneno kama asanteni sana, nashukuru,<br />
ahsante kwa kushukuru na kadhalika<br />
3.<br />
4.<br />
5. Waongoze wanafunzi kuangalia picha katika vitabu vyao sura ya tano zoezi D kuhusu somo<br />
la kushukuru kwa adabu<br />
6. Waongoze wanafunzi waigize matendo yaliyomo katika picha hizo.Wanafunzi warudie<br />
kufanya matendo ya kuigiza mpaka kila mmoja wao ayamudu vizuri.<br />
7. Mwalimu tunga wimbo au mazungumzo yanayohusu kushukuru kwa adabu kisha<br />
wanafunzi waimbe au waigize mazungumzo hayo..<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Unawashukuruje wazazi wako wanapokupa zawadi?<br />
NIMEKOMEA HAPA KWA LEO<br />
Somo la 5: Tuombe Radhi<br />
Ujuzi: Kujieleza kwa ufasaha katika kuomba radhi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuomba radhi kwa ufasaha..<br />
Muda: Vipindi 6<br />
Zana: Kadi mbalimbali zilizochorwa picha zinazoonesha matendo mbalimbali ya kuomba<br />
radhi. Kwa mfano: Mwanafunzi msichana anaomba radhi kwa mwalimu kwa<br />
kutohudhuria masomo kwa sababu ya kuumwa.<br />
Mfanyakazi mwanamume anaomba radhi kwa mwajiri wake kwa kuchelewa kufika<br />
kazini<br />
1. Hatua: Waulize wanafunzi, unapotaka kuomba radhi unasemaje?<br />
2. Wapange wanafunzi katika jozi kisha wachunguze picha zilizochorwa kwenye kadi<br />
zinazoonesha matendo mbalimbali ya kuomba radhi<br />
22
3. .<br />
4. Waongoze wanafunzi waigize matendo yaliyomo katika kadi hizo wakitumia maneno kama<br />
Samahani, naomba radhi, naomba nisamehe na kadhalika.<br />
5. Waongoze wanafunzi watazame picha katika vitabu vyao sura ya tano zoezi E kuhusu<br />
kuomba radhi.<br />
6. Waongoze waigize matendo yalio katika picha hizo.<br />
7. Wanafunzi warudie kufanya matendo ya kuigiza mpaka kila mmoja wao ayamudu vizuri.<br />
8. Mwalimu, tunga wimbo au mazungumzo yanayohusu kuomba radhi ili wanafunzi<br />
wayaigize.<br />
9. Waongoze wanafunzi wafanye zoezi F la marudio lililomo katika sura ya tano ili waweze<br />
kufanya marudio ya kuomba kitu au huduma kwa adabu, kukubali kwa adabu, kukataa kwa<br />
adabu, kushukuru kwa adabu na kuomba radhi kwa ufasaha..<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi maswali ili aweze kutafakari waliyojifunza katika somo hili.<br />
Kwa mfano, kumwomba mwenzako radhi kuna faida gani?<br />
23
Kusoma Kwa Utambuzi Na Kuandika<br />
Sura ya sita<br />
Somo la 1 a): Kusoma irabu a:<br />
Ujuzi: Kusoma herufi usahihi na kwa utambuzi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi a<br />
Muda: vipindi 2<br />
Zana: Kadi za herufi a na picha ya birika.<br />
Chora irabu hizi kwa kufuata zilivyoandikwa katika:Kitabu cha Kufundishia Kusoma na<br />
Kuandika, TPH<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi a ubaoni.<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne a a a a a ………..<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi a kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe unavyosoma,<br />
kwa safu na kisha mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi anaweza kuitambua<br />
vizuri herufi hiyo.<br />
8. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi a kwenye kadi hizo, baadaye<br />
iliyochorwa kikombe.<br />
9. Andika ubaoni herufi a nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome a hizo kwa pamoja, kwa vikundi na kisha mmoja mmoja<br />
Somo la 1 (b): Kuandika irabu a<br />
Ujuzi: kuandika herufi kwa usahihi Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi a kwa hati ya<br />
chapa yenye vikonyo.<br />
Muda: Kipindi 3<br />
Zana: Vijiti, kalamu, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni.<br />
Mchoro wa herufi a<br />
aaaaaaaaaaaaaaaaaaa<br />
24
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani kwa kutumia penseli..<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Kila mwanafunzi apewe kibao cha kuandikia kisha achore mchoro huo kwenye kibao kwa<br />
kutumia chaki.<br />
6. Waelekeze wanafunzi namna ya kushika penseli kwa usahihi.<br />
7. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na mwalimu apite akiwasaidia<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
8. Fuatisha herufi a kwa kurudia mchoro<br />
(Mchoro wa herufi a)<br />
10. Waongoze wanafunzi waandike herufi a ikiwa peke yake bila kuwa kwenye mchoro.<br />
11. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi a kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Kitu gani kimekufurahisha katika kujifunza<br />
kuandika herufu a ?<br />
Somo la 2 (a): Kusoma irabu e<br />
Ujuzi: Kusoma kwa usahihi na kwa utambuzi .<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi e<br />
Muda: Kipindi 2<br />
ZanaVifaa: Kadi za herufi e na picha ya pete<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi e ubaoni.<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne e e e e e ……..<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi e kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma, kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi anaweza kuitambua<br />
vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi e kwenye kadi hizo.<br />
6. Andika ubaoni herufi e nyingi za ukubwa tofauti kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome e hizo kwa pamoja, kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
25
Somo la 2 (b): Kuandika irabu e.<br />
Ujuzi: Kuandika he<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi e kwa hati ya chapa yenye vikonyo.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana/vifaa: Vijiti, kalamu, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
Mchoro wa herufi e<br />
eeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Waongoze wanafunzi waandike herufi e kwenye vibao vyao. Pia wajaze vibao vyao kwa<br />
kuandika herufi hiyo.<br />
6. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo madaftarini mwao na mwalimu apite akiwasaidia namna<br />
ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
(Mchoro wa herufi e)<br />
10. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi e kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Tafakuri: Kwa nini herufi e inafananishwa na umbo la embe?<br />
Somo la 3 (a): Kusoma irabu i<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi i<br />
Muda: Kipindi 2<br />
Zana: Kadi za herufi i na picha ya fimbo<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi i.<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne i i i i i ……<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi i kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi kwenye kadi hizo.<br />
6. Andika ubaoni herufi nyingi za ukubwa tofauti kwa kutumia chaki za rangi mbalimbali.<br />
26
7. Waongoze wanafunzi wasome i hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
Somo la 3 (b): Kuandika irabu i<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi i kwa hati ya chapa yenye vikonyo.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: vijiti, kalamu, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
Mchoro wa herufi i<br />
iiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii<br />
2. Rudia michoro iliyoonyeshwa hapo juu kwa kuiandika hewani, mchangani, ukisema kwa<br />
Kwa sauti “chini, panda juu chini panda juu”<br />
“Nukta, nukta, nukta”……………………………<br />
4. Baada ya kurudi darasani rudia tena kuandika mchoro huo huo ubaoni, wanafunzi wote<br />
wafuatishe hewani wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo madaftarini mwao na mwalimu apite akiwasaidia namna<br />
ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
6. Fundisha herufii kwa kurudia michoro<br />
(Michoro ya herufi i)<br />
7.Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi i kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Somo la 4 (a): Kusoma irabu O<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi na picha ya mpira<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
27
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi anaweza kuitambua<br />
vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi kwenye kadi hizo.<br />
6. Andika ubaoni herufi nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
Somo la 18(b): Kuandika irabu<br />
Ujuzi: kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: vijiti, kalamu, vibao.<br />
Hatua:<br />
kwa hati ya chapa yenye vikonyo.<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia kalamu.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia kijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na mwalimu apite akiwasaidia<br />
namnaya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
6. Fundisha herufi kwa kurudia mchoro<br />
(Mchoro wa herufi<br />
7.Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Kuna tofauti gani katika kuandika herufi e na herufi O.<br />
Somo la 5 (a): Kusoma irabu u<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi u<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi u na picha ya kikombe<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi u<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne u u u u<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi u kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
28
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi anaweza kuitambua<br />
vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waonyeshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi kwenye kadi hizo.<br />
6. Andika ubaoni herufi nyingi za ukubwa mbalimbali kutumia chaki za rangi mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome u katika vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Andika maneno yafuatayo ubaoni kisha wanafunzi wayasome mmojammoja na katika vikundi<br />
ua, au oa<br />
Somo la 5 (b): Kuandika irabu u<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi u kwa hati ya chapa yenye vikonyo.<br />
Muda: kipindi 1.<br />
Zana: vijiti, kalamu, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
Mchoro wa herufi u<br />
2. Rudia michoro iliyoonyeshwa hapo juu kwa kuiandika hewani kisha mchangani<br />
“<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na mwalimu apite akiwasaidia<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
6. Fundisha herufi u kwa kurudia mchoro<br />
(Mchoro wa herufi u<br />
7. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi u kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Marudio ya herufi zilizofundishwa<br />
a e i o u<br />
Tunga wimbo wowote unaohusiana na irabu na kuunda sauti kama ufuatao:<br />
Wimbo wa irabu<br />
1. Hiyo ndiyo a<br />
a a a<br />
29
iko kama birika<br />
a a a<br />
2. Hiyo ndiyo e<br />
e e e<br />
iko kama pete<br />
e e e<br />
3. Hii ndiyo i<br />
i<br />
i i<br />
iko kama fimbo<br />
i<br />
i i<br />
3. Hii ndiyo o<br />
o o o<br />
iko kama mpira<br />
o o o<br />
3. Hii ndiyo u<br />
u<br />
u u<br />
iko kama kikombe<br />
u u u<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Kitu gani kimekufurahisha katika somo hili. Ni<br />
sehemu gani ambayo hukuielewa?<br />
Somo la 6 (a): Kusoma herufi b<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Kusudi: Mwanafunzi aweze kusoma herufi b<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Vifaa: Kadi za herufi b<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi b<br />
2. Isome hiyo herufi zaidi ya mara nne b b b b……………<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi b kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
30
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi anaweza kuitambua<br />
vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waonyeshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi b kwenye kadi hizo.<br />
6. Andika ubaoni herufi b nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome b hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Andika silabi zifuatazo ba be bi bo bu kisha wanafunzi wazizome kwa sauti mmoja mmoja<br />
na katika vikundi.<br />
Somo la 6 (b): Kuandika herufi b<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi b<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
Mchoro wa herifi b<br />
b b b b b b b b b b b b b b b b b b<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia kijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na mwalimu apite akiwasaidia<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
6. Fuatisha herufi b kwa kurudia mchoro.<br />
(Mchoro wa herufi b)<br />
7. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi b kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
Marudio ya herufi zilizofundishwa<br />
a e i o u b<br />
bibo bei bia bao bua iba boa bibi aibu bubu<br />
Wanafunzi waorodheshe maneno zaidi wanayoyajua katika madaftari yao.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili. Herufi b unaweza kuifananisha na kitu gani?<br />
31
Somo la 7 (a): Kusoma herufi ch<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi Ch<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana/Vifaa: Kadi za herufi Ch na Kadi za silabi cha che chi cho chu<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi Ch<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne Ch Ch Ch Ch………….<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi Ch kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuzisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waonyeshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi Ch kwenye kadi hizo. Kisha<br />
waelekeza wazisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Wape wanafunzi kadi za silabi cha, che, chi, cho, chu kisha waelekeze wazisome kwa sauti<br />
mmoja mmoja.<br />
7. Andika ubaoni maneno haya kisha waongoze wanafunzi wayasome mmoja mmoja:<br />
chai, cheche, chui, chache, acha, choo, chachu<br />
12. Waongoze wanafunzi wachunguze picha zipi?...... na kisha waongoze wasome maneno<br />
yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 7 (b): Kuandika herufi ch<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi Ch<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi Ch, vibao<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi wachore mchoro wa ch kwa kuanza na hatua ya hewani na kisha<br />
vibaoni mwao.<br />
2. Mwalimu aandike michoro ifuatayo ubaoni.<br />
cccccccccccccccccccccccccccccccccccccccccccccccccc<br />
C C C C C C C C C C C C C C C C C C C<br />
3. Endelea kufundisha mchoro ufuatao ubaoni.<br />
32
h<br />
h h h h h h h h h h h h<br />
4. Mwalimu awaongoze wanafunzi kufuatisha michoro hiyo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
5. Waongoze wanafunzi wanakili kwenye madaftari yao michoro iliyopo ubaoni kujaza ukurasa.<br />
6. Waelekeze wanafunzi waandike herufi Ch ubaoni kwa kufuata hatua zifuatazo<br />
Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch Ch<br />
7. Wanafunzi wafanye mazoezi ya kuandika herufu Ch kujaza mistari miwili.<br />
8. Waongoze wanafunzi waandike silabi cha, Che, Chi, Cho, chu kwenye vibao vyao. Kila<br />
silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
9. Waongoze warudie kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi<br />
ameweza kuitambua na kuiandika vizuri silabi hiyo.<br />
13. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2). Waongoze wachunguze picha na<br />
waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo kwa kujaza nafasi.<br />
Tafakuri: Taja maneno mengine matatu yanayoanza na ch.<br />
Somo la 8 (a): Kusoma herufi d<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi d<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi d na kadi za silabi za da de di do du<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi d<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne d d d d…………<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi d kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi d kwenye kadi hizo. Kisha<br />
waelekeze wazisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi d nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome d hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi da de di do du kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu sura ya sita (6.2). Kisha wachunguze picha na wasome<br />
kwa sauti mmoja mmoja majina yaliyo chini ya picha hizo.<br />
33
Somo la 8 (b): Kuandika herufi d<br />
Ujuzi: kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi d<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni<br />
Mchoro wa herifi d<br />
ddddddddddddddddddddddddddddd<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na mwalimu upite ukiwaelekeza<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
(Mchoro wa herufi d)<br />
6. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi d kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike silabi da de di do du kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
8. Waelekeze wanafunzi waandike silabi na maneno yafuatayo: madaftarini mwao<br />
Marudio ya herufi zilizofundishwa<br />
da de di do du<br />
dada debe dobi dua ibua bibi abudu bubu<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.D inatifautianaje na b?<br />
Somo la 9 (a): Kusoma herufi f<br />
34
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi f<br />
Muda: kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi f kadi za silabi za fa, fe, fi, fo, fu<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi f<br />
2. Isome kwa utaratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne f f f f…………………..<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi f kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi f kwenye kadi hizo. Kisha<br />
waelekeze wazisome kwa sauti kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi f nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome f hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi fa fe fi fo fu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) kisha wachunguze picha na<br />
wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 9 (b): Kuandika herufi f<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi f<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa f ubaoni<br />
Mchoro wa herifi f<br />
f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f f<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na upite ukiwaelekeza<br />
Namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika pensili<br />
(c) Kuchora<br />
(Mchoro wa herufi f)<br />
35
6. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi f kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike silabi fa fe fi fo fu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
8. Waelekeze wanafunzi wanakili silabi na maneno yafuatayo:<br />
Marudio ya herufi zilizofundishwa<br />
a e i o u<br />
b ch d e f<br />
dafu fua bafu adui fofofo dau doa cheo udi chui<br />
Tafakuri: Kwa nini herufi f inafananishwa na bakora?<br />
Somo la 10 (a): Kusoma herufi g<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi g<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi g na kadi za silabi ga ge gi go gu<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi g ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne g g g g………..<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi g kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi g kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi g nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome g hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ga ge gi go gu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) kisha wachunguze picha na<br />
wasome kwa sauti maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 10 (b): Kuandika herufi g<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi g.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
36
Hatua:<br />
1. Andika mchoro g ubaoni.<br />
Mchoro wa herifi g<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na upitie ukiwaelekeza<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika penseli<br />
(c) Kuchora<br />
(Mchoro wa herufi g)<br />
6. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi g kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
7. Wape wanafunzi kadi za silabi ga ge gi go gu kisha waelekeze waziandike kwenye vibao<br />
vyao. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
8. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao sura ya sita (6.2) kisha wachunguze picha na<br />
waandike majina ya vitu vilivyo kwenye picha hizo.<br />
9. Waelekeze wanafunzi wanakili kwenye madaftari yao maneno yaliyo kwenye jedwali<br />
lifuatalo:<br />
gogo gego iga figo dogo<br />
gofu figa fagio fua dafu<br />
Tafakuri: Taja maneno matatu mengine ambayo yanaweza kuundwa na herufi g.<br />
Somo la 11 (a): Kusoma herufi h<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi h<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi h na za silabi ha, he, hi ho hu<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi h ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne h h h h ………..<br />
3. Waongoze wanafunzi wasoma herufi h kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
37
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi h. Kisha waelekeze wazisome<br />
kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi h nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome hizo h kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ha he hi ho hu kisha waelekeze wazisome kwa sauti<br />
mmoja mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao sura ya sita (6.2) kisha wachunguze picha na<br />
wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 11 (b): Kuandika herufi h<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi h<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa h ubaoni.<br />
Mchoro wa herifi h<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na upite ukiwaelekeza<br />
namna ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika penseli<br />
(c) Kuchora<br />
(Mchoro wa herufi h)<br />
6. Wape wanafunzi kazi ya kuandika herufi h kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
7. Wape wanafunzi kadi za silabi ha he hi ho hu kisha waelekeze waziandike kwenye vibao<br />
vyao. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
8. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na kunakili<br />
majina yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Taja majina mengine yanayoanzia na herufi h.<br />
Somo la 12 (a): Kusoma herufi j<br />
38
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi j<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi j na za silabi ja je ji jo ju<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi j ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne j j j j…………………..<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi j kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi j. Kisha waelekeze wasoma kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi j nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome j hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ja je ji jo ju kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 12 (b): Kuandika herufi j<br />
Ujuzi: kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi j<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa j ubaoni.<br />
Mchoro wa herifi j<br />
j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j j<br />
2. Waongoze wanafunzi wafuatishe kuandika mchoro huo hewani kwa kutumia penseli.<br />
3. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
4. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi j pamoja na irabu zote kuunda ja, je, ji, jo, ju. Kila<br />
silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Andika silabi hizi ubaoni kisha wape wanafunzi kazi ya kuziandika madaftarini mwao: ja je<br />
39
ji jo ju kujaza ukurasa ili wapate mazoezi ya kutosha.<br />
7. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi j kisha<br />
wachunguze picha na waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Kwa nini tunapenda kuifananisha herufi na vitu halisi?<br />
Somo la 13 (a): Kusoma herufi k<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi k.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za silabi ka, ke, ki, ko, ku<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi k ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne k k k k ………….<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi k wa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
Unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi k kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi k nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome k hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ka ke ki ko ku kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi<br />
kwachunguze picha na wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 13 (b): Kuandika herufi k<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao au picha za manila.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro huu ubaoni k.<br />
Mchoro wa herifi k<br />
40
k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k k<br />
2. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia kijiti.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
4. Wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari ya na mwalimu apite akiwasaidia namna<br />
ya: (a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
5. Wape wanafunzi kazi ya kuandika silabi ka, ke, ki, ko, ku kujaza ukurasa.<br />
6. Waelekeze wanafunzi waandike herufi k pamoja na irabu zote kuunda ka, ke, ki, ko, ku.<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike silabi ka ke ki ko ku kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
Tafakuri: Taja maneno matatu yenye herufi k<br />
Somo la 14 (a): Kusoma herufi l<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi l.<br />
Muda: kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za silabi la, le, li, lo, lu<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi l ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne l l l l ………….<br />
3. Waongoze wanafunzi kusoma herufi l wa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi l kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi l nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome l hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi la le li lo lu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya l<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 14 (b): Kuandika herufi l<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
41
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi l.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa l ubaoni.<br />
Mchoro wa herifi k<br />
l l l l l<br />
2. Waongoze wanafunzi kuandika mchoro huo mchangani kwa kutumia vijiti.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika mchoro huo ubaoni, wanafunzi wote wafuatishe hewani<br />
wakiwa wameshika vijiti vyao.<br />
4. Waongoze wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na upite ukiwaelekeze<br />
namna ya:<br />
(a) Kukaa<br />
(b) Kushika kalamu<br />
(c) Kuchora<br />
5. Andika silabi hizi ubaoni la, le, li, lo, lu kisha waelekeze wanafunzi waziandike silabi<br />
hizo kujaza ukurasa.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike silabi la le li lo lu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
7. Wanafunzi wasome kwa sauti na wanakili maneno yafuatayo:<br />
lile, lala, lea, lilia, loa, lako, kile, kila,<br />
10. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyaoura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi l<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Taja majina matatu ya watu yanayoanza na l.<br />
Somo la 15 (a): Kusoma herufi m<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi m.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi m na silabi ma me mi mo mu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi m ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne m m m m …………<br />
42
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi m kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi m kisha waelekeze wazisome<br />
kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi m nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome m hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ma me mi mo mu kisha waelekeze wazisome kwa sauti<br />
mmoja mmoja.<br />
11. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya<br />
m wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 15 (b) Kuandika herufi m<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi m<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana/vifaa: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi m ubaoni<br />
m m m<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi m ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
m m m m m m m m m m m<br />
4. Waongoze wanafunzi wafuatishe mchoro huo kwenye madaftari yao na upite ukiwaelekeze<br />
namna ya:<br />
(a) Kukaa<br />
43
(b) Kushika penseli<br />
(c) Kuchora<br />
5. Wanafunzi wafanye mazoezi ya kuandika herufi m kujaza mistari miwili.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike silabi ma me mi mo mu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike silabi ma me mi mo mu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
8. Waelekeze wanafunzi waandike herufi m pamoja na irabu zote kuunda silabi ma me mi mo<br />
mu. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
9. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
mama, madafu maua, madoido, mia<br />
12. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi m<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Watunge sentensi kutumia maneno mama na mimi.<br />
Somo la 16 (a): Kusoma herufi n<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma herufi n.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi n na silabi na ne ni no nu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi n ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne n n n n …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi n kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi n kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi n nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome n hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi na ne ni no nu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
11. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya<br />
n wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 30 (b): Kuandika herufi n<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi n<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, penseli, vibao.<br />
Hatua:<br />
44
1. Andika mchoro wa herufi n ubaoni<br />
n n n n n n n n n n<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi n ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
n n n n n n n n n n n n n n n<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike silabi na ne ni no nu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
7. Waelekeze wanafunzi waandike herufi n pamoja na irabu zote kuunda silabi na ne ni<br />
no nu. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
8. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
nia, noa nani nena nane nne<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi n<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Kuna tofauti gani kati ya herufi n na m?<br />
Somo la 17 (a): Kusoma herufi p<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi p.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi p na silabi pa pe pi po pu<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi p ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne p p p p …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi p kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi p kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
45
6. Andika ubaoni herufi p nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome p hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8Wape wanafunzi kadi za silabi pa pe pi po pu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya p<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 17 (b): Kuandika herufi p<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi p<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi p ubaoni<br />
P p p p p p p<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi p ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
P p p p p p p p p p p<br />
13. Waongoze wanafunzi waandike silabi pa pe pi po pu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
6. Waelekeze wanafunzi waandike herufi p pamoja na irabu zote kuunda silabi pa pe pi po pu.<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
paa, poa papi popo pona pipi<br />
14. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi p<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
46
Tafakuri: Tumia maneno yafuatayo kutunga sentensi kwa mdomo: popo na parura<br />
Somo la 18 (a): Kusoma herufi r<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi r<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi r na silabi ra re ri ro ru<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi r ubaoni<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne r r r r…………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi r kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi r kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi r nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome r hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ra re ri ro ru kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
15. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya r<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Somo la 18 (b): Kuandika herufi r<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi r<br />
Muda: kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
47
1. Andika mchoro wa herufi r ubaoni<br />
r r r r r r r r r r<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi r ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze wanafunzi<br />
wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
r r r r r r r r r r r r<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike silabi ra re ri ro ru kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi r pamoja na irabu zote kuunda silabi ra re ri ro ru.<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
rula, raha, ruka, reli, roho<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi r<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakari: Taja maneno matatu yenye kutumia r<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Somo la 33 (a): Kusoma herufi s<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi S.<br />
Muda: Kipindi1<br />
Zana: Kadi za herufi s na silabi sa se si so s<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi S ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne s s s s …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi s kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
48
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi s kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi s nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome s hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi sa se si so su kisha waelekeze wazisome kwa sauti<br />
mmommoja.<br />
16. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya s<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 19 (b): Kuandika herufi s<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi s<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi S ubaoni<br />
S s s s s s s<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi S ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
S s s s s s s s s s s s<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike silabi sa se si so su kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi s pamoja na irabu zote kuunda silabi sa se si so<br />
su. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo: Saa, sasa, soma, sura, soko,<br />
sumu, sio, senema, sisi<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi s<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tumia maneno yafuatayo katika sentensi: soko, sasa na soma.<br />
Somo la 20 (a): Kusoma herufi t<br />
49
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi t.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za herufi t na silabi za ta te ti to tu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi S ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne t t t t …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi t kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi t kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi t nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome t hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ta te ti to tu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya t<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 20 (b): Kuandika herufi t<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi t<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi t ubaoni<br />
t t t t t t t t t t t<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
50
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi t ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze wanafunzi<br />
wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
t t t t t t t t t t t t t t<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike ta te ti to tu kwenye vibao vyao. Kila silabi iandikwe<br />
mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi t pamoja na irabu zote kuunda silabi ta te ti to tu<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo: tano tikiti tega tisa tone tuma toa tafuta<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi t<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakari: Umefurahia nini kutokana na kujifunza herufi t?<br />
Somo la 21 (a): Kusoma herufi v<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi v.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi v na silabi za va ve vi vo vu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi v ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne v v v v …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi v kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi v kisha waelekeze wazisome<br />
kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi v nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome v hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi va ve vi vo vu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya v<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
51
Somo la 21 (b): Kuandika herufi v<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi v<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi v ubaoni<br />
v v v v v v v v v v v v v v<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi v ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
v v v v v v v v v v v v v v<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike va ve vi vo vu kwenye vibao vyao. Kila silabi iandikwe<br />
mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi v pamoja na irabu zote kuunda silabi va ve vi vo vu<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:Vaa, vua, vuta, viatu, vaeni, vumili,<br />
vuma,<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi v<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Taja maneno matatu yanayoanza na herufi v<br />
Somo la 22 (a): Kusoma herufi w<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi W<br />
Muda: Kipindi 1<br />
52
Zana: Kadi za herufi w na silabi wa we wi wo wu<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi w ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne w w w w w …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi w kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi w kisha waelekeze wazisome<br />
kwa sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi w nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome w hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi wa we wi wo wu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya w<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 22 (b): Kuandika herufi w<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi w<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi w ubaoni<br />
w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w w<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi w ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
w w w w w w w w w w w w<br />
53
4. Waongoze wanafunzi waandike wa we wi wo wu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi v pamoja na irabu zote kuunda silabi wa we wi wo<br />
wu. Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
Waite, wao, wenu wote, watu, wima, wodi, wino, weusi, wiki, woga wetu<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi w<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Kuna tofauti yoyote kati ya herufi w na v?<br />
Somo la 23 (a): Kusoma herufi y<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi y.<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi y na silabi ya ye yi yo yu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi y ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne y y y y …………<br />
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi y kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi y kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi y nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome y hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi ya ye yi yo yu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya y<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 23 (b): Kuandika herufi y<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi y<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
54
1. Andika mchoro wa herufi y ubaoni<br />
y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y y<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi y ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
y y y y y y y y y y<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike ya ye yi yo yu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi y pamoja na irabu zote kuunda silabi ya ye yi yo yu<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
yai, yao, yenu yote, yetu, yowe, yule.<br />
7. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi y<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Unaweza kutaja maneno yanayoanza na y?<br />
Somo la 24 (a): Kusoma herufi z<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma herufi z.<br />
Muda: kipindi 1<br />
Zana: Kadi za herufi z na silabi za ze zi zo zu.<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi y ubaoni.<br />
2. Isome taratibu hiyo herufi zaidi ya mara nne z z z z …………<br />
55
3. Waongoze wanafunzi wasome herufi z kwa sauti, wote kwa pamoja wafuatishe<br />
unavyosoma kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
4. Rudia kufanya hivyo mara nyingi hadi uhakikishe kuwa kila mwanafunzi ameweza kuitambua<br />
na kuisoma vizuri herufi hiyo.<br />
5. Waoneshe wanafunzi kadi za rangi mbalimbali zenye herufi z kisha waelekeze wazisome kwa<br />
sauti mmoja mmoja.<br />
6. Andika ubaoni herufi z nyingi za ukubwa mbalimbali kwa kutumia chaki za rangi<br />
mbalimbali.<br />
7. Waongoze wanafunzi wasome z hizo kwa pamoja kwa vikundi na kisha mmoja mmoja.<br />
8. Wape wanafunzi kadi za silabi za ze zi zo zu kisha waelekeze wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja.<br />
9. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao katika sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi ya z<br />
wachunguze picha na kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo<br />
Somo la 24 (b): Kuandika herufi z<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika herufi z<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Vijiti, vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika mchoro wa herufi z ubaoni<br />
z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z z<br />
2. Waongoze wanafunzi kufuatisha mchoro huo hewani, mchangani na vibaoni.<br />
3. Baada ya kurudi darasani andika herufi z ubaoni kwa kufuata hatua zake, waongoze<br />
wanafunzi wote wafuatishe kwa kufuata hatua zifuatazo:<br />
z z z z z z z z z z<br />
4. Waongoze wanafunzi waandike za ze zi zo zu kwenye vibao vyao. Kila silabi<br />
iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja<br />
56
5. Waelekeze wanafunzi waandike herufi y pamoja na irabu zote kuunda silabi za ze zi zo zu<br />
Kila silabi iandikwe mara nyingi kujaza mstari mmoja.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike maneno yafuatayo:<br />
Zabibu, zamani, zetu, zeze, zogo, zana, zagaa zimia, zaidi, zege, zizi, zulia<br />
17. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) kwenye somo la herufi z<br />
wachunguze picha na kisha waandike maneno yaliyo chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno zagaa.<br />
Somo la 25 (a) Kusoma herufi bw<br />
Herufi-mwambatano<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano bw:<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za silabi bwa, bwe, bwi, bwo, bwu na maneno yenye herufi mwambatano bw<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya bwawa, uulize: Hili nini? Wanafunzi wajibu: Hilo ni<br />
bwawa.<br />
2. Andika neno bwawa ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi neno ubwabwa waulize: Huu ni nini ? Wanafunzi wajibu huo ni<br />
Ubwabwa. Waelekeze wanafunzi warudie neno ubwabwa kwa sauti ili waweze<br />
kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya kabwela ubwabwa, bweni, mbweha.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
bw wanafunzi wachunguze picha kisha wasome neno bweka lililo chini ya picha hiyo.<br />
6. Changanya silabi za herufi mwambatano na silabi nyingine kisha waelekeze wanafunzi<br />
waunde maneno kutokana na silabi hizo. Maneno kama:<br />
m- bwa, ma- bwa-wa, bwe- ni, bwa-lo<br />
Somo la 25 (b): Kuandika herufi bw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano bw:<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
57
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano bw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye vibao vyao.<br />
Herufi bw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya kuandika herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye madaftari yao.<br />
bwa bwe bwi bwo bwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi<br />
mwambatano bw.<br />
bwawa<br />
bweni<br />
ubwabwa<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano<br />
bw na silabi zingine.<br />
mbwana ni kabwela<br />
bwawa limejaa maji<br />
mbweha ni mnyama mkali sana<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hiyo.<br />
Tafakari: Tunga sentensi kwa kutumia neno bweka.<br />
Somo la 26 (a): Kusoma herufi mwambatano chw<br />
58
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano chw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi chwa chwe chwi chwo chwu na maneno yenye herufi mwambatano chw.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya kichwa, uulize: Hiki ni nini? Wanafunzi wajibu: Hicho<br />
ni kichwa.<br />
2. Andika neno kichwa ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi neno mchwa waulize: Huyu ni nani ? Wanafunzi wajibu huyo ni<br />
mchwa. Waelekeze wanafunzi warudie neno ubwabwa kwa sauti ili waweze kulitamka<br />
vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya kichwa Mchwa. Waongoze<br />
wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
chw wanafunzi wachunguze picha kisha wasome neno kumekuchwa lililo chini ya<br />
picha hiyo.<br />
6. Changanya silabi za herufi mwambatano na silabi nyingine kisha waelekeze<br />
wanafunzi waunde maneno kutokana na silabi hizo. Maneno kama:<br />
ki- chwa, ma- chew-o, ku-chwa, ku-chwe, m-chwa.<br />
Somo la 26 (b): Kuandika herufi chw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano chw:<br />
Muda: Kipindi<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano chw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye vibao vyao.<br />
Herufi chw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya kuandika herufi mwambatano zifuatazo: Kisha wanakili<br />
silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
59
Chwa chwe chwi chwo chwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
chw.<br />
kichwa<br />
mchwa<br />
machweo<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano bw<br />
na silabi zingine.<br />
mchwa umekula mti<br />
sasa hivi kumekuchwa<br />
aliondoka machweo<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hiyo.<br />
6. Tafakuri: Kutunga sentensi kwa kutumia neno mchwa<br />
Somo la 27 (a): Kusoma herufi dh<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano dh:<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi dha, dhe, dhi, dho, dhu na maneno yenye herufi mwambatano dh.<br />
Hatua:<br />
60
1. Waoneshe wanafunzi picha ya pete ye dhahabu, uulize: Hii ni nini? Wanafunzi wajibu:<br />
Hiyo ni pete ya dhahabu.<br />
2 Andika neno dhahabu ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3.Waonesha wanafunzi kadi ya neno fedha waulize: Hii ni nini ? Waelekeze wanafunzi<br />
wajibu hiyo ni fedha. Waelekeze wanafunzi warudie neno ubwabwa kwa sauti ili waweze<br />
kulitamka vizuri.<br />
4.Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya fedha, dhahabu, dhambi,<br />
dhoruba,dharau, fedheha, dhuluma. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi<br />
na mmoja mmoja.<br />
5 Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
dh wanafunzi wachunguze picha kisha wasome neno dhofu lililo chini ya picha hiyo.<br />
6 Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome haya maneno kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama:<br />
fe- dha, dha-ra-u, dhu-lu-ma, dha-mbi, dha-ha-bu, fe-dhe-ha.<br />
Somo la 27 (b): Kuandika herufi dh<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano dh:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano dh. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi dh<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya kuandika herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
dha dhe dhi dho dhu<br />
61
3 Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
dhambi<br />
dhahabu<br />
fedha<br />
fedheha<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano dh<br />
na silabi zingine.<br />
Mama amevaa pete ya dhahabu<br />
kuiba ni dhambi<br />
dada ana fedha na dhahabu<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hizo.<br />
6. Tafakuri: Tumia neno fedha katikaa sentensi<br />
Somo la 28 (a): Kusoma herufi fy<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano fy:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kai za silabi fya, fye, fyi, fyo, fyu na kadi za maneno yenye herufi mwambatano fy<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya fyekeo, uulize: Hili ni nini? Wanafunzi wajibu: Hilo ni<br />
fyekeo<br />
2. Andika neno fyekeo ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno fyonza waulize: Nyuki anafyonza nini ? Waelekeze<br />
wanafunzi wajibu nyuki anafyonza maua. Waelekeze wanafunzi warudie neno ubwabwa<br />
kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
62
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya afya, chafya, fyatuka, fyekeo, .<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano fy<br />
wanafunzi wachunguze picha kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama:<br />
fyekeo, afya, fyonza, chafya, fyatuka<br />
Somo la 28 (b): Kuandika herufi fy<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano fy:<br />
Muda: Kipindi1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano fy. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi fy<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya kuandika herufi mwambatano zifuatazo: Kisha wanakili<br />
silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
fya fye fyi fyo fyu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
fy<br />
fyatuka<br />
fyekeo<br />
afya<br />
63
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano fy<br />
na silabi zingine.<br />
Nimefyeka majani<br />
Nina afya nzuri<br />
Mtego umefyatuka<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno chafya.<br />
Somo la 29 (a): Kusoma herufi gw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano gw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi gwa gwe gwi gwo gwu na za maneno yenye herufi mwambatano gw<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya ngwanda, uulize: Hili ni nini? Wanafunzi wajibu: Hilo ni<br />
gwanda.<br />
2. Andika neno gwanda ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno gwaride waulize: Mara nyingi askari hucheza nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu Askari hucheza gwaride. Waelekeze wanafunzi warudie<br />
neno ubwabwa kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya gwaride, gwiji na gwanda.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
64
7 Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
gw wanafunzi wachunguze picha kisha wasome maneno yaliyo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
8 Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama:<br />
Gwanda, gwaride, gwiji, gwaya<br />
Somo la 29 (b): Kuandika herufi gw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano gw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano gw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi gw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya kuandika herufi mwambatano zifuatazo: Kisha wanakili<br />
silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
gwa gwe gwi gwo gwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano f<br />
gwanda<br />
gwaride<br />
gwiji<br />
65
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano gw<br />
na silabi zingine.<br />
wanafunzi wanacheza gwaride<br />
kaka amevaa gwanda<br />
Mjomba ni gwiji wa mziki<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno gwaya.<br />
Somo la 30 (a): Kusoma herufi kw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano kw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi kwa kwe kwi kwo kwu na maneno yenye herufi mwambatano kw.<br />
Maneno kama: kwato kwea, kwale, kwikwi, kwetu.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya kwato, uulize: Hii ni nini? Wanafunzi wajibu: Hiyo ni<br />
kwato.<br />
2.Andika neno kwato ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno kwale waulize wanafunzi: Ndege pori anayefanana na<br />
kuku anaitwaje ? Waelekeze wanafunzi wajibu ndege huyo anaitwa kwale. Waelekeze<br />
wanafunzi warudie kutamka neno kwale kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4.Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya kwenu, kwetu, kwao, kwikwi, kwea,<br />
kwato, kwale na kwama . Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja<br />
mmoja.<br />
66
9 Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
kw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
10 Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama:<br />
Kwama, kwamba, kwale, kwato, kwetu,kwikwi<br />
Somo la 30 (b): Kuandika herufi kw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano kw.<br />
Muda: Kipindi1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano kw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi kw<br />
7. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
kwa kwe kwi kwo kwu<br />
8. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
kw kwenye madaftari yao.<br />
kwato<br />
kwale<br />
kwetu<br />
67
9. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano kw<br />
na silabi zingine.<br />
Kwetu kuna kwale<br />
Kaka alikwea mti<br />
Mtoto ana kwikwi<br />
10. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno kwetu.<br />
Somo la 31 (a): Kusoma herufi mb<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mb:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi na za maneno yenye herufi mwambatano mb. Maneno kama: mboga,<br />
mbele, mbolea, jembe. mbegu. mbuzi, mbalamwezi.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mbuzi, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu: Huyo<br />
ni mbuzi.<br />
2. Andika neno mbuzi ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno jembe waulize wanafunzi: Tunalima kwa kutumia<br />
nini? Waelekeze wanafunzi wajibu, tunalima kwa kutumia jembe . Waelekeze<br />
wanafunzi warudie kutamka neno jembe kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mbata, mbegu, mbolea,<br />
jembembuzi, mbalamwezi. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na<br />
mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mb wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama: mboga, mbavu,<br />
mbele, mbolea, mbugani.<br />
Somo la 31 (b): Kuandika herufi mb<br />
68
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mb.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mb. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mb<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mba mbe mbi mbo mbu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mb kwenye madaftari yao.<br />
mboga<br />
mbegu<br />
mbalamwezi<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mb<br />
na silabi zingine.<br />
mhicha ni mboga<br />
mbegu zimeota<br />
69
watoto wameiona mbalamwezi<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) wachunguze picha na<br />
kunakili maneno na sentensi yaliyo ndani ya visanduku chini ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mbalamwezi.<br />
Somo la 32 (a): Kusoma herufi mf<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwnafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mf:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi na za maneno yenye herufi mwambatano mf. Maneno kama: mfano,<br />
mfuko, mfenesi, mfiwa mfuasi, mfu.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mfuko, uulize: Huu ni nini? Wanafunzi wajibu: Huo ni<br />
mfukoi.<br />
2. Andika neno mfuko ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
7. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mfenesi waulize wanafunzi: Mfenesi unazaa<br />
matunda gani? Waelekeze wanafunzi wajibu, mfenesi unazaa mafenesi. Waelekeze<br />
wanafunzi warudie kutamka neno mfenesi kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mfano, mfuko, mfenesi, mfiwa mfuasi,<br />
mfu. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano mf<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama:<br />
mfano, mfuko, mfenesi, mfiwa mfuasi, mfuasi, mfu, mfiwa.<br />
Somo la 32 (b): Kuandika herufi mf<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mf.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
70
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mf. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mf<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mfa mfe mfi mfo mfu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mf kwenye madaftari yao.<br />
mfenesi<br />
mfano<br />
mfu<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mf<br />
na silabi zingine.<br />
Mfenesi ni mti<br />
dada alitoa mfano<br />
mfuko umechanika<br />
71
8. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mf wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mfuko.<br />
Somo la 33 (a): Kusoma herufi mk<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano mk<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mka, mke, mki, mko, mku na za maneno yenye herufi mwambatano mk.<br />
Maneno kama: mkufu, mkorofi, mkate, mkazi, mkoa, mkemia.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mkate, uulize: Huu ni nini? Wanafunzi wajibu: Huo ni<br />
mkate.<br />
2. Andika neno mkate ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mkufu waulize wanafunzi: Dada hupenda kuvaa nini<br />
shingoni? Waelekeze wanafunzi wajibu, dada huvaa mkufu. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mfenesi kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mkufu, mkorofi, mkate. mkeka, mkoa,<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano mk<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mkebe, mkoba,<br />
mkeka, mkimbizi, mkasi, mkato.<br />
Somo la 33 (b): Kuandika herufi mk<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mk.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mk. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye<br />
72
vibao vyao.<br />
Herufi mk<br />
6. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mka mke mki mko mku<br />
7. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mk kwenye madaftari yao.<br />
mkeka<br />
mkokoteni<br />
mkoba<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mk<br />
na silabi zingine.<br />
Mkeka umechanika<br />
Mama amenunua mkoba<br />
Mkokoteni umejaa mizigo.<br />
8. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mk wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
9. Tafakuri: Tunga sentensi kutumia neno mkeka.<br />
73
Somo la 34(a) Kusoma herufi ml<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano ml:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mla, mle, mli, mlo, mlu na za maneno yenye silabi mwambatano ml.<br />
Maneno kama mlima, mlezi, mluzi, mlowezi<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mlango, uulize: Huu ni nini? Wanafunzi wajibu: Huo ni<br />
mlango.<br />
2. Andika neno mlango ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mlima. Waulize wanafunzi: Huu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huo ni mlima. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mlima kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mlima, mlango, mluzi, mlezi, mlowezi.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano ml<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mlezi, mlima, mluzi,<br />
,mlowezi.<br />
Somo la 34 (b): Kuandika herufi ml<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano ml.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
2. Andika ubaoni herufi-mwambatano ml. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi ml<br />
10. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
74
mla mle mli mlo mlu<br />
11. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
ml kwenye madaftari yao.<br />
mlo<br />
mluzi<br />
mlezi<br />
mlima<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ml na<br />
silabi zingine.<br />
mlo wetu ni mtamu<br />
Mama mlezi amekuja<br />
Mtoto anaelekea mlimani<br />
9. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ml wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kutumia neno mlima<br />
Somo la 35 (a): Kusoma herufi mp<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mp: mpera<br />
mpapai, mpingo, mpira, mpokela, mpendwa.<br />
75
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mpa, mpe, mpi, mpo, mpu na maneno yenye herufi mwambatano mp.<br />
Maneno kama: mpera, mpapai, mpole, mpira, mparachichi, mpilipili.mpini.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mpapai, uulize: Huu ni nini? Wanafunzi wajibu: Huo ni<br />
mpapai.<br />
2. Andika neno mpapai ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mpira. Waulize wanafunzi: Huu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huo ni mpira. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mpira kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mpera, mpapai, mpole, mpira,<br />
mparachichi, mpilipili.mpini. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na<br />
mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mp wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mpira mpera mpapai,<br />
mparachichi.<br />
Somo la 35 (b): Kuandika herufi mp<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mp.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
3. Andika ubaoni herufi-mwambatano mp. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mp<br />
12. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
76
mpa mpe mpi mpo mpu<br />
13. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mp kwenye madaftari yao.<br />
mpo<br />
mpe<br />
mpole<br />
mpiganaji<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ml na<br />
silabi zingine.<br />
mpo darasani<br />
mpe mtoto chakula<br />
mama yetu ni mpole<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mp wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini<br />
ya picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mpole<br />
Somo la 36 (a): Kusoma herufi mt<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mt:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
77
Zana: Kadi za silabi mta, mte, mti, mto, mtu na maneno yenye herufi mwambatano mt.<br />
Maneno kama: mtutu mtaalamu, mtoro, mto, mtu, mti, mtoto.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mtu, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu: Huyo ni<br />
mtu.<br />
2. Andika neno mtu ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mti. Waulize wanafunzi: Huu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huo ni mti. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka neno<br />
mti kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mto, mtu, mtoto, mtego, mtutu<br />
mtaalamu. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano mt<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mti, mto, mtoto,<br />
mtoro, mtego, mtaalamu na mtutu.<br />
Somo la 36 (b): Kuandika herufi mt<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mt.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mt. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mt<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mta mte mti mto mtu<br />
78
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mp kwenye madaftari yao.<br />
mto<br />
mti<br />
mtu<br />
mtoro<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mt<br />
na silabi zingine.<br />
mto una kina kirefu<br />
Mti mkubwa umekatwa<br />
Mtoto mtoro amerudi<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi<br />
mwambatano<br />
mt wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Somo la 39 (a): Kusoma herufi mv<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mv:<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Kadi za silabi mva, mve, mvi, mvo, mvi na maneno yenye herufi mwambatano mv.<br />
Maneno kama: mvuvi mvulana, mvuto, mvaaji, mvi, mvumilivu, mvua, mvuke, mvivu<br />
Hatua:<br />
79
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mvuvi, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu: Huyo ni<br />
mvuvi.<br />
2. Andika neno mvuvi ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mvulana. Waulize wanafunzi: Huyu ni nani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huyo ni mvulana. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mvuvi kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mvuvi, mvaaji,mvulana, mvuto, mvi,<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano mv<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mvuvi mvulana,<br />
mvuto, mvaaji, mvi, mvumilivu, mvua, mvuke, mvivu.<br />
Somo la 37 (b): Kuandika herufi mv<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mv.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mv. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mv<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mva mve mvi mvo mvu<br />
80
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mw kwenye madaftari yao.<br />
mvuvi<br />
mvi<br />
mvulana<br />
mvaaji<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ml na<br />
silabi zingine.<br />
Mvuvi anavua samaki<br />
Babu ana mvi<br />
Mvulana anasoma kitabu<br />
4. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mvwachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
5. Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mvuvi<br />
Somo la 38 (a): Kusoma herufi mw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mwa, mwe, mwi, mwo, mwu, na maneno yenye herufi mwambatano mw.<br />
Maneno kama: mwanadamu, mwamuzi, mwamba, mweusi, mwizi, mwaga, mwoga.<br />
81
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha ya mwamuzi, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu: Huyo<br />
ni mwamuzi.<br />
2. Andika neno mwamuzi ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mwalimu. Waulize wanafunzi: Huyu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huyo ni mwalimu. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mwenge kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mwanadamu, mwamuzi, mwamba,<br />
mweusi, mwizi, mwaga, mwoga, mwaliko, mwali, mwaka. Waongoze wanafunzi<br />
wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano mw<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mwanadamu,<br />
mwamuzi, mwamba, mweupe, mwito, mwaliko, mwaka, mwali.<br />
Somo la 38 (b): Kuandika herufi mw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mwa mwe mwi mwo mwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
82
mw kwenye madaftari yao.<br />
mweupe<br />
mwito<br />
mwanadamu<br />
mwoga<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mw<br />
na silabi zingine.<br />
mwiba umenichoma<br />
mwamba umepasuka<br />
kaka amemwaga maji<br />
4. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
5. Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mwamba<br />
Somo la 39 (a): Kusoma herufi mz<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano mz:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mza, mze, mzi, mzo, mzu na maneno yenye herufi- mwambatano mz.<br />
Maneno kama: mzigo, mzazi, mzuri, mzembe, mzaha, mzoga, mzabibu, mzambarau, mzee,<br />
mzizi.mzito,<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya mzigo, uulize: Huu ni nini? Wanafunzi wajibu:<br />
Huo ni mzigo.<br />
83
2. Andika neno mzigo ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno mzazi. Waulize wanafunzi: Huyu ni nani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huyo ni mzazi. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mzazi kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mzigo, mzazi, mzuri,mzembe,<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
6. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mz wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mzigo, mzazi, mzuri,<br />
mzembe, mzaha, mzoga, mzabibu, mzambarau, mzee, mzizi, mzito,<br />
Somo la 39 (b): Kuandika herufi mz<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mz.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mz. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mz<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mza mze mzi mzo mzu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
84
mw kwenye madaftari yao.<br />
mzigo<br />
mzazi<br />
mzuri<br />
mzembe<br />
6. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mz<br />
na silabi zingine.<br />
mzazi anampeleka mtoto shule<br />
mzigo umepelekwa dukani<br />
ule ni mzoga wa mbuzi<br />
7. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mz wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mzuri.<br />
Somo la 40 (a): Kusoma herufi nd<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano nd: ndama, kondoo<br />
nderemo, ndogo, ndiyo, ndimu, ndumbaro, andazi.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi nda, nde,ndi, ndo, ndu na maneno yenye herufi mwambatano nd. Maneno<br />
kama: ndama, kondoo, nderemo, ndogo, ndiyo, ndimu, andazi, mwandiko, ndoo, ndugu,<br />
ndizi.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya ndizi, uulize: Hii ni nini? Wanafunzi wajibu: Hiyo<br />
ni ndizi.<br />
85
2. Andika neno ndizi ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno ndimu. Waulize wanafunzi: Hii ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, hiyo ni ndimu. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno mzazi kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
7. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya ndama, kondoo, nderemo, ndogo,<br />
ndiyo. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano nd<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama ndimu, andazi,<br />
mwandiko, ndoo, ndugu, ndizi.<br />
Somo la 54 (b): Kuandika herufi nd<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano nd.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano nd. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi nd<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
nda nde ndi ndo ndu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
nd kwenye madaftari yao.<br />
86
kondoo<br />
ndama<br />
nderemo<br />
mwandiko<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano nd na<br />
silabi zingine.<br />
kondoo anakula majani<br />
mdama amekula ndimu<br />
kule kuna nderemo leo<br />
8. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
nd wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno ndizi<br />
Somo la 41 (a): Kusoma herufi ng<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano ng:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi nga, nge, ngi, ngo, ngu na maneno yenye herufi mwambatano ng. Maneno<br />
kama: ingia, nguzo, unga, ngoma, zonga, zingira, ngonjera, ngurumo, nguvu, ngumi,<br />
ngamia, nguo, ngozi.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya ngamia, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu:<br />
Huyo ni ngamia.<br />
87
2. Andika neno ngamia ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno unga. Waulize wanafunzi: Huu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huo ni unga. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno unga kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya ingia, nguzo, unga, ngoma, zonga,<br />
zingira. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano ng<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama ngonjera, ngurumo,<br />
nguvu, ngumi, ngamia, nguo, ngozi. nguchiro.<br />
Somo la 5 (b): Kuandika herufi ng<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano ng.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao.<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano ng. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi ng<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
nga nge ngi ngo ngu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
ng kwenye madaftari yao.<br />
ngoma<br />
88
unga<br />
ngamia<br />
nguo<br />
3. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ng<br />
na silabi zingine.<br />
ngoma ya mganda inachezwa<br />
ugali huu unatosha kwa ugali<br />
ngamia ni mpole<br />
4. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ng wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya picha<br />
hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno ngozi.<br />
Somo la 42 (a): Kusoma herufi ng’<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano ng’:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi ng’a, ng’e, ng’i, ng’o, ng’u na maneno yenye herufi mwambatano ng’.<br />
Maneno kama: ng’ombe, ng’ang’ania, ng’ambo, ng’oa, ng’ata, ng’oka, ng’aa<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya ng’ombe, uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi<br />
wajibu: Huyo ni ng’ombe.<br />
2. Andika neno ng’ombe ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno ng’aa. Waulize wanafunzi: Kioo kikimulikwa na<br />
juu kinafanyaje? Waelekeze wanafunzi wajibu, kioo kinang’aa. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno ng’aa kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
89
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya ng’ombe, ng’ang’ania, ng’ambo,<br />
ng’oa, ng’ata, ng’oka, ng’aa. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na<br />
mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ng wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama ng’oa, ng’ata, ng’oka.<br />
Somo la 56 (b): Kuandika herufi ng’<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano ng’.<br />
Muda: kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano ng’. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi ng’<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
ng’a ng’e ng’i ng’o ng’u<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
ng’ kwenye madaftari yao.<br />
ng’oka<br />
ng’oa<br />
ng’ang’ania<br />
90
ng’ata<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ng na<br />
silabi zingine.<br />
Ng’ombe yuko ng’ambo yamto<br />
ng’oa hicho kisiki<br />
dada ameng’ang’ania shule ya bweni<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ng’ wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kutumia neno ng’ambo.<br />
Somo la 43 (a): Kusoma herufi ny<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano ny:<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi nya nye nyi nyo nyu na maneno yenye herufi mwambatano ny.Maneno<br />
kama: nyoka, nyika, nyumba, nyanya, mnyama, nyumbu, nyie, nyundo, nyanyua,<br />
nyota,nyima.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya nyundo, uulize: Hii ni nini? Wanafunzi wajibu:<br />
Huyo ni nyundo.<br />
2. Andika neno nyundo ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno nyanya. Waulize wanafunzi: Hii ni nini? Waelekeze<br />
wanafunzi wajibu, hiyo ni nyundo. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka neno ng’aa<br />
kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya nyoka, nyanya, nyika, nyanyua,<br />
nyofoa. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ny wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
91
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama nyima, nyie, nyumbu,<br />
nyundo, nyumba,nyanya, mnyama.<br />
Somo la 43 (b): Kuandika herufi ny<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano ny.<br />
Muda: Kipindin 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano ny. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi ny<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
nya nye nyi nyo nyu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
ny kwenye madaftari yao.<br />
nyanya<br />
nyumba<br />
nyoka<br />
mnyama<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ny na<br />
silabi zingine.<br />
92
nyumbu anaishi porini<br />
nyanya ni kiungo cha mboga<br />
kaka alinyanyua mzigo<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ny wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno nyanya<br />
Somo la 44 (a): Kusoma herufi py<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano py:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi pya pye pyi, pyo, pyu na maneno yenye herufi mwambatano py. Maneno<br />
kama: kipya, mpya, papya, kupya<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya shati jipya uulize: Hii ni nini? Wanafunzi wajibu:<br />
Hilo ni shati jipya.<br />
2. Andika maneno shati jipya ubaoni kisha uyasome kwa sauti mara mbili. Waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya maneno daftari jipya. Waulize wanafunzi: Hili ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, hilo daftari jipya. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
maneno daftari jipya kwa sauti ili waweze kuyatamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya kipya, mpya, papya, kupya,<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
py wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama kipya, mpya, papya,<br />
kupya<br />
Somo la 44 (b): Kuandika herufi py<br />
93
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano py.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano py. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi py<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
pya pye pyi pyo pyu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
py’ kwenye madaftari yao.<br />
kipya<br />
jipya<br />
mapya<br />
kupya<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano<br />
py na silabi zingine.<br />
pori lile ni jipya kabisa.<br />
shule yenu ni mpya<br />
94
aba ana gari jipya<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
py wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waelekeze wanafunzi waandike sentensi walizotunga kwenye somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mpya.<br />
Somo la 45 (a): Kusoma herufi pw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano pw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi pwa, pwe, pwi, pwo, pwu na maneno yenye herufi mwambatano pw.<br />
Maneno kama: mpwa, pwani, pweza, upweke, upwa, tupwa, pwaya, pweteka<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya pweza uulize: Huyu ni nani? Wanafunzi wajibu:<br />
Huyo ni pweza.<br />
2. Andika neno pweza ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno pwani. Waulize wanafunzi: Hapa ni wapi?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, hapo ni pwani. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
neno pwani kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mpwa, pwani, pweza, upweke,<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
pw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama upwa, tupwa, pwaya,<br />
pweteka.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
95
Somo la 45 (b): Kuandika herufi pw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano pw.<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano pw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi pw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
pwa pwe pwi pwo pwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
pw kwenye madaftari yao.<br />
mpwa<br />
pwani<br />
pwaya<br />
tupwa<br />
4.Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano pw na<br />
silabi zingine.<br />
machicha yametupwa jalalani.<br />
96
mjomba amekwenda pwani kuvua.<br />
viatu hivi vinanipwaya<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
pw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno tupwa.<br />
Somo la 46 (a): Kusoma herufi sh<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano sh:<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Zana: Kadi za silabi sha, she, shi, sho, shu na maneno yenye herufi mwambatano sh. Maneno<br />
kama: shule, shime shukuru, shati, shemeji, shika, shuka, shehe.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya shati uulize: Hii ni nini? Wanafunzi<br />
wajibu: Hili ni shati<br />
2. Andika neno shati ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno shule. Waulize wanafunzi: Hii ni nini? Waelekeze<br />
wanafunzi wajibu, hii ni shule. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno shule kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya shati, shule, shuka. Waongoze<br />
wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano sh<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama shati, shemeji, shika,<br />
shuka .<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
97
Somo la 46 (b): Kuandika herufi sh<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano sh.<br />
Muda: Kipindi 1.<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano sh. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi sh<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
sha she shi sho shu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
Sh kwenye madaftari yao.<br />
shati<br />
shule<br />
shuka<br />
shukuru<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano sh<br />
na silabi zingine.<br />
98
ukipewa kitu shukuru.<br />
shati la kaka ni jipya<br />
shule yetu ni nzuri<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
sh wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno shule.<br />
Somo la 47 (b): Kusoma herufi sk<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano sk:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi ska, ske, ski, sko, sku na maneno yenye herufi mwambatano sk. Maneno<br />
kama: askari, sketi, askofu, skafu, skauti, skonzi.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya sketi uulize: Hii ni nini? Wanafunzi<br />
wajibu: Hili ni sketi.<br />
2. Andika neno sketi ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno askari. Waulize wanafunzi: Huyu ni nani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huyu ni askari. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno askari kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya askari, sketi, askofu. Waongoze<br />
wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano sh<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
99
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama skafu, skauti, skonzi.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 47 (b): Kuandika herufi sk<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano sk.<br />
Muda: Tunga sentensi kwa kutumia neno skafu.<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano sk. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi sk<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
ska ske ski sko sku<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
sk kwenye madaftari yao.<br />
skauti<br />
skafu<br />
askari<br />
skonzi<br />
100
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano sk na<br />
silabi zingine.<br />
askari amevaa sketi<br />
shati la kaka ni jipya<br />
Sconzi ni tamu<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
sk wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno skafu<br />
Somo la 48 (a): Kusoma herufi st<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano st:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi sta, ste, sti, sto, stu na maneno yenye herufi mwambatano st. Maneno<br />
kama: bustani, mstari, posta, stesheni, stendi, stimu, stoo, studio.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya bustani uulize: Hii ni nini? Wanafunzi<br />
wajibu: Hiyo ni bustani.<br />
2. Andika neno bustani ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi ya neno posta. Waulize wanafunzi: Hapa ni wapi?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, hapo ni posta. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno posta kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
101
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya bustani, mstari, posta, stesheni.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano st<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama stendi, stimu, stoo,<br />
studio.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 62 (b): Kuandika herufi st<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano st.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano st. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi st<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
sta ste sti sto stu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
st kwenye madaftari yao.<br />
bustani<br />
102
posta<br />
mstari<br />
stesheni<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano st na<br />
silabi zingine.<br />
Shule yetu ina bustani kubwa<br />
juzi nilikwenda posta<br />
treni ipo stesheni<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
st wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno stesheni.<br />
Somo la 49 (a): Kusoma herufi sw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano sw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi swa, swe, swi, swo, swu na maneno yenye herufi mwambatano sw. Maneno<br />
kama: swala, sweta, swichi, swaga, swahibu, swali, swila.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya sweta uulize: Hili ni nini? Wanafunzi<br />
wajibu: Hilo ni sweta.<br />
2. Andika neno sweta ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
103
3. Waonesha wanafunzi kadi ya picha ya swala. Waulize wanafunzi: Huyu ni nini?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu, huyo ni swala. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
neno swala kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya swala, sweta, swichi na swaga.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
sw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama swahibu, swali, swila<br />
na swaumu<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 49 (b): Kuandika herufi sw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano sw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano sw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi sw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
swa swe swi swo swu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
st kwenye madaftari yao.<br />
104
swahibu<br />
swali<br />
swaga<br />
swichi<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano sw<br />
na silabi zingine.<br />
Swichi inawashia taa<br />
Kaka anaswaga mbuzi<br />
Swahibu wangu amekuja<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
sw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno sweta.<br />
Somo la 50 (a): Kusoma herufi th<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano th:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi tha, the, thi, tho, thu na maneno yenye herufi mwambatano th. Maneno<br />
kama: theluji, themanini, thelathini, thamani, thawabu, thabiti,<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya mlima wenye theluji. Uulize: Juu ya mlima kuna<br />
nini? Wanafunzi wajibu: Juu ya mlima kuna theluji.<br />
105
2. Andika neno theluji ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye namba themanini. Waulize wanafunzi: Hii ni namba<br />
gani? Waelekeze wanafunzi wajibu: Hiyo ni namba themanini. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno swala kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya theluji, themanini na thelathini<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano th<br />
wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na yaliyo<br />
kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
Wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama thamani, thawabu,<br />
thabiti.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 50 (b): Kuandika herufi th<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano th.<br />
Muda; Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano th. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi th<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
tha the thi tho thu<br />
106
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
th kwenye madaftari yao.<br />
thamani<br />
thabiti<br />
thawabu<br />
thelathini<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano th na<br />
silabi zingine.<br />
darasani kwetu tupo thelathini.<br />
ukisali unapata thawabu<br />
Mbuzi anauzwa shilingi elfu thelathini.<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
th wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno theluji;<br />
Somo la 51 (a): Kusoma herufi tw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano tw:<br />
Muda: Kipindi 1<br />
107
Zana: Kadi za silabi twa, twe, twi, two, twu, picha ya mtu anayetwanga na anayetwika mzigo<br />
na maneno yenye herufi mwambatano tw. Maneno kama: twanga, tweta, patwa, kutwa,<br />
okotwa, twika, twisha, tweka, twaibu<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha mtu anatwanga. Uulize: Juu ya mlima kuna<br />
nini? Wanafunzi wajibu: Juu ya mlima kuna theluji.<br />
2. Andika neno twanga ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya mtu anayetwika mzigo. Waulize wanafunzi:<br />
Huyu anafanya ni nini? Waelekeze wanafunzi wajibu: Huyo anajitwika mzigo<br />
Waelekeze wanafunzi warudie kutamka neno twika kwa sauti ili waweze kulitamka<br />
vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya twanga, tweta, patwa, kutwa na<br />
okotwa. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
tw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama twika, twisha, tweka,<br />
twaibu<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 51 (b): Kuandika herufi tw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano tw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano tw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi tw<br />
108
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
twa twe twi two twu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
tw kwenye madaftari yao.<br />
twanga<br />
patwa<br />
kutwa<br />
twiga<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano tw na<br />
silabi zingine.<br />
twiga ana shingo ndefu.<br />
dada anatwanga kisamvu<br />
tumesoma mchana kutwa<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
tw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno kutwa.<br />
109
Somo la 52 (a): Kusoma herufi vy<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano vy.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi vya, vye, vyi, vyo, vyu, picha ya vyura na vyungu na maneno yenye herufi<br />
mwambatano vy. Maneno kama: vyura, vyungu, vyanzo, vyuma, vyote. Vyao, vyenu, vyangu,<br />
vyetu, vyovyote,<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha vyura wawili. Uulize: Hawa ni nani?<br />
Wanafunzi wajibu: Hao ni vyura.<br />
2. Andika neno vyura ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya vyungu viwili. Waulize wanafunzi: Hivi ni<br />
nini? Waelekeze wanafunzi wajibu: Hivi ni vyungu. Waelekeze wanafunzi warudie<br />
kutamka neno vyungu kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya vyura, vyungu, vyanzo, vyuma,<br />
vyote. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
vy wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama vyao, vyenu, vyangu,<br />
vyetu, vyovyote.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 51 (b): Kuandika herufi vy<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano vy.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
110
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano vy. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi vy<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
vya vye vyi vyo vyu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
vy kwenye madaftari yao.<br />
vyungu<br />
vyura<br />
vyetu<br />
vyao<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano vy na<br />
silabi zingine.<br />
vyungu vyetu vimepambwa<br />
vyura wapo visimani<br />
vitabu hivi ni vyetu<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
111
vy wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno vyungu<br />
Somo la 53 (a) :Kusoma herufi chw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano chw<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi chwa, chwe, chwi, chwo, chwu, picha ya kichwa na mchwa na maneno<br />
yenye herufi mwambatano chw. Maneno kama: kichwa, mchwa, kuchwa, machweo<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya kichwa. Uulize: Hiki ni nini?<br />
Wanafunzi wajibu: Hiki ni kichwa.<br />
2. Andika neno kichwa ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kichwa kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya mchwa. Waulize wanafunzi: Hawa ni nani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu: Hao ni mchwa. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
neno mchwa kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya kichwa, mchwa, kuchwa, machweo.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
chw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama kichwa, mchwa,<br />
kuchwa, machweo.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 53 (b): Kuandika herufi chw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano chw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
112
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano chw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi chw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
chwa chwe chwi chwo chwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
chw kwenye madaftari yao.<br />
kuchwa<br />
kichwa<br />
machweo<br />
mchwa<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mbw<br />
na silabi zingine.<br />
jua limekuchwa<br />
kichwa kinaniuma<br />
mchwa wanarudi shimoni<br />
113
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
chw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini<br />
ya picha hizo.<br />
8. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mchwa.<br />
Somo la 54: Kusoma herufi mbw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano mbw<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi mbwa, mbwe, mbwi, mbwo, mbwu, picha ya mbweha na vyungu na<br />
maneno yenye herufi mwambatano mbw. Maneno kama: mbwa, mbwembwe, mbweha,<br />
mbwamwitu<br />
Hatua:<br />
6. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya mbweha. Uulize: Huyu ni nani?<br />
Wanafunzi wajibu: Huyo ni mbweha.<br />
7. Andika neno mbweha ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
8. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya mbwa. Waulize wanafunzi: Huyu ni nani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu: Huyo ni mbwa. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
neno mbwa kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
9. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mbwa, mbwembwe, mbweha,<br />
mbwamwitu. Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
10. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mbw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mbwa, mbwembwe,<br />
mbweha, mbwamwitu.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
114
Somo la 54 (b): Kuandika herufi mbw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mbw.<br />
Mada: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
2. Andika ubaoni herufi-mwambatano mbw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi mbw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mbwa mbwe mbwi mbwo mbwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mbw kwenye madaftari yao.<br />
mbwamwitu<br />
mbweha<br />
mbwembwe<br />
mbwa<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mbw<br />
na silabi zingine.<br />
mbwamwitu ni mnyama makali<br />
115
mbweha ni mwoga<br />
swahibu wangu anapenda mbwembwe<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mbw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini<br />
ya picha hizo.<br />
9. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mbweha.<br />
Somo la 55 (a): Kusoma herufi ngw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kusoma maneno yanye herufi-mwambatano ngw<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za silabi ngwa, ngwe, ngwi, ngwo, ngwu, picha ya chungwa na ya mtu anayepigwa<br />
ngwara na maneno yenye herufi mwambatano ngw. Maneno kama: chungwa, gongwa, ngwara,<br />
shangwe, pangwa, kungwi, ungwa.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi ya picha ya chungwa. Uulize: Hili ni nini?<br />
Wanafunzi wajibu: Hilo ni chungwa.<br />
2. Andika neno chungwa ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya mtu anayepigwa ngwara. Waulize<br />
wanafunzi: Huyu anafanywa nini? Waelekeze wanafunzi wajibu: Huyo anapigwa<br />
ngwara. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka neno ngwara kwa sauti ili waweze<br />
kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya chungwa, gongwa, ngwara, shangwe.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ngw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama pangwa, kungwi, ungwa<br />
116
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 55 (b): Kuandika herufi ngw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano ngw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano ngw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye<br />
vibao vyao.<br />
Herufi ngw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
ngwa ngwe ngwi ngwo ngwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
ngw kwenye madaftari yao.<br />
ungwa<br />
pangwa<br />
chungwa<br />
shangwe<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano ngw<br />
na silabi zingine.<br />
117
Chungwa ni tunda tamu<br />
Jana kulikuwa na shangwe<br />
Mbuzi wetu amegongwa na gari<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
ngw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini<br />
ya picha hizo.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno chungwa.<br />
Somo la 56 (a): Kusoma herufi mpw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano mpw<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Zana: Kadi za silabi mpwa, mpwe, mpwi, mpwo, mpwu, na maneno yenye herufi<br />
mwambatano mpw. Maneno kama: mpwa, mpweke, mpwito.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi yenye neno mpwa. Uulize: Hili ni neno gani?<br />
Wanafunzi wajibu: Neno hilo ni mpwa.<br />
2. Andika neno mpwa ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waonesha wanafunzi kadi yenye picha ya mtu mpweke. Waulize wanafunzi: Huyu mtu<br />
yuko hali gani? Waelekeze wanafunzi wajibu: Huyo ni mpweke. Waelekeze wanafunzi<br />
warudie kutamka neno ngwara kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya mpwa, mpweke, mpwito. Waongoze<br />
wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mpw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
118
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama mpwa, mpweke,<br />
mpwito.<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 56 (b): Kuandika herufi mpw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano mpw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano mpw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye vibao vyao.<br />
Herufi mpw<br />
2. Waelekeze wanafunzi namna ya waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha<br />
wanakili silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
mpwa mpwe mpwi mpwo mpwu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
mpw kwenye madaftari yao.<br />
mpwa<br />
mpweke<br />
mbwembwe<br />
119
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano mpw<br />
na silabi zingine.<br />
si vizuri kuwa mpweke<br />
jibu limapwita<br />
mpwa wangu ananiita shangazi<br />
5. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
mpw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini ya<br />
picha hizo.<br />
6. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno mpwa<br />
Somo la 57 (a): Kusoma herufi nyw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi aweze kusoma maneno yenye herufi-mwambatano nyw<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Zana: Kadi za silabi nywa, nywe, nywi, nywo, nywu, picha ya kinywa na maneno yenye<br />
herufi mwambatano nyw. Maneno kama: nywele, kinywaji, kinywa, finywa, nywea, hanywi,<br />
kunywa, nywesha.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi kadi yenye neno nywele. Uulize: Juu ya vichwa vyenu kuna nini?<br />
Wanafunzi wajibu: Kuna nywele.<br />
2. Andika neno nywele ubaoni kisha ulisome kwa sauti mara mbili. Waongoze wanafunzi<br />
walisome neno kwa sauti mmoja mmoja.<br />
3. Waoneshe wanafunzi kadi yenye picha kinywa. Waulize wanafunzi: Hiki ni kitu gani?<br />
Waelekeze wanafunzi wajibu: Hicho ni kinywa. Waelekeze wanafunzi warudie kutamka<br />
neno kinywa kwa sauti ili waweze kulitamka vizuri.<br />
120
4. Andika maneno haya ubaoni kwa kuyachanganya nywele, nywesha, kunywa, kinywaji.<br />
Waongoze wanafunzi wayasome pamoja kwa vikundi na mmoja mmoja.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
nyw wachunguze picha kisha wasome maneno na sentensi zilizo chini ya picha hizo na<br />
yaliyo kwenye kisanduku.<br />
6. Changanya kadi za maneno yenye herufi mwambatano. Kisha waelekeze wanafunzi<br />
wayasome maneno hayo kwa sauti mmoja mmoja. Maneno kama kinywa, finywa, nywea<br />
hanywi<br />
7. Waongoze wanafunzi watunge sentensi kwa kutumia maneno hayo.<br />
Somo la 57 (b): Kuandika herufi nyw<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika maneno yenye herufi-mwambatano nyw.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Penseli na vibao<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi-mwambatano nyw. Kisha waongoze wanafunzi waziandike<br />
kwenye vibao vyao.<br />
Herufi nyw<br />
2. Waelekeze wanafunzi waandike silabi za herufi mwambatano zifuatazo: Kisha wanakili<br />
silabi hizo kwenye vibao vyao.<br />
nywa nywe nywi nywo nywu<br />
3. Waelekeze wanafunzi waandike maneno yafuatayo yanayotokana na herufi mwambatano<br />
nyw kwenye madaftari yao.<br />
nywea<br />
finywa<br />
121
nywesha<br />
4. Waelekeze wanafunzi wanakili sentensi zifuatazo zitokanazo na herufi mwambatano nyw<br />
na silabi zingine.<br />
nilikata nywele jana<br />
ninasafisha kinywa changu kila siku<br />
Mtoto ananyweshwa maziwa<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye kitabu chao sura ya sita (6.2) somo la herufi mwambatano<br />
nyw wachunguze picha na kunakili maneno na sentensi zilizo ndani ya visanduku chini<br />
ya picha hizo.<br />
7. Waongoze wanafunzi waandike sentensi walizotunga katika somo la kusoma katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Tunga sentensi kwa kutumia neno kinywa<br />
KUSOMA NA KUANDIKA NAMBA<br />
Somo la 58: Tusome na kuandika namba 0, 1, 2<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma na kuandika namba 0, 1.2.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana/vifaa: Kadi za namba 0, 1 na 2<br />
Hatua:<br />
122
1. Andika ubaoni namba 0. Kisha uisome kwa sauti sifuri<br />
2. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 0<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
3. Waoneshe kadi ya namba 0 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
4. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 0 hatua kwa hatu<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 0<br />
5. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 0 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
6. Andika ubaoni namba 1. Kisha uisome kwa sauti moja.<br />
7. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 1<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
8. Waoneshe kadi ya namba 1 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
9. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 1 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 1<br />
10. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 1 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
11. Andika ubaoni namba 2. Kisha uisome kwa sauti mbili.<br />
12. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 2<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
13. Waoneshe kadi ya namba 2 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
14. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 2 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 2<br />
15. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 2 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Andika kwa maneno namba 0 mpaka 2<br />
Somo la 73: Tusome na kuandika namba 3, 4, 5<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma na kuandika namba 3, 4, 5.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za namba 3, 4 na 5<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni namba 3. Kisha uisome kwa sauti tatu.<br />
123
2. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 3<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
3. Waoneshe kadi ya namba 3 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
4. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 3 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 3<br />
5. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 3 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
6. Andika ubaoni namba 4. Kisha uisome kwa sauti nne.<br />
7. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 4<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
8. Waoneshe kadi ya namba 4 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
9. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 4 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 4<br />
10. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 4 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
11. Andika ubaoni namba 5. Kisha uisome kwa sauti tano.<br />
12. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 5<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
13. Waoneshe kadi ya namba 5 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
14. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 5 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 5<br />
15. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 5 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Andika kwa maneno namba 3 mpaka 5<br />
Somo la 74: Tusome na kuandika namba 6, 7, 8 na 9<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma na kuandika namba 6, 7, 8.9<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Zana: Kadi za namba 6, 7, 8 na 9<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni namba 6. Kisha uisome kwa sauti sita.<br />
2. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 6<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
124
3. Waoneshe kadi ya namba 6 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
4. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 6 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 6<br />
5. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 6 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
6. Andika ubaoni namba 7. Kisha uisome kwa sauti saba.<br />
7. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 7<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
8. Waoneshe kadi ya namba 7 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
9. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 7 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 7<br />
10. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 7 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
11. Andika ubaoni namba 8. Kisha uisome kwa sauti nane.<br />
12. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 8<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
13. Waoneshe kadi ya namba 8 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
14. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 8 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 8<br />
15. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 8 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
16. Andika ubaoni namba 9. Kisha uisome kwa sauti tisa.<br />
17. Waongoze watamke kwa sauti kwa pamoja na mmoja mmoja huku ukionesha 9<br />
ulioiandika ubaoni.<br />
18. Waoneshe kadi ya namba 9 kisha waelekeze wasome kwa sauti.<br />
19. Waongoze wanafunzi kwa kuonesha hewani jinsi ya kuandika 9 hatua kwa hatua<br />
kama ifuatavyo:<br />
Chora hatua za uandishi wa tarakimu 9<br />
20. Waongoze wanafunzi waandike tarakimu 9 nyingi kisha kwa maneno katika<br />
madaftari yao.<br />
Tafakuri: Andika kwa maneno namba 6 mpaka 9<br />
Somo la 70 : Herufi Aa<br />
HERUFI KUBWA<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa<br />
125
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Chora ubaoni mchoro ufuatao na wanafunzi waunakili katika madaftari yao.<br />
Mchoro wa zigizagi<br />
2. Andika herufi kubwa A kwa kufuata hatua zilivyooneshwa.<br />
Waongoze wanafunzi wanakili hadi kujaza mstari mmoja.<br />
Mchoro wa herufi A<br />
3. Andika ubaoni herufi A kama ifuatavyo kisha wanafunzi wazinakili kwenye<br />
Madaftari yao.<br />
ziandikwe Aa<br />
4. Andika ubaoni majina yafuatayo kisha wanafunzi wayasome kwa sauti mmoja<br />
mmoja. Waongoze wanafunzi wayanakili majina hayo kwenye madaftari yao.<br />
Ni muhimu uzingatie utaratibu wa hati ya wima yenye vikonyo katika kuandika<br />
maneno na sentensi. Herufi kubwa hazina vikonyo, lakini baadhi ya herufi zingine<br />
zina vikonyo. Kwa hiyo vikonyo vionekana kwenye herufi husika.<br />
Amoni Anna Anita Amani Arumeru Amina Agakani<br />
Amazoni<br />
Adamu Akida Aneti ada<br />
126
5. Andika ubaoni sentensi zifuatazo kisha wanafunzi wazisome kwa sauti mmoja.<br />
mmoja. Waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari yao.<br />
Amina anapenda amani.<br />
Adamu anaishi Arusha.<br />
Amazoni ni mto mkubwa<br />
Tafakuri: A kubwa hutumika kuandika vitu gani?<br />
Somo la 71: Herufi Bb<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa B<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi B nyingi ubaoni kwa kufuata hatua zake. Waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
B B B B B B<br />
B<br />
B<br />
Mchoro wa herufi B kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa B ikiambatana na herufi ndogo b kisha waongoze<br />
wanafunzi wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Bb Bb Bb Bb Bb Bb Bb Bb<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa B kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti mmojammoja na kuyanakili.<br />
127
Bunda Biharamlo Bamaga Bulombora Buhari Bihawana<br />
bakuli<br />
4.Andika ubaoni sentensi zifuatazo kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti<br />
mmoja mmoja na kuzinakili:<br />
Bulombola ni kambi la jeshi.<br />
Bukoba ni karibu na Uganda.<br />
Bibi anakaanga mahindi.<br />
Bakari amekwenda Bagamoyo.<br />
Tafakuri: Mwalimu uwasomee imla ya sentensi hii na wanafunzi waiandike<br />
daftarini mwao: imla ya sentensi hii: Baba amekwenda Babati.<br />
Somo la 72: Herufi Ch<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa Ch<br />
Muda: Kipindi kimoja.<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa Ch nyingi. Waongoze wanafunzi wazinakili madaftarini<br />
mwao.<br />
Ch Ch Ch Ch Ch Ch<br />
Mchoro wa herufi Ch kubwa<br />
2. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa Ch. Waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti mmoja mmoja kisha wazinakili.<br />
128
Chausiku Chimala Chabruma Chacha China Chambo<br />
Chimwaga<br />
chekecheke<br />
3. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti mmoja<br />
mmoja kisha wazinakili.<br />
Chausiku ni jirani yetu<br />
Chimala kuna maduka mengi<br />
Chabruma alikuwa chifu wa kabila la wangoni.<br />
Chacha ni mtu mwenye nguvu<br />
Tafakuri: Mwalimu uwasome imla ya sentensi hii na wanafunzi waiandike daftarini mwao:<br />
Chonya amekwenda Chikundi<br />
Somo la 73: Herufi Dd<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Wanafunzi waweze kuandika harufi kubwa<br />
Muda: kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa D nyingi. Waongoze wanafunzi wazinakili madaftarini<br />
mwao.<br />
D D D D D D D D<br />
Mchoro wa herufi D kubwa<br />
129
2. Andike ubaoni herufi D ikiambatana na herufi ndogo d kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao<br />
Dd Dd Dd Dd Dd Dd Dd Dd Dd Dd Dd<br />
3 Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa Dd. Waongoze wanafunzi wayasome<br />
kwa sauti mmoja mmoja kisha wazinakili.<br />
Dina Dakawa Daniel Dula Dindimo Dumila dada<br />
3. Andike ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti<br />
mmoja mmoja na wazinakili.<br />
Dina na Domi wamewahi shule.<br />
Dar es Salaam ni mji wa biashara<br />
Dakawa kuna chuo cha ualimu.<br />
Dodoma ni makao makuu<br />
Tafakuri: Mwalimu uwasomee imla ya sentensi hii na wanafunzi waiandike daftarini mwao:<br />
Damasi hajafika Dodoma.<br />
Somo la 74: Herufi Ee<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa E<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
130
1. Andika herufi E nyingi ubaoni kwa kufuata hatua zake. Waongoze wanafunzi wazinakili<br />
kwenye madaftari yao.<br />
E E E E E E E E<br />
Mchoro wa herufi E kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa E ikiambatana na herufi ndogo e kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Ee Ee Ee Ee Ee Ee Ee<br />
Ee Ee<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa E. Waongoze wanafunzi<br />
wayasome na wayanakili.<br />
Emma Elizabeti Eliamini Esta Emili embe<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Waongoze wanafunzi wazisome na kuzinakili.<br />
Embe ni tunda zuri sana<br />
Emma anaweza kutoa na kujumlisha namba.<br />
Elizabeti ni mwanafunzi wa darasa la kwanza<br />
Emili na Esta ni wachezaji wa mpira wa mikono.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi, kwa nini tunajifunza kuandika herufi E<br />
Somo la 75: Herufi Ff<br />
131
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa F<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa F kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari<br />
yao.<br />
F F F F F F<br />
F<br />
Mchoro wa herufi F kubwa inatangulia<br />
2. Andike ubaoni herufi F ikiambatana na herufi ndogo f kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao<br />
Ff Ff Ff Ff Ff Ff<br />
Ff Ff<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa F. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti mmoja mmoja na wayanakili.<br />
Farida Fikiri Furaha Forodhani Farahani<br />
Fentu fungo<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
wazinakili.<br />
Farahani anahesabu fedha<br />
132
Nimefurahi kucheza na Furaha<br />
Fahali wawili hawaishi zizi moja.<br />
Fentu anazungumza vizuri<br />
Tafakuri: Uwaulize wanafunzi swali hili: Ni sehemu gani ya somo hii ambayo hujaelewa<br />
vizuri?<br />
Somo la 76: Herufi Gg<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa G<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa G nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili<br />
daftarini.<br />
G G G G G G<br />
G<br />
Mchoro wa herufi G kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa G ikiambatana na herufi ndogo g kisha waongoze<br />
wanafunzi wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Gg Gg Gg Gg Gg<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa G. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti mmoja mmoja na wayanakili.<br />
Goliati Gadau Godegode Gairo Gidioni Gangironga<br />
genge<br />
133
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
wazinakili.<br />
Gadau anakwenda Geita.<br />
Gongolamboto kuna nyumba nyingi<br />
Gonga mlango utafunguliwa.<br />
Genge la baba limejaa vitu vingi<br />
Tafakuri: Ni sehemu gani ya somo hili ambayo umeifurahia sana?<br />
Somo la 77: Herufi Hh<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika harufi kubwa H<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa kama H. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili<br />
daftarini.<br />
H H H H H H<br />
H<br />
Mchoro wa herufi H kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa H ikiambatana na herufi ndogo h kisha waongoze<br />
wanafunzi wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Hh Hh Hh Hh Hh Hh<br />
Hh Hh<br />
134
3. Andike ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa H. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Haule Hale Horohoro Hosea Hangu<br />
Hidaya Holili<br />
hema<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Haule anabisha hodi mlangoni kwetu.<br />
Bwawa la Hale ni maarufu kwa utoaji wa umeme<br />
Hosea anazijua sana sheria.<br />
Hangu ni kijana mzuri sana.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili, Ukitaka kuandika jina la Halima utaanza na<br />
herufi gani?<br />
Somo la 78: Herufi li<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa I<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa I . Kisha waongoze wanafunzi wazinakili<br />
daftarini.<br />
135
I I I I I<br />
Mchoro wa herufi l kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa I ikiambatana na herufi ndogo i kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Ii Ii Ii Ii Ii<br />
Ii<br />
Ii<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa I kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Ilula Ibrahimu Iringa Imakulata Isa<br />
Itigi ini<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Isaya amekwenda Ifakara<br />
Mimi ninaishi Iringa<br />
Isa anapenda kucheza mpira<br />
Imakulata anasomma shule ya msingi Itigi<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Taja majina matatu ya watu ambayo yanaanza na<br />
herufi kubwa I<br />
136
Somo la 79: Herufi Jj<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa J.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa J nyingi kisha waongoze wanafunzi wazinakili<br />
daftarini.<br />
J J J J J<br />
Mchoro wa herufi J kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa J ikiambatana na herufi ndogo j kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Jj Jj Jj Jj Jj<br />
Jj Jj<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa J kisha wanafunzi wayasome kwa<br />
sauti na kuyanakili.<br />
Jamila Jerome Joisi John Jabiri<br />
Jokolo juisi<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Jamila ni mwanafunzi wa darasa la kwanza<br />
Jongo na Jabiri wanamfahamu Juma<br />
Jirani mwema amempokea Jokolo.<br />
Jengo ni mchoraji bora<br />
137
Tafakuri: Ni sehemu gani ya somo hili umeipenda sana.<br />
Somo la 80: Herufi Kk<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa K<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa K nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili<br />
daftarini.<br />
K K K K K<br />
Mchoro wa herufi K kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa K ikiambatana na herufi ndogo k kisha waongoze<br />
wanafunzi wazinakili kwenye madaftari yao.<br />
Kk Kk Kk Kk Kk<br />
Kk Kk<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa K. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti mmoja mmoja na wayanakili.<br />
Kurasini Kalosi Kinampanda Korogwe Korea<br />
Kisimayu kiazi<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
138
daraja mpya na la kisasa limejengwa Kurasini.<br />
kisima kile kimechimbwa na Kalosi.<br />
Kulwa ni mkufunzi wa chuo cha ualimu Korogwe.<br />
Reli ya kati imepita karibu na Kinampanda.<br />
Tafakuri: Waulize wanafunzi swali hili.Umefaidikaje na somo kipindi hiki?<br />
Somo la 81: Herufi Ll<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa L<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa L nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
.<br />
L L L L L<br />
Mchoro wa herufi L kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa L ikiambatana na herufi ndogo l kisha waongoze wanafunzi<br />
wazinakili kwenye madaftari yao<br />
139
Ll Ll Ll Ll Ll<br />
Ll Ll<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa L kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili<br />
Lugano Ludewa Lulu Ligunga Lugalo<br />
Longido leso Lema<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Lugano anafuga kuku..<br />
Ludewa kuna machimbo ya makaa ya mawe.<br />
Longato anafuga ng’ombe wa maziwa<br />
Lomwe ni shule nzuri.<br />
Tafakuri: Taja majina mawili yenye kutumia L kubwa<br />
Somo la 82: Herufi Mm<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa M<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa M nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
140
M M M M M<br />
Mchoro wa herufi M kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa M ikiambatana na herufi ndogo m kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao<br />
Mm Mm Mm Mm<br />
Mm<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa M. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Mariamu Mamea Maria Mombasa Msamvu Mungu maziwa<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Monika amebeba mzigo.<br />
Mombasa ni mji maarufu nchini Kenya<br />
Watu wote wanamwabudu Mungu<br />
Morogoro kuna mpunga mwingi<br />
Tafakuri: Somo limekufurahisha kwa kiasi gani?<br />
Somo la 83: Herufi Nn<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika harufi kubwa N<br />
Muda: Kipindi 1<br />
141
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa N nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari<br />
yao.<br />
N N N N N<br />
Mchoro wa herufi N kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa N ikiambatana na herufi ndogo n kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Nn Nn Nn Nn Nn<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa N. Kisha waongoze wanafunzi<br />
Wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Nana Nairobi Nurudini Newala Noel Nuru neno<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Nana hana nauli ya ndege.<br />
Namanga ni mpakani mwa Kenya na Tanzania.<br />
Nurudini ana watoto watatu.<br />
Tafakuri: andika majina matatu yanayoanza na herufi n<br />
Somo la 84: Herufi Oo<br />
142
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa O<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa O nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari<br />
yao.<br />
O O O O O<br />
Mchoro wa herufi O kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa O ikiambatana na herufi ndogo o kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Oo Oo Oo Oo Oo<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa O kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Otilia Onyango Onesmo Oliva Ore Oman oka<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome na kuzinakili.<br />
Omari ni mwimbaji<br />
Onyango ni mwigizaji mashuhuri.<br />
Oliva na Otilia ni watoto pacha.<br />
Oresti na Ore wanasoma darasa la kwanza<br />
Tafakuri: Unawezaje kutofautisha herufi o na a?<br />
143
Somo la 85: Herufi Pp<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Kusudi: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa P.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa P nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
maaftari yao.<br />
P P P P p<br />
Mchoro wa herufi P kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa P ikiambatana na herufi ndogo p kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
.<br />
Pp Pp Pp Pp Pp<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa P. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Pili Paskali Paulo Porona Pondamali<br />
pipi<br />
4. Andike ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Pondamali alikuwa golikipa hodari.<br />
Pangaro ni kijiji cha wafugaji.<br />
Pongwe ipo karibu na Tanga<br />
144
Pili ni binti mpole.<br />
Tafakuri: Andika majina matatu yanayoanza na herufi P?<br />
Somo la 86: Herufi Rr<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa R.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa R nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
R R R R R R R<br />
Mchoro wa herufi R kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa R ikiambatana na herufi ndogo r kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Rr Rr Rr Rr Rr<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa R. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Raisi Regina Rozi Rukwa Rufiji Razia<br />
reli<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Raisi ni kiongozi mkuu nchini.<br />
Regina ana bidii darasani.<br />
145
Nilikwenda Rukwa wiki iliyopita.<br />
Razia ni rafiki yake Regina.<br />
Tafakari: Ni sahihi kuandika maneno rangi na rungu kwa kutumia herufi ndogo<br />
r?<br />
Somo la 87: Herufi Ss<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa S.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa S nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari<br />
yao.<br />
S S S S S S S<br />
Mchoro wa herufi S kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa S ikiambatana na herufi ndogo s kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Ss Ss Ss Ss Ss<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa S. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Sesilia Somalia Sima Salome Sirili Samsoni sasa<br />
3. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
146
Sara ana kalamu saba.<br />
Sima alikula sima ya ugali.<br />
Nimeiona sinema ya Samsoni na Delila.<br />
Sarafina anaishi Same.<br />
Tafakuri: Sehemu gani umeifurahia sana katika somo hili?<br />
Somo la 88: Herufi Tt<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa T.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika herufi kubwa T nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika madaftari<br />
yao.<br />
T T T T T T T<br />
Mchoro wa herufi T kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa T ikiambatana na herufi ndogo t kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
.<br />
Tt Tt Tt Tt Tt<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa T. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
147
Tomaso Tobaldi Tanzania Teresia Tatu<br />
Turuka Tarime<br />
teke<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Tatu ni mchezaji bora wa netiboli.<br />
Tanzania ni nchi yenye amani.<br />
Turuka alisafiri kutoka Tanga hadi Tarime.<br />
Tingi kuna tangi bovu<br />
Tafakuri: Kwa nini tunaandika kwa kutumia herufi kubwa?<br />
Somo la 89: Herufi Uu<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa U.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa U nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
U U U U U U U<br />
Mchoro wa herufi U kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa U ikiambatana na herufi ndogo u kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
3.<br />
148
Uu Uu Uu Uu Uu<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa U. Kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili<br />
Usangi Ulaya Ukonga Ulanga Umatumbi<br />
unga<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Utengano ni udhaifu.<br />
Ulanga kuna madini ya ulanga.<br />
Usangi ni kijiji bora<br />
Utengule kunalimwa viazi.<br />
Tafakuari: Kwa nini tunajifunza herufi kubwa?<br />
Somo la 90: Herufi Vv<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa V.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa V nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
V V V V V V V<br />
Mchoro wa herufi V kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa V ikiambatana na herufi ndogo v kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
149
Vv Vv Vv Vv Vv<br />
3. Mwalimu aandike ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa V. Kisha waongoze na<br />
wanafunzi wayasome na kuyanakili.<br />
Veronika Victoria Vumilia Volka Vivian vua<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Voluka amevaa viatu.<br />
Msichana yule anaitwa Veronika.<br />
Vumilia anavumilia njaa.<br />
Vaileti ni fundi mjenzi.<br />
Tafakuri: Andika maneno matatu ya watu yanayoanza na herufi v<br />
Somo la 91: Herufi Ww<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa W.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa W nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
150
W W W W W W<br />
W<br />
Mchoro wa herufi W kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa W ikiambatana na herufi ndogo w kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Ww Ww Ww Ww<br />
Ww<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa W kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Waridi Wiliamu Wete Wino Wangari wazi<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
niliwaona Wiliam na Werema wanasalimiana.<br />
Wangari alipanda miti mingi.<br />
Wete ipo Pemba.<br />
Waridi anaandika kwa kalamu ya wino.<br />
Tafakari: Mwalimu uwaelekeze watumie neno wembe kwenye sentensi<br />
151
Somo la 92: Herufi Yy<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa Y.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa Y nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
Y Y Y Y Y Y Y<br />
Mchoro wa herufi Y kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa Yy ikiambatana na herufi ndogo y kisha waongoze<br />
wanafunzi wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Yy Yy Yy Yy Yy<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa Y kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili<br />
Yeremia Yusufu Yona Yasinta Yombo<br />
Yanga yeye<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Yona ni rafiki yangu.<br />
Timu ya Yanga ni machachari sana.<br />
152
Yeremia anachora picha za wanyama.<br />
Mjomba wangu anaishi Yombo Dovya.<br />
Tafakuri: Unafikiri kuna umuhimu gani wa kujua kusoma na kuandika?<br />
Somo la 93: Herufi kubwa Zz<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuandika herufi kubwa Z.<br />
Muda: Kipindi 1<br />
Hatua:<br />
1. Andika ubaoni herufi kubwa Z nyingi. Kisha waongoze wanafunzi wazinakili katika<br />
madaftari yao.<br />
Z Z Z Z Z Z Z<br />
Mchoro wa herufi Z kubwa<br />
2. Andika ubaoni herufi kubwa Z ikiambatana na herufi ndogo z kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili kwenye madaftari yao.<br />
Zz Zz Zz Zz Zz<br />
3. Andika ubaoni majina yanayoanza na herufi kubwa Z kisha waongoze wanafunzi<br />
wayasome kwa sauti na kuyanakili.<br />
Zuma Zainabu Zuberi Zuhura Zakaria Zena<br />
ziwa<br />
4. Andika ubaoni sentensi zifuatazo. Kisha waongoze wanafunzi wazisome kwa sauti na<br />
kuzinakili.<br />
Zuma ni rais wa Afrika ya Kusini.<br />
Zainabu anapenda kuimba nyimbo<br />
153
Zuberi ni mwenyeji wa Tanga.<br />
Zakaria anatoa zaka.<br />
Tafakuri: Andika maneno haya: Waridi amekwenda Zambia<br />
Somo la: Tutii amri<br />
SURA YA SABA<br />
TUTOA NA TUTEKELEZA AMRI<br />
Ujuzi: Kuwasiliana katika shughuri mbalimbali katika mazingira yake ya karibu.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kutoa na kutii amri<br />
Muda: Vipindi 14<br />
Zana: Kadi zilizoandikwa maneno yanayotumika kutoa amri. Maneno kama: simama, kaa,<br />
rudi, tembea, kimbia, njoo, lala, ruka, kula, andika.<br />
Hatua:<br />
1. Mwite kwa kumshitua mwanafunzi mmoja ukisema: Rashidi simama. Mwanafunzi<br />
asimame huku akisema Nimesimama. Kisha mwambie Rashidi Kaa. Mwanafunzi<br />
akiwa anakaa aseme: ninakaa.<br />
2. Umsimamishe mwanafunzi wa pili ukimwambia: Kayombo Njoo hapa. Mwanafunzi<br />
akiwa anakukaribia aseme: Ninakuja. Kisha umwambie Kayombo : Rudi.<br />
Mwanafunzi akiwa anarudi aseme: Ninarudi.<br />
3. Wagawe wanafunzi katika makundi mawili, kundi A na B.<br />
4. Wape kadi za maneno wazitumie katika kutoa na kutii amri katika vikundi na mmoja<br />
mmoja. Maneno ni kama: simama, kaa chini, tembea, ruka na andika.<br />
5. Waongoze wanafunzi muigize dayolojia ifuatayo;<br />
Mwalimu: Mvungi funga mlango<br />
Mvungi: Ninafunga mlango<br />
Mwalimu: John toka nje<br />
John:<br />
Ninatoka nje.<br />
Mwalimu: John rudi ndani<br />
John: Ninarudi ndani<br />
6. Warejeshe kwenye Kitabu cha mwanafuzi sura ya saba (7.1) somo la kutoa na kutii<br />
amri waongoze wachunguze picha kisha wajaze nafasi katika sentensi kwa kutumia<br />
154
maneno ya kutoa amri. Zoezi hili lifanywe kwa kutamka kisha kwa kuandika kwenye<br />
madaftari yao.<br />
7. Waongoze wanafunzi wafanye zoezi la marudio la kutoa na kutii amri lililopo vitabuni<br />
mwao katika sura ya saba.<br />
Tafakuri: Je? Umeyaonaje mazungumzo kati ya mwalinu na mwanafuzi wakati wa somo?<br />
Somo la 1: Matukio ya wakati uliopo<br />
SURA YA NANE<br />
TUSIMULIE MATUKIO<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kueleza matukio ya wakati uliopo<br />
Muda: Vipindi 11<br />
Zana: Picha ya mwanafunzi aliyevaa viatu na soksi anayetembea<br />
155
kwenye mvua akiwa na mwavuli na barabara zimejaa maji.<br />
Hatua;<br />
1. Wasimulie wanafunzi tukio fupi la wakati uliopo.<br />
2. Tumia onesho mbinu kuwaongoza wanafunzi kuelezea matukio yanayotokea hivi<br />
sasa. Kwa mfano:<br />
Mvua kubwa inanyesha. kuna upepo mkali, miti inayumba na matawi yanaanguka.<br />
Baadhi ya nyumba zimeezuliwa mabati na zingine zimeanguka.Mito imefurika na<br />
barabara zimejaa maji na hazipitiki.<br />
Zoezi<br />
3. Waongoze wanafunzi mmoja mmoja wasimulie matukio mengine yanayofanyika<br />
katika wakati uliopo kulingana na mazingira ya shule yenu. Wakati wa kusimulia<br />
matukio hayo wasahihishe matamshi yao na mtiririko wa matukio.<br />
4. Waongoze wanafunzi katika vikundi waigize na kueleza matukio mbalimbali<br />
yanayotokea wakati uliopo.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya nane (8.1) somo la matukio ya<br />
wakati uliopo kisha waongoze wasome hadithi kwa sauti mmoja mmoja. Kisha<br />
waongoze wafanye mzaoezi yafuatayo kutokana na habari waliyosoma:<br />
1. Nani ni dada mkuu wa shule ya Namabengo?<br />
2. Shule ya namabengo ipo katika wilaya gani?<br />
3. Wilaya ya Namtumbo ipo katika mkoa gani?<br />
4. Kuna umuhimu wa kuwa na uongozi mzuri shuleni?<br />
5. Yeremia anasoma darasa la saba?<br />
6. Kwanini shule ya Namabengo inajulikana katika ngazi zote?<br />
7. Walimu na wanafunzi wanajivunia nini?<br />
8. Yeremia na Fatuma wana vipaji gani?<br />
B: Jaza maneno yafuatayo katika nafasi zilizoachwa wazi.<br />
Kaka mkuu, sambamba, busara, vipaji, ufunguo, uongozi<br />
1. Yeremia na Fatuma walikuwa na …………..vya uongozi<br />
2. Elimu huweza kuwa ni…………..wa maisha<br />
3. Yeremia alikuwa……………katika shule ya Namabengo<br />
4. Elimu huenda …………….na maisha ya mtu<br />
5. Ukiwa na …………watu hukuthamini kwa lolote utakalosema<br />
156
C: Jibu kweli au si kweli<br />
1. Shule ya Namabengo ilikosa sifa ya uongozi.<br />
2. Fatuma alikuwa kaka mkuu katika shule ya Namabengo<br />
3. Katika maisha elimu haina nafasi.<br />
4. Sifa moja ya mwanafunzi ni kusoma kwa bidii.<br />
5. Usafi ni moja ya sifa za mwanafunzi shuleni.<br />
Tafakuri: Masimulizi haya mawili yaliyotolewa wakati wa somo yana faida gani kwako?<br />
Somo la 2: Matukio ya wakati uliopita<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kueleza matukio ya wakati uliopita<br />
Muda: Vipindi 10<br />
Zana: Mpira, kamba, aliyevaa viatu na soksi anayetembea<br />
kwenye mvua akiwa na mwavuli na barabara zimejaa maji.<br />
Hatua<br />
1. Wasimulie wanafunzi tukio fupi la wakati uliopita.<br />
2. Tumia hadithi fupi kuwaongoza wanafunzi kuelezea matukio yaliopita. Kwa mfano:<br />
Bibi anasimulia hadithi kwa mjukuu wake.<br />
Hapo zamani za kale Nyoka na Jongoo walikuwa marafiki. Nyoka alikuwa na miguu<br />
lakini hana macho. Siku moja Nyoka alimwambia Jongoo: Rafiki yangu, niazime<br />
macho yako niende harusini. Nikirudi nitakurudidhia. Jongoo akamjibu: Ooh rafiki<br />
nitakuazima macho yangu lakini na wewe niazime miguu yako nitembelea mpaka<br />
utakaporudisha macho yangu. Nyoka akafikiri na kusema ; Ahsante sana rafiki<br />
yangu. Wewe ni rafiki wa kweli.Wakabalishana viungo vyao na hadi sasa Nyoka<br />
hajarudisha macho ya Jongoo. Jongoo anamtafuta Nyoka hamwoni.<br />
3. Waongoze wanafunzi mmoja mmoja wasimulie matukio mengine yaliyofanyika katika<br />
wakati uliopita kulingana na mazingira ya nyumbani kwao. Wakati wa kusimulia matukio<br />
hayo wasahihishe matamshi yao na mtiririko wa matukio.<br />
4. Warejeshe wanafunzi katika kitabu chao sura ya nane (8.2) somo la matukio ya wakati<br />
uliopita kisha waongoze wasome hadithi kwa sauti mmoja mmoja. Kisha waongoze<br />
wafanye mzaoezi yanayotokana na hadithi hiyo.<br />
Tafakuri: Masimulizi ya hadithi zilizopo katika sura hii yanakusaidiaje?<br />
157
SURA YA TISA<br />
TUTAMBUE RANGI<br />
Somo la 1: Tuzijue rangi<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuzitambua rangi mbalimbali.<br />
Muda: Vipindi 8<br />
Zana: Picha au vitu halisi venye rangi mbalimbali. Kwa mfano nyanya, maua,<br />
nguo,ubao, papai, mkaa, karatasi na kadhalika.<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi kutaja rangi za vitu mbalimbali mmoja mmoja kwa sauti.<br />
2. Wapange wanafunzi katika makundi ya wanafunzi watano watano.<br />
3. Waoneshe picha au vitu halisi venye rangi mbalimbali. Kisha waongoze wanafunzi<br />
katika makundi wataje rangi za vitu hivyo.<br />
4. Watoe wanafunzi nje ya darasa. Kisha waongoze kila mmoja achukue kitu chenye<br />
rangi na kurudi darasani.<br />
5. Waongoze wanafunzi wazitaje rangi za vitu walivyochukua kisha wataje rangi ya vitu<br />
vingine vilivyo nje ya darasa.<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao sura ya tisa (9.1) somo la tuzijue rangi<br />
kisha waongoze wazichunguze picha na kujibu maswali yaliyo chini ya picha hizo.<br />
7. Waongoze wanafunzi wazisome hadithi ziliopo kwenye vitabu vyao. Kisha waongoze<br />
wajibu maswali yafuatayo:<br />
Maswali:<br />
158
Angalia picha hapo juu kisha:<br />
1. Taja rangi ya chungwa.<br />
2. Taja rangi ya ndizi.<br />
3. Taja rangi ya tairi la gari<br />
4. Taja rangi ya ukuta<br />
5. Je tairi ni la rangi ya kijani?<br />
6. Je ukuta ni wa rangi nyekundu?<br />
Katika picha ya hadithi ya Dandu:<br />
Onesha mtu aliyevaa nguo nyekundu<br />
Onesha mtu aliyevaa nguo ya manjano<br />
Onesha mtu aliyevaa nguo ya zambarau<br />
Onesha mtu aliyevaa nguo ya buluu<br />
Mazoezi<br />
A: Jibu maswali yafuatayo:<br />
1. Njiani kwa akina Dandu yalipambwa matawi ya miti ya rangi gani?<br />
2. Maua yalikuwa ni ya rangi gani?<br />
3. Marafiki wa Dandu walivaa nguo za rangi gani?<br />
B: Andika kweli au si kweli<br />
1. Damu ya mnyama ina rangi ya buluu<br />
2. Mzungu ana rangi nyeusi<br />
3. Mkaa una rangi nyeusi<br />
4. Viazi mviringo vina rangi ya kahawia<br />
5. Mkate una rangi nyeusi.<br />
Tafakuri: Waelekeze wanafunzi wataje rangi wanazozipenda<br />
Somo la 2: Tutumie rangi mbalimbali<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kuzitumia rangi mbalimbali.<br />
Muda: Vipindi 8<br />
159
Zana: Kalamu za rangi mbalimbali na picha za vitu visivyo na rangi kama: ndoo, embe, paka,<br />
mgomba, nyanya, chungwa, jani la mgomba.<br />
Hatua:<br />
1. Waoneshe wanafunzi picha anuwai za vitu mbalimbali ambavyo havikupakwa rangi.<br />
2. Waongoze wanafunzi wavitaja kwa sauti vitu hivyo visivyo na rangi.<br />
3. Wapange wanafunzi katika makundi ya wanafunzi watano watano. Kisha wagawie picha<br />
hizo wazipake rangi.<br />
4. Warejeshe kwenye vitabu vyao sura ya tisa (9.2) somo la Tutumie rangi. Kisha waongoze<br />
wanafunzi wachore picha zilizopo vitabuni mwao na kuzipaka rangi.<br />
5. Waongoze wanafunzi wafanye zoezi la kuchagua rangi zinazofaa kuchorea vitu<br />
vilivyoorodheshwa vitabuni mwao.<br />
Tafakuri: Upinde wa mvua una rangi gani?<br />
Somo la 1: Kusoma kwa ufahamu<br />
SURA YA KUMI<br />
UFAHAMU<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma kwa sauti habari fupi kwa kuzingatia vituo.<br />
Muda: Vipindi 12<br />
Zana: Chati ioneshayo vituo anuwai katika matini mbalimbali.<br />
160
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi wasome kwa sauti hadithi ya Nyoka na Jongoo iliopo kwenye<br />
vitabu vyao sura ya kumi somo la Ufahamu kwa kuzingatia vituo (,), (.), (?) na (!).<br />
Mwalimu, unaweza kutumia vifungu vingine vya habari.<br />
Mazoezi<br />
2. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao sura ya 10 somo la Kusoma kwa ufahamu<br />
wasome kwa sauti hadithi ya vipepeo kwa kuzingatia vituo (.), (,), (?) na (!). kwa<br />
matamshi sahihi na lafudhi ya Kiswahili.<br />
3. Waongoze wanafunzi wajibu maswali ya Nyoka na Jongoo kwa sauti mmoja mmoja.<br />
4. Warejeshe wanafunzi vitabuni mwao katika sura ya kumi. Waongoze wanafunzi<br />
wajibu maswali yatokanayo na hadithi ya vipepeo kwa kuandika madaftarini mwao<br />
A. Jibu maswali yafuatayo:<br />
1. Je, vipepeo ni wadudu au wanyama?<br />
2. Vipepeo wanaopatikana katika eneo<br />
lenu wana rangi gani?<br />
3. Vipepeo wana miguu mingapi?<br />
4. Chakula cha vipepeo ni…………<br />
5. Mikidadi alipewa siri gani?<br />
6. Je, mbinu hiyo ni ya ukweli?<br />
B. Chagua maneno yaliyo kwenye mabano kukamilisha<br />
sentensi zifuatazo:<br />
Kitenge, urembo, mabawa, porini, migomba<br />
1. Kuku ana………………….<br />
2. Chui anaishi……………….<br />
3. ……wa nguo ile unavutia sana.<br />
4. Kaka amevaa shati la ……………….<br />
5. ……imepandwa nyuma ya nyumba yetu<br />
C. Andika maneno haya kwa kujaza herufi zinazokosekana kwenye nafasi zilizoachwa<br />
wazi.<br />
D. Kwa mfano<br />
1. K-pepeo 2. M-no 3. Mku-wa<br />
4. Man-no 5. Ki-enge 6. U-embo<br />
7. N-uri 8. Kidol- 9. –kon<br />
Tafakuri: Kwa nini tunazingatia vituo wakati wa kusoma kwa sauti?<br />
161
Somo la 2: Kusoma kwa burudani<br />
Ujuzi: Kusoma kwa utambuzi na kuandika sentensi na habari fupi.<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kusoma kimya matini fupi na vitabu kwa ziada na kwa<br />
kujiburudisha.<br />
Muda: Vipindi 11<br />
Zana: Vijitabu vya hadithi fupi fupi vyenye picha.<br />
Hatua:<br />
1. Andaa na uwape wanafunzi matini sahili na vitabu mbalimbali vinavyovutia.<br />
2. Waongoze wanafunzi wasome kimya matini na vitabu hivyo.<br />
3. Waongoze wanafunzi wasimulie hadithi na picha zake. Wakati wanafunzi wakisimulia<br />
hadithi hizo uwasahihishe matamshi sahihi na lafudhi ya Kiswahili.<br />
4. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao kisha waongoze watazame picha na wasome<br />
hadithi. Waongoze wajibu maswali yafuatayo kutokana na hadithi waliyoisoma.<br />
Maswali<br />
a) Watu wangapi walikuwa shambani?<br />
b) Tumbili wanaishi wapi?<br />
c) Kwa nini baba alisema tumbili ni wakorofi?<br />
d) Kwa nini watu wananawa wakati wa kula?<br />
e) Taja kazi tatu za nyumbani<br />
Tafakuri: Kusoma hadithi mbalimbali kuna faida gani?<br />
162
Somo la Vitendawili<br />
SURA YA KUMI NA MOJA<br />
TUJIELEZA KWA LUGHA YA KIFASIHI<br />
Ujuzi: Kutega na kutegua vitendawili<br />
Lengo: Mwanafunzi aweze kutega na kutegua vitendawili.<br />
Zana: Picha na chati za vitendawili.<br />
Hatua:<br />
1. Waongoze wanafunzi watege na kutegua vitendawili wanavyovijua.<br />
2. Tega kitendawili hiki “ kuku wangu katagia mibani” kisha wanafunzi wakitegue kwa<br />
kujibu “Nanasi”Waulize wanafunzi: Kwanini jibu lake ni nanasi? Wanafunzi wajibu:<br />
Nanasi lipo katikati ya miiba. Kwa hiyo miiba inalilinda nanasi.<br />
3. Waongoze wanafunzi waeleze maana na ujumbe kwa kila jibu la kitendawli.<br />
4.<br />
5. Warejeshe wanafunzi katika vitabu vyao sura ya kumi na moja somo la vitendawili<br />
wafanye mazoezi ya kutegua vitendawili vilivyopo kwenye picha kwa sauti na kisha<br />
kuviandika madaftarini mwao.<br />
6. Warejeshe wanafunzi kwenye vitabu vyao. Waongoze wanafunzi wafanye mazoezi ya<br />
marudio yaliopo kwenye vitabu vyao sura ya kumi na moja kwa sauti na kwa kuandika.<br />
Tafakuri: Waongoze wanafunzi watafakari waliyojifunza katika somo hili kwa<br />
kuwauliza maswali. Kwa mfano,katika somo hili la kutega na kutegua vitendwili ni<br />
sehemu gani imekufurahisha zaidi? Kuna faida gani ya kujifunza kutega na<br />
163