24.10.2015 Views

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

86 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />

(vi)<br />

(vii)<br />

(viii)<br />

(ix)<br />

Kupanga bei: Kupanga bei ni utaratibu wa kupanga mapato yatakavyokuwa<br />

ili kufidia gharama zako zote na kupata faida unayotaka kutokana na kuuza<br />

bidhaa au huduma yako.<br />

‣ Unaweza ukapanga bei sawa na wengine.<br />

‣ Unaweza ukapunguza bei ya soko ili mzunguko wa mauzo uwe haraka<br />

mfano photocopy 1 shs 50 badala ya shs 100.<br />

‣ Unaweza ukapanga bei ya juu ya soko bali ukaboresha maeneo mengine<br />

(Eleza nini unaboresha)<br />

Kufunga bidhaa: Ni lazima kufunga bidhaa ili kuepuka uharibifu, kurahisisha<br />

ubebaji, uuzaji na kutangaza bidhaa.<br />

Kutangaza: Ili kuuza unalazimika kutangaza.<br />

‣ Kutangaza ni kuwafahamisha wateja juu ya bidhaa au huduma utowayo,<br />

uko wapi na wanaweza kukufikiaje.<br />

‣ Kutangaza ni kuwavutia wateja waje kwako badala ya kwenda kwa<br />

washindani wako kwa kuwaeleza “ kitu cha ziada ulichonacho”<br />

‣ Kutangaza ni kuwapatia wateja ujumbe muhimu ili wanunue kwako mfano<br />

kuwapa punguzo la bei, nyongeza na zawadi wanaponunua kwako.<br />

‣ Tangaza ubora wa bidhaa ,matumizi yake na faida zake kupitia<br />

magazeti,redio,TV, ubao wa matengenezo , mtandao, vipeperushi,<br />

ufadhili na michango n.k<br />

Kuwahudumia wateja:<br />

‣ Huduma kwa wateja ni vitendo vyote vizuri unavyoweza kumfanyanyia<br />

mteja ajisikie kuwa ni wa maana.<br />

‣ Huduma kwa wateja katika dunia hii ya utandawazi , ndivyo imebaki<br />

silaha pekee ya kutofautisha wewe na washindani wako .<br />

‣ Mjasiliamali sharti awatosheleze wateja wake, na iwapo mteja<br />

utamtosheleza atanunua tena na tena bidhaa zako na mteja huyo<br />

ataziba masikio kwa bidhaa za watu wengine.<br />

Kwa upande mwingine zifuatazo ni mbinu za kuwatunza wateja waliopo.<br />

<br />

<br />

<br />

Uwaminifu kwa wateja: Mjasiliamali anatakiwa kuwa mwaminifu na mkweli kwa<br />

wateja wake, mathalani kuwauzia vitu halisi na vipimo sahihi,mteja amesahau chenji<br />

yake , mjasiliamali amkumbushe juu ya jambo hilo kwa njia hii mjasiliamali ataweza<br />

kuwatunza wateja alionao.<br />

Lugha nzuri kwa wateja:<br />

‣ Mjasiliamali anatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wateja wake , jali wateja<br />

wako, acha kiburi cha pesa, onyesha kila wakati wewe ni mhitaji wa pesa ya<br />

mteja wako.<br />

‣ Kumbuka kuwa wateja ulinao ndiyo mabalozi wako kwa watu wengine<br />

hivyo basi kama mjasiriamali ukitoa lugha ya kejeli, dharau , matusi au jeuri<br />

kwa mteja itakua ni vigumu kuwatunza wateja wako.<br />

Jizuie hasira: Japokuwa wateja wanatabia tofauti onyesha utu kwa wateja wako

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!