You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
86 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
(vi)<br />
(vii)<br />
(viii)<br />
(ix)<br />
Kupanga bei: Kupanga bei ni utaratibu wa kupanga mapato yatakavyokuwa<br />
ili kufidia gharama zako zote na kupata faida unayotaka kutokana na kuuza<br />
bidhaa au huduma yako.<br />
‣ Unaweza ukapanga bei sawa na wengine.<br />
‣ Unaweza ukapunguza bei ya soko ili mzunguko wa mauzo uwe haraka<br />
mfano photocopy 1 shs 50 badala ya shs 100.<br />
‣ Unaweza ukapanga bei ya juu ya soko bali ukaboresha maeneo mengine<br />
(Eleza nini unaboresha)<br />
Kufunga bidhaa: Ni lazima kufunga bidhaa ili kuepuka uharibifu, kurahisisha<br />
ubebaji, uuzaji na kutangaza bidhaa.<br />
Kutangaza: Ili kuuza unalazimika kutangaza.<br />
‣ Kutangaza ni kuwafahamisha wateja juu ya bidhaa au huduma utowayo,<br />
uko wapi na wanaweza kukufikiaje.<br />
‣ Kutangaza ni kuwavutia wateja waje kwako badala ya kwenda kwa<br />
washindani wako kwa kuwaeleza “ kitu cha ziada ulichonacho”<br />
‣ Kutangaza ni kuwapatia wateja ujumbe muhimu ili wanunue kwako mfano<br />
kuwapa punguzo la bei, nyongeza na zawadi wanaponunua kwako.<br />
‣ Tangaza ubora wa bidhaa ,matumizi yake na faida zake kupitia<br />
magazeti,redio,TV, ubao wa matengenezo , mtandao, vipeperushi,<br />
ufadhili na michango n.k<br />
Kuwahudumia wateja:<br />
‣ Huduma kwa wateja ni vitendo vyote vizuri unavyoweza kumfanyanyia<br />
mteja ajisikie kuwa ni wa maana.<br />
‣ Huduma kwa wateja katika dunia hii ya utandawazi , ndivyo imebaki<br />
silaha pekee ya kutofautisha wewe na washindani wako .<br />
‣ Mjasiliamali sharti awatosheleze wateja wake, na iwapo mteja<br />
utamtosheleza atanunua tena na tena bidhaa zako na mteja huyo<br />
ataziba masikio kwa bidhaa za watu wengine.<br />
Kwa upande mwingine zifuatazo ni mbinu za kuwatunza wateja waliopo.<br />
<br />
<br />
<br />
Uwaminifu kwa wateja: Mjasiliamali anatakiwa kuwa mwaminifu na mkweli kwa<br />
wateja wake, mathalani kuwauzia vitu halisi na vipimo sahihi,mteja amesahau chenji<br />
yake , mjasiliamali amkumbushe juu ya jambo hilo kwa njia hii mjasiliamali ataweza<br />
kuwatunza wateja alionao.<br />
Lugha nzuri kwa wateja:<br />
‣ Mjasiliamali anatakiwa kuwa na lugha nzuri kwa wateja wake , jali wateja<br />
wako, acha kiburi cha pesa, onyesha kila wakati wewe ni mhitaji wa pesa ya<br />
mteja wako.<br />
‣ Kumbuka kuwa wateja ulinao ndiyo mabalozi wako kwa watu wengine<br />
hivyo basi kama mjasiriamali ukitoa lugha ya kejeli, dharau , matusi au jeuri<br />
kwa mteja itakua ni vigumu kuwatunza wateja wako.<br />
Jizuie hasira: Japokuwa wateja wanatabia tofauti onyesha utu kwa wateja wako