You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
84 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
‣ Ufugaji wa kibiashara.<br />
‣ Uvuvi<br />
‣ Mradi wa biashara.n.k<br />
16.6 MRADI WA BIASHARA<br />
16.6.1 Maana ya biashara<br />
Biashara ni mradi wa uzalishaji mali unaofanywa na mtu, kikundi, shirika au kampuni kwa<br />
lengo la kupata faida.<br />
16.6.2 Namna ya kuanzisha mradi wa biashara<br />
(i)<br />
Kunakili biashara zilizopo (copy and paste). Biashara nyingi zinaanzishwa kwa<br />
kunakili biashara zilizopo, mtu anangalia biashara wanayoifanya wengine na kujaribu<br />
kufanya hivyo hivyo.<br />
Dhana ya kuwa wengine wanatengeneza faida, kupata faida kutokana na biashara<br />
hii “kwa nini na mimi nisifanye hivyo” (utaratibu huu ni hatari hasa biashara ukiiweka<br />
palepale na ukinakili vibaya)<br />
(ii)<br />
(iii)<br />
Kujazilizia biashara zilizopo. Biashara zingine zinaanzishwa kwa kuainisha mahitaji<br />
yasiyojitosheleza na kuzijazilia.<br />
Kubuni bidhaa mpya na huduma mpya.<br />
‣ Biashara zingine zinaanzishwa kwa kubuni bidhaa mpya na huduma mpya.<br />
‣ Angalia uwezekano wa kuibua biashara mpya kwa kutafuta matatizo ya<br />
kiuchumi na kijamii.<br />
‣ Angalia nini mahitaji ya lazima.<br />
16.6.3 Mambo muhimu katika biashara.<br />
(a)<br />
(b)<br />
Mtaji: Mtaji ni jumla ya rasiliamali zinazohitajika katika uzalishaji wa mali kama vile<br />
fedha taslimu,nyumba, gari, zana mbalimbali, mali ghafi, shamba n.k.<br />
‣ Ni muhimu kujua aina ya mtaji ulionao kama unatosheleza mahitaji ya<br />
biashara unayotarajia kuanzisha.<br />
‣ Iwapo mahitaji hayatoshelezi ni muhimu kujua njia nyingine za kuongeza<br />
mtaji kama vile mkopo, msaada, uchangishaji, ruzuku, ubia na mwekezaji n.k.<br />
‣ Aina mbili za mtaji ni Mtaji Anzia na Mtaji Endeshea.<br />
Mahali pa biashara:<br />
‣ Mfanyabiashara yeyote sharti awe mahali sahihi pa kufanyia biashara<br />
(biashara sharti iwekwe mahali inapo uzika)<br />
‣ Mahali pa biashara panaweza kuathiri biashara kwa upande wa gharama za<br />
uendeshaji, upatikanaji wa wateja na mapato kwa ujumla.