Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
80 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
(iii)<br />
(iv)<br />
(v)<br />
(vi)<br />
(vii)<br />
(viii)<br />
(ix)<br />
Wajasiriamali wengi hawawezi kukopesheka kwa sababu hawana cha kumshawishi mtoa<br />
mkopo ili aone kama fedha yake itarudi kwa kukosa mpango biashara.<br />
Wajasiriamali wengi wameshindwa kujua gharama halisi za biashara yao kwa kukosa mpango<br />
wa biashara.<br />
Wajasiriamali wengi hawajui washindani wao na mbinu za washindani wao, hivyo kushindwa<br />
kuweka mkakati wa kukabiliana na washindani.<br />
Biashara nyingi hukwama kufikia matarajio ya mjasiriamali kwa kukosa kuzifahamu shughuli<br />
za masoko kwa undani.<br />
Upangaji wa bei unachangia kuua biashara nyingi ndogondogo kwa sababu kazi nyingi<br />
wanazozifanya wajasiriamali wanadhani hazina gharama kwa kuwa wanatekeleza wao. Na<br />
hivyo huendelea kupunguza uwezo wa biashara kidogo na hatiamaye hufa.<br />
Wajasiriamali wengi wasiokuwa na stadi za ujasiriamali na stadi za biashara huwa wanakimbilia<br />
sana kwa waganga wa kienyeji wakati biashara zao zinayumba bila kufanya tathimini ya kina.<br />
Biashara nyingi zinazoendeshwa na wajasiriamali wadogo zinakabiliwa na tatizo kubwa la<br />
kutokutunza kumbukumbu kwa usahihi kwa kutokujua umuhimu na faida zake. Biashara za<br />
namna hii mara nyingi haziwezi kujibu maswali kama vile kipindi hiki faida katika biashara ni<br />
shilingi ngapi. Ni marekebisho gani yanatakiwa kufanyika katika biashara ili kuongeza ufanisi<br />
na tija, mjasiriamali amejipangia mshahara kiasi gani, kiasi gani kimetumika kutoka kwenye<br />
biashara kwa matumizi binafsi.<br />
15.5 Namna ya kukabiliana na changamoto<br />
(i)<br />
(ii)<br />
Kuhamasisha wananchi wengi wapende kujifunza stadi za ujasiriamali na stadi za biashara<br />
kwani hazihitaji elimu ya juu.<br />
Kuimarisha utoaji mafunzo kwa wajasiriamali watarajiwa na wale ambao wameanza biashara<br />
zao hatua za mwanzo.<br />
15.6 Kuibuka kwa mjasiriamali<br />
Nini kinachomlazimisha mjasiriamali aibuke katika jamii?<br />
Utafiti uliofanyika umekuja na mitazamo mbalimbali ifuatayo juu ya kuibuka kwa wajasiriamali.<br />
15.6.1 Mtazamo wa mazingira (the environment school of thought).<br />
Kuwa mjasiriamali au kutokuwa mjasiriamali kunaweza kuathiriwa na mazingira unayoishi.<br />
15.6.2 Mtazamo wa mtaji ( Financial School of thought).<br />
Huwezi kuwa mjasiriamali kama hauna mtaji, mahali panapokuwa na taasisi za fedha zinazotoa