SACCOS_Traing_Guide
SACCOS_Traing_Guide SACCOS_Traing_Guide
78 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 15. ELIMU YA UJASIRIAMALI NA STADI ZA BIASHARA 15.1 Ujasiriamali katika sekta ya biashara (Entrepreneurship) Ujasiriamali ni kuanza na kuendesha na kumiliki biashara inayojitegemea. 15.2 Mjasiriamali ni nani? Mtu yeyote anayeamua kuchukua uamuzi hatarishi kwa kuwekeza mtaji katika kuanzisha mradi ili kuingiza kipato na kupata faida. 15.3 Sifa za mjasiriamali Mjasiriamali ana sifa kuu tatu:- ‣ Ni mwenye ufahamu. ‣ Ni mwenye stadi. ‣ Ni mwenye tabia za kijasiriamali. (i) Ni mwenye ufahamu Mjasiriamali lazima awe na ufahamu wa mambo yote yanayohusu kuanzisha na kuendesha miradi ya kuongeza kipato/biashara. Ufahamu wa kujua nini maana ya biashara, kujua kutathmini wazo la mradi, kutengeneza mchanganuo wa mradi na habari zote za masoko. (ii) Ni mwenye stadi Mjasiriamali lazima awe na ujuzi wa mradi anaoamua kuanzisha. (iii) Ni mwenye tabia za kiujasiriamali Ujasiriamali si tu kufanya biashara bali ni ile tabia unayoweza kuionyesha kwenye biashara yako. Mjasiriamali ana tabia zifuatazo:- (a) Ni mbunifu (Innovative) Mjasiriamali ni mbunifu katika biashara kwa kuweka kitu kipya, mambo mapya, taratibu mpya, mipango mipya, kuweka huduma tofauti na wenzake wenye biashara ileile. (b) Ni mwenye kuthubutu (Risk-taking) Kuthubutu kwa mjasiriamali kuna kuja kwa njia nyingi kama vile: ‣ Kufanya uamuzi wa kuwekeza.
Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 79 ‣ Kufanya uamuzi wa kuanzisha mradi au kufanya Biashara. Mjasiriamali huwa hajutii uamuzi na ushauri alioufanyia kazi pale anapoanguka kibiashara au kupata hasara, hukaa chini na kutafakari na kurekebisha makosa na kuendelea na biashara. (c) Ni mwepesi wa kuona fursa (Opportunistic). Mjasiriamali ni mwepesi wa kuona fursa na kuitumia, anazitafuta fursa, anaziendeleza, na anapata maendeleo. (d) Ni mwenye kuwa na malengo [achievement oriented] Mjasiriamali huweka malengo ya shughuli anazozifanya, huwa haridhiki, anajitahidi kupanua kila wakati biashara yake, anaiendeleza na kuikuza na baadaye malengo yake yanakuwa makubwa.Wafanyabiashara walioridhika siyo wajasiriamali. (e) Ni mwenye bidii (Hard working). Mjasiriamali ni mwenye bidii ya kufanya kazi na hakati tamaa kirahisi. (f) Anayejitegemea (Independent). Ni mwenye kushughulikia matatizo yake kwanza mwenyewe, anatafuta ni jinsi gani ya kujikwamua mwenyewe, anafikiria kwanza mwenyewe kabla ya kutafuta msaada. (g) Ni mwenye kujenga uhusiano (Networking). Mjasiriamali anajitahidi kufahamiana na watu wengine wengi, anapojenga uhusiano na watu mbalimbali inamsaidia kuondoa matatizo mengi ya kibiashara. (h) Ni mwenye kuona mbali (Future oriented). Mjasiriamali anaangalia mbali katika biashara. Hata akifa biashara yake inaendelea kuwepo. (i) Ni mwenye kutunza kumbukumbu. Mjasiriamali ni mtunzaji wa kumbukumbu zinazomsaidia kukumbuka, kuona kama anapata faida au hasara na inamsaidia kujua mambo muhimu yanayohusu biashara zake kwa ajili ya maboresho. 15.4 Changamoto zinazowakabili wajasiriamali (i) (ii) Miradi mingi ya kuongeza kipato inayoendeshwa haina sifa ya kujiendesha kwa faida. Wajasiriamali wengi hufanya biashara zao kwa kubahatisha bila kujua wanatarajia nini na kwa kipindi gani.
- Page 34 and 35: 28 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS ya
- Page 36 and 37: 30 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 6.
- Page 38 and 39: 32 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS au
- Page 40 and 41: 34 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 7.
- Page 42 and 43: 36 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 44 and 45: 38 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS fe
- Page 46 and 47: 40 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS [B
- Page 48 and 49: 42 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Ma
- Page 50 and 51: 44 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 8.
- Page 52 and 53: 46 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS wa
- Page 54 and 55: 48 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Ba
- Page 56 and 57: 50 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (i
- Page 58 and 59: 52 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 28
- Page 60 and 61: 54 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS M
- Page 62 and 63: 56 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS MZ
- Page 64 and 65: 58 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 9.
- Page 66 and 67: 60 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 9.
- Page 68 and 69: 62 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 10
- Page 70 and 71: 64 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS n.
- Page 72 and 73: 66 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 11
- Page 74 and 75: 68 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 12
- Page 76 and 77: 70 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 12
- Page 78 and 79: 72 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 2.
- Page 80 and 81: 74 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Fu
- Page 82 and 83: 76 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 14
- Page 86 and 87: 80 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (i
- Page 88 and 89: 82 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 16
- Page 90 and 91: 84 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 92 and 93: 86 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (v
- Page 94 and 95: 88 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Wa
- Page 96 and 97: 90 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 17
- Page 98: 92 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS TO
78 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
15. ELIMU YA UJASIRIAMALI NA STADI ZA BIASHARA<br />
15.1 Ujasiriamali katika sekta ya biashara (Entrepreneurship)<br />
Ujasiriamali ni kuanza na kuendesha na kumiliki biashara inayojitegemea.<br />
15.2 Mjasiriamali ni nani?<br />
Mtu yeyote anayeamua kuchukua uamuzi hatarishi kwa kuwekeza mtaji katika kuanzisha mradi ili<br />
kuingiza kipato na kupata faida.<br />
15.3 Sifa za mjasiriamali<br />
Mjasiriamali ana sifa kuu tatu:-<br />
‣ Ni mwenye ufahamu.<br />
‣ Ni mwenye stadi.<br />
‣ Ni mwenye tabia za kijasiriamali.<br />
(i)<br />
Ni mwenye ufahamu<br />
Mjasiriamali lazima awe na ufahamu wa mambo yote yanayohusu kuanzisha na kuendesha miradi ya<br />
kuongeza kipato/biashara. Ufahamu wa kujua nini maana ya biashara, kujua kutathmini wazo la mradi,<br />
kutengeneza mchanganuo wa mradi na habari zote za masoko.<br />
(ii)<br />
Ni mwenye stadi<br />
Mjasiriamali lazima awe na ujuzi wa mradi anaoamua kuanzisha.<br />
(iii)<br />
Ni mwenye tabia za kiujasiriamali<br />
Ujasiriamali si tu kufanya biashara bali ni ile tabia unayoweza kuionyesha kwenye biashara yako.<br />
Mjasiriamali ana tabia zifuatazo:-<br />
(a)<br />
Ni mbunifu (Innovative)<br />
Mjasiriamali ni mbunifu katika biashara kwa kuweka kitu kipya, mambo mapya, taratibu mpya,<br />
mipango mipya, kuweka huduma tofauti na wenzake wenye biashara ileile.<br />
(b)<br />
Ni mwenye kuthubutu (Risk-taking)<br />
Kuthubutu kwa mjasiriamali kuna kuja kwa njia nyingi kama vile:<br />
‣ Kufanya uamuzi wa kuwekeza.