24.10.2015 Views

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />

1<br />

1. CHAMA CHA USHIRIKA CHA AKIBA NA MIKOPO NA<br />

UMUHIMU WAKE KWA WANACHAMA NA JAMII<br />

Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo hujulikana kama <strong>SACCOS</strong> katika lugha ya Kiingereza. Kirefu<br />

cha <strong>SACCOS</strong> ni kama ifuatavyo:<br />

S A C C O S<br />

Savings And Credit Co-operative Society.<br />

1.1 Maana ya <strong>SACCOS</strong><br />

<strong>SACCOS</strong> ni Asasi ya fedha ya ushirika inayoundwa na watu waliojiunga pamoja kwa HIARI yao wenyewe<br />

ambao wamekubaliana kuweka fedha zao pamoja na kukopeshana kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi<br />

na kijamii. Wanachama wa <strong>SACCOS</strong> mara nyingi huwa na fungamano la pamoja. Fungamano hilo<br />

linaweza kuwa eneo wanaloishi, kuajiriwa na mwajiri mmoja, kuwa na ajira zinazofanana (kama vile<br />

walimu katika shule binafsi na serikali), kusali katika msikiti, kanisa na au dhehebu au dini moja n.k.<br />

1.2 Historia ya <strong>SACCOS</strong>.<br />

[i]<br />

[ii]<br />

[iii]<br />

[iv]<br />

[v]<br />

<strong>SACCOS</strong> zilianzia Ujerumani katika jimbo la Rhine River mwaka 1847 kutokana na tatizo la ukame<br />

ambapo Friedrick Reiffein Taylor alibadilisha duka la walaji ili kupata mtaji wa kununulia ng’ombe<br />

na kuwakopesha wakulima ambao walikuwa wanarejesha kwa awamu. Utaratibu huu hata sasa<br />

unatumika kwa kwa baadhi ya <strong>SACCOS</strong> kununua na kuwakopesha wanachama wake vifaa badala<br />

ya kuwakopesha fedha Taslimu.<br />

Mwaka 1883 <strong>SACCOS</strong> iliyojulikana kama benki ya watu “peoples bank” ilianzishwa na Mjerumani<br />

Schutze Deltizch. Mjerumani huyu alisisitiza sana katika <strong>SACCOS</strong> misingi ya kusaidiana na<br />

kujitosheleza na msingi mwingine ni kupendana katika shughuli za <strong>SACCOS</strong>. Wote hawa walihusika<br />

na watu wenye matatizo ya aina moja wale wa mjini na vijijini.<br />

Mwaka 1936 <strong>SACCOS</strong> ya kwanza ilianzishwa Tanzania na Watanzania wenye asili ya Kiasia. <strong>SACCOS</strong><br />

hiyo illitwa Ismailia <strong>SACCOS</strong> ilianzishwa Moshi mjini nab ado inaendelea kutoa huduma hadi leo.<br />

Katika Tanzania kabla ya uhuru, <strong>SACCOS</strong> zilienezwa na kanisa Katoliki [RC] na marehemu Kadinali<br />

Lauriana Rugambwa amabaye aliwateua watu watatu kujifunza uendeshaji wa <strong>SACCOS</strong> Kanada.<br />

Shughuli za kufunza wananchi zilianzia Mission ya Nyegezi baadae kuenea katika maeneo mengine.<br />

Bwana Joseph Mutayoba ambaye alikuwa momjowapo waliopata mafunzo alichaguliwa kuwa<br />

Mweneykiti wa Kwanza wa Muungano wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Tanganyika<br />

(SCULT)<br />

Baada ya uhuru mwaka 1961, kampeni ya uanzishwaji wa <strong>SACCOS</strong> ilizidi kuenezwa zaidi katika<br />

madhehebu ya RC ambapo watu waliweza kupelekwa nchini Kanada na Marekani kwa ajili ya<br />

kujifunza uendeshaji wa <strong>SACCOS</strong>.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!