You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
1<br />
1. CHAMA CHA USHIRIKA CHA AKIBA NA MIKOPO NA<br />
UMUHIMU WAKE KWA WANACHAMA NA JAMII<br />
Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo hujulikana kama <strong>SACCOS</strong> katika lugha ya Kiingereza. Kirefu<br />
cha <strong>SACCOS</strong> ni kama ifuatavyo:<br />
S A C C O S<br />
Savings And Credit Co-operative Society.<br />
1.1 Maana ya <strong>SACCOS</strong><br />
<strong>SACCOS</strong> ni Asasi ya fedha ya ushirika inayoundwa na watu waliojiunga pamoja kwa HIARI yao wenyewe<br />
ambao wamekubaliana kuweka fedha zao pamoja na kukopeshana kwa lengo la kujiendeleza kiuchumi<br />
na kijamii. Wanachama wa <strong>SACCOS</strong> mara nyingi huwa na fungamano la pamoja. Fungamano hilo<br />
linaweza kuwa eneo wanaloishi, kuajiriwa na mwajiri mmoja, kuwa na ajira zinazofanana (kama vile<br />
walimu katika shule binafsi na serikali), kusali katika msikiti, kanisa na au dhehebu au dini moja n.k.<br />
1.2 Historia ya <strong>SACCOS</strong>.<br />
[i]<br />
[ii]<br />
[iii]<br />
[iv]<br />
[v]<br />
<strong>SACCOS</strong> zilianzia Ujerumani katika jimbo la Rhine River mwaka 1847 kutokana na tatizo la ukame<br />
ambapo Friedrick Reiffein Taylor alibadilisha duka la walaji ili kupata mtaji wa kununulia ng’ombe<br />
na kuwakopesha wakulima ambao walikuwa wanarejesha kwa awamu. Utaratibu huu hata sasa<br />
unatumika kwa kwa baadhi ya <strong>SACCOS</strong> kununua na kuwakopesha wanachama wake vifaa badala<br />
ya kuwakopesha fedha Taslimu.<br />
Mwaka 1883 <strong>SACCOS</strong> iliyojulikana kama benki ya watu “peoples bank” ilianzishwa na Mjerumani<br />
Schutze Deltizch. Mjerumani huyu alisisitiza sana katika <strong>SACCOS</strong> misingi ya kusaidiana na<br />
kujitosheleza na msingi mwingine ni kupendana katika shughuli za <strong>SACCOS</strong>. Wote hawa walihusika<br />
na watu wenye matatizo ya aina moja wale wa mjini na vijijini.<br />
Mwaka 1936 <strong>SACCOS</strong> ya kwanza ilianzishwa Tanzania na Watanzania wenye asili ya Kiasia. <strong>SACCOS</strong><br />
hiyo illitwa Ismailia <strong>SACCOS</strong> ilianzishwa Moshi mjini nab ado inaendelea kutoa huduma hadi leo.<br />
Katika Tanzania kabla ya uhuru, <strong>SACCOS</strong> zilienezwa na kanisa Katoliki [RC] na marehemu Kadinali<br />
Lauriana Rugambwa amabaye aliwateua watu watatu kujifunza uendeshaji wa <strong>SACCOS</strong> Kanada.<br />
Shughuli za kufunza wananchi zilianzia Mission ya Nyegezi baadae kuenea katika maeneo mengine.<br />
Bwana Joseph Mutayoba ambaye alikuwa momjowapo waliopata mafunzo alichaguliwa kuwa<br />
Mweneykiti wa Kwanza wa Muungano wa Vyama vya Ushirika wa Akiba na Mikopo Tanganyika<br />
(SCULT)<br />
Baada ya uhuru mwaka 1961, kampeni ya uanzishwaji wa <strong>SACCOS</strong> ilizidi kuenezwa zaidi katika<br />
madhehebu ya RC ambapo watu waliweza kupelekwa nchini Kanada na Marekani kwa ajili ya<br />
kujifunza uendeshaji wa <strong>SACCOS</strong>.