24.10.2015 Views

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SACCOS_Traing_Guide

SHOW MORE
SHOW LESS

Create successful ePaper yourself

Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.

Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />

57<br />

(a)<br />

Maana ya Urari wa Hesabu.<br />

‣ Urari ni taarifa inayoonyesha masalio yote ya Hesabu za MPE na MTOE kila Akaunti<br />

iliyoko kwenye leja kuu kwa kipindi maalum.<br />

‣ Urari ni Orodha ya akaunti zote zilizo kwenye leja kuu pamoja na salio la kila akaunti<br />

katika safu mbili za MPE na MTOE hasa siku ya mwisho wa mwezi au mwisho wa<br />

mwaka.<br />

(b)<br />

Kuandaa Urari<br />

‣ Kuandaa urari kunahusu kuorodhesha akaunti zote zilizo kwenye leja kuu [isipokuwa<br />

zisizo na masalio] na kuandika masalio yake MPE na MTOE.<br />

‣ Masalio ya mpe yaingizwe katika safu ya mpe na masalio ya mtoe ya mtoe yaingizwe<br />

katika safu ya mtoe, na hatimaye jumla ya safu ya MPE ilingane na safu ya Mtoe.<br />

‣ Jumla ya mpe iwe sawa na Jumla ya mtoe.<br />

‣ Kwa kawaida salio anzia la fedha Taslimu na Salio anzia la Benki hupelekwa upande<br />

wa Mpe katika urari na salio ishia la fedha Taslimu na Benki hupelekwa upande wa<br />

mtoe katika Urari.<br />

(c)<br />

Kwa nini Urari wa hesabu hutengenezwa?<br />

‣ Urari wa hesabu hutengenezwa ili kuonesha usahihi wa maingizo vitabuni. Ili<br />

kuthibitisha kuwa kanuni ya uandishi wa miamala ni sahihi, Jumla ya akaunti zenye<br />

salio la MPE lazima ziwe sawa na Jumla ya akaunti zenye salio la MTOE.<br />

[JUMLA YA MPE = JUMLA YA MTOE]<br />

‣ Ikitokea kuwa Jumla ya MPE na MTOE hazilingani hii itakuwa imetokana na:<br />

(i) Kujumlisha vibaya.<br />

(ii)<br />

(iii)<br />

Kunakili salio tofauti na lililopo kwenye akaunti.<br />

kukosea wakati wa kuingiza kwenye leja kuu toka daftari la fedha na kitabu<br />

cha Jono.<br />

‣ Ili kuendelea na taarifa nyingine lazima Jumla hizo ziwe zimekubaliana. Hii inatokana<br />

na ukweli kuwa taarifa ya mapato na matumizi, mizania na taarifa ya mtiririko wa<br />

fedha zinatokana na Urari.<br />

(d)<br />

Matumizi ya Urari.<br />

‣ Kuthibitisha kwamba vitabu vya mahesabu ya fedha vimeandikwa kwa makini kwa<br />

kuzingatia kanuni za kihasibu hususani kanuni ya MPE na MTOE.<br />

‣ Urari hurahisisha uandaaji wa taarifa ya mapato na matumizi, taarifa ya mtiririko wa<br />

fedha na mizania.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!