SACCOS_Traing_Guide
SACCOS_Traing_Guide SACCOS_Traing_Guide
46 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS wa udhibiti wa hesabu za ushirika maana utaelezea kwa ufasaha mali zilizopo katika himaya ya ushirika, zimetokana na nini na zimefika vipi, katika chama na wenyewe ni akina nani na zinaangaliwa vipi. 8.4.3 USHIRIKIANO WA MPE NA MTOE (Kanuni za MPE na MTOE) Katika masuala ya miamala ya kifedha ni lazima pawepo matukio mawili:- ‣ Tukio la kutoa na lile la kupokea. ‣ Ni lazima awepo anayetoa na anayepokea. ‣ Ni lazima iwepo akaunti inayotoa na inayopokea. Matukio haya mawili ni pacha, moja likitokea na lingine linatendeka muda huohuo na kuwa hitimisho la tukio lililotangulia. Kutendeka kwa tukio la pili ni kuthibitisha kuwa tukio la kwanza limefika salama mahali panapostahili. MPE (+) VS MTOE (-) MPE- anayepokea VS MTOE- anayetoa MPE-Kinachoingia VS MTOE-kinachotoka MPE-Viingiavyo VS Mtoe-vitokavyo Ili kuhitimisha matendo ya mpe na mtoe ni lazima kila chama cha ushirika kiwe na akaunti za kuingiza miamala hii, akaunti hizi zitatunzwa ndani ya kitabu kinachoitwa Leja kuu. Kila akaunti ndani ya kitabu cha leja kuu ni lazima iwe na pande mbili yaani upande wa MPE na upande wa MTOE ili kuonyesha ni thamani gani imeingizwa au kutolewa kwenye akaunti hiyo. 8.5 KUANDAA TAARIFA SAHIHI NA KWA WAKATI UNAOSTAHILI Bodi inatakiwa kuhakikisha kwamba taarifa zote za mahesabu ya SACCOS ziko sahihi wakati wote. Taarifa sahihi zinaweza kupatikana endapo kama bodi:- a) Itaanzisha mfumo mzuri wa utawala na uhasibu. b) Kuajiri wafanyakazi wenye ujuzi na uzoefu katika uhasibu. c) Kuajiri meneja ambaye ataendesha na kusimamia shughuli za kila siku. d) Kuweka mazingira mazuri ya kufanya kazi kama vile kuwa na ofisi, ulinzi n.k. e) Kuwapatia wafanyakazi wake vitendea kazi bora kama vile vikokotozi, samani, kasiki, ofisi nzuri na imara.
Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 47 8.6 KUANDAA TAARIFA ZA KILA MWEZI Taarifa za kila mwezi zinatokana na taarifa sahihi za kila siku ambazo nazo hutokana na kukamilika kwa kazi za kila siku. Taarifa za kila siku ni pamoja na makusanyo ya kila siku, malipo ya kila siku na ulinganisho wa fedha taslimu kila siku n.k. Taarifa za kila mwezi ni lazima zipatikane kila mwisho wa mwezi ni lazima zipatikane kila mwisho wa mwezi ili ziweze kujadiliwa na kuona kama mipango ya SACCOS inaenda kama ilivyokusudiwa na kuangalia sehemu zinazohitaji marekebisho na ufuatiliaji. Taarifa za kila mwezi ni pamoja na:- ‣ Mapato na matumizi. ‣ Ulinganisho wa fedha taslimu. ‣ Ulinganisho wa fedha benki. ‣ Taarifa za mikopo (kiasi kilichotolewa, kilichorejeshwa, kiasi ambacho hakijarejeshwa na orodha ya wadaiwa na kiasi wanachodaiwa). Taarifa hizi ni muhimu sana na bodi inatakiwa kuwa nazo na zinapokosekana ni wajibu wa bodi kupata sababu za kukosekana na hali hiyo lazima irekebishwe mapema ili ziweze kupatikana na kutumika. Kama ni uzembe basi aliyepewa jukumu la kutayarisha achukuliwe hatua zinazostahili na bodi. 8.7 UPATIKANAJI WA TAARIFA ZA MWAKA Uwezo wa kusimamia shughuli za SACCOS umekasimiwa na wanachama kwenye bodi, kwa hiyo ni wajibu wa bodi kuhakikisha kwamba taarifa za fedha, kisheria zinapatikana kwa wakati unaostahiki na kuwasilishwa kwenye vyombo husika kama vile wakaguzi wa hesabu ili wazikague na kuthibitisha kama ni sahihi. Taarifa hizi ni:- ‣ Taarifa ya bodi (inayohusu shughuli zilizofanyika kipindi husika). ‣ Mizania. ‣ Taarifa ya mapato na matumizi. ‣ Mtiririko wa fedha. Endapo bodi itashindwa kuandaa taarifa hizi katika kipindi cha miezi mitatu baada ya kumalizika kwa mwaka wa fedha husika, kila mjumbe wa bodi kwa kipindi hicho atavuliwa madaraka ya ujumbe na hataruhusiwa kuchaguliwa kwenye ujumbe mpaka ipite miaka sita na kama hakutakuwa na hasara iliyotokana na uongozi wao watatozwa adhabu ya kila mmoja Sh. 100,000 na kuchukuliwa hatua ya kufidia hasara waliyosababisha. 8.8 WATUMIAJI WA TAARIFA ZA SACCOS Mwisho wa mzunguko wa uhasibu ni kuandaa taarifa mbalimbali kwa walengwa kwa wakati mwafaka ili waweze kufanya uamuzi sahihi wanapotakiwa.
- Page 1: Mradi wa Kukuza Uchumi, Kuleta Maen
- Page 4 and 5: ii Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS MW
- Page 6 and 7: iv Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 8 and 9: 2 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 1.3
- Page 10 and 11: 4 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS ata
- Page 12 and 13: 6 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (xi
- Page 14 and 15: 8 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS {I}
- Page 16 and 17: 10 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Ai
- Page 18 and 19: 12 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS hu
- Page 20 and 21: 14 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 3.
- Page 22 and 23: 16 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS NA
- Page 24 and 25: 18 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 26 and 27: 20 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS [i
- Page 28 and 29: 22 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 4.
- Page 30 and 31: 24 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (e
- Page 32 and 33: 26 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 34 and 35: 28 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS ya
- Page 36 and 37: 30 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 6.
- Page 38 and 39: 32 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS au
- Page 40 and 41: 34 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 7.
- Page 42 and 43: 36 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 44 and 45: 38 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS fe
- Page 46 and 47: 40 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS [B
- Page 48 and 49: 42 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Ma
- Page 50 and 51: 44 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 8.
- Page 54 and 55: 48 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Ba
- Page 56 and 57: 50 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (i
- Page 58 and 59: 52 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 28
- Page 60 and 61: 54 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS M
- Page 62 and 63: 56 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS MZ
- Page 64 and 65: 58 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 9.
- Page 66 and 67: 60 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 9.
- Page 68 and 69: 62 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 10
- Page 70 and 71: 64 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS n.
- Page 72 and 73: 66 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 11
- Page 74 and 75: 68 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 12
- Page 76 and 77: 70 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 12
- Page 78 and 79: 72 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 2.
- Page 80 and 81: 74 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Fu
- Page 82 and 83: 76 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 14
- Page 84 and 85: 78 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 15
- Page 86 and 87: 80 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (i
- Page 88 and 89: 82 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 16
- Page 90 and 91: 84 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS
- Page 92 and 93: 86 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS (v
- Page 94 and 95: 88 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS Wa
- Page 96 and 97: 90 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS 17
- Page 98: 92 Mwongozo wa Mafunzo ya SACCOS TO
Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
47<br />
8.6 KUANDAA TAARIFA ZA KILA MWEZI<br />
Taarifa za kila mwezi zinatokana na taarifa sahihi za kila siku ambazo nazo hutokana na kukamilika<br />
kwa kazi za kila siku. Taarifa za kila siku ni pamoja na makusanyo ya kila siku, malipo ya kila siku na<br />
ulinganisho wa fedha taslimu kila siku n.k.<br />
Taarifa za kila mwezi ni lazima zipatikane kila mwisho wa mwezi ni lazima zipatikane kila mwisho wa<br />
mwezi ili ziweze kujadiliwa na kuona kama mipango ya <strong>SACCOS</strong> inaenda kama ilivyokusudiwa na<br />
kuangalia sehemu zinazohitaji marekebisho na ufuatiliaji. Taarifa za kila mwezi ni pamoja na:-<br />
‣ Mapato na matumizi.<br />
‣ Ulinganisho wa fedha taslimu.<br />
‣ Ulinganisho wa fedha benki.<br />
‣ Taarifa za mikopo (kiasi kilichotolewa, kilichorejeshwa, kiasi ambacho hakijarejeshwa na<br />
orodha ya wadaiwa na kiasi wanachodaiwa). Taarifa hizi ni muhimu sana na bodi inatakiwa<br />
kuwa nazo na zinapokosekana ni wajibu wa bodi kupata sababu za kukosekana na hali<br />
hiyo lazima irekebishwe mapema ili ziweze kupatikana na kutumika. Kama ni uzembe basi<br />
aliyepewa jukumu la kutayarisha achukuliwe hatua zinazostahili na bodi.<br />
8.7 UPATIKANAJI WA TAARIFA ZA MWAKA<br />
Uwezo wa kusimamia shughuli za <strong>SACCOS</strong> umekasimiwa na wanachama kwenye bodi, kwa hiyo ni<br />
wajibu wa bodi kuhakikisha kwamba taarifa za fedha, kisheria zinapatikana kwa wakati unaostahiki<br />
na kuwasilishwa kwenye vyombo husika kama vile wakaguzi wa hesabu ili wazikague na kuthibitisha<br />
kama ni sahihi. Taarifa hizi ni:-<br />
‣ Taarifa ya bodi (inayohusu shughuli zilizofanyika kipindi husika).<br />
‣ Mizania.<br />
‣ Taarifa ya mapato na matumizi.<br />
‣ Mtiririko wa fedha.<br />
Endapo bodi itashindwa kuandaa taarifa hizi katika kipindi cha miezi mitatu baada ya kumalizika kwa<br />
mwaka wa fedha husika, kila mjumbe wa bodi kwa kipindi hicho atavuliwa madaraka ya ujumbe na<br />
hataruhusiwa kuchaguliwa kwenye ujumbe mpaka ipite miaka sita na kama hakutakuwa na hasara<br />
iliyotokana na uongozi wao watatozwa adhabu ya kila mmoja Sh. 100,000 na kuchukuliwa hatua ya<br />
kufidia hasara waliyosababisha.<br />
8.8 WATUMIAJI WA TAARIFA ZA <strong>SACCOS</strong><br />
Mwisho wa mzunguko wa uhasibu ni kuandaa taarifa mbalimbali kwa walengwa kwa wakati mwafaka<br />
ili waweze kufanya uamuzi sahihi wanapotakiwa.