You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
39<br />
sana ukubwa wa mtaji wa chama husika, mtaji ukiwa mdogo, inafaa Kamati ya<br />
Usimamizi iendelee kufanya kazi za Mkaguzi wa Ndani kwa kuwa mojawapo ya<br />
majukumu yao ni kulinda mali za <strong>SACCOS</strong> na maslahi ya wanachama. Vinginevyo<br />
<strong>SACCOS</strong> inaweza kujiunga na Mtandao kama upo ambao utakuwa unatoa huduma<br />
hiyo kwa gharama nafuu zitakazochangiwa na kila Mwanachama kulingana na<br />
huduma iliyotolewa.<br />
(vii)<br />
Kuwa na Ushirikiano Mzuri na Kamati ya Usimamizi:<br />
Kila Chama cha Ushirika cha Akiba na Mikopo kitakuwa na kamati ya usimamizi kusimamia<br />
shughuli za kifedha katika chama. Kamati hii itaundwa na wajumbe watatu waliochaguliwa<br />
na wanachama katika Mkutano Mkuu, wajumbe hawa hawatakuwa wajumbe wa Bodi au<br />
wajumbe wa Kamati ya Mikopo.<br />
Wajumbe wa Kamati ya kamati ya usimamizi wanawajibika na kuwajibishwa na Mkutano<br />
Mkuu wa <strong>SACCOS</strong>. Wajumbe wa Kamati hii ni wawakilishi wa wanachama na moja ya kazi za<br />
kamati ya usimamizi ni kuwa Mkaguzi na mshauri wa <strong>SACCOS</strong>.<br />
<br />
<br />
(viii)<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
(ix)<br />
<br />
<br />
Kamati ya usimamizi iwe inaamuru Mikopo kusimamishwa mara tu pale mikopo<br />
inayotarajiwa kurejeshwa inazidi 5% ya jumla ya mikopo inayotarajiwa kurejeshwa.<br />
Kila mwisho wa miezi mitatu, orodha ya Mikopo yote isiyorejeshwa itatolewa. Kamati<br />
ya usimamizi itaamuru kusimamishwa utoaji wa mikopo endapo orodha hiyo<br />
haitolewi na kupatikana kwa wanachama mnamo wiki ya kwanza baada ya mwezi<br />
husika kumalizika.<br />
Kuimarisha Udhibiti wa Ndani wa Mfumo wa Uhasibu:<br />
Fedha zote zinazopokewa na Karani/Mhasibu ni lazima zikatiwe stakabadhi ya fedha<br />
baada ya mhusika kujaza fomu ya kuweka fedha.<br />
Malipo yote yatalipwa na Mhasibu baada ya mhusika kujaza fomu ya kuchukua fedha<br />
na malipo hayo kuidhinishwa.<br />
Hati zote zitakazohusika kulipia fedha zitatakiwa kuwa na saini ya Mlipaji, Mlipwaji na<br />
Mwidhinishaji.<br />
Kiwango cha Mikopo inayotolewa na <strong>SACCOS</strong> wakati wowote, hakiwezi kuzidi<br />
kiwango ambacho kinalingana na robo tatu ya Mtaji wa Msingi na Akiba au Amana za<br />
<strong>SACCOS</strong>.<br />
Kuhakikisha Taarifa za Fedha na Utawala Zinatayarishwa kwa Wakati<br />
Unaostahili na Kuwasilishwa Zinakohitajika:<br />
Taarifa sharti itayarishwe kwa kuzingatia muda la sivyo itapoteza thamani yake kwa<br />
watumiaji. Taarifa inayotolewa baada ya kipindi chake kupita haina maana kabisa.<br />
Bodi ya Chama cha Akiba na Mikopo itaandaa taarifa za hesabu ikiwemo mizania ya<br />
mwaka, taarifa ya mapato na Matumizi ya Mwaka ilivyokuwa tarehe ya mwisho ya<br />
mwaka wa fedha uliopita na kuiwasilisha kunakohusika .