Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
36 Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
‣ Hatua za kufuata wakati wa kuandaa Bajeti<br />
[a]<br />
[b]<br />
[c]<br />
Panga muda wa kuanza kuandaa bajeti kabla ya kuanza mwaka mpya wa fedha.<br />
Hakikisha kwamba shughuli zilizoainishwa kwenye mpango mkakati za kutekelezwa<br />
mwaka wa fedha unaofuata zinaingizwa katika mpango wa mwaka.<br />
Bajeti ya <strong>SACCOS</strong> iandaliwe kwa kuzingatia mpango kazi.<br />
‣ Uandaaji wa bajeti<br />
[i]<br />
Andaa makadirio ya mapato na matumizi.<br />
Makadirio ya mapato yanayokusudiwa kukusanywa na makadirio ya matumizi ya asasi kwa<br />
kipindi husika cha mwaka wa fedha. Baada ya kuandaa mchanganuo wa mapato na matumizi,<br />
andaa muhtasari wa bajeti ulio na muundo ufuatao:<br />
[i]<br />
[ii]<br />
Kifungu [code], jina la akaunti, makisio ya mwaka uliopita, hali halisi ya mwaka uliopita<br />
na makisio ya mwaka huu. Kumbuka kifungu cha 4000 – 4999 ni Mapato.<br />
Kifungu cha 5000 – 5999 ni matumizi.<br />
Andaa makadirio ya bajeti ya maendeleo.<br />
Matumizi ya maendeleo ni makadirio yanayohusika na matumizi kwenye kifungu cha matumizi<br />
kinachohusisha zaidi ya mwaka mmoja au ununuzi wa mali za kudumu za chama.<br />
Bajeti hii itaonyesha shughuli inayokusudiwa kufanywa, gharama, na orodha ya vyanzo vya<br />
fedha na msimamizi wa shughuli, muda ambao shughuli itaanza na kumalizika.<br />
7.3.2 Kuimarisha Udhibiti wa Ndani wa Mfumo wa Uhasibu:<br />
Udhibiti wa ndani ni mfumo mzima unaohusu vipengele viwili vinavyohusiana ambavyo ni<br />
udhibiti wa Mazingira ya kazi na taratibu za kudhibiti kazi za chama cha Ushirika ukiwemo ule<br />
wa kifedha na ule wa kiutawala uliowekwa na Uongozi wa <strong>SACCOS</strong>.<br />
[A]<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
Maeneo muhimu ya kutiliwa maanani na Bodi za <strong>SACCOS</strong> katika udhibiti wa<br />
ndani ni kama ifuatavyo:-<br />
Kuweka kanuni na sera za Uhasibu na hili si jambo la Hiari.<br />
Kuweka utaratibu wa kuidhinisha na kuruhusu Miamala.<br />
Kuweka mgawanyo wa kazi kwa Watendaji.<br />
Kulinganisha Miamala ya <strong>SACCOS</strong> mara kwa mara.<br />
Kuhakikisha taarifa za fedha na utawala zinatayarishwa kwa wakati unaostahili na<br />
kuwasilishwa zinakohitajika.<br />
Kuimarisha udhibiti wa ndani wa mfumo wa uhasibu.<br />
Kuweka kiwango cha fedha cha kubaki katika Kasiki/Mkononi.<br />
Kuwa na Ukaguzi wa ndani.<br />
Kuweka Ushirikiano mzuri na Kamati ya usimamizi.