You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
Mwongozo wa Mafunzo ya <strong>SACCOS</strong><br />
9<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
<br />
[d]<br />
Inasaidia katika kujenga na kukuza mtaji wa ndani wa <strong>SACCOS</strong>. Suala la uwekaji akiba ya fedha<br />
mara kwa mara ni la msingi sana katika kujenga mtaji wa ndani wa kukopeshana.<br />
Inawezesha <strong>SACCOS</strong> kuwa na chanzo nafuu cha fedha za kuwakopesha wanachama. Akiba ni<br />
chanzo cha uhakika cha fedha na gharama yake ni ndogo ukilinganisha na vyanzo vingine.<br />
Wawekaji akiba hupata faida ya akiba au amana walizoziweka.<br />
Inawapatia wanachama fursa ya kupata mitaji ya kutekeleza miradi yao binafsi kwa njia ya<br />
mikopo huku akiba zao zinaendelea kuwepo.<br />
Ili chama kiweze kukopesheka zaidi, kinahitaji kuwa na akiba zaidi.<br />
Akiba huimarisha nafasi ya <strong>SACCOS</strong> kifedha na kuondoa utegemezi wa fedha za mkopo<br />
toka nje. Akiba hukiwezesha chama kisiwe tegemezi na wanachama wanafaidika na chama<br />
kinapokuwa na nguvu ya mtaji.<br />
Kutowekwa akiba mara kwa mara matokeo yake uwezo wa chama kutoa mikopo kupungua<br />
na kuongezeka foleni ya maombi ya mikopo.<br />
Uwekaji wa akiba huijengea <strong>SACCOS</strong> mazingira mazuri ya kutoa huduma zake kwa wanachama<br />
na hivyo kuhimili ushindani kutoka asasi nyingine za fedha.<br />
Mambo ya kuwavutia wanachama kuweka akiba<br />
Katika kuhakikisha <strong>SACCOS</strong> inawapa wanachama wake na jamii mvuto na ushawishi wa kuweka akiba<br />
katika <strong>SACCOS</strong> inayohusika, yafuatayo ni baadhi ya mambo yanayopaswa kuzingatiwa:<br />
(i)<br />
(ii)<br />
<strong>SACCOS</strong> kuwa na sera ya uwekaji akiba na amana.<br />
‣ Uwepo wa sera inayoelezea bidhaa za <strong>SACCOS</strong> zinazotolewa na utaratibu wa kuzipata<br />
bidhaa hizo unawarahisishia wanachama kuzifahamu bidhaa hizo na kupata muda<br />
wa kupangilia namna ya kuzitumia.<br />
‣ Uwekwe utaratibu wa uwekaji akiba mara kwa mara na usimamiwe.<br />
Kuwepo na viashiria vya kutosha vya usalama wa fedha.<br />
Watu wengi wanapenda kuweka fedha zao mahali penye usalama wa kutosha, mahali ambapo fedha<br />
zinatunzwa vizuri na zinapatikana wakati watakapozihitaji. Viashiria vya usalama wa kutosha ni pamoja<br />
na:-<br />
‣ Ofisi nzuri na madhubuti ya chama yenye vifaa vya ulinzi kama vile nondo katika<br />
milango na madirisha.<br />
‣ Kuwepo kwa walinzi wenye Silaha.<br />
‣ Kuwepo kwa uongozi unaozingatia sheria na taratibu za chama.<br />
‣ Kuwepo kwa watendaji wenye upeo katika masuala ya fedha na mwonekano<br />
maridadi.<br />
‣ Kuwepo kwa ukaguzi na usimamizi maalumu wa shughuli za chama.<br />
‣ Matengo yote ya kisheria ya chama na sehemu za Akiba zihifadhiwe Benki.<br />
(iii)<br />
Kuwepo na urahisi wa kuweka na kuchukua fedha.<br />
Watu wengi hupenda kuweka fedha mahali ambapo ni karibu na maeneo yao, mahali panapofikika<br />
kirahisi pasipo kutumia gharama kubwa za usafiri au muda mwingi.