You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
<strong>Je</strong>, <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>?<br />
Kuhesabu na Kusoma katika Afrika Mashariki<br />
Juni 2011
<strong>Je</strong>, <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>?<br />
Kuhesabu na Kusoma katika Afrika Mashariki
Uwezo ni juhudi katika Afrika Mashariki inayofanya kazi yake kupitia TEN/MET<br />
nchini Tanzania; WERK nchini Kenya na UNNGOF nchini Uganda, na hupata msaada<br />
wa kudhibiti ubora na usimamizi kutoka Twaweza/Hivos. Ripoti hii imeandaliwa<br />
na kitengo cha Uwazi kilichopo Twaweza. Waandishi wakuu ni Hans Hoogeveen na<br />
Dorica Andrew. Shukrani nyingi kwa Fenohasina Mareth kwa msaada wake katika<br />
kutayarisha seti za data na kutengeneza seti ya kwanza ya majedwali na michoro.<br />
Sara Ruto na Rakesh Rajani walitoa ushauri wa jumla na kusimamia ubora. Uhariri<br />
ulifanywa na Stephanie McDonald na Maggie Bangser.<br />
Data zote zilizotumiwa katika ripoti hii zimetolewa na Uwezo na zinapatikana kutoka<br />
www.uwezo.net.<br />
Picha kwenye ukurasa wa nje: Hisani ya Uwezo<br />
Uwezo Uwezo Afrika East Africa Mashariki (managed (ikisimamiwa by Twaweza) na Twaweza)<br />
S.L.P. P.O Box 19875, 19875, 00200 00200 Nairobi, Nairobi, Kenya Kenya<br />
Simu: Tel: +254 20 3861372<br />
Baruapepe: Email: info@uwezo.net. Web: Tovuti: www.uwezo.net<br />
Twaweza Afrika East Africa Mashariki<br />
127 Mtaa Mafinga wa Mafinga, Rd, Off Kando Kinondoni ya barabara Rd ya Kinondoni<br />
S.L.P. P.O Box 38342, 38342, Dar es Dar Salaam, es Salaam, Tanzania. Tanzania<br />
Simu: Tel: +255 22 266 4301. Nukushi: Fax +255 +255 22 266 22 266 43084308.<br />
Barua Email: pepe: info@twaweza.org. Web: Tovuti: www.twaweza.org<br />
Barua Email: pepe: info@uwazi.org. Web: Tovuti: www.uwazi.org<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>?<br />
ii
Dibaji<br />
Kazi hii inatupatia matokeo yaliyotafitiwa vema kuhusu mafanikio ya mfumo wa elimu hususan katika kusoma na kuhesabu.<br />
Uwezo na Twaweza zimeonesha umadhubuti mkubwa na viwango vya juu vya ubora katika kukusanya, kuchambua na<br />
kufasiri takwimu za msingi katika elimu na uwezo wa jumla wa watoto katika kusoma na kuhesabu. Matokeo ya msingi<br />
yanaonesha ukubwa wa changamoto iliyo mbele yetu sote, na hasa kama ukanda wa Afrika Mashariki unahitaji kuongeza<br />
kasi ya maendeleo kuendana na ulimwengu wa sasa ambao umejengwa katika maarifa na ushindani mkali.<br />
Katika ngazi ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki (EAC), ushirikiano katika maendeleo ya rasilimali watu, sayansi na teknolojia<br />
ni moja ya mihimili muhimu katika kufikia malengo ya Jumuiya. Kifungu cha 102 cha Mkataba wa Kuanzishwa kwa<br />
Jumuiya ya Afrika Mashariki kinaeleza bayana jinsi Nchi Wanachama walivyokubali kuchukua hatua madhubuti za pamoja<br />
kuendeleza ushirikiano katika elimu na mafunzo ndani ya Jumuiya. Ili kuchukua hatua hizo katika ngazi za kanda na nchi,<br />
taarifa nyingi zinahitajika ili kuandaa na kutekeleza sera na mikakati inayofaa.<br />
Kwa hiyo, umuhimu wa taarifa zilizokusanywa katika taftishi hii kuhusiana na kusoma na kuhesabu katika nchi tatu za<br />
Afrika Mashariki utasaidia sana Nchi Wanachama katika juhudi zao za kuwa na mfumo wa elimu ulioandaliwa vema na<br />
kurandanishwa; hasa katika kurandanisha mitaala, mitihani, utoaji vyeti na uthibitishaji wa kitaaluma wa taasisi za elimu<br />
na mafunzo. Miongoni mwa vipengele muhimu katika ripoti hii ni jinsi inavyoshughulikia suala la jinsia, ukuzaji mitaala,<br />
kuhusika kwa sekta binafsi na viwango vya uhamasishaji kuelekea ngazi inayofuata. Maeneo yote haya ni muhimu kwa<br />
Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ambazo zimejikita katika kutekeleza sera muhimu za elimu na mafunzo<br />
ya msingi, zaidi sana sera ya elimu kwa wote ambayo inahitaji taarifa za kina kuwasaidia watoa maamuzi kufanya uamuzi<br />
makini wakijua bayana nini wanachokifanya.<br />
Ripoti hii inachambua zaidi uhusiano kati ya kipato cha kaya na vigezo vya elimu kama vile mafanikio, uwezekano wa<br />
kuacha masomo, uandikishaji kwa kutazama jinsia, umri n.k. Kwa miongo mingi tumetumia viwango vya uandikishaji<br />
watoto shuleni kama vigezo muhimu vya maendeleo ya elimu. Ripoti ya Uwezo inaonesha kwamba uandikishaji pekee<br />
hautoshi kwa sababu watoto walio shuleni bado hawawezi kusoma na kuhesabu, ambazo ni stadi za msingi katika kujifunza<br />
na kuendelea (kukua kimaarifa). Hata hivyo, matokeo ya ripoti hii yatakuwa muhimu katika mchakato unaoendelea<br />
wa kurandanisha sera za elimu na mafunzo katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kwa mfano, baada ya kudhibitishwa na<br />
kupimwa ufaaji wake, taarifa zilizokusanywa katika taftishi zinaweza kutumiwa katika kufanya mapitio ya sheria na kufanya<br />
marekebisho yanayostahili katika ngazi ya kanda na kitaifa.<br />
Ni matarajio yangu kwamba kazi hii inayostahili pongezi itatumiwa kwa mapana na marefu na pande zinazohusika na<br />
kwamba Uwezo na Twaweza kama taasisi zitaendelea kujibainisha kama wanaharakati muhimu katika eneo hili. Jambo<br />
hili pia linahusisha changamoto ya kuhakikisha ubora wa matokeo. Wakati kuongeza idadi ya watoto walio mashuleni ni<br />
muhimu, kipengele cha muhimu zaidi cha kupima mafanikio ni kuthibitisha kama watoto wanaokwenda shule kwa hakika<br />
wanajifunza au la. Hili ni eneo lingine ambalo linastahili kuchunguzwa na Uwezo na Twaweza. Vilevile, ni matumaini yangu<br />
kwamba utafiti kama huu utakaofuata utahusisha Nchi Wanachama tano za Jumuiya ya Afrika Mashariki.<br />
Dkt Richard Sezibera<br />
Katibu Mkuu<br />
Jumuiya ya Afrika Mashariki<br />
Juni 2011<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki<br />
iii
1. Utangulizi<br />
Ni wachache wanaohoji umuhimu wa kujifunza, kama haki ya msingi na umuhimu wake katika kuandaa vizazi vijavyo<br />
kwa kuwajengea uwezo wa kuishi maisha yenye ustawi. Serikali za Tanzania, Uganda na Kenya zinaunga mkono<br />
mtazamo huu. Nchi zote tatu zinatekeleza sera ya Elimu ya Msingi bure kwa matarajio kwamba itawezesha watoto<br />
kupata elimu, ili walau wawe raia wenye uwezo wa kuhesabu na kusoma. Ili kufanikisha lengo hili kiasi kikubwa cha<br />
fedha kimewekezwa na kinaendelea kuwekezwa katika elimu ya msingi. Mathalan, katika mwaka 2009/10, Serikali<br />
ya Tanzania ilitenga asilimia 14 ya bajeti yake (sawa na asilimia 4 ya Pato la Taifa) kwa ajili ya elimu ya msingi pekee 1 .<br />
Kenya na Uganda nazo zinatumia kiasi kikubwa cha fedha, na katika muongo uliopita takwimu zinaonesha kwamba<br />
bajeti ya elimu imeongezeka kwa kiwango kikubwa katika nchi hizi.<br />
Katika nchi hizi kufutwa kwa ada ya elimu ya msingi kulifuatiwa na ongezeko kubwa la idadi ya watoto wanaokwenda<br />
shule. Ukweli huu unaoneshwa na wiano za idadi ya uandikishaji watoto katika shule kama inavyoonekana katika<br />
Kielelezo cha 1 (uwiano wa jumla wa uandikishaji ni jumla ya idadi ya watoto wanaosoma katika shule za msingi<br />
ikilinganishwa na watoto wenye umri wa kwenda shule). Nchini Uganda, ambako elimu ya msingi bure ilianza<br />
kutolewa kwa mara ya kwanza mwaka 1997, idadi ya jumla ya watoto walioandikishwa ilipanda kutoka pungufu<br />
kidogo ya asilimia 70 mwaka 1997 hadi kufikia zaidi ya asilimia 120 mwaka 2000. Nchini Tanzania, baada ya ada<br />
za shule kufutwa mwaka 2001, uandikishaji uliongezeka kutoka karibu asilimia 70 hadi karibu asilimia 110. Nchini<br />
Kenya, ongezeko halikuwa kubwa sana hasa kwa sababu tayari uandikishaji ulikuwa juu, lakini hata katika nchi hii,<br />
kuanzishwa upya kwa elimu ya msingi bure katika mwaka 2003 kulifanikisha uandikishaji kuongezeka hadi kufikia<br />
karibu asilimia 105.<br />
Kielelezo cha 1: jumla ya uandikishaji katika shule za msingi 1990-2008 (katika %)<br />
Chanzo cha data: Taasisi ya Takwimu ya UNESCO 2<br />
Mafanikio ya kuvutia yaliyopatikana katika uandikishaji watoto shuleni yalitoa fursa kwa jitihada kuelekezwa katika<br />
kusimamia kujifunza. <strong>Je</strong>, watoto wote hawa ambao sasa wanakwenda shule kweli wanafanikiwa kujenga uwezo wa<br />
kuhesabu na kusoma? <strong>Je</strong>, uwekezaji huu mkubwa unaofanywa na serikali hizi katika elimu ya msingi unazaa matunda<br />
yanayotarajiwa na watunga sera na wazazi?<br />
Ili kutathmini kiwango cha uwezo wa kusoma na kuhesabu walichonacho watoto wa umri wa kwenda shule, Uwezo<br />
ilifanya tafiti katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda. Tafiti zilihusisha kuwapima maelfu ya watoto katika mazingira<br />
ya nyumbani. Majaribio yaliyotumika yalikuwa ya ngazi ya Darasa la 2 kwa Kiingereza, Kiswahili na Kuhesabu.<br />
Majaribio haya yalitayarishwa kwa kuzingatia mitaala ya kila nchi inayohusika. Ripoti hii inatumia data hizi ili<br />
kutathmini ustadi wa watoto wa umri wa kwenda shule kutokana na majaribio ya Uwezo yaliyofanywa katika nchi hizi<br />
tatu.<br />
1 Basic Education Statistics in Tanzania 2010<br />
2 http://stats.uis.unesco.org<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 1
Jambo muhimu ambalo upimaji huu umebaini ni kwamba uwezo wa watoto katika nchi hizi tatu ulikuwa katika<br />
kiwango cha chini sana. Wanafunzi wengi waliokuwa katika Darasa la 3, ambao wote walitarajiwa wangekuwa<br />
wamepata stadi za kusoma na kuhesabu za ngazi ya Darasa la 2, hawakufaulu majaribio ya Uwezo. Kwa kulinganisha<br />
nchi hizi tatu tunaona kwamba watoto nchini Kenya walifanya vizuri zaidi na wale wa Tanzania walifanya vibaya zaidi.<br />
Vilevile uchambuzi unaonesha kwamba karibu wanafunzi wote wa Darasa la 7 nchini Kenya na Uganda walionesha<br />
kuwa wanamudu stadi za ngazi ya Darasa la 2. Hali ni tofauti nchiniTanzania ambako ni kati ya asilimia 50 hadi 80 tu<br />
ya wanafunzi wa Darasa la 7 ndiyo walioweza kukamilisha vizuri majaribio ya ngazi ya Darasa la 2 ya Uwezo.<br />
Ripoti hii inazingatia pia vipengele vingine. Inalinganisha fursa za upatikanaji wa elimu ya msingi katika nchi hizi tatu,<br />
inachambua na kulinganisha uwezo wa wanafunzi katika shule za serikali na zile za binafsi, na inazingatia tofauti za<br />
kijinsia, upatikanaji wa nyenzo shuleni na uwezo wa kiuchumi wa kaya.<br />
Ripoti hii imepangwa kwa sehemu. Sehemu ya 2 ya ripoti inaeleza zaidi kuhusu mbinu ya utafiti iliyotumiwa na<br />
Uwezo, wakati na namna ulivyotekelezwa na kiwango ambacho majaribio yanalingana katika nchi hizi tatu. Sehemu<br />
ya 3 inazungumzia upatikanaji wa elimu ya msingi; na sehemu ya 4 inajadili matokeo ya ujifunzaji. Sehemu ya 5<br />
inaangalia upatikanaji wa vifaa/nyenzo katika shule. Sehemu ya 6 na ile ya 7 zinajadili shule binafsi na tofauti za<br />
kijinsia. Wakati ambapo sehemu za 4 hadi 7 zinazingatia uhusiano baina ya vipengele mbalimbali (jinsia, madaraja ya<br />
utajiri wa kaya, kiwango cha ubora wa shule) na uwezo wa wanafunzi kwa upekee, sehemu ya 8 inawasilisha matokeo<br />
ya uchambuzi wa vipengele vilivyojadiliwa mapema katika ripoti kupitia matokeo ya ukokotozi wa kihesabu. Sehemu<br />
hii inawasilisha uchambuzi wa athari za vipengele mbalimbali katika ujumla wake. Hitimisho linawasilishwa katika<br />
sehemu ya 9.<br />
2. Taftishi na majaribio ya Uwezo<br />
Uwezo ilifanya tafiti kubwa za kaya na kupima uwezo wa kusoma na kufanya hesabu kwa watoto wenye umri wa kati<br />
ya miaka 6-16 (5-16 nchini Tanzania) katika mazingira ya nyumbani. Tafiti za Uwezo ndizo zilizotumia sampuli kubwa<br />
sana kuliko tafiti nyingine zozote zilizowahi kufanywa katika kanda hii. Vilevile, timu za utafiti zilikusanya data kutoka<br />
katika shule moja katika kila kijiji.<br />
Nchini Kenya, utafiti wa awali ulifanywa mwaka 2009. Taarifa za wilaya 70 kati ya 158 (zilizojumuishwa katika sensa)<br />
za Kenya zilikusanywa na jumla ya watoto 68,945 wenye umri wa miaka 6-16 kutoka kaya 40,286 walipimwa. Taarifa<br />
za shule zilikusanywa kutoka shule za msingi za serikali 2,030 343 Nchini Uganda, utafiti wa kwanza wa Uwezo ulifanyika<br />
mwaka 2010. Utafiti ulikusanya taarifa za wilaya 27 (kati ya wilaya 80 za Uganda wakati huo). Jumla ya vijiji 810 na<br />
kaya 16,200 zilitembelewa na watoto 34,752 wenye umri wa miaka 6-16 walipimwa.<br />
Nchini Tanzania, utafiti ulifanyika mwaka 2010. Ulihusisha wilaya 38 kati ya 133, vjijiji 1,140 na kaya 22,800<br />
zilitembelewa. Jumla ya watoto 42,033 wenye umri wa miaka 5-16 walipimwa.<br />
Majaribio yaliyotumiwa naUwezo katika upimaji yalikuwa ya ngazi ya Darasa la 2 na yalizingatia mitaala ya kila nchi.<br />
Nchini Kenya na Tanzania, watoto walipimwa katika kuhesabu na kusoma Kiswahili na Kiingereza. Nchini Uganda<br />
watoto walipimwa katika kuhesabu na kusoma Kiingereza. Ngazi ya Darasa la 2 imechaguliwa kwa sababu kwa<br />
mujibu wa viwango vya kimataifa baada ya ngazi hiyo ya kujifunza mwanafunzi anatarajiwa kuwa amepata stadi za<br />
msingi katika kuhesabu na kusoma, stadi ambazo ni muhimu katika kujifunza masomo mengine yote katika miaka ya<br />
baadaye.<br />
3 Kwa sasa kuna wilaya zaidi nchini Kenya, lakini wakati wa utafiti, wilaya 158 zilikuwa zimeorodheshwa katika gazeti la Serikali na kushirikishwa katika sensa ya<br />
watu ya mwaka 2009.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 2
<strong>Je</strong>dwali la 1: Utafiti wa Uwezo nchini Kenya, Tanzania na Uganda—muhtasari wa taarifa muhimu<br />
Kenya Tanzania Uganda<br />
Tarehe ya utafiti Sept/Okt 2009 Mei 2010 Aprili 2010<br />
Idadi ya wilaya 70 (kati ya 158) 38 (kati ya 133) 27 (kati ya 80)<br />
Idadi ya kaya 40,386 22,800 16,200<br />
Idadi ya watoto waliopimwa 68,945 43,033 34,752<br />
Idadi ya shule zilizotembelewa 2,030 1,140 810<br />
Ngazi za umri 6-16 5-16 6-16<br />
Jaribio la kuhesabu Ndiyo Ndiyo Ndiyo<br />
Jaribio la Kiswahili Ndiyo Ndiyo Hapana<br />
Jaribio la Kiingereza Ndiyo Ndiyo Ndiyo<br />
Chanzo cha data: Ripoti za kitaifa za Uwezo 54<br />
Majaribio yote yalitayarishwa kwa namna ambayo wanafunzi wangeweza kupimwa katika ngazi mbalimbali.<br />
Mathalani, jaribio la kusoma lililenga kubaini uwezo wa kusoma herufi mojamoja, kisha maneno, sentensi na/au aya,<br />
na mwisho hadithi iliyofuatiwa na maswali ya ufahamu. Vivyo hivyo, jaribio la hesabu lilianza na utambuzi wa namba,<br />
kujumlisha, kutoa, kuzidisha na kugawanya. <strong>Watoto</strong> walipewa alama za ziada iwapo walifanya fumbo la hesabu<br />
lililojumuisha shughuli na/au vitendo vya nyumbani vya kila siku, fumbo hilo lilitolewa katika lugha aliyoipendelea<br />
mtoto.<br />
Kwa kuwa majaribio yaliakisi mitaala ya kitaifa, hayakuweza kulinganishwa moja kwa moja. Badala yake, ulinganishaji<br />
alama za majaribio unaonesha iwapo watoto katika kila nchi wamepata stadi za ngazi ya Darasa la 2 za mtaala wa<br />
elimu wa taifa lao. Katika kila nchi, iwapo mfumo wa elimu ungekuwa mzuri, watoto wote (asilimia 100) walio katika<br />
Darasa la 3 wangekuwa wamepata stadi za ngazi ya Darasa la 2.<br />
Japo haiwezi kulinganishwa sawasawa, matarajio ya ufahamu wa wanafunzi katika Darasa la 2 si tofauti sana katika<br />
nchi hizi tatu. Hali hii inaonekana katika <strong>Je</strong>dwali la 3 ambalo linawasilisha majaribio yaliyotumika katika upimaji<br />
kwenye kila nchi. Jaribio la Kiswahili lingeweza kulinganishwa katika nchi za Kenya na Tanzania, huku ikionekana<br />
kwamba maswali ya ufahamu kwa Tanzania yalikuwa magumu zaidi kuliko yale ya Kenya. Jaribio la Kiingereza lilikuwa<br />
sawa katika nchi zote tatu, japo hadithi ya Tanzania ilikuwa fupi na rahisi kuliko zile za Kenya na Uganda. Vilevile<br />
majaribio ya kuhesabu yalikuwa sawa, isipokuwa tu kwamba jaribio la Tanzania lilikuwa na maswali ya kujumlisha kwa<br />
kuhamisha, na maswali ya kutoa kwa kuhamisha ambayo hata hivyo hayakuulizwa Kenya na Uganda. Kwa upande<br />
mwingine, nchini Uganda na Kenya wanafunzi walifanya hesabu za kugawanya, maswali ambayo watoto wa Tanzania<br />
hawakuulizwa.<br />
Inaweza kusemwa kwamba majaribio haya yalipima uwezo wa watoto katika kuhesabu na kusoma, na si kujifunza.<br />
Ili kupima kujifunza, ambacho ni kipimo cha kuonesha mabadiliko, mtafiti angepaswa kuchunguza tofauti katika<br />
viwango vya kufikiri tangu wakati wanafunzi wanapoanza shule katika nchi hizi zinazohusika. Kwa ujumla, inaelezwa<br />
kwamba katika nchi za Uganda na Kenya, Kiingereza kinazungumzwa kwa upana zaidi kuliko ilivyo nchini Tanzania.<br />
Kwa hiyo, kama ubora wa viwango vya ufundishaji vitabaki kuwa sawa katika nchi zote tatu, na jaribio kuwa na<br />
kiwango cha ugumu kilicho sawa, inatarajiwa kuwa watoto nchini Kenya na Uganda wangefanya vizuri zaidi katika<br />
jaribio la Kiingereza kuliko wale wa Tanzania. Kwa mantiki hiyo, hali kama hiyo inaweza kujitokeza kwa lugha ya<br />
Kiswahili ambayo inazungumzwa kwa upana zaidi nchini Tanzania kuliko Kenya na kwa kawaida haizungumzwi nchini<br />
Uganda. Pia, kiwango cha elimu ya wazazi kinaweza kusababisha tofauti wakati watoto wanapoingia shule.<br />
Mathalan, kwa mujibu wa tafiti za idadi ya watu na afya (Demographic and Health Surveys), nchini Kenya asilimia<br />
19 ya akina mama hawana elimu; takwimu kama hizo nchini Tanzania ni asilimia 33 na Uganda asilimia 23. Iwapo<br />
mazingira ya nyumbani yanaathiri uwezo wa watoto wakati wanapoanza shule, basi tofauti katika matokeo ya<br />
majaribio ya kuhesabu na kusoma hayamaanishi moja kwa moja uwepo wa tofauti katika kujifunza. Wakati huo huo<br />
uhusiano wa karibu unatarajiwa baina ya matokeo ya majaribio ya kuhesabu na kusoma na ujifunzaji katika shule.<br />
4<br />
Uwezo 2010, Are our children learning? Annual Learning Assessment Report. Kenya 2009; Uganda 2010; Tanzania 2010. Zote zinapatikana kutoka www.uwezo.<br />
net<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 3
Ripoti hii, kwa kiasi kikubwa, inawasilisha takwimu za kitaifa. Hii ni kwa kuzingatia kwamba utaratibu wa kupata<br />
sampuli za wilaya ulikuwa wa kinasibu. Ndani ya wilaya, vijiji vilichaguliwa kinasibu, na pia ndani ya vijiji taratibu za<br />
kinasibu zilitumika (japo taratibu zilizotumika Tanzania ziliwaruhusu watafiti kwa kiasi fulani kufanya uchaguzi huru<br />
ambao huenda ulisababisha upendeleo). Ili kuthibitisha kiwango ambacho matokeo ya kitaifa ya Uwezo yanafanana<br />
na yale yaliyopatikana katika tafiti nyingine za kitaifa zilizohusisha kaya, <strong>Je</strong>dwali la 2 linawasilisha idadi ndogo ya<br />
sifa za kaya, zilizopatikana kutoka tafiti za Uwezo na nyinginezo. Ulinganishaji wa data za Uganda (ambao ulifuata<br />
kanuni kali za kinasibu) unaonesha kufanana kwa karibu kwa matokeo ya Uwezo na yale ya Taftishi za Kaya katika<br />
Mambo ya Binadamu (Demographic Household Survey (DHS)). Kumekuwa na tofauti ndogo katika umiliki wa redio<br />
na runinga lakini tofauti hizi huenda zinaakisi kipindi cha miaka minne kilichopita katikati ya tafiti hizi mbili. Vilevile<br />
kwa Kenya, matokeo ya Uwezo yanafanana na yale ya DHS. Kuna tofauti ndogo, kama ambavyo ingetarajiwa, pale<br />
zinapolinganishwa sampuli za tafiti mbili, hata hivyo tofauti hizo si kubwa.<br />
Inaweza kusemwa, hata hivyo, kwamba sampuli ya Uwezo kwa upande wa Kenya inaonekana kuelemea zaidi<br />
kwa kaya masikini na zenye elimu ya chini. Nchini Tanzania kwa upande mwingine, tofauti kubwa zaidi zinaweza<br />
kuonekana. Katika nchi hii sampuli ya Uwezo inaonekana kuegemea zaidi kwenye kaya zenye elimu nzuri kidogo na<br />
zilizojaliwa kiuchumi. Tofauti katika kipengele cha akina mama wasio na elimu (asilimia 30 katika HBS; asilimia 14<br />
katika utafiti wa Uwezo) inastusha zaidi. Pia ukweli kwamba Uwezo inaripoti asilimia 19 ya kaya zenye umeme dhidi<br />
ya asilimia 12 katika utafiti wa HBS ni tofauti kubwa.<br />
Katika sehemu zinazofuata za ripoti hii masuala haya yanajadiliwa, lakini msomaji anatahadharishwa kwamba sampuli<br />
ya Tanzania inaweza kuwa imeegemea zaidi katika kaya zenye hali nzuri, na sampuli ya Kenya kuegemea zaidi kwenye<br />
kaya zenye hali duni.<br />
<strong>Je</strong>dwali la 2: Mlinganisho wa matokeo ya kitaifa ya Uwezo na tafiti nyingine za kitaifa za kaya<br />
Tanzania Kenya Uganda<br />
Uwezo HBS Uwezo<br />
2009<br />
DHS<br />
Uwezo 2010<br />
DHS<br />
Elimu ya mama<br />
2010 2007<br />
2009<br />
2006<br />
Hana elimu 14 30 24 19 Hakuna taarifa kuhusu elimu ya mama<br />
Elimu ya msingi 1-4 8 9 53 60<br />
katika utafiti wa Uwezo<br />
Elimu ya msingi 5-7/8 66 52<br />
Elimu ya sekondari 1-4 6 6 23 20<br />
Zaidi ya sekondari 2 2<br />
Mali &Umeme<br />
Umeme 19 12 11 23 8 9<br />
Redio 70 66 73 74 74 61<br />
Runinga 18 8 22 28 13 6<br />
Chanzo cha data: Uwezo, DHS (Uganda naKenya) na HBS (Tanzania) 65<br />
5<br />
www.measuredhs.com; Idara ya takwimu 2009; Utafiti wa Bajeti za Kaya 2007.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 4
<strong>Je</strong>dwali la 3: Sampuli za majaribio ya Kuhesabu, Kiingereza na Kiswahili yaliyotumiwa na Uwezo<br />
3a: Jaribio la Kuhesabu<br />
Utambuzi wa<br />
Namba 1-9<br />
Utambuzi wa<br />
Namba<br />
Kujumlisha bila kubeba Kujumlisha na<br />
kubeba<br />
Kutoa bila kukopa Kutoa na kukopa<br />
Kuzidisha Kugawanya Hesabu zenye uhusiano na utamaduni<br />
10-99<br />
TZ 2 8<br />
87 31<br />
55 49<br />
77 45 89 76 33 62 12 15<br />
Shilingi 300 + Shilingi 200 = Shilingi<br />
+23 +30<br />
+25 +48 -42 -33 -15 -25 x 4 x 4<br />
6 0<br />
51 60<br />
24 33<br />
23 12 66 48 70 97 11 9<br />
7 5<br />
28 99 +71 +42<br />
+68 +64 - 55 - 4 -34 -48 x 5 x24<br />
KE 3 6<br />
16 34<br />
32 60<br />
+24 +15<br />
46 59<br />
-24 -38<br />
3 x 4 =<br />
5 ÷1 =<br />
Una shilingi 80. Utabaki na shilingi ngapi<br />
baada ya kununua mfuko mmoja wa<br />
unga unaouzwa kwa shilingi 60?<br />
2 7 33 78<br />
5 x 2 =<br />
15 ÷3 =<br />
24 43<br />
53 74<br />
4 5 50 99 +71 +51<br />
-41 -21<br />
3 x 2 =<br />
8 ÷2 =<br />
UG 9 5<br />
1 3<br />
11 91<br />
91 47<br />
14 88<br />
+12 +11<br />
71 46<br />
-60 -14<br />
7 x 3 =<br />
3 x 4 =<br />
6 ÷2 =<br />
2 ÷2 =<br />
Jane anataka kamba ambayo inauzwa<br />
shilingi 250. John anampa Jane shilingi<br />
300. <strong>Je</strong>, Jane atabaki na shilingi ngapi<br />
baada ya kununua kamba?<br />
15 13<br />
66 89<br />
8 6<br />
72 69 +13 +14<br />
- 15 -14<br />
5 x 1 =<br />
8 ÷2 =<br />
3b Jaribio la Kiingereza<br />
Herufi Maneno Sentensi/Aya Hadithi<br />
TZ e n<br />
d u<br />
w f<br />
boy tall<br />
good best<br />
come sing<br />
This is my cat.<br />
That dog is big.<br />
I like my school.<br />
My home is small.<br />
Juma is living in a small village. He gets a letter once a month. The letter is from his son Musa. Musa lives in Dodoma. Juma cannot<br />
read the letters. He asks Sara to read the letters for him.<br />
Questions: 1. Where does Juma live?<br />
2. What does Sara read?<br />
3. What is the name of Juma’s son?<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 5
KE e x<br />
d w<br />
k c<br />
Room face<br />
table dog<br />
desk pen<br />
My mother works in Lamu.<br />
Lamu is the busy town.<br />
The people there are good.<br />
They are very kind.<br />
Juma reads to us a story from his book every day. He reads the story aloud in class. We enjoy listening to the stories. Yesterday, he<br />
read about the sun and the wind. Both of them lived in the same sky. The wind did not like the sun .It wanted to be the head of<br />
the sky. One day, the wind chased the sun away. It told sun to go to another sky. The sun did not go. The next morning, the wind<br />
ran after the sun. The sun fell down and started crying. That is how it began to rain. We clapped for Juma.<br />
Questions: 1. What does Juma do every day?<br />
2. How did rain begin?<br />
UG i o<br />
w y<br />
cow mat<br />
car sing<br />
This is our goat.<br />
She has two kids.<br />
Tom is our best football player. He stays far away from school. One day we had a big match. Tom had not come to school that day.<br />
The teacher went to look for Tom. The teacher found Tom weeding cassava. The teacher called Tom from the garden. All pupils<br />
were happy when Tom came. Our school won the match. We danced the whole day.<br />
s h bus leg She likes her kids.<br />
Questions: 1. Where was Tom?<br />
She feeds them well.<br />
2. Why were the children dancing?<br />
3c Majaribio ya Kiswahili<br />
Silabi Maneno Aya Hadithi<br />
TZ fa ki Chai sherehe Baba amejenga nyumba nzuri.<br />
mwa njo<br />
le chi<br />
vuta maziwa<br />
mama kaka<br />
Nyumba yetu imezungukwa na<br />
miti.<br />
Miti huzuia upepo mkali.<br />
Hapo zamani za kale samaki waliishi nchi kavu. Waliishi kwa kula wadudu kama vile panzi, mende na sisimizi. Siku moja wadudu<br />
hawa walikaa kikao na kupanga namna ya kuwaondoa samaki. Kikao chao wengi walichangia. Ikafika zamu ya sisimizi. Sisimizi<br />
alisimama na kusema, “Umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu”. Wote walisimama na kupiga kelele “samaki wauaweee”. Samaki<br />
waliposikia hivi walikimbia na kujificha majini. Hadi hivi leo samaki wanaishi majini.<br />
Maswali: 1. Hapo zamani samaki waliishi wapi?<br />
Miti hutupatia hewa safi.<br />
2. Zamani samaki walikuwa wanakula wadudu gani?<br />
3. Hadithi hii inatufundisha nini?<br />
KE be di<br />
na tu<br />
ho le<br />
kiti taa<br />
soko uso<br />
mali choo<br />
Mama anapika uji.<br />
Juma anasoma kitabu.<br />
Maria anacheza mpira.<br />
Naye baba analima shambani.<br />
Jina langu ni Fatuma Abdi. Ninaishi Nakuru na familia yetu kwenye nyumba kubwa. Baba yangu ni mwalimu katika shule ya upili.<br />
Wanafunzi wanampenda mama yangu kwakuwa ni mwalimu mzuri. Nao nyanya na babu wanaishi kule kijijini. Wao wana mbuzi<br />
na kondoo wengi. Mimi huwatembelea siku za likizo. Nyanya hunipa hadithi nzuri za kuchekesha. Mimi hucheka hadi mbavu zikaniuma.<br />
Likizo ikiisha, nyanya hunipa maziwa nimletee mama yangu.<br />
Maswali: 1. Mama ya Fatuma hufanya kazi gani?<br />
2. Fatuma huwatembelea Nyanya na Babu wakati gani?<br />
(*) Angalizo: Wilaya za Kenya zina rangi ya buluu, wilaya za Ugandani kijani, wilaya za Tanzania ni nyekundu.<br />
Chanzo cha data: Ripoti za kitaifa za Uwezo<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 6
3. Upatikanaji wa Elimu<br />
3.1 Uandikishaji katika shule za msingi uko juu lakini si kila mahali<br />
Kielelezo cha 2 kinaonesha uandikishaji katika shule za msingi kulingana na umri wa watoto katika nchi<br />
zinazohusika. 76 Mihimili katika kilelelezo inaonesha tofauti katika mifumo ya elimu miongoni mwa nchi hizi. Nchini<br />
Kenya elimu ya msingi hutolewa kwa miaka nane na watoto wanatarajiwa kwenda shule tangu wakiwa na umri wa<br />
miaka 6 hadi 13. Katika nchi za Tanzania na Uganda, elimu ya msingi huchukua miaka saba. Nchini Uganda watoto<br />
wanaanza shule wanapokuwa na miaka 6 na kumaliza wanapokuwa na umri wa miaka 12, wakati nchini Tanzania<br />
wanaanza shule wanapokuwa na miaka 7 na kumaliza wakiwa na miaka 13. Kielelezo kinaonesha pia watoto walio nje<br />
ya viwango hivi vya umri.<br />
Mihimili katika kielelezo inaonesha jinsi uandikishaji ulivyo wa chini sana nchini Tanzania. Bila kujali umri, idadi ya<br />
watoto waliojiunga na shule nchini Tanzania bado ni ndogo kuliko katika nchi nyingine. Vilevile kielelezo kinaonesha<br />
jinsi nchini Uganda, ikilinganishwa na Kenya, watoto wengi zaidi walivyoandikishwa katika shule za msingi walipokuwa<br />
na umri wa miaka sita. Nchini Kenya, kwa kiasi fulani kutokana na kuwa na mtaala wenye nyongeza ya mwaka mmoja<br />
zaidi, sehemu kubwa ya watoto wenye umri mkubwa (wale waliokuwa na miaka 14-16) walikwenda shule.<br />
Kielelezo cha 2: Uandikishaji katika shule za msingi kwa umri<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
3.2 Fursa za kujiandikisha zinabaki kuwa si sawa na hutegemea utajiri wa kaya<br />
Kielelezo cha 3 kinaonesha jinsi uandikishaji ndani ya nchi unavyotofautiana kulingana na uwezo wa kimapato wa<br />
kaya ya mtoto. Madaraja matano ya viwango vya utajiri yaliainishwa: masikini zaidi, masikini, hali ya kati (kipimo cha<br />
kati), tajiri na tajiri sana na kila daraja lilikuwa na kaya asilimia 20. Madaraja ya utajiri yaliundwa kwa kutumia data<br />
zilizokusanywa toka katika nchi husika, ikimaanisha kwamba inawezekana kaya masikini katika Kenya ni bora zaidi<br />
kuliko zile zilizo katika kiwango cha kati nchini Tanzania. Kielelezo hiki kinajikita katika uandikishaji wa watoto ndani<br />
ya umri rasmi wa kwenda shule katika kila nchi. Viwango vya uandikishaji vilikuwa vya chini sana katika Kenya (karibu<br />
asilimia 84) na juu sana katika Uganda (karibu asilimia 90). Kielelezo kinaonesha vilevile kwamba watoto kutoka<br />
katika kaya masikini walikuwa na uwezekano mkubwa wa kutoandikishwa shule. Tofauti hizi zimeonekana zaidi katika<br />
Kenya na kwa kiwango kidogo katika Uganda na Tanzania.<br />
6<br />
Kipengele hiki kinatokana na maswali kwa wazazi kuhusu uandikishaji mashuleni. Matokeo yake tunatumia maneno “uandikishwaji shuleni”, japokuwa inawezekana<br />
wazazi walielewa swali waliloulizwa kama swali kuhusu mahudhurio. Dhana ya uwezekano wa wazazi kuongelea mahudhurio wakati wameulizwa kuhusu<br />
uandikishaji inatokana na ukweli kwamba viwango vya uandikishwaji vilivyoonekana kutoka kwenye data za Uwezo vinakaribiana sana na viwango vya mahudhurio<br />
kama ilivyooneshwa na tafiti za DHS (angalia mathalan takwimu katika www.measuredhs.com)<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 7
kwendashulekatikakilanchi.ViwangovyauandikishajivilikuwavyachinisanakatikaKenya(karibu<br />
asilimia84)najuusanakatikaUganda(karibuasilimia90).Kielelezokinaoneshavilevilekwamba<br />
watotokutokakatikakayamasikiniwalikuwanauwezekanomkubwawakutoandikishwashule.<br />
TofautihizizimeonekanazaidikatikaKenyanakwakiwangokidogokatikaUgandanaTanzania.<br />
Kielelezo cha 3: Uandikishaji wa watoto walio katika umri wa lazima kwenda shule (*) kwa madaraja matano ya<br />
Kielelezocha3:Uandikishajiwawatotowaliokatikaumriwalazimakwendashule utajiri<br />
(*) kwa<br />
madarajamatanoyautajiri<br />
100<br />
82<br />
86 88 90<br />
92<br />
87<br />
82<br />
86 87 86<br />
90 91 92 93<br />
90<br />
80<br />
74<br />
70<br />
60<br />
50<br />
40<br />
30<br />
20<br />
10<br />
0<br />
Asilimiayawatotowaumriwa<br />
kwendashulewalioandikishwa<br />
Maskinizaidi<br />
Maskini<br />
Kipimochakak<br />
Tajiri<br />
Tajirisana<br />
Maskinizaidi<br />
Maskini<br />
<br />
(*) Nchini Kenya umri wa lazima kwenda shule ni miaka 6-13; Tanzania ni 7-13 na Uganda ni 6-12.<br />
(*)NchiniKenyaumriwalazimakwendashulenimiaka6‐13;Tanzaniani7‐13naUgandani6‐12.<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Chanzochadata:Uwezo<br />
<br />
Namna nyingine ya kuonesha taabu za watoto kutoka kaya masikini sana ni kwa kuangalia watoto ambao kamwe<br />
hawakwenda Namnanyingineyakuoneshataabuzawatotokutokakayamasikinisananikwakuangaliawatoto<br />
shule ya msingi. Kama inavyoonekana wazi katika Kielelezo cha 4, watoto kutoka kaya masikini sana<br />
ndiyo ambaokamwehawakwendashuleyamsingi.KamainavyoonekanawazikatikaKielelezocha4,<br />
walioathirika zaidi. Nchini Kenya asilimia 64 watoto wa umri wa miaka 5-16 hawakwenda<br />
shule watotokutokakayamasikinisanandiyowalioathirikazaidi.NchiniKenyaasilimia64yawatotowa<br />
walitoka kaya sana katika madaraja umasikini ambapo nchini Uganda idadi hiyo ilikuwa asilimia 45<br />
na umriwamiaka5‐16ambaokamwehawakwendashulewalikuwakutokakayamasikinisanakatika<br />
nchini Tanzania asilimia 45 87 .<br />
madarajayaumasikiniambaponchiniUgandaidadihiyoilikuwaasilimia45nanchiniTanzania<br />
asilimia45 7 . <br />
Kielelezo cha 4: Asilimia ya watoto wenye umri wa miaka 5-16 ambao hawakuwahi kwenda shule ya msingi, kwa<br />
madaraja matano ya utajiri<br />
Kipimochakak<br />
Tajiri<br />
Tajirisana<br />
Maskinizaidi<br />
Maskini<br />
Kipimochakak<br />
Tajiri<br />
Tajirisana<br />
<br />
<br />
7 KwaTanzaniaumriulikuwakatiyamiaka5‐16.<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
13<br />
Kama ilivyo idadi ya watoto ambao hawakuandikishwa, idadi ya wale walioacha shule ilikuwa juu miongoni mwa kaya<br />
masikini zaidi, ingawa tofauti zilikuwa ndogo ikilinganishwa na ile ya wasioandikishwa. Miongoni mwa wale walioacha<br />
<br />
shule, nchini Kenya asilimia 61 walitoka katika kaya masikini au masikini zaidi ikilinganishwa na asilimia 50 kutoka<br />
Uganda na 41 kutoka Tanzania.<br />
7<br />
Kwa Tanzania umri ulikuwa kati ya miaka 5-16.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 8
Kielelezo cha 5: <strong>Watoto</strong> wa miaka 5 hadi 16 walioacha shule, kwa vipimo vya utajiri wa kaya<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Hitimisho: Licha ya ongezeko kubwa la uandikishaji kufuatia kuanzishwa kwa sera ya elimu ya msingi bure, data za<br />
utafiti wa Uwezo zinaonesha kwamba uandikishaji haukuwa umejumuisha watoto wote wenye umri wa kwenda<br />
shule. Kutegemeana na kiwango cha utajiri, kati ya asilimia 7 na 26 ya watoto wa umri wa kwenda shule walikuwa<br />
hawaendi shuleni . Viwango hivi vinalingana na viwango vya mahudhurio vilivyopatikana katika tafiti nyingine. Tafiti<br />
za DHS zinaonesha viwango vya mahudhurio vya asilimia 73 kwa Tanzania (2004/5), 79 kwa Kenya (2008/9), na 82<br />
kwa Uganda (2006).<br />
<strong>Watoto</strong> kutoka makundi ya kaya masikini na masikini zaidi walikuwa na uwezekano mdogo wa kuhudhuria wote<br />
shuleni ikilinganishwa na watoto wanaotoka kwenye kaya zenye kipato bora zaidi. Hivyo si tu kwamba mpango<br />
wa kufikisha elimu kwa watoto wote haukufanikiwa kikamilifu, lakini pia fursa za kwenda shule hazikuwa sawa, na<br />
zilitegemea kiwango cha kipato cha kaya.<br />
4. Ujifunzaji<br />
4.1 Uwezo (umahiri) katika majaribio ya Kiingereza, Kuhesabu na Kiswahili<br />
Lengo kuu la jaribio la Uwezo lilikuwa kupima uwezo wa watoto katika stadi za kusoma na kuhesabu. Kwa kuwa<br />
majaribio yanaonesha ufahamu ambao wanafunzi walipaswa kuwa nao baada ya kukamilisha masomo ya ngazi<br />
ya Darasa la 2, watoto wote katika madarasa ya juu walipaswa kufaulu vizuri katika jaribio la Darasa la 2. Kama<br />
itakavyooneshwa katika sehemu hii, matokeo yalikuwa kinyume cha matarajio hayo. Jambo hili lilijidhihirika hata<br />
miongoni mwa watoto wa ngazi ya Darasa la 7, wengi hawakuwa na stadi za kuhesabu na kusoma za ngazi ya Darasa<br />
la 2.<br />
Kiingereza: Kielelezo cha 6 kinawasilisha jinsi watoto walivyofanya katika jaribio la Kiingereza huku kikionesha tofauti<br />
baina ya madarasa tofauti. Kielelezo kinaonesha jinsi ambavyo katika kila nchi watoto wachache wa Darasa la 3 ndiyo<br />
waliokuwa na stadi za kiwango cha Darasa la 2 katika jaribio la kusoma. Nchini Kenya ni asilimia 28 tu ya watoto<br />
wa Darasa la 3 ndiyo waliokamilisha jaribio kwa mafanikio, yaani waliweza kusoma hadithi bila shida. Katika nchi za<br />
Uganda na Tanzania viwango vya ufaulu vilikuwa vya chini zaidi, asilimia 4 kwa asilimia 8 kwa mpangilio wa nchi hizo.<br />
<strong>Watoto</strong> katika madarasa ya juu walionekana kufanya vizuri katika majaribio ya Uwezo kama ilivyotarajiwa. Nchini<br />
Kenya asilimia 94 ya watoto wa ngazi ya Darasa la 7 walionesha kumudu stadi za Darasa la 2 katika kusoma kifungu<br />
cha maneno cha Kiingereza. Umahiri ulionekana kuimarika kulingana na ngazi ya darasa katika nchi za Uganda na<br />
Tanzania vilevile. Bila kuangalia darasa, asilimia ya watoto wa Kenya waliokuwa katika kiwango cha juu cha uelewa<br />
ilikuwa kubwa kuliko ile ya wenzao katika nchi za Uganda na Tanzania. Nchini Tanzania matokeo yanakatisha tamaa; ni<br />
asilimia 51 tu ya watoto katika Darasa la 7 ndiyo waliofaulu jaribio la Kiingereza lililokuwa katika kiwango cha Darasa<br />
la 2.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 9
Kadri muda wa kuwa shule unayoongezeka ndivyo tofauti kati ya Kenya na Uganda katika asilimia ya watoto ambao<br />
wamepata stadi za kiwango cha Darasa la 2 polepole inavyopungua. Wakati katika Darasa la 4 tofauti katika viwango<br />
vya ufaulu kati ya nchi hizi mbili ilikuwa ni asilimia 39, ilipofika Darasa la 7 tofauti ilikuwa imepungua hadi asilimia<br />
14. Kwa Kenya na Tanzania hali hii haikujitokeza na karibu mara mbili ya watoto katika Kenya walifaulu jaribio la<br />
Kiingereza katika Darasa la 7 ikilinganishwa na ilivyokuwa katika Tanzania.<br />
Kielelezo cha 6: Umahiri wa wanafunzi katika jaribio la Kiingereza la Uwezo,kwa darasa<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kuhesabu: Matokeo katika jaribio la kuhesabu yalifanana na yale ya Kiingereza, watoto wa Kenya wakiwa wamefanya<br />
vizuri (japokuwa ‘vizuri’ ni kwa kiwango cha wastani tu) wakilinganishwa na watoto wa Uganda na Tanzania. Kama<br />
ilivyokuwa katika jaribio lililotangulia watoto wa Tanzania ndiyo waliofanya vibaya zaidi. Kama ilivyokuwa katika<br />
jaribio la Kiingereza, uwezo wa watoto uliimarika kulingana na wakati na walipofika Darasa la 7 wengi wao walikuwa<br />
wamepata stadi za msingi katika kuhesabu na walikuwa na stadi zilizotarajiwa katika ngazi ya Darasa la 2. Lakini hata<br />
katika Kenya, nchi yenye ufaulu wa juu, asilimia 12 ya watoto katika Darasa la 7 walishindwa kufanya vizuri katika<br />
mazoezi ya kuhesabu yaliyotarajiwa katika kiwango cha Darasa la 2.<br />
Ikilinganishwa na kusoma Kiingereza, tofauti kiuwezo katika jaribio la kuhesabu kati ya Tanzania kwa upande<br />
mmoja na Kenya na Uganda kwa upande mwingine, ni dogo. Inawezekana, ingawa hii ni kwa kukisia, pengo kubwa<br />
kwa Kiingereza kuliko kuhesabu linaakisi kuwa watoto katika Kenya na Uganda wanaishi katika mazingira ambapo<br />
Kiingereza kinasikika na kinazungumzwa kwa upana zaidi. Matokeo yake watoto hao wananufaika zaidi kuliko watoto<br />
wa Tanzania ambao nje ya shule hawapati fursa hiyo na walimu wao wana uzoefu mdogo katika Kiingereza. Tofauti<br />
katika alama za kuhesabu inaonesha kwamba haya si maelezo pekee kuhusu udhaifu wa stadi walizo nazo watoto<br />
wa Tanzania. Kwa kuwa kiwango cha ufaulu katika majaribio yote mawili (Kiingereza na Kuhesabu) ni wa chini zaidi<br />
chini Tanzania, inaonekana kwamba huenda kwa kiasi kikubwa watoto wa Tanzania wanajifunza kwa kiasi kidogo<br />
wanapokuwa shuleni kuliko watoto wenzao katika nchi za Kenya na Uganda.<br />
Kielelezo cha 7: Umahiri wa wanafunzi katika jaribio la kuhesabu la Uwezo, kwa darasa<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 10<br />
Chanzo cha data: Uwezo
Kiswahili: Hitimisho hili linaungwa mkono na matokeo yaliyoonekana katika jaribio la Kiswahili. Jaribio hili<br />
liliendeshwa katika nchi ya Kenya na Tanzania pekee (kwa sababu Kiswahili hakitumiwi kwa upana nchini Uganda).<br />
Ruwaza iliyoonekana awali ya matokeo mabaya kwa wanafunzi wa Darasa la 3 na hali ya uwezo kuimarika polepole<br />
jinsi watoto wanavyopanda katika madarasa ya juu ilijirudia. <strong>Watoto</strong> wa Kenya walifanya vizuri zaidi kuliko watoto<br />
wa Tanzania. Tofauti inayoonekana katika uwezo wa watoto kati ya Tanzania na Kenya katika Kiswahili ilikuwa<br />
ndogo kuliko ile iliyopo katika Kiingereza na kuhesabu (huenda matokeo haya yanaakisi ukweli kwamba Kiswahili<br />
kinazungumzwa kwa upana zaidi katika Tanzania ikilinganishwa na Kenya), lakini bado tofauti ilikuwepo. Hivyo hata<br />
katika jaribio ambalo watoto wa Tanzania wangepaswa kuwa na nafasi nzuri zaidi ya kufaulu kuliko wale wa Kenya,<br />
watoto wa Tanzania walifanya vibaya. Kielelezo cha 8 kinaonesha zaidi uwezo wa watoto katika Kiswahili, kwa darasa,<br />
katika Kenya na Tanzania.<br />
Kielelezo cha 8: Umahiri wa wanafunzi katika jaribio la Kiswahili la Uwezo, kwa darasa<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
4.2 Tofauti katika uwezo wa watoto ki-wilaya<br />
Licha ya tofauti katika uwezo wa watoto miongoni mwa nchi hizi tatu, kuna tofauti nyingine kubwa zilizokuwepo<br />
miongoni mwa wilaya ndani ya kila nchi. <strong>Je</strong>dwali la 5 linaonesha asilimia ya watoto katika Darasa la 3 wenye stadi za<br />
kuhesabu na kusoma za Darasa la 2. Nchini Tanzania asilimia 33 ya watoto katika wilaya ya Moshi Mjini, iliyofanya<br />
vizuri zaidi, walifaulu jaribio la Kiingereza lakini hakuna mtoto hata mmoja (asilimia 0) katika wilaya ya Liwale<br />
aliyefaulu jaribio hilo. Nchini Kenya, asilimia 66 ya watoto katika wilaya ya Kikuyu walifaulu jaribio la kuhesabu, lakini<br />
ni asilimia 5 tu ya watoto walifaulu katika wilaya ya Lagdera. Na nchini Uganda, asilimia 40 ya watoto katika wilaya<br />
ya Bushenyi walifaulu jaribio la kuhesabu, lakini ni asilimia 7 tu walifaulu katika wilaya ya Nakapiripirit. Tofauti hizo<br />
zinaweza kuonekana katika kila jaribio katika majaribio matatu, na katika kila nchi. Tofauti hizi zinaleta wasiwasi.<br />
Hakuna sababu kwa nini watoto wa Nakapiripirit, Lagdera au Liwale wafanye vibaya kuliko watoto wenzao wa<br />
Bushenyi, Kikuyu au Moshi Mjini. Mahali anapozaliwa mtoto na kwenda shule pasiathiri uwezekano wa yeye kupata<br />
stadi za msingi na uwezo wa kufanya vizuri katika kusoma na kuhesabu. Ukweli kwamba matokeo yako hivyo ni<br />
kiashiria cha kutosha kuonesha kwamba hakuna usawa katika mifumo ya elimu katika kila nchi.<br />
<strong>Je</strong>dwali la 4 linawasilisha wilaya kumi zilizofanya vizuri na zilizofanya vibaya nchini Kenya, Uganda na Tanzania. Katika<br />
majaribio ya Kiingereza na Kuhesabu , wilaya zote 10 bora za mwanzo zilikuwa za Kenya. Katika zile za chini, kulikuwa<br />
pia na wilaya chache za Kenya lakini nyingi kati ya hizo zilikuwa za Uganda na Tanzania. Ruwaza ya jumla ilionesha<br />
kwamba wilaya kutoka Kenya zilikuwa juu katika chati, wilaya za Tanzania zilikuwa chini, na za Uganda zilikuwa<br />
k a ti k a ti .<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 11
<strong>Je</strong>dwali la 4: Wilaya zilizofanya vizuri sana na vibaya sana, wanafunzi wa Darasa la 3 katika majaribio ya Kiingereza<br />
na Kuhesabu<br />
Jaribio la Kiingereza<br />
Jaribio la Kuhesabu<br />
Zilizofanya vizuri sana Zilizofanya<br />
Zilizofanya vizuri<br />
Zilizofanya vibaya sana<br />
vibaya sana<br />
sana<br />
1 Kikuyu Adjumani Kikuyu Kasulu<br />
2 Naivasha Liwale Kaloleni Lagdera<br />
3 Pokot Kaskazini Katakwi Naivasha Bukoba Vijijini<br />
4 Taita Bundibugyo Meru Kusini Nakapiripirit<br />
5 Nandi Mashariki Shinyanga Vijijini Nandi Kaskazini Gulu<br />
6 Imenti Kaskazini Gulu Mbeere Kotido<br />
7 Nyeri Kusini Kamuli Kibwezi Mwanga<br />
8 Ruiru Mayuge Gatanga Singida Vijijini<br />
9 Nakuru Kaskazini Yumbe Keiyo Mayuge<br />
10 Gatanga Amuru Imenti Kaskazini Shinyanga Vijijini<br />
(*) Angalizo: Wilaya za Kenya ni buluu, wilaya za Uganda ni kijani, wilaya za Tanzania ni nyekundu.<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
<strong>Je</strong>dwali la 5 linaonesha kwamba wilaya zilizofanya vizuri katika jaribio moja, ziliweza pia kufanya vizuri katika<br />
majaribio mengine. Katika Tanzania, wilaya za Moshi Vijijini na Rombo zilikuwa miongoni mwa wilaya tatu bora<br />
katika kila jaribio katika majaribio matatu. Nchini Kenya, wilaya za Kikuyu na Naivasha ndizo zilizofanya vizuri katika<br />
kila jaribio, na kule Uganda wilaya za Wakiso na Masaka zimejitokeza. <strong>Je</strong>, wilaya hizi zinafanana kwa namna gani?<br />
Miongoni mwa wilaya zilizofanya vibaya kulikuwa na tofauti nyingi japo wilaya za Muleba na Kasulu katika Tanzania,<br />
na Lagdera na Wajir Mashariki katika Kenya zinaonekana zaidi ya mara moja katika orodha ya wilaya zinazofanya<br />
vibaya zaidi. Kwa ufupi inaonekana kwamba wilaya zinazofanya vizuri zote zinafanana, wilaya zinazofanya vibaya<br />
zinafanya vibaya kwa namna yao.<br />
<strong>Je</strong>dwali la 5: Wilaya zilizofanya vizuri sana na vibaya sana kwa Darasa la 3, kwa wilaya na nchi<br />
Tanzania Kenya Uganda<br />
Kiingereza Waliofanya vizuri<br />
sana<br />
Waliofanya Waliofanya vizuri<br />
sana<br />
Waliofanya vibaya<br />
sana<br />
Waliofanya vizuri<br />
sana<br />
Waliofanya<br />
vibaya sana<br />
vibaya sana<br />
1 Moshi Mjini 33% Liwale 0% Kikuyu 64% Lagdera 4% Wakiso 12% Adjumani 0%<br />
2 Rombo 23% Shinyanga<br />
Vijijini<br />
1% Naivasha 53% Trans Mara 9% Masaka 8% Katakwi 0%<br />
3 Moshi<br />
Vijijini<br />
23% Muleba 2% Pokot<br />
North<br />
52% Rachuonyo 10% Nakasongola<br />
8% Bundibugyo<br />
1%<br />
Kuhesabu<br />
1 Moshi Mjini 40% Kasulu 5% Kikuyu 66% Lagdera 5% Busheni 40% Nakapiripirit<br />
7%<br />
North<br />
2 Rombo 39% Bukoba Vijijini 7% Kaloleni 65% Samburu 14% Masaka 38% Gulu 7%<br />
3 Moshi 35% Mwanga 8% Naivasha 57% Wajir 17% Wakiso 38% Kotido<br />
Vijijini<br />
Mashariki<br />
8%<br />
1<br />
Kiswahili<br />
Rombo 63% Muleba 9% Naivasha 68% Lagdera 4% Hawakufanya<br />
2 Moshi Mjini 58% Mwanga 16% Taita 64% Wajir 12%<br />
Mashariki<br />
3 Kisarawe 57% Kasulu 17% Kikuyu 62% Trans Mara 14%<br />
(*) Angalizo: Wilaya za Kenya ni buluu, wilaya za Ugandani kijani, wilaya za Tanzania ni nyekundu<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
4.3 Tofauti katika umahiri wa wanafunzi kwa mujibu wa utajiri wa kaya<br />
Sifa za kaya vilevile zilionesha kuathiri umahiri wa watoto katika majaribio. Kielelezo cha 9 na 10 hapa chini<br />
vinaonesha jinsi utajiri wa kaya unavyohusiana na uwezo wa wanafunzi. <strong>Watoto</strong> kutoka kaya tajiri sana walifanya<br />
vizuri zaidi katika majaribio ya Uwezo kuliko watoto kutoka kaya zenye hali ya chini. Mathalan, nchini Kenya karibu<br />
nusu (asilimia 47) ya watoto wa Darasa la 3 kutoka kaya tajiri sana walionesha kuwa na stadi za kusoma za Darasa<br />
la 2, kinyume na asilimia 19 tu ya watoto kutoka katika kaya maskini zaidi. Vivyo hivyo, asilimia 48 ya watoto kutoka<br />
kaya tajiri sana katika Kenya walifaulu jaribio la kuhesabu, kinyume na asilimia 28 tu ya watoto kutoka kaya maskini<br />
zaidi.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 12
Kielelezo cha 9: Ufaulu wa wanafunzi wa Darasa la 3 katika jaribio la Kiingereza la Uwezo, kwa madaraja ya utajiri<br />
na nchi<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kielelezo cha 10: Umahiri wa wanafunzi wa Darasa la 3 katika jaribio la kuhesabu, kwa madaraja ya utajiri na nchi<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kulikuwa na uwezekano mdogo kwa watoto kutoka kaya masikini zaidi nchini Kenya kufaulu majaribio ya Kuhesabu<br />
na Kiingereza kuliko watoto kutoka kaya tajiri. Hata hivyo, uwezekano wa kufanikiwa ulikuwa bado juu kwa mtoto<br />
kutoka kaya masikini zaidi nchini humo kuliko mtoto kutoka kaya tajiri sana katika Uganda au Tanzania. Mathalani,<br />
asilimia 19 ya watoto kutoka kaya masikini zaidi nchini Kenya walifaulu jaribio la Kiingereza, ikilinganishwa na asilimia<br />
16 ya watoto kutoka kaya tajiri sana za Uganda na asilimia 11 ya watoto kutoka Tanzania. Kwa jaribio la Kuhesabu,<br />
matokeo yanafanana, isipokuwa watoto wa Kenya kutoka kaya masikini zaidi walifaulu kwa kiwango kinachokaribiana<br />
na watoto wenzao kutoka kaya tajiri zaidi za Uganda na Tanzania.<br />
Hitimisho: Matokeo ya utafiti wa Uwezo yanaonesha kwamba stadi za kuhesabu na kusoma zilikuwa dhaifu katika<br />
nchi zote tatu na watoto walio wengi katika Darasa la 3 hawakufikia stadi za kiwango cha Darasa la 2 katika kuhesabu<br />
na kusoma. Kati ya waliofanya vibaya, Kenya ilifanya vizuri zaidi kuliko Uganda na Tanzania. Tanzania inaonesha<br />
udhaifu mkubwa zaidi katika majaribio ya Uwezo. Tofauti kubwa katika umahiri wa watoto zimeonekana katika<br />
wilaya ndani na kati ya nchi na kwa watoto kutoka kaya zenye viwango tofauti vya kipato. Inawezakana kukawa na<br />
matumaini kutokana na tofauti za msingi katika ufaulu zilizojitokeza ndani ya kila nchi. Kuwepo kwa tofauti hizo<br />
kunaashiria kwamba umahiri wa watoto unaweza kuimarika katika mifumo ya elimu iliyopo sasa na inatoa fursa ya<br />
kutafuta sababu zilizopelekea kuwepo kwa tofauti hizi.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 13
5. Upatikanaji wa nyenzo shuleni<br />
Inawezekana tofauti zilizobainika katika umahiri wa watoto ki-wilaya ni kutokana na tofauti ya upatikanaji wa nyenzo<br />
shuleni au tofauti katika ufundishaji. Japokuwa utafiti wa Uwezo haukujumuisha taarifa kuhusu ubora wa ufundishaji,<br />
taarifa katika dodoso la shule ziliruhusu kwa namna fulani kuangalia mahitaji yaliyokuwa yanapatikana katika shule.<br />
Kwa kila moja ya nchi hizi tatu dodoso la shule la Uwezo lilikusanya taarifa ambazo zingeweza kukokotolewa kuhusu<br />
idadi ya wanafunzi kwa mwalimu, wanafunzi kwa darasa, na wanafunzi kwa choo.<br />
Ulinganishi kwa mujibu wa nchi unaonesha kwamba shule za Kenya zilikuwa na uwiano mdogo wa<br />
wanafunzi:mwalimu, wanafunzi:darasa, na wanafunzi wachache kwa vyoo kuliko shule za Uganda na Tanzania.<br />
Tofauti kati ya Kenya na Tanzania na Uganda ilikuwa kubwa. Mathalan, nchini Tanzania kulikuwa na wanafunzi 60<br />
kwa mwalimu mmoja, nchini Kenya ni wanafunzi 38. Uganda kulikuwa na wanafunzi 83 kwa darasa, wakati Kenya<br />
ni 48. Kwa ujumla viashiria vya upatikanaji wa mahitaji ya elimu nchini Kenya vinakaribiana sana na viwango rasmi<br />
vinavyotakiwa kufikiwa kuliko hali ilivyo katika nchi za Uganda na Tanzania.<br />
Kielelezo cha 11: Viashiria vya upatikanaji wa mahitaji shuleni kwa Kenya, Uganda na Tanzania<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Ndani ya nchi hizi tofauti kubwa zilionekana. Tofauti hizi zinaweza kuonekana katika <strong>Je</strong>dwali la 6 linaloonesha nafasi<br />
za wilaya kulingana na upatikanaji wa mahitaji ya shule kwa kuzingatia wiano hizi tatu. Nafasi ya jumla ya wilaya<br />
ilipatikana baada ya kukokotoa nafasi ya wilaya katika kila kiashiria kwa viashiria vyote vitatu na kuzipa wilaya namba<br />
kulingana na nafasi iliyopata. Jumla ya namba zinazoambatana na nafasi zilizopata wilaya kwa viashiria vyote vitatu<br />
ndizo zinazotoa nafasi za jumla ambazo wilaya zilipewa kutoka wilaya ya juu kabisa hadi ya chini kabisa katika <strong>Je</strong>dwali<br />
la 6.<br />
<strong>Je</strong>dwali linaonesha kwamba wastani ulitofautiana sana: kutoka wanafunzi 25 kwa mwalimu (chini kabisa) kama<br />
iliyokuwa katika wilaya ya Imenti Kusini, Kenya, hadi wanafunzi 91 kwa mwalimu (juu kabisa) katika wilaya ya Muleba,<br />
Tanzania. Vilevile wiano za mwanafunzi: darasa zilitofautiana kutoka wanafunzi 23 (chini kabisa pia) katika wilaya<br />
ya Imenti Kusini, hadi kufikia 173 (juu kabisa) katika wilaya ya Buliisa, Uganda. Uwiano wa wanafunzi kwa choo pia<br />
ulitofautiana, kutoka uwiano wa chini kabisa wa wanafunzi 14 kwa choo katika wilaya ya Nyeri Kusini, Kenya hadi<br />
kufikia kiwango cha juu kabisa, kiasi cha wanafunzi 110 kwa choo kimoja katika wilaya ya Kamuli, Uganda. Hizi wiano<br />
ni wastani katika ngazi ya wilaya, ikimaanisha kuwa zinaficha tofauti kubwa zaidi zilizopo baina ya shule. Kwa shule<br />
moja moja na madarasa, tofauti zilikuwa za juu zaidi. Mathalan, nchini Kenya data za Uwezo zinaonesha kwamba<br />
wiano za mwanafunzi:mwalimu zinaanzia 10:1, chini kabisa hadi kufikia zaidi ya 200:1.<br />
Jambo jingine lililoonekana ni kwamba wilaya za Kenya zilikuwa katika nafasi za juu, ambapo za Tanzania na Uganda,<br />
na chache za Kenya zilionekana katika nafasi za chini ya orodha. Katika upangaji wa nafasi uliofanywa na Uwezo katika<br />
Afrika Mashariki, wilaya za Kenya zilionekana kuwa katika nafasi 24 za juu. Wilaya ya kwanza isiyo ya Kenya ilikuwa<br />
ya Tanzania katika nafasi ya 25, ambapo wilaya ya kwanza ya Uganda ilionekana katika nafasi ya 44. Hakuna wilaya za<br />
Kenya zilizokuwa miongoni mwa zile zilizoshika nafasi 10 za chini.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 14
<strong>Je</strong>dwali la 6: Wilaya zilizofanya vizuri na vibaya sana katika kipimo kinachojumuisha uwiano wa<br />
mwanafunzi:mwalimu, mwanafunzi: darasa na mwanafunzi: choo<br />
Wanafunzi kwa<br />
Nafasi Jina la wilaya Wanafunzi kwa mwalimu darasa<br />
Wanafunzi kwa choo<br />
Wilaya 10 za juu<br />
1 ImentiKusini 25 23 14<br />
2 Mbeere 27 28 17<br />
3 Meru Kusini 28 25 17<br />
4 Imenti Kaskazini 28 29 23<br />
5 Nyeri Kusini 33 28 14<br />
6 Kericho 28 35 30<br />
7 Nyandarua Kaskazini 35 33 17<br />
8 Kikuyu 35 31 25<br />
9 Tharaka 29 29 39<br />
10 Wareng 31 35 31<br />
Wilaya 10 za chini<br />
126 Muleba 91 83 79<br />
127 Kamuli 66 86 110<br />
128 Mayuge 64 99 100<br />
129 Urambo 86 110 69<br />
130 Amuru 70 117 76<br />
131 Amuria 69 100 89<br />
132 Budaka 69 101 87<br />
133 Geita 83 108 92<br />
134 Buliisa 67 173 112<br />
135 Ilemela 87 140 107<br />
(*) Angalizo: wilaya za Kenya ni buluu, wilaya za Uganda ni kijani, wilaya za Tanzaniani nyekundu<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kielelezo cha hali ya upatikanaji mahitaji shuleni kinaweza kuundwa kwa kutumia utaratibu uleule uliotumika kuunda<br />
kielelezo cha utajiri wa kaya 98 . Madaraja matano ya upatikanaji wa mahitaji, kila moja likiwa na asilimia 20 ya shule<br />
zilizotembelewa, yaliainishwa kwa kila nchi. Madaraja hayo matano hayakuweza kulinganishwa moja kwa moja<br />
miongoni mwa nchi zote tatu kwa kuwa viashiria tofauti vilitumika kuunda kielelezo cha kila nchi. Ndani ya nchi, kwa<br />
kiasi kikubwa ufaulu wa wanafunzi wa Darasa la 3 katika majaribio ya Uwezo haukutofautiana sana kulingana na<br />
daraja la hali ya mahitaji katika shule. Tofauti moja iliyojitokeza ni kwamba katika nchi za Kenya na Tanzania umahiri<br />
wa wanafunzi katika jaribio la Kiingereza ulikuwa mkubwa zaidi kwa watoto waliosoma katika shule iliyokuwa katika<br />
daraja la juu la upatikanaji wa mahitaji.<br />
Kielelezo cha 12: <strong>Watoto</strong> wa Darasa la 3 wenye stadi za kusoma Kiingereza za Darasa la 2, kwa madaraja ya<br />
upatikanaji wa nyenzo shuleni<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
8<br />
Angalia, mathalani Filmer D na Pritchett LH. Estimating wealth effect without expenditure data-or tears: an application to educational enrollments in states of<br />
India. Demography 2001; 38:115-32.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 15
Kielelezo cha 13: <strong>Watoto</strong> wa Darasa la 3 wenye stadi za kuhesabu za Darasa la 2, kwa madaraja ya upatikanaji wa<br />
nyenzo shuleni<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kielelezo cha 14 na kile cha 15 vinawasilisha ubora wa shule kwa kuzingatia hali ya upatikanaji nyenzo katika shule<br />
walizohudhuria watoto kutoka daraja la chini na la juu la utajiri. Inaonekana kwamba, kwa ujumla, watoto kutoka<br />
kaya masikini walihudhuria shule duni, ambapo watoto kutoka familia bora walihudhuria shule bora. Nchini Kenya,<br />
tofauti zilionekana zaidi na watoto asilimia 37 kutoka asilimia 20 ya kaya masikini zaidi walihudhuria shule duni zaidi,<br />
ambapo ni asilimia 9 tu kutoka kaya masikini zaidi ndiyo walihudhuria shule bora zaidi. Nchini Uganda, mgawanyo<br />
ulionekana kuwa wa usawa zaidi, wakati Tanzania ikichukua nafasi ya katikati.<br />
Kielelezo cha 14: Hali ya nyenzo katika shule walizosoma watoto kutoka kaya masikini zaidi<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kielelezo cha 15: Hali ya nyenzo katika shule walizosoma watoto kutoka kaya tajiri zaidi<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 16
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Hitimisho: Kuna tofauti kubwa katika hali ya upatikanaji wa mahitaji baina ya shule. Ubora wa shule ukitafsiriwa kwa<br />
kutumia seti ya viashiria sahili vya mahitaji (wanafunzi kwa mwalimu, wanafunzi kwa darasa, na wanafunzi kwa choo)<br />
ulionesha kuwepo kwa tofauti kubwa miongoni mwa nchi hizi tatu, kati ya wilaya ndani ya nchi, na kati ya shule zilizo<br />
katika wilaya moja. Kwa jumla shule nchini Kenya zilikuwa zina hali nzuri zaidi kuliko shule za Uganda na Tanzania;<br />
shule za Uganda ndizo zilizokuwa na hali duni zaidi.<br />
Uhusiano kati ya hali ya upatikanaji mahitaji shuleni na umahiri wa watoto katika majaribio ya Uwezo ulionekana<br />
kuwa hafifu. Hali hii inapaswa kuwatahadharisha wale wanaoamini kuwa utendaji katika shule utakuwa bora zaidi<br />
kwa kupunguza uwiano wa mwanafunzi:mwalimu au uwiano wa mwanafunzi:darasa. Data za Uwezo zinaashiria kuwa<br />
vipengele hivi ni muhimu ila vipengele ambavyo havikuangaliwa katika utafiti vinaweza kuwa ni muhimu zaidi. Namna<br />
ya ufundishaji, uwajibikaji wa mwalimu na motisha ni baadhi ya vipengele vingine muhimu vinavyoathiri ufaulu wa<br />
shule. Kwa bahati mbaya hakuna taarifa zilizokusanywa kuhusu vipengele hivi.<br />
Mwisho, watoto kutoka kaya masikini walikuwa na mazingira magumu zaidi kwa maana si tu kwamba kulikuwa na<br />
uwezekano mkubwa wa wao kutokwenda shule au kuacha shule, wao vilevile walikuwa na uwezekano mkubwa zaidi<br />
wa kusoma katika shule zilizo na hali duni ya mahitaji.<br />
6. Shule binafsi<br />
Mpaka sasa ripoti hii imejikita katika stadi za kuhesabu na kusoma katika shule za msingi za serikali. Lakini kuna idadi<br />
kubwa ya watoto wanaosoma katika shule binafsi katika nchi za Afrika Mashariki. Nchini Kenya asilimia 9 ya watoto<br />
wenye umri wa kwenda shule wanasoma katika shule binafsi na nchini Uganda watoto wanaofikia asilimia 28 ya<br />
watoto wote walioandikishwa shule wanahudhuria shule binafsi. Tanzania ndiyo nchi ambayo ina watoto wachache<br />
zaidi wanaosoma katika shule binafsi (asilimia 2).<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 17
Kielelezo cha 16: Mgawanyo wa wanafunzi wa elimu ya msingi katika shule za serikali na binafsi<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Haishangazi, bila shaka, kwamba watoto walio wengi waliosoma katika shule binafsi walitoka katika kaya tajiri sana;<br />
wachache walitoka katika kaya masikini. Ruwaza hii ilijitokeza zaidi katika Tanzania, ambako watoto waliosoma katika<br />
shule binafsi kwa kawaida walitoka katika kaya zilizo katika madaraja mawili ya juu ya kipimo cha utajiri. Nchini<br />
Uganda, elimu katika shule za binafsi ilipatikana pia kwa watoto kutoka kaya masikini, ingawa watoto kutoka kaya<br />
tajiri bado ndiyo waliokuwa na nafasi kubwa zaidi ya kusoma katika shule hizo. Kenya inashika nafasi ya katikati.<br />
Kielelezo cha 17: Uandikishaji watoto katika shule za binafsi kwa mujibu wa madaraja ya utajiri<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 18<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi walifanya vizuri katika majaribio ya Uwezo kuliko wale wanaosoma katika<br />
shule za serikali. Matokeo haya yamejidhihirisha katika nchi zote tatu. Nchini Kenya asilimia 60 ya watoto katika shule<br />
binafsi Darasa la 3 walifaulu majaribio ya Kiingereza na Kuhesabu. Matokeo haya yalikuwa pungufu ya asilimia 100<br />
yaliyoyatarajiwa lakini mazuri mara mbili zaidi ikilinganishwa na matokeo katika shule za serikali. Nchini Tanzania<br />
tofauti katika uwezo wa watoto wa Darasa la 3 kati ya shule za serikali na binafsi ilikuwa dhahiri zaidi. Wakati watoto<br />
chini ya asilimia 10 katika shule za serikali walifaulu jaribio la Kiingereza, karibu nusu ya wale waliokuwa katika<br />
shule binafsi walifaulu. Tofauti kama hiyo, japo ndogo ilionekana pia katika jaribio la kuhesabu. Pengine matokeo<br />
yanayostusha zaidi yalikuwa kutoka Uganda ambako shule binafsi zilifanya vizuri kuliko shule za serikali lakini ni<br />
asilimia 10 tu ya watoto katika Darasa la 3 wanaohudhuria shule binafsi ndio waliofaulu jaribio la Kiingereza. Hii ni<br />
licha ya kuwa lugha ya Kiingereza inatumiwa kwa kiasi kikubwa katika baadhi ya shule za Uganda. Matokeo haya<br />
ndiyo yaliyokuwa mabaya zaidi katika Afrika Mashariki. Miongoni mwa wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi<br />
wanafunzi katika shule binafsi za Uganda pia walifanya vibaya sana katika jaribio la kuhesabu.
Wakati watoto wanapokuwa wamefika Darasa la 7, tofauti katika ufulu haionekani kati ya wale wanaosoma katika<br />
shule za serikali na wanaosoma katika shule binafsi, isipokuwa kwa Tanzania ambako wanafunzi wa Darasa la 7<br />
katika shule za serikali wameonekana kufanya vibaya zaidi kuliko wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi. Wakati<br />
huohuo, nchini Uganda na Tanzania idadi kubwa ya wanafunzi katika shule binafsi katika Darasa la 7 waliendelea<br />
kushindwa katika majaribio ya Uwezo. Mathalan, mwanafunzi mmoja kati ya watano wa Darasa la 7 wa shule binafsi<br />
nchini Uganda walishindwa jaribio la hesabu la Uwezo. Nchini Tanzania, mwanafunzi mmoja kati ya watatu wa darasa<br />
la saba toka shule binafsi walishindwa jaribio la hesabu la Uwezo.<br />
Kielelezo cha 18: Umahiri katika majaribio ya Uwezo ya Kiingereza na Hesabu kwa mujibu wa<br />
aina ya shule na darasa<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Hitimisho: Mahudhurio ya wanafunzi katika shule binafsi yametofautiana sana katika nchi za Afrika Mashariki, kukiwa<br />
na mtoto mmoja kati ya watoto wanne anayesoma katika shule za binafsi nchini Uganda, na mtoto mmoja kati ya<br />
watoto 50 nchini Tanzania. Kama ilivyotarajiwa, ni watoto kutoka kaya tajiri sana ndiyo wanaosoma katika shule<br />
binafsi, ingawa nchini Uganda upatikanaji wa shule ulionesha mgawanyo wenye usawa zaidi miongoni mwa matabaka<br />
ya utajiri.<br />
Umahiri wa wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi katika majaribio ya Uwezo ulikuwa mzuri zaidi kuliko ya wale<br />
wanaosoma katika shule za serikali, lakini bado hayaridhishi. Wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi kwa kiasi<br />
fulani walifanya vibaya hasa katika nchi za Tanzania na Uganda. Hata Kenya, ambako watoto kutoka shule zake za<br />
binafsi walifanya vizuri zaidi, mtoto mmoja katika watoto watatu wa Darasa la 3 alishindwa katika majaribio ya Uwezo<br />
ya kuhesabu na Kiingereza.<br />
Matokeo mazuri ya shule binafsi yanatoa fursa ya kuchunguza ni nini hasa chanzo cha matokeo hayo mazuri. <strong>Je</strong>, shule<br />
za binafsi zina vitendea kazi bora kama vile vitabu, walimu wenye sifa bora kitaaluma, uwajibikaji, mishahara mizuri<br />
ya walimu, au vichocheo vingine? Wakati huo huo ni wazi kwamba shule binafsi zenyewe si ufumbuzi, kwa kuwa<br />
matokeo ya wanafunzi wao bado hayaridhishi sana.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 19
7. Usawa wa Kijinsia<br />
Sehemu hii inajadili usawa wa kijinsia kwenye shule. Kama ilivyojadiliwa katika Sehemu ya 3, zilionekana tofauti<br />
katika viwango vya uandikishaji katika nchi hizi tatu. Hata hivyo, kama Kielelezo cha 19 kinavyoonesha, nchi zote<br />
zimefanikiwa kukuza usawa wa kijinsia katika uandikishaji. Katika nchi za Uganda na Kenya uandikishaji ulikuwa juu<br />
kidogo kwa wanafunzi wavulana ukilinganishwa na ule wa wasichana, wakati Tanzania kiwango cha uandikishaji<br />
kilikuwa juu kidogo kwa wasichana.<br />
Kielelezo cha 19: Uandikishaji kwa mujibu wa jinsia kwa watoto wenye umri wa kwenda shule<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Wakati ambapo tofauti za kijinsia katika uandikishaji wanafunzi zimepungua sana, majaribio ya Uwezo yameonesha<br />
kuwepo kwa tofauti kidogo katika viwango vya ufaulu baina ya wanafunzi wa kike na wa kiume kama inavyoonekana<br />
katika <strong>Je</strong>dwali la 20. Nchini Kenya, wanafunzi wa kike walifanya vibaya kidogo katika majaribio matatu ya Uwezo,<br />
wakati katika nchi za Uganda na Tanzania ushahidi ulichanganyika. Nchini Uganda, wanafunzi wa kike walifanya<br />
vizuri kidogo katika jaribio la Kiingereza tofauti na wavulana na vibaya katika jaribio la kuhesabu. Nchini Tanzania,<br />
wanafunzi wa kike pia walifanya vibaya kidogo katika jaribio la kuhesabu, vizuri katika jaribio la Kiingereza, na vizuri<br />
zaidi katika jaribio la Kiswahili.<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 20
Kielelezo cha 20: Ufaulu wa wanafunzi wa Darasa la 3 katika majaribio ya Uwezo, kwa mujibu wa jinsia<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Hitimisho: Ubaguzi wa kijinsia mara nyingi huonekana katika nyanja za siasa-jamii. Hali hii haikuonekana katika<br />
elimu ya msingi, angalau katika uandikishaji au umahiri wa wanafunzi katika stadi za msingi za kusoma na kuhesabu:<br />
wanafunzi wa kike na wa kiume walikuwa na ufaulu usiotofautiana sana. Nchini Kenya, wanafunzi wa kike waliachwa<br />
nyuma kidogo katika uandikishaji na pia hawakufanya vizuri katika majaribio ya Uwezo ukilinganisha na wenzao wa<br />
kiume. Kwa upande wa Uganda na Tanzania matokeo yalichanganyika, na inaweza kuwa haki kuhitimisha kuwa kwa<br />
ujumla wasichana na wavulana walionesha umahiri sawa.<br />
8. Ni vipengele vipi vinaathiri zaidi ufaulu wa watoto?<br />
Hadi hapa ripoti hii inaonesha kwamba stadi za msingi za kuhesabu na kusoma zilihusiana kwa karibu zaidi na<br />
darasa analosoma mtoto, iwapo alitoka katika kaya tajiri, na kama alisoma katika shule ya binafsi. Stadi za msingi za<br />
kuhesabu na kusoma hazina uhusiano wa karibu na upatikanaji wa nyenzo au mahitaji shuleni, na jinsia ya mtoto.<br />
Kwa kuwa wanafunzi waliosoma katika shule duni pia walitarajiwa kukabiliwa na changamoto nyingine kama vile<br />
kipato kidogo katika kaya, ni vigumu kuchanganua athari za hali ya upatikanaji wa nyenzo shuleni kwa mafanikio ya<br />
watoto. Katika sehemu hii tunachunguza uhusiano wa vipengele tulivyojadili kwa ujumla na umahiri wa wanafunzi<br />
shuleni. Tunaangalia pia vipengele vingine vinavyoweza kuwa na uhusiano na ufaulu wa wanafunzi kama vile<br />
kiwango cha elimu ya mama au umri wa mtoto. Kwa kufanya ukokotozi wa kimahesabu tunajaribu kukadiria athari ya<br />
vipengele hivi kila kimoja, kikiwa peke yake, bila kuwepo kwa athari ya kipengele kingine katika ufaulu wa mtoto.<br />
Tunawasilisha matokeo kwa nchi moja moja kwa kuwa data za Uwezo zinaruhusu kuingiza vigezo tofauti tofauti katika<br />
kila nchi. Mathalan, katika utafiti wa Uwezo nchini Uganda maswali kuhusu elimu ya mama hayakuulizwa, wakati<br />
yaliulizwa katika Tanzania na Kenya.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 21
Katika nchi zote tatu na kwa majaribio matatu tofauti, ruwaza ya kufanana inajitokeza. Darasa alilokuwa anasoma<br />
mwanafunzi ni kipengele kilichoonekana kuwa na uhusiano wa karibu zaidi na uwezekano wa mtoto kuwa na stadi<br />
za msingi za kuhesabu na kusoma. Elimu ya mama nayo vilevile ilikuwa na athari kubwa kwa uwezekano wa mtoto<br />
kumudu stadi hizi za msingi lakini, na hii ilionekana dhahiri zaidi, hasa kwa kinamama wenye elimu ya sekondari na<br />
kuendelea. Ilipotokea kuwa mama ana elimu ya shule ya msingi au chini ya hapo, athari chanya kwenye umahiri wa<br />
mtoto katika kumudu stadi za msingi shuleni haikuonekana. Vipengele vya utajiri wa kaya na mtoto kusoma katika<br />
shule za binafsi vilikuwa na athari chanya kubwa katika ufaulu shuleni. Vipengele vya jinsia na upatikanaji wa nyenzo/<br />
mahitaji ya shule vilikuwa na athari kidogo sana.<br />
Kielelezo cha 21: Athari za ziada kutokana na vipengele mbalimbali kwa umahiri wa wanafunzi katika jaribio la<br />
Uwezo: Kenya<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kielelezo cha 22: Athari za ziada kutokana na vipengele mbalimbali katika uwezo wa wanafunzi katika jaribio la<br />
Uwezo:Tanzania<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 22
Figure 23: Athari za ziada kutokana na vipengele mbalimbali kwa umahiri wa wanafunzi katika jaribio la Uwezo:<br />
Uganda<br />
9. Hitimisho<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Muhtasari wa matokeo makuu<br />
Ripoti hii imechunguza uwezo wa kuhesabu na kusoma kwa maelfu ya wanafunzi wenye umri wa kati ya miaka 6 na<br />
16 katika nchi za Kenya, Tanzania na Uganda kwa kutumia majaribio ya Uwezo yaliyofanywa mwaka 2009/10. Kwa<br />
mujibu wa matokeo haya, watoto katika nchi zote tatu walifanya vibaya ikilinganishwa na viwango vya mitaala ya<br />
nchi zao. Wanafunzi wa shule za msingi za Kenya ndiyo walioonekana kuwa wanajifunza zaidi. Katika majaribio yote<br />
matatu–Kiswahili, Kiingereza na kuhesabu–wanafunzi wa Kenya walikuwa juu, wakifuatiwa na wanafunzi wa Uganda.<br />
Wanafunzi wa Tanzania ndiyo waliofanya vibaya zaidi hata katika jaribio la Kiswahili, lugha ambayo watoto wa<br />
Tanzania wanaitumia zaidi kuliko watoto wa Kenya.<br />
Wakati watoto wa Kenya wameonesha kuwa na stadi bora zaidi katika kuhesabu na kusoma, nao pia hawakufanya<br />
vizuri sana. Katika Darasa la 3, watoto kama wawili kati ya watatu hawakuweza kufaulu majaribio ya Uwezo ya<br />
Kiingereza, Kiswahili na kuhesabu. Matokeo haya yanatia wasiwasi, kwa kuwa matarajio yalikuwa asilimia 100 au<br />
watoto wote katika Darasa la 3 wangeweza kufaulu jaribio la Darasa la 2. Ni pale wanafunzi walipofika Darasa la 7<br />
ndipo karibu wote walionesha kuwa wamepata stadi za msingi za kuhesabu na kusoma za Darasa la 2, japo katika<br />
Tanzania nusu ya wanafunzi wa Darasa la 7 bado hawakuweza kufanya jaribio la Kiingereza la Darasa la 2.<br />
Shule nchini Kenya zilionekana kuwa na hali nzuri zaidi ya upatikanaji wa mahitaji ya shule (kwa kuangalia uwiano<br />
wa wanafunzi kwa mwalimu; uwiano wa wanafunzi kwa darasa, na vilevile wa wanafunzi kwa choo) zikilinganishwa<br />
na shule katika nchi za Uganda na Tanzania. Hata hivyo, jambo muhimu tuliloliona, ukizingatia rasilimali nyingi<br />
zimewekezwa katika miaka ya karibuni ili kuongeza ubora wa miundo mbinu ya shule, ni kwamba upatikanaji<br />
wa nyenzo hizi ulikuwa na uhusiano mdogo sana na viwango vya ustadi wa watoto katika kusoma na kuhesabu.<br />
Wanafunzi katika maeneo yenye shule zenye miundombinu bora hawakufanya vizuri kuliko wale wanaosoma katika<br />
shule zenye miundombinu isiyotosheleza au katika madarasa yenye msongamano mkubwa.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 23
Kenya ilikuwa nchi pekee ambako tofauti za kiusawa zilionekana wazi zaidi. Miongoni wa kaya masikini zaidi, watoto<br />
wachache zaidi waliofikia umri wa lazima kwenda shule waliandikishwa katika shule za msingi za Kenya (asilimia 74)<br />
ikilinganishwa na Tanzania (asilimia 82) na Uganda (asilimia 86). <strong>Watoto</strong> masikini wa Kenya walikuwa na uwezekano<br />
mkubwa wa kusoma katika shule zenye hali ya chini kuliko watoto masikini katika nchi za Uganda au Tanzania. <strong>Watoto</strong><br />
masikini Kenya walikuwa na uwezekano mkubwa zaidi wa kutokwenda shule ya msingi na kuacha shule kuliko watoto<br />
wenzao wa Tanzania.<br />
Licha ya hali hii, kwa upande wa matokeo ya kujifunza, watoto masikini nchini Kenya walikuwa na uwezekano<br />
mkubwa wa kufanya vizuri katika majaribio ya Uwezo kuliko watoto kutoka kaya tajiri zaidi katika nchi ya Tanzania<br />
na Uganda.Nchini Kenya asilimia ya watoto kutoka kaya masikini katika Darasa la 3 waliofaulu jaribio la kuhesabu<br />
walikuwa asilimia 31, ikilinganishwa na asilimia 28 ya watoto kutoka kaya tajiri zaidi Uganda waliofaulu jaribio hili.<br />
Asilimia ya watoto wa Kenya kutoka kaya masikini zaidi waliofaulu jaribio la Kiingereza ilikuwa 19, ikilinganishwa na<br />
asilimia 16 ya watoto kutoka kaya tajiri sana katika Tanzania waliofaulu jaribio hili.<br />
Nchini Uganda, watoto walifanya vibaya sana katika madarasa ya chini lakini walipofika katika madarasa ya juu<br />
waliimarika na kuweza kuonesha ustadi wa kumudu majaribio ya viwango vya Darasa la 2. Walipofika Darasa la 7,<br />
kiwango cha ufaulu cha watoto wa Uganda kilikuwa karibu sawa na cha watoto wa Kenya. Matokeo kwa upande<br />
wa watoto wa Tanzania yalikuwa tofauti: kiwango cha ufaulu wa watoto kilibadilika kwa kiasi kidogo sana kadri<br />
walivyoendelea kupanda madarasa. Matokeo yake ni kwamba, ni asilimia 51 tu ya watoto wa Tanzania katika Darasa<br />
la 7 walifaulu jaribio la Kiingereza la Uwezo na ni asilimia 68 tu katika Darasa la 7 walifaulu jaribio la kuhesabu la<br />
Darasa la 2.<br />
<strong>Watoto</strong> wanaosoma katika shule za binafsi walifanya vizuri kiasi wakilinganishwa na wale wanaosoma katika shule<br />
za serikali. Utafiti unathibitisha kwamba elimu ya mama ilikuwa na athari kubwa katika uwezo wa mtoto shuleni<br />
iwapo mama alikuwa angalau na elimu ya sekondari. Tofauti za kijinsia katika uandikishaji au ufaulu shuleni hazikuwa<br />
kubwa.<br />
Nini kifanyike<br />
Ukiangalia matokeo haya bila shaka utagundua kuna changamoto kubwa zinazokabili serikali za Afrika Mashariki,<br />
walimu na wazazi katika kuhakikisha kwamba watoto wanapata stadi za msingi za kuhesabu na kusoma. Tofauti katika<br />
ujifunzaji vilevile zinapunguza matumaini ya ushirikiano mkubwa na maendeleo kati ya nchi za ukanda wa Afrika<br />
Mashariki. Hali katika Tanzania ni mbaya zaidi, lakini matokeo ya Kenya na Uganda yanatoa faraja kidogo. Jitihada<br />
zaidi zinahitajika sana kushughulikia viwango vya watoto kutokwenda shule na kuacha shule. Vile vile kuna haja ya<br />
kuhakikisha kwamba watoto si tu waende shuleni lakini pia wajifunze wakiwa shuleni. Kimataifa inazidi kutambuliwa<br />
kuwa watoto wanahitaji kuwa shuleni na kujifunza pia.<br />
Matokeo mabaya lazima huibua swali, nini kifanyike? Matokeo katika ripoti hii yanaashiria kwamba watunga sera<br />
wangefanya vizuri iwapo wangehoji ufanisi wa mbinu zilizotumika hadi kufikia sasa, badala ya kuendelea kutekeleza<br />
mbinu zile zile zilizozoeleka. Japo uwekezaji wa aina tofauti tofauti unaweza kuleta matokeo chanya, viwango vya<br />
ufanisi wa uwekezaji vinatofautina. Uwekezaji wa aina fulani unaweza kuleta mabadiliko bora na ya haraka zaidi<br />
kuliko mwingine, au kuonesha kuwa na manufaa zaidi kwa thamani ya matumizi ya fedha. Katika muktadha ambapo<br />
rasilimali hazitoshelezi, ni muhimu kupima ushahidi uliopo kwa uangalifu zaidi ili kutambua kile kinachoweza<br />
kuchangia zaidi katika kuleta mafanikio.<br />
Matokeo ya Uwezo yanatoa uelekezi kidogo kuhusu mambo yanayoweza kufanyika ili kusukuma mbele maendeleo.<br />
Kwanza, kuwepo kwa uhusiano mdogo kati ya wiano za mwanafunzi:mwalimu na mwanafunzi:darasa na kujifunza<br />
ni taarifa muhimu, kwa kuwa inauliza swali iwapo vitendea kazi na fedha katika maeneo haya vitakuwa suluhisho<br />
katika kukabili hali ya hatari iliyopo. Huu ni wakati muafaka wa kushughulikia ubora wa ufundishaji na vichocheo na<br />
motisha kwa walimu. Licha ya yote, inawezekana kabisa kwamba sababu mojawapo ya watoto wanaokwenda shule<br />
kujifunza kidogo inatokana na motisha zisizowaridhisha walimu, mahudhurio ya walimu shuleni yakiwa hafifu pia.<br />
Kwa mfano, ushahidi kutoka Tanzania unaonesha kwamba asilimia 23 ya walimu hawahudhurii shuleni kila siku na<br />
hata wanapokuwa shuleni, walimu wanatumia karibu nusu ya muda wao nje ya madarasa. Matokeo yake watoto<br />
wanafundishwa kwa masaa mawili tu na dakika nne kwa siku, badala ya masaa matano yanayotarajiwa. 109 Tafiti katika<br />
nchi za Uganda na Kenya zinabaini kuwepo kwa hali inayofanana na ya Tanzania.<br />
9<br />
Worldbank Service Delivery Indicators:Education and Health Care in Africa,iliyowasilishwa REPOA, Machi 4,2011<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 24
Tofauti zilizoonekana katika kiwango cha ufaulu wa wanafunzi miongoni mwa wilaya ndani ya kila nchi hizi tatu,<br />
na baina ya shule za serikali na zile za binafsi, zinaashiria kwamba baadhi ya shule ‘zimetafuta’ namna ya kupata<br />
matokeo mazuri katikati ya vikwazo vilivyopo. Tukichunguza kwa nini baadhi ya wilaya, na ndani ya wilaya baadhi ya<br />
shule zinafanya vizuri kuliko nyingine huenda tukapata dokezo kuhusu mambo ya msingi zaidi yanayotakiwa kufanywa<br />
ili kuboresha ujifunzaji.<br />
Mbinu rahisi na isiyo na gharama kubwa ingekuwa kuanza kwa kubainisha ni shule zipi zinafanya vizuri (au vibaya)<br />
kuliko inavyotarajiwa ikilinganishwa na rasilimali zilizopo, kuzitembelea shule hizi na kubainisha mambo yale<br />
yanayoweza kueleza matokeo yao, na kutokana na ziara hizi, kuweza kujifunza yale mambo ya msingi yanayofanana.<br />
Mbinu nyingine zinaweza kutumika. Kuna ushahidi mwingi kutoka Kenya unaotokana na tafiti za kimajaribio,<br />
unaoonesha kwamba programu zilizoongeza vitendea kazi vya shule kwa kiasi kikubwa hazikuleta matokeo<br />
yaliyotarajiwa katika ufanisi. Kwa mfano kuongeza vitabu na vifaa vya walimu kuandikia, havikusaidia kuongeza ubora<br />
wa uwezo wa wanafunzi, na kupunguza ukubwa wa darasa kwa kuongeza walimu vilevile hakukubadilisha matokeo.<br />
1110<br />
Hatua zilizoongeza viwango vya ufaulu wa wanafunzi shuleni ni zile zilizobadili vichocheo kwa walimu kwa namna<br />
inayoridhisha. Hatua ya kuwalipa walimu kwa kuhudhuria kazini au kwa maksi za mitihani walizopata wanafunzi wao<br />
zilionesha matokeo mchanganyiko, na utaratibu wa kuwapa wazazi taarifa kuhusu hali ya shule vilevile haikuwa na<br />
manufaa. Lakini, programu zilizowezesha shule kuajiri walimu zaidi kwa mikataba ya muda mfupi na zile zilizozipa<br />
kamati za shule mamlaka juu ya walimu zilifanikiwa kuongeza viwango vya ufaulu wa wanafunzi. Kujaribu mbinu hizi<br />
mpya, kwa kutumia utaratibu wa majaribio yanayosimamiwa vizuri, kunaweza kuwa njia mojawapo ya kuhamasisha<br />
kuimarisha ujifunzaji katika shule.<br />
Mbinu mojawapo kama hiyo, ambayo bado haijathibitishwa lakini mpango wake umeundwa kutokana na ushahidi<br />
kuhusu mbinu zinazoweza kuwa na matokeo yenye ufanisi, unaitwa malipo baada ya matokeo (Cash on Delivery) 1211 .<br />
Wazo kuu hapa ni kwamba badala ya kugharimia vitendea kazi, kuundwe mfumo ambao malipo yatatolewa<br />
kwa kufuata ufanisi katika viashiria vya matokeo vilivyoanishwa na kuthibitishwa, kwa mfano, dola 50 kwa kila<br />
mwanafunzi atakayemaliza Darasa la 2 akiwa amefaulu kwa asilimia 80 katika stadi za kusoma na kuhesabu. Mbinu hii<br />
awali ilibuniwa ili kuboresha ufanisi katika misaada iliyotolewa kwa serikali za kitaifa, lakini huenda mbinu hii ikawa<br />
na manufaa zaidi katika namna serikali za kitaifa zinavyounda vichocheo vyake ili kuboresha ufaulu katika ngazi za<br />
wilaya na shule.<br />
Kuna hali ya hatari katika ujifunzaji Kenya, Tanzania na Uganda. Serikali zinajivunia mafanikio yake katika kupanua<br />
uandikishaji wa wanafunzi. Lakini vilevile sasa zisijifiche nyuma ya mafanikio haya, ila badala yake ziweke malengo<br />
yake katika kuhakikisha kwamba watoto wanapokwenda shule wanajifunza. Ushahidi kutoka mapitio mbalimbali<br />
na tafiti za kimajaribio zilizofanywa kwa umakini, pamoja na data za Uwezo zilizowasilishwa katika ripoti hii<br />
zinabaini kwa kiasi kikubwa kwamba kuwekeza katika vitendea kazi pekee hakutoshi, na kwamba fikra mpya<br />
zinahitajika kuhusu suala la vichocheo 1312 . Mabilioni ya shilingi na masaa yanayotumiwa katika elimu ya msingi kila<br />
mwaka na wazazi, serikali na wafadhili yatakuwa yametumika vizuri iwapo watoto watajifunza, na kupata stadi<br />
katika kusoma na kuhesabu. Huu ni wakati wa kulikabili sakata hili ipasavyo, na kufikiri kuhusu suluhisho linalofaa<br />
ambalo si tu lina lengo jema, bali linaweza pia kuleta mabadiliko chanya.<br />
10<br />
“Improving Education in the Developing World: What have we Learned from Randomized Evaluations?” Michael Kremer na Alaka Holla,Novemba 10,2008.<br />
Inapatikana<br />
http://www.economics.harvard.edu/faculty/kremer/files/Annual_Review_081110%20-%20NO%20TRACK%20CHANGES.pdf.<br />
11<br />
Wazo hili lilibuniwa na Centre for Global Development, angalia katika<br />
http://www.cgdev.org/section/initiative/_active/codaid. For a comment on its strength and value in local application<br />
Angalia :http://blogs.cgdev.org/globaldevelopment/2011/04/guest-post-five-reason-i-am-a-fan-of-cash-on-delivery-and-five-ways-to-make-it-sharper.php<br />
12<br />
Mathalan, angalia http://siteresources.worldbank.org/EDUCATION/Resources/278200-1298568319076/makingschoolwork.pdf na thamani ya mbinu za kitafiti<br />
angalia Banerjee, A and Duflo, E, Poor Economics:A radical rethinking of the way to fight global poverty, Public Affairs,2011, sana katika sura ya 4.<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 25
Kiambatisho cha 1: Ngazi za Wilaya<br />
Jina la wilaya Viashiria vya uwezo wa wanafunzi Viashiria vya upatikanaji nyenzo shuleni<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Uandikishaji<br />
Nafasi ya<br />
ufaulu (*)<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa<br />
mwalimu<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa darasa<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa choo<br />
Nafasi ya<br />
shule (*)<br />
Adjumani 0% 93% 89% 107 66 57 47 78<br />
Amuria 2% 60% 93% 76 69 100 89 131<br />
Amuru 2% 67% 89% 112 70 117 76 130<br />
Apac 3% 80% 89% 94 69 97 65 119<br />
Babati 3% 58% 92% 78 58 58 42 72<br />
Budaka 3% 62% 91% 97 69 101 87 132<br />
Bukoba Vijijini 1% 39% 82% 130 64 78 47 90<br />
Bukoba Mjini 6% 36% 86% 117 36 73 62 71<br />
Buliisa 2% 84% 92% 66 67 173 112 134<br />
Bundibugyo 1% 49% 94% 98 65 83 108 124<br />
Bungoma Kaskazini 7% 78% 91% 48 42 61 31 51<br />
Bunyala 9% 83% 82% 79 43 68 37 55<br />
Buret 25% 85% 81% 46 34 96 81 92<br />
Bushenyi 4% 67% 91% 81 40 47 45 50<br />
Busia 9% 80% 95% 21 48 88 49 88<br />
Busia 2% 79% 87% 109 64 93 90 125<br />
Butere 11% 77% 91% 39 40 45 37 39<br />
Chunya 10% 55% 82% 115 56 73 50 83<br />
Eldoret Mashariki 26% 92% 93% 4 28 34 36 11<br />
Gatanga 38% 89% 94% 1 41 34 14 16<br />
Geita 6% 59% 81% 120 83 108 92 133<br />
Gucha 30% 95% 89% 8 43 57 40 54<br />
Gulu 0% 90% 93% 73 59 78 63 100<br />
Hamis 20% 84% 91% 17 37 39 53 45<br />
Ibanda 3% 66% 91% 91 42 52 54 60<br />
Igembe 11% 91% 89% 26 45 44 24 36<br />
Ijara 19% 94% 79% 44 41 50 154 82<br />
Ilemela 13% 68% 81% 105 87 140 107 135<br />
Iment Kusini 38% 85% 88% 18 25 29 23 1<br />
Imenti Kaskazini 36% 95% 89% 5 28 23 14 4<br />
Kabale 2% 56% 94% 75 41 53 59 61<br />
Kakamega Kati 14% 80% 88% 52 44 90 39 74<br />
Kakamega Kaskazini 14% 79% 79% 85 35 44 45 34<br />
Kaloleni 34% 95% 72% 31 60 59 104 109<br />
Kamuli 0% 74% 92% 95 66 86 110 127<br />
Karagwe 2% 24% 87% 128 65 78 53 99<br />
Kasulu 4% 18% 79% 129 90 77 67 116<br />
Katakwi 0% 88% 95% 64 63 89 84 121<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 26
Jina la wilaya Viashiria vya uwezo wa wanafunzi Viashiria vya upatikanaji nyenzo shuleni<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Uandikishaji<br />
Nafasi ya<br />
ufaulu (*)<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa<br />
mwalimu<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa darasa<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa choo<br />
Nafasi ya<br />
shule (*)<br />
Keiyo 24% 90% 83% 34 28 58 27 23<br />
Kericho 18% 94% 85% 32 28 35 30 6<br />
Kibaale 2% 82% 87% 113 65 107 70 123<br />
Kibaha 7% 35% 90% 102 37 53 58 56<br />
Kibwezi 21% 90% 91% 9 33 37 40 24<br />
Kikuyu 53% 87% 94% 3 35 31 25 8<br />
Kilifi 19% 96% 70% 42 57 59 68 91<br />
Kilombero 2% 43% 91% 106 55 81 80 112<br />
Kilosa 0% 36% 89% 124 53 85 68 108<br />
Kinondoni 6% 48% 92% 77 38 83 120 98<br />
Kisarawe 1% 46% 91% 114 45 41 29 38<br />
Kisii Kusini 14% 84% 84% 58 39 45 42 41<br />
Kisumu Magharibi 7% 81% 87% 72 35 38 59 46<br />
Kitui Kaskazini 19% 95% 91% 7 49 39 36 47<br />
Koibatek 16% 89% 86% 38 32 32 46 19<br />
Kongwa 4% 46% 91% 100 59 91 82 120<br />
Kotido 1% 14% 44% 134 92 92 52 115<br />
Kuria East 10% 83% 84% 70 52 51 66 81<br />
Kyenjojo 2% 78% 90% 93 64 78 65 107<br />
Kyuso 10% 92% 79% 63 36 36 49 31<br />
Lagdera 2% 69% 82% 118 64 38 65 76<br />
Laikipia Kaskazini 34% 79% 61% 62 38 161 35 65<br />
Lamu 18% 88% 91% 15 32 31 43 17<br />
Lari 17% 59% 93% 22 37 33 13 13<br />
Limuru 23% 66% 87% 50 42 41 78 68<br />
Liwale 0% 16% 79% 135 57 61 50 79<br />
Loitoktok 25% 82% 83% 51 50 46 34 52<br />
Makueni 15% 87% 90% 24 33 37 39 21<br />
Mandera Kati 12% 83% 74% 86 51 47 58 73<br />
Manga 27% 91% 89% 11 31 35 31 12<br />
Marakwet 17% 91% 87% 33 30 33 53 29<br />
Masaba 21% 82% 92% 13 31 38 33 15<br />
Masaka 7% 76% 92% 53 49 67 75 96<br />
Maswa 4% 33% 84% 125 54 61 79 97<br />
Mayuge 1% 61% 93% 87 64 99 100 128<br />
Mbeere 35% 94% 92% 2 27 28 17 2<br />
Mbeya Mjini 0% 50% 95% 99 40 46 51 53<br />
Mbulu 13% 68% 84% 101 45 62 68 85<br />
Meru Kusini 23% 95% 91% 6 28 25 17 3<br />
Misungwi 4% 34% 91% 108 65 68 53 94<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 27
Jina la wilaya Viashiria vya uwezo wa wanafunzi Viashiria vya upatikanaji nyenzo shuleni<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Uandikishaji<br />
Nafasi ya<br />
ufaulu (*)<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa<br />
mwalimu<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa darasa<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa choo<br />
Nafasi ya<br />
shule (*)<br />
Molo 14% 87% 90% 29 42 45 41 49<br />
Morogoro Vijijini 1% 25% 80% 133 48 67 66 89<br />
Morogoro Mjini 9% 32% 92% 82 49 72 78 101<br />
Moshi Vijijini 16% 54% 87% 92 30 49 33 25<br />
Moshi Mjini 27% 72% 89% 43 41 94 85 106<br />
Moyale 12% 89% 83% 59 56 48 69 86<br />
Mpanda 2% 40% 89% 119 44 90 68 103<br />
Mpwapwa 7% 48% 89% 103 65 87 53 104<br />
Mubende 2% 69% 91% 89 59 76 78 110<br />
Mukono 2% 69% 88% 111 43 65 68 84<br />
Muleba 1% 22% 84% 131 91 83 79 126<br />
Musoma Mjini 13% 52% 91% 68 48 86 66 102<br />
Mwala 14% 82% 93% 19 31 49 25 20<br />
Mwanga 1% 17% 89% 127 45 44 28 40<br />
Naivasha 41% 85% 86% 23 44 78 39 64<br />
Nakapiripirit 2% 90% 65% 123 85 78 55 111<br />
Nakasongoria 5% 78% 94% 49 42 55 55 63<br />
Nakuru Kaskazini 31% 88% 84% 27 36 42 21 22<br />
Nandi Kati 17% 87% 83% 54 33 63 39 44<br />
Nandi Mashariki 32% 91% 88% 14 28 48 37 26<br />
Nandi Kaskazini 37% 96% 85% 12 27 35 38 14<br />
Narok Kaskazini 28% 91% 74% 40 37 52 35 35<br />
Newala 2% 34% 91% 116 78 54 44 80<br />
Ngara 5% 38% 83% 122 69 76 79 118<br />
Njombe 6% 52% 87% 110 65 60 40 75<br />
Nyandarua Kaskazini 18% 79% 89% 35 35 33 17 7<br />
Nyeri Kusini 35% 93% 88% 10 33 28 14 5<br />
Pokot Kaskazini 37% 83% 47% 56 43 93 64 95<br />
Rachuonyo 9% 75% 88% 69 38 63 48 58<br />
Rakai 3% 65% 93% 71 45 69 72 93<br />
Rombo 20% 70% 91% 36 47 68 42 69<br />
Ruiru 27% 80% 84% 45 45 43 29 37<br />
Rukingiri 5% 76% 92% 60 70 80 64 113<br />
Samburu Kati 18% 66% 65% 96 34 35 45 28<br />
Samburu Kaskazini 8% 97% 69% 65 34 31 49 27<br />
SamburuMashariki 5% 95% 56% 88 35 38 57 43<br />
Shinyanga Vijijini 1% 27% 82% 132 71 76 82 122<br />
Singida Vijijini 1% 39% 88% 126 68 66 48 87<br />
Singida Mjini 4% 44% 84% 121 39 74 53 70<br />
Sotik 12% 85% 91% 25 35 57 60 57<br />
<strong>Je</strong> <strong>Watoto</strong> <strong>Wetu</strong> <strong>Wanajifunza</strong>? 28
Jina la wilaya Viashiria vya uwezo wa wanafunzi Viashiria vya upatikanaji nyenzo shuleni<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Ufaulu Darasa<br />
la 3<br />
Uandikishaji<br />
Nafasi ya<br />
ufaulu (*)<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa<br />
mwalimu<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa darasa<br />
Uwiano wa<br />
wanafunzi<br />
kwa choo<br />
Nafasi ya<br />
shule (*)<br />
Suba 24% 90% 85% 28 36 38 47 32<br />
Sumbawanga 11% 45% 92% 67 70 101 54 117<br />
Taita 31% 86% 89% 16 38 35 25 18<br />
TanaRiver 17% 92% 66% 57 41 40 70 62<br />
Tanga 6% 29% 93% 84 48 142 59 105<br />
Taveta 23% 88% 86% 30 46 45 59 66<br />
Tharaka 20% 76% 89% 37 29 29 39 9<br />
Thika Magharibi 19% 77% 88% 47 32 66 38 42<br />
Trans Mara 6% 81% 80% 104 41 83 53 77<br />
Trans Nzoia Mashariki 16% 91% 84% 41 37 57 30 33<br />
Urambo 4% 52% 92% 80 86 110 69 129<br />
Wajir Mashariki 7% 92% 84% 55 48 42 63 67<br />
Wajir Kaskazini 21% 69% 52% 83 43 34 51 48<br />
Wakiso 8% 76% 91% 61 40 58 51 59<br />
Wareng 20% 78% 75% 74 31 35 31 10<br />
West Pokot 24% 98% 84% 20 33 40 43 30<br />
Yumbe 0% 78% 92% 90 54 84 80 114<br />
Angalizo: Wilaya za Kenya ni buluu, wilaya za Uganda ni kijani, wilaya za Tanzania ni nyekundu<br />
(*) Faharasa hizi hizi mbili zimetengeneza kwa kujumlisha alama zinazoambatana na nafasi ya wilaya kwa kila kimoja ya viashiria<br />
vitatu vilivyozingatiwa, na kutengeneza faharasa nyingine inayoonesha nafasi ya jumla kuanzia ya chini kabisa hadi ya juu kabisa.<br />
Chanzo cha data: Uwezo<br />
Kuhesabu na Kusoma Katika Afika Mashariki 29
Serikali za Kenya, Uganda na Tanzania zinatekeleza sera za elimu ya msingi kwa wote kuwawezesha watoto<br />
wote kwenda shule na angalau wajue kusoma, kuandika na kufanya hesabu. Katika muongo uliopita nchi hizi<br />
zimeongeza sana bajeti zao za elimu na mafanikio makubwa yameonekana katika kuandikisha wanafunzi.<br />
Lakini wakati watoto wengi sasa wanakwenda shule, je wanajifunza?<br />
Uwezo ilifanya taftishi katika nchi hizi tatu, kwa kuwatembelea maelfu ya watoto majumbani kwao, na<br />
kuwapa majaribio ya kiwango cha darasa la pili kwa somo la Kiingereza, Kiswahili na Hisabati. <strong>Watoto</strong><br />
wengi sana walishindwa majaribio haya. Katika nchi zote tatu watoto walipata matokeo ya chini sana<br />
ikilinganishwa na kiwango kinachotarajiwa katika mitaala ya nchi zao. Katika mazoezi yote matatu watoto<br />
wa Kenya walikua juu wakifuatiwa na Uganda.<br />
Nini huchochea ujifunzaji? Taftishi ya Uwezo imegundua vitu vya kushangaza. Hali bora ya uchumi wa<br />
familia imeonekana kushabihiana na umahiri au werevu wa watoto katika stadi za msingi; watoto kutoka<br />
katika familia zenye hali nzuri walifanya vizuri zaidi. Jinsia ya mtoto haikuonekana kuwa na uhusiano na<br />
werevu wa mtoto. Matokeo toka shule binafsi yalileta sura mchanganyiko; zaidi ya kuongeza ufahamu wa<br />
lugha ya Kiingereza katika madarasa ya chini wanafunzi toka shule za binafsi hawakuonesha tofauti kubwa<br />
ya umahiri katika stadi za msingi. Kwa watunga sera matokeo muhimu zaidi ni kuwa uwekezaji katika<br />
miundombinu na uwiano wa mwalimu na wanafunzi si muarobaini wa kuboresha ufahamu wa wanafunzi.<br />
<strong>Watoto</strong> toka maeneo yenye shule zenye majengo bora hawakufanya vizuri kupindukia kuwazidi wale<br />
wanaosoma shule zenye miundombinu hafifu ama waliorundikana madarasani. Hivyo basi, wazazi, serikali<br />
na wahisani wanaweza tu kujiridhisha kuwa mabilioni ya shilingi wanazowekeza kila mwaka kwenye sekta ya<br />
elimu yametumika vizuri iwapo watoto wakimaliza shule wataingia kutika dunia yenye ushindani wakiwa na<br />
ufahamu wa kiwango cha juu wa kusoma, wakijua Hisabati na wakijiamini.<br />
Uwezo Uwezo Afrika East Africa Mashariki (managed (ikisimamiwa by Twaweza) na Twaweza)<br />
S.L.P. P.O Box 19875, 19875, 00200 00200 Nairobi, Nairobi, Kenya Kenya<br />
Simu: Tel: +254 20 3861372<br />
Baruapepe: Email: info@uwezo.net. Web: Tovuti: www.uwezo.net<br />
Twaweza Afrika East Africa Mashariki<br />
127 Mtaa Mafinga wa Mafinga, Rd, Off Kando Kinondoni ya barabara Rd ya Kinondoni<br />
S.L.P. P.O Box 38342, 38342, Dar es Dar Salaam, es Salaam, Tanzania. Tanzania<br />
Simu: Tel: +255 22 266 4301. Nukushi: Fax +255 +255 22 266 22 266 43084308.<br />
Barua Email: pepe: info@twaweza.org. Web: Tovuti: www.twaweza.org<br />
Barua Email: pepe: info@uwazi.org. Web: Tovuti: www.uwazi.org