SEHEMU YA SITA 49

amani na utulivu bungeni amani na utulivu bungeni

parliament.go.tz
from parliament.go.tz More from this publisher
30.08.2015 Views

. SEHEMU YA SITA AMANI NA UTULIVU BUNGENI 72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote la utaratibu utakuwa ni wa mwisho. (2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na vilevile Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na kumfahamisha Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika kufanya hivyo, atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka utaratibu uliokiukwa. Mamlaka ya Spika kusimamia utaratibu 49

.<br />

<strong>SEHEMU</strong> <strong>YA</strong> <strong>SITA</strong><br />

AMANI NA UTULIVU BUNGENI<br />

72.-(1) Spika atakuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa, utaratibu<br />

bora unafuatwa Bungeni, na uamuzi wa Spika kuhusu jambo lolote<br />

la utaratibu utakuwa ni wa mwisho.<br />

(2) Mbunge atakayekiuka utaratibu uliowekwa na Kanuni hizi<br />

anaweza papo hapo kutakiwa na Spika afuate utaratibu na vilevile<br />

Mbunge mwingine yeyote anaweza kusimama na kumfahamisha<br />

Spika kuhusu ukiukwaji wa utaratibu huo na katika kufanya hivyo,<br />

atalazimika kutaja Kanuni ya Bunge iliyoweka utaratibu uliokiukwa.<br />

Mamlaka<br />

ya<br />

Spika<br />

kusimamia<br />

utaratibu<br />

<strong>49</strong>


(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa jambo<br />

au suala alilolisema Bungeni na hadi kufikia mwisho wa muda<br />

aliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika<br />

anaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bunge<br />

visivyozidi vitano.<br />

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi<br />

kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika<br />

atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka<br />

ya Bunge kwa mujibu wa masharti ya Kanuni ya 71 ya Kanuni hizi ili<br />

Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu hatua za kinidhamu zinazostahili<br />

kuchukuliwa dhidi ya Mbunge huyo.<br />

Adhabu<br />

zinazoweza<br />

kutolewa<br />

na<br />

Spika<br />

kwa<br />

ukiukaji<br />

wa<br />

Kanuni<br />

73.-(1) Mbunge au Waziri atakayezungumzia jambo au mambo<br />

ambayo hayaruhusiwi na Kanuni hizi, anaweza kuamriwa na Spika<br />

au Naibu Spika au Mwenyekiti akatishe hotuba yake na kukaa mahali<br />

pake.<br />

(2) Endapo Mbunge au Waziri atatumia maneno au lugha<br />

isiyotakiwa Bungeni, yaani lugha ya matusi, usafihi, uchokozi au<br />

lugha ya maudhi na akitakiwa na Spika ajirekebishe kwa kufuta<br />

maneno au lugha hiyo atakataa kufanya hivyo, Spika anaweza<br />

kumwamuru Mbunge huyo atoke mara moja nje ya Ukumbi wa<br />

Bunge na abaki huko nje kwa muda wote uliosalia wa kikao cha<br />

siku hiyo.<br />

(3) Endapo Mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa<br />

maneno aliyoyasema na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa,<br />

amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza<br />

kumsimamisha Mbunge huyo asihudhurie vikao vya Bunge<br />

visivyozidi vitano.<br />

(4) Endapo Mbunge atafanya kosa ambalo alikwishawahi<br />

kuadhibiwa kwa mujibu wa fasili ya (2) na (3) ya Kanuni hii, Spika<br />

atalipeleka suala lake kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka<br />

ya Bunge ili Kamati hiyo ilishauri Bunge kuhusu adhabu inayostahili<br />

kutolewa kwa Mbunge mhusika.<br />

Adhabu<br />

zinazoweza<br />

kutolewa<br />

na<br />

Bunge<br />

kwa<br />

ukiukaji<br />

wa<br />

Kanuni<br />

74.-(1) Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau<br />

Mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye Kamati ya<br />

Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge ikiwa:-<br />

(a)<br />

kwa maneno au vitendo, Mbunge huyo<br />

anaonesha dharau kwa mamlaka ya Spika; au<br />

50


(b)<br />

Mbunge huyo atafanya kitendo chochote cha<br />

makusudi cha kudharau Shughuli ya Bunge au<br />

Mbunge yeyote anayeongoza shughuli hiyo.<br />

(2) Ikiwa maneno au vitendo vya Mbunge vilivyoainishwa katika<br />

fasili ya (1) ya Kanuni hii vimetokea wakati Bunge likiwa katika<br />

Kamati ya Bunge Zima, basi Mwenyekiti atasimamisha shughuli za<br />

Kamati na ataagiza Bunge kurudia ili kumpatia Spika fursa ya kutoa<br />

taarifa kwa Bunge kuhusu mwenendo wa Mbunge huyo na<br />

kuwasilisha suala hilo kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka<br />

ya Bunge.<br />

(3) Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge itajadili suala<br />

hilo na ikithibitika kuwa Mbunge husika ametenda kosa inaweza<br />

kushauri kwamba:-<br />

(a)<br />

(b)<br />

ikiwa ni kosa lake la kwanza Mbunge huyo<br />

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi kumi; au<br />

ikiwa ni kosa lake la pili au zaidi Mbunge huyo<br />

asihudhurie vikao vya Bunge visivyozidi ishirini;<br />

(4) Bunge linaweza kuzingatia ushauri mwingine wowote<br />

utakaotolewa na Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge<br />

kuhusu adhabu anayostahili kupewa Mbunge aliyekiuka masharti<br />

ya Kanuni hii.<br />

(5) Bila ya kujali masharti ya fasili ya (4) ya Kanuni hii, Bunge linaweza<br />

kumchukulia hatua nyinginezo za kinidhamu, ikiwa ni pamoja na<br />

kumsimamisha kazi Mbunge yeyote aliyetenda kosa chini ya Kanuni<br />

hii.<br />

(6) Adhabu yoyote itakayotolewa kwa Mbunge aliyekiuka masharti<br />

ya Kanuni hii itatolewa kupitia Azimio la Bunge ambalo litataja<br />

adhabu hiyo pamoja na sababu zake.<br />

75.- Mbunge aliyesimamishwa kazi atatoka katika Bunge na<br />

hataingia tena katika sehemu yoyote ya Ukumbi wa Bunge na<br />

maeneo ya Bunge kwa muda wote atakapokuwa amesimamishwa,<br />

na atalipwa nusu mshahara na nusu posho zinazoambatana na<br />

mshahara huo.<br />

76.-(1) Kwa madhumuni ya kudhibiti fujo endapo itatokea ndani ya<br />

Ukumbi wa Bunge na Spika ataona kuwa kuna haja ya kutumia<br />

51<br />

Masharti<br />

kwa<br />

Mbunge<br />

aliyesimamishwa<br />

kazi<br />

Udhibiti<br />

wa fujo<br />

Bungeni


nguvu, basi anaweza kuahirisha Shughuli za Bunge bila ya hoja<br />

yoyote kutolewa au kusitisha kikao kwa muda atakaoutaja ili fujo<br />

hiyo iweze kudhibitiwa na Mpambe wa Bunge.<br />

(2) Baada ya utulivu kurudia, Spika atalipeleka kwenye Kamati ya<br />

Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge suala ambalo lilisababisha<br />

kutokea kwa fujo ikiwa ni pamoja na jina la Mbunge au majina ya<br />

Wabunge waliohusika na fujo hiyo ili Kamati hiyo iweze kulishauri<br />

Bunge kuhusu adhabu inayostahili kutolewa.<br />

52

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!