12.07.2015 Views

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

constitution of kenya review commission (ckrc ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

93Vitalis Wamalwa: Naitwa Vitalis Wamalwa. Ningependa kuongea matatu hivi. Jambo la kwanza, ni wasted knowledge.Wasted knowledge, pengine ningependa kuguzia ya kwamba kuna watu wengi wakubwa wamesoma kabisa, wako skilled invarious fields, lakini kwa sababu ya hii mambo ya retirement, wanaenda retirement na sisi tunaendelea kusumbuka. Tena,kulingana na hayo maneno, unaona ni mtoto wa shangazi, au wa nyanya analetwa pale. Ningependekeza kwamba, hawa watuwamesoma sana, hata kama miaka yao imeisha na wame-retire wameenda nyumbani, wangekuwa kwa advising committeeswawe wakiwa consulted everytime, wakija kuona maneno yako namna gani. Kwa mfano, sijui kama itawezekana- lakini kamamzee akienda nyumbani, ni vizuri aje ashauri watu---Interjection. Com. Bishop Njoroge: ----------(inaudible)Vitalis Wamalwa: Pointi nyingine ni kwa upande wa miwa. Hasa sisi wakulima tungependa tujue utaratibu wa miwa. Kwamfano, miwa inapokatwa kutoka shambani, ikibebwa kilometer fulani unalipa kiasi fulani. Ikifika weigh bridge wakipima tonesfulani, hujui wanalipa pesa ngapi. Kutoka hapo inapoingia ndani, vitu vyote vinakatwa tujue kama ni stake wamekuletea, stakemoja ya kupanda ina-cost pesa ngapi- ili, mkulima awe ukijua umebeba stake ngapi unajua ulikatwa pesa kiasi fulani kwasababu hapa Nzoia, miwa inaenda huko na wanakuambia walikupa stake tano na kumbe walikupa stake moja ya kupanda.Sasa tunataka waki-supply hiyo seed, we sign somewhere, tujue tuli-receive hii, tukienda huko tunajitetea. Kwa sababu hataunaweza shikanisha wewe na jirani yako ako huko, wanasema “enda uchukuwe huko mbegu”. Wanamwaga mara tatu watuwanaenda usiku wanabeba lakini wanaku-charge. Sasa hiyo tunaona ni hasara.Way <strong>of</strong> worship: mimi ningependa serikali pia kama wameruhusu kila mtu ashiriki kwa kanisa lake anapenda, lakini pia Serikaliingeteua kamati wafuate njia vile watu wanaomba. Sisi tunaona wakubwa wetu haswa, wamejenga makanisa especially ileinaitwa Free Masons, inaingiwa makubwa makubwa kama makubwa kama haya yamesimama hapa. Tunasikia wanaenda kwamgongo- na hao ni wakubwa. Sasa tunashindwa watasema namna gani. Wakati ule unaenda kusema huko, unawekwa ndaniya gari kwa boot. Utashtukia uko kwa nyumba yenye hakuna mlango. Sasa tunaomba serikali ichunguze vile watu wanaendakuomba, wafuate utaratibu. Kwa mfano, tuseme mimi ni Mkatoliki, waende waone hawa watu wanaeneza neno la Mungu auwanaeneza maneno ya shetani.Com. Bishop Njoroge: Tumepata hiyo.Vitalis Wamalwa: La mwisho, ningependa kuona- sijui serikali itatumia mbinu gani- mwenzagu ameguzia maneno ya askari.Kwa sababu, mambo ya TKK wamesema yamekwisha lakini ukienda kama gari imejaa. Tungependa utaratibu uwe kama waUganda. Kama Nissan tunajua inachukua watu kumi na wawili na inaenda, tungependa ichukue watu exactly. Sijui wata-effectnamna gani kwa sababu bado haya mambo ya kujaza kwa barabara yako na accidents bado zinatokea lakini kwa sababuutakuwa na kijisanduku cha kiberiti uweke kitu ndani utupe chini mzee achukue, wewe utaenda lakini accident itakuwa mbele.Asante.

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!