verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
72 hiyo. Ningependekeza, hawa wazee wapatiwe kaputi na serikali, na wapatiwe kofia. Wakati mwingine, mzee anapiga bibi yake usiku, na huyu mzee anaitwa. Anaenda na baridi, saa zingine anaenda na mvua, na anaamua hiyo kesi, na hiyo kesi inakuwa safi sana, asubuhi tunapewa ma report, tunaambiwa huyu mzee alienda nyumba fulani na alisuluhisha tatizo fulani na hilo tatizo sasa limekwisha. Mimi ningesema, wale watu wanasema Provincial administration iondoke, labda hawaoni vile tumekaa. Katika nchi za ulaya, hao watu wameweka kila nyumba kuandika wakili. Kila nyumba ina advocate wake. Hapa umasikini hautuwezeshi kila mtu kuwa na wakili wake. Na ndio mnaona serikali imetia assistant chief, imetia chief, imetia D.O. ili wawe wakisaidia watu kule mashambani. Ningependa, provincial administration, - na sio kusema kwa sababu mimi ni chief, mimi ninaondoka,- lakini kwa maoni yangu naona provincial administration inafanya kazi kubwa sana kwa sababu Kenya yetu ina umasikini mwingi, na hatuwezi kujiandikia mawakili wa kututetea huko makotini. Kesi zingine ni kesi ndogo sana na kuandika mawakili ni kupoteza wakati. Kile kingine ningesema ni umasikini. Mtu asiende jela kwa sababu yeye ni masikini. Katika sheri zetu za Kenya, -huko kotini, - unakuta jaji anakuambia utoe shilingi elfu moja, unafainiwa shilingi elfu moja, na ukikosa utafungwa miezi mitatu? Tajiri anatoa elfu moja, masikini anakosa elfu moja, kwa hivyo, masikini atafungwa kwa kukosa shilingi elfu moja. Na amefungwa kwa sababu ya makosa au kwa sababu ya umasikini? Answer from the audience: umasikini Stanley wa Wanyeki: Mtu asifungwe kwa sababu ya umasikini, afungwe kwa sababu amefanya jambo. Tunataka, ikiwa ni kufungwa, tajiri afungwe na masikini afungwe. Ikiwa ni pesa tajiri apigwe fine na masikini apigwe fine. Masikini akikosa fine, arudi… (Interjection – by Com. Wanjiku). Inaudible. Stanley wa Wanyeki: Aa hiyo nimewacha. Ile ingine ningesema, zile kesi ambazo zinaenda kotini, ningesema mimi isizidi miezi mitatu. Ikizidi miezi mitatu, iondolewe kotini halafu itupiliwe mbali. Kwa sababu watu wanasema “Justice delayed is justice denied.” Kesi ifanywe haraka iwezekanavyo. Hapa unaweza kuona kuna makesi ya miaka miwili, mitatu hata miaka kumi. Na vile kesi inakaa ndio inakula pesa za wananchi. Ma judge wafanye kesi haraka iwezekanavyo, na kama si hivyo hiyo kesi itupiliwe mbali. Kwa sababu ikikaa sana, inasumbua watu. La mwisho, mimi nasema juu ya elimu. Mtoto, - kama vile wengine wamesema, - mtoto asikose elimu kwa sababu ni masikini. Ikiwa wa tajiri ataenda shule, hata wa masikini ijulikane ataenda namna gani. Ikiwa ni magonjwa, mtu asife kwa sababu ni masikini. Free medical treatment kwa wote.
73 Ya mwisho, mimi ningeuliza barabarani. Kuna vifo vingi barabarani. Na vifo hivi vinasababishwa na madereva ambao pengine ni wanyuaji wa madawa za kulevya, na mimi, ningependa, in every three months, madereva wawe wakifanyiwa kitu kinaitwa medical examination. Mabarabara yetu (inaudible). Watu wamekufa kwa mabarabara zetu hata kuliko reli. Kwa hivyo ningependa madereva wetu wa P.S.V. wale wako na P.S.V. barua ya kubeba watu, ambao wana barua ya kubeba watu, - in every three months – wengine wanakuwa vichaa, wengine wanakunywa dawa za kulevya na nini… wawe wakifanyiwa medical examination. Mimi la mwisho ningesema, hatuwezi kubadilisha Katiba sisi watu wa Kenya ikiwa sisi hatujajibadilisha sisi wenyewe. Katiba ni namna hiyo. (Clapping) Tabia zetu lazima tuzibadilishe. Mimi nimesema na nimeuliza, kila mtu awe mtu wa kulinda Katiba. Unaona kwa magari wananchi wamebebwa na matatu na wamejaa. Na badala ya kusema hii ni makosa, wanamwambia turn boy, kwenda pelekea huyo polisi pesa sisi tuendelee na safari yetu. Ni lazima tujibadilishe kabla hatujabadilisha Katiba yetu. Ahsante sana. Com. Wanjiku: Okay, ahsante sana bwana chief, thank you very much. Now this gentleman just has a message, todo… memorandum ya kwogu urida urecommendate as the person who presented it niukothoma uuge ritwa riaku ushoke uuge point imwe iria (inaudible) Speaker: Ahsante sana madam Commissioner na wanaomsaidia… (Interjection) Com. Wanjiku: Tafadhali sema jina lako. Speaker: My name is Geofrey Kahotho. Tulikuwa na swali na tukatoka, lakini kuna swali moja ama mbili na sitaweka. Na hiyo tunafikiria wakati tunaandika Katiba, hilo swala ni muhimu sana, kwa sababu hiyo Katiba ndio tunataka iwekwe itekeleze ile mambo ambayo tunataka sisi wananchi kutoka pale tuliko. Geofrey: Sasa lile swala ningezungumzia sana ni ile ya environment ama mazingira. Ingekuwa vizuri sana wale watu wako kwa mtaa fulani wapatiwe nguvu ya kulinda mazingara na kufaidika zaidi na hii mazingara, kwa sababu uchumi ndio ngumu sana. Na hii Katiba na hata ile itaendelea, haistahili kuchagua kwa sababu ya kuendeleza uchumi ama economy. Sasa sisi tumeonelea ya kwamba, kama watu wa hapa Kinangop, tuko na shida moja. Yale mapato tunapata hapa, yote yanaenda kwa serikali kuu from the local government. Tunalipa ushuru, levy, (inaudible), na hii mambo yote inaenda kwa central government. Ndiposa
- Page 21 and 22: 21 (Translation is done in Kikuyu).
- Page 23 and 24: 23 Haya, ile jambo lingine nilikuwa
- Page 25 and 26: 25 Com. Wambua: Okay, twendelee sas
- Page 27 and 28: 27 Administration: ………… (Co
- Page 29 and 30: 29 come up with conclusive ideas. F
- Page 31 and 32: 31 Com. Wanjiku: Thank you very muc
- Page 33 and 34: 33 chake. Nafikiria nitafikia hapo,
- Page 35 and 36: 35 maruna matari miga noria magerer
- Page 37 and 38: 37 Then we come to Judiciary: ♦ J
- Page 39 and 40: 39 kulingana na vile tunataka,- zet
- Page 41 and 42: 41 David Macharia: I think what the
- Page 43 and 44: 43 there-Thomano Kiaire, Martha Nya
- Page 45 and 46: 45 Interjection from Com. Wanjiku:
- Page 47 and 48: 47 naona. Lakini nyinyi wenyewe mfi
- Page 49 and 50: 49 Interjection. Com. Wanjiku: tafa
- Page 51 and 52: 51 walichaguliwa ma- D.O na ma-Chie
- Page 53 and 54: 53 But they were not, - it was not
- Page 55 and 56: 55 credible, people with good integ
- Page 57 and 58: 57 Corruption nio niyagerero kunino
- Page 59 and 60: 59 Kwa kuhesabu, (inaudible) hapa n
- Page 61 and 62: 61 Chairman to be elected by the ma
- Page 63 and 64: 63 Another speaker: (repitation. It
- Page 65 and 66: 65 Kama anasaidiwa nanjia mzuri…
- Page 67 and 68: 67 wanalingana na serikali. Sio ati
- Page 69 and 70: 69 Councilor: Karibu sana… karibu
- Page 71: 71 be disciplined because of bad be
- Page 75: 75 Meeting ended at 5.30 p.m. &&&&&
72<br />
hiyo. Ningependekeza, hawa wazee wapatiwe kaputi na serikali, na wapatiwe k<strong>of</strong>ia.<br />
Wakati mwingine, mzee anapiga bibi yake usiku, na huyu mzee anaitwa. Anaenda na baridi, saa zingine anaenda na mvua, na<br />
anaamua hiyo kesi, na hiyo kesi inakuwa safi sana, asubuhi tunapewa ma <strong>report</strong>, tunaambiwa huyu mzee alienda nyumba fulani<br />
na alisuluhisha tatizo fulani na hilo tatizo sasa limekwisha. Mimi ningesema, wale watu wanasema Provincial administration<br />
iondoke, labda hawaoni vile tumekaa. Katika nchi za ulaya, hao watu wameweka kila nyumba kuandika wakili. Kila nyumba<br />
ina advocate wake. Hapa umasikini hautuwezeshi kila mtu kuwa na wakili wake. Na ndio mnaona serikali imetia assistant chief,<br />
imetia chief, imetia D.O. ili wawe wakisaidia watu kule mashambani. Ningependa, provincial administration, - na sio kusema<br />
kwa sababu mimi ni chief, mimi ninaondoka,- lakini kwa maoni yangu naona provincial administration inafanya kazi kubwa sana<br />
kwa sababu Kenya yetu ina umasikini mwingi, na hatuwezi kujiandikia mawakili wa kututetea huko makotini. Kesi zingine ni<br />
kesi ndogo sana na kuandika mawakili ni kupoteza wakati.<br />
Kile kingine ningesema ni umasikini. Mtu asiende jela kwa sababu yeye ni masikini. Katika sheri zetu za Kenya, -huko kotini, -<br />
unakuta jaji anakuambia utoe shilingi elfu moja, unafainiwa shilingi elfu moja, na ukikosa utafungwa miezi mitatu? Tajiri anatoa<br />
elfu moja, masikini anakosa elfu moja, kwa hivyo, masikini atafungwa kwa kukosa shilingi elfu moja. Na amefungwa kwa<br />
sababu ya makosa au kwa sababu ya umasikini?<br />
Answer from the audience: umasikini<br />
Stanley wa Wanyeki: Mtu asifungwe kwa sababu ya umasikini, afungwe kwa sababu amefanya jambo. Tunataka, ikiwa ni<br />
kufungwa, tajiri afungwe na masikini afungwe. Ikiwa ni pesa tajiri apigwe fine na masikini apigwe fine. Masikini akikosa fine,<br />
arudi…<br />
(Interjection – by Com. Wanjiku). Inaudible.<br />
Stanley wa Wanyeki: Aa hiyo nimewacha. Ile ingine ningesema, zile kesi ambazo zinaenda kotini, ningesema mimi isizidi miezi<br />
mitatu. Ikizidi miezi mitatu, iondolewe kotini halafu itupiliwe mbali. Kwa sababu watu wanasema “Justice delayed is justice<br />
denied.” Kesi ifanywe haraka iwezekanavyo. Hapa unaweza kuona kuna makesi ya miaka miwili, mitatu hata miaka kumi. Na<br />
vile kesi inakaa ndio inakula pesa za wananchi. Ma judge wafanye kesi haraka iwezekanavyo, na kama si hivyo hiyo kesi<br />
itupiliwe mbali. Kwa sababu ikikaa sana, inasumbua watu.<br />
La mwisho, mimi nasema juu ya elimu. Mtoto, - kama vile wengine wamesema, - mtoto asikose elimu kwa sababu ni masikini.<br />
Ikiwa wa tajiri ataenda shule, hata wa masikini ijulikane ataenda namna gani. Ikiwa ni magonjwa, mtu asife kwa sababu ni<br />
masikini. Free medical treatment kwa wote.