verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
Create successful ePaper yourself
Turn your PDF publications into a flip-book with our unique Google optimized e-Paper software.
47<br />
naona. Lakini nyinyi wenyewe mfikirie, siku moja itafika, wewe mama wewe baba, watoto wako watakuuliza swali,<br />
tulitengeneza tukatoa maoni yetu, kwa nini nchi yetu imetupitishia kwa ule moto tu, na zile shida zilikuwa hapo mbeleni. Hiyo<br />
nimewatuma, mjaribu muone vile mambo yanayotolewa, ni ya kutawala nchi hii yetu bila ubaguzi na bila chochote cha<br />
mapendeleo. Basi wacha niende kwa mambo yangu.<br />
Jambo la kwanza ni mambo ya shida ya kuajiriwa kazi, ama lack <strong>of</strong> employment. Na ningesema kwa kifupi hivi, niseme kwa<br />
kifupi badala ya tafsiri, itakuwa muda mrefu. (Speaks in Kikuyu),……………. Ukabila na undugu, na nyinyi ndio mko katika<br />
pale top. Wale watoto wa masikini hawapati kazi, si ni kweli? Wale watoto wa matajiri wanachukuliwa mbele, hata kama<br />
hawajahitimu mtihani sawa, sawa, anaendesha hiyo <strong>of</strong>isi kubwa, kwa sababu baba yake ama mama yake ana uwezo. Ama<br />
ndugu zake ama dada zake wana uwezo. Tunaomba sasa kwa Katiba mpya, muone kwamba hiyo imeondolewa, kusiwe na<br />
ubaguzi kwa mtu yeyote, kazi ziajiriwe watu kulingana na vile wamepita. Wale hawajapita sawasawa watafutiwe mambo<br />
mengine na serikali. Iwekwe katika Katiba.<br />
Shida ya wale ambao wamesoma na wameacha masomo,- yaani school leavers.- Mapendekezo yangu ni hivi: wawe registered<br />
na serikali, kama tu wangekuwa wameandikwa, kutoka standard seven ama eight, form four na university. Na wapewe kazi,<br />
ama training kulingana na vile wamepita. Wale wamepita vizuri hata kama ni mtoto wa masikini, ama kama ni mtu kiwete,<br />
apewe ile <strong>of</strong>isi inalingana na yeye. Hiyo ndiyo maombi yangu. Yule anayebaki, kuna kazi ya polisi, kazi ya askari, kazi ya<br />
labour, apatiwe huko, na uwe ni mzigo wa serikali maanake tumesema tumeomba masomo ya bure, kwa nini tupoteze wale<br />
watoto wengine? Na zaidi wale wa masikini? Tunajua kweli, tukiulizwa maswali mengi, watoto wa masikini ni werevu, na<br />
wengine wana akili sana na wanatupiliwa mbali, kwa sababu hawajulikani popote, tunaomba hiyo.<br />
Wakiwa wanachukuliwa kwa register, tuondoe mzigo kutoka kwa wazazi wa watoto. Wakiwa wamemaliza masomo, ni wa<br />
serikali. Mnaelewa vile ninasema? Huu mzigo wa mzazi mwingine ambaye hana elimu, asije akashughulike, nilitaka kumuuliza<br />
nani; – M.P. wetu ni nani nishikilie atanisaidia ama ni ndugu yangu, - awe ni mtoto wa serikali. Apatiwe kazi kulingana na vile<br />
alivyo. Kazi ni nyingi ya kupatia. Na asipotosheka kwenda university aende training, na asipotosheka training, aende kwa kazi<br />
nyingine yeyote ambayo haihitaji watu wa masomo. Lakini kwa wakati huu tunajua, kuna ubaguzi.<br />
Sitaendelea kujifafanua sana. Wacha nimalize hapo.<br />
Mambo ingine, nimesema awe mzigo wa serikali. Ningependa muandike, mmeandika?<br />
Interjection – laughter from the crowd.<br />
Jambo lingine langu ni hili, nimezipeleka haraka sana. Ni mambo ya electon: Imezungumzwa sana. Ili tumalize mambo haya ya<br />
wizi wa kura, Ningewaomba nyinyi Commissioners,- mimi huona ya kwamba, kutoka,- from now onwards, kwa ile election<br />
inakuja karibu, tunafanya polling station hapa kama Njabini kwa hii <strong>of</strong>isi. Zihesabiwe hapo, na agent wa yule mtu wa parliament,