verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet
You also want an ePaper? Increase the reach of your titles
YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.
32<br />
La pili, ni kuhusu umaskini: Ningependekeza kwamba, tuwe na sheria kwamba, watu ambao ni maskini watengewe angalau hata<br />
kama ni mshahara kwa kila mwezi, wawe wakipewa pesa kila mwezi ya kuweza kuendeleza mahitaji yao ya mara kwa mara.<br />
Kama nchi nyingi tunazo ambazo zinagharimia watu ambao hawajiwezi, ambao sisi hapa tunaita masikini. Wanaangalia masilahi<br />
yao kwa kuwapa at least kila mwezi, kiwango fulani cha pesa ambazo zinaweza kufanya huyu mtu ajiendeleze katika maisha<br />
yake ya kawaida.<br />
Jambo la tatu ni kuhusu mashamba. Watu wengi wameongea kuhusu mashamba hapa, na ni jambo ambalo linagusia kila<br />
Mkenya. Kuna mashamba mengi sana ambayo yanakaa bure; watu wamesema kwamba kuna wanyama ambao wakaa hapo.<br />
Ndio, sio vibaya. Wanyama wanatuletea pesa kupitia kwa watalii, lakini kuna wengine ambao wana mashamba makubwa na ni<br />
mtu mmoja pekee yake. Mimi ningependekeza kwamba, Commission hii irecord chini kwamba, Mkenya yeyote ambaye hana<br />
shamba, ama wale ambao wanaitwa squtters, angalau serikali iangalie na iwape kila mtu acre mbili mbili, ili tusije tukawa na<br />
squatters. Miaka arobaini tukijitawala, ni vibaya sana kuwa bado na jambo la squatters.<br />
La nne ni kuhusu trespass. Hili neno trespass lilikuwa wakati wa ukoloni, na mkoloni alileta neno trespass kwa sababu hakutaka<br />
uingie mahali pake wewe mtu mweusi. Lakini sasa saa hii sisi watu weusi wenyewe ndio tunajitawala, neno ‘trespass’<br />
liondolewe kabisa katika Katiba ya Kenya. Mkenya awe huru, anaweza kuingia mahali popote na ahudumiwe. Ukienda mahali<br />
pengine, kama vile reli, kule ukienda pale ndani ya reli, utaambiwa kwamba umekanyaga reli. Na hata ukikanyaga hiyo reli ni<br />
chuma, haiumii lakini utaenda kushtakiwa. Kwa hivyo hiyo maneno ya trespass iondolewe, kila Mkenya awe huru kutembea<br />
mahali popote.<br />
La tano ni kuhusu elimu- education: Ni hivi tu mwaka huu tulitangaziwa na Rais wetu ya kwamba Primary education iwe free,<br />
lakini sisi wazazi bado tunalipa. Ingekuwa bora iwe kwa Katiba kwamba,- na itiliwe maanani- kwamba elimu ya kutokea<br />
standard one mpaka standard eight iwe ni free, na iwe ni free. Sio eti kwamba tunaambiwa ni bure, na hali sisi wazazi huku<br />
tunaambiwa tutoe shilingi mia tano. Hiyo sio bure. Kwa hivyo iwe ni elimu ya bure, vile tulikuwa tukisoma tu zamani. Zamani sisi<br />
tuliposoma, hakuna siku tuliambiwa kwamba utanunua ruler, utanunua vitabu, hivyo vitu ulikuwa ukivipata darasani, mpaka<br />
rubber unapata. Lakini siku hizi tunaambiwa elimu ni ya bure, lakini mtoto kesho anakuja anakwambia kwamba baba,<br />
nimefukuzwa school fees, unashindwa hii school fees mnasema ni ya bure, inatokea wapi. Tafadhali elimu kama ni ya bure, iwe<br />
ndani ya Katiba ni ya bure.<br />
Jambo la sita,- na nitamalizia hapo-, ni kuhusu vyama vya upinzani. Mimi ninapendekeza kwamba tuwe na vyama vya upinzani<br />
vitatu vyenye nguvu. Vitatu pekee yake vyenye nguvu. Hivi vyama vingine vyote vifagiliwe viwekwe kando. Na hivi vyama<br />
vitatu, serikali iwe ikivigharimia tukienda kwa uchaguzi. Na hiyo pia, tukiwa na vyama vichache kama hivyo, tutapoteza ile neno<br />
ambalo kila wakati tunaimbiwa: “ukabila”. Kwa sababu tukiwa na vyama vitatu, tutajumuisha makibila arobaini na mbili yote ya<br />
Kenya na ambapo neno ‘ukabila’ litapotea. Ukabila unatokea kwa sababu, vyama ni vingi na kila kabila kitakuwa na chama