04.11.2014 Views

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

verbatim report of constituency public hearings ... - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

32<br />

La pili, ni kuhusu umaskini: Ningependekeza kwamba, tuwe na sheria kwamba, watu ambao ni maskini watengewe angalau hata<br />

kama ni mshahara kwa kila mwezi, wawe wakipewa pesa kila mwezi ya kuweza kuendeleza mahitaji yao ya mara kwa mara.<br />

Kama nchi nyingi tunazo ambazo zinagharimia watu ambao hawajiwezi, ambao sisi hapa tunaita masikini. Wanaangalia masilahi<br />

yao kwa kuwapa at least kila mwezi, kiwango fulani cha pesa ambazo zinaweza kufanya huyu mtu ajiendeleze katika maisha<br />

yake ya kawaida.<br />

Jambo la tatu ni kuhusu mashamba. Watu wengi wameongea kuhusu mashamba hapa, na ni jambo ambalo linagusia kila<br />

Mkenya. Kuna mashamba mengi sana ambayo yanakaa bure; watu wamesema kwamba kuna wanyama ambao wakaa hapo.<br />

Ndio, sio vibaya. Wanyama wanatuletea pesa kupitia kwa watalii, lakini kuna wengine ambao wana mashamba makubwa na ni<br />

mtu mmoja pekee yake. Mimi ningependekeza kwamba, Commission hii irecord chini kwamba, Mkenya yeyote ambaye hana<br />

shamba, ama wale ambao wanaitwa squtters, angalau serikali iangalie na iwape kila mtu acre mbili mbili, ili tusije tukawa na<br />

squatters. Miaka arobaini tukijitawala, ni vibaya sana kuwa bado na jambo la squatters.<br />

La nne ni kuhusu trespass. Hili neno trespass lilikuwa wakati wa ukoloni, na mkoloni alileta neno trespass kwa sababu hakutaka<br />

uingie mahali pake wewe mtu mweusi. Lakini sasa saa hii sisi watu weusi wenyewe ndio tunajitawala, neno ‘trespass’<br />

liondolewe kabisa katika Katiba ya Kenya. Mkenya awe huru, anaweza kuingia mahali popote na ahudumiwe. Ukienda mahali<br />

pengine, kama vile reli, kule ukienda pale ndani ya reli, utaambiwa kwamba umekanyaga reli. Na hata ukikanyaga hiyo reli ni<br />

chuma, haiumii lakini utaenda kushtakiwa. Kwa hivyo hiyo maneno ya trespass iondolewe, kila Mkenya awe huru kutembea<br />

mahali popote.<br />

La tano ni kuhusu elimu- education: Ni hivi tu mwaka huu tulitangaziwa na Rais wetu ya kwamba Primary education iwe free,<br />

lakini sisi wazazi bado tunalipa. Ingekuwa bora iwe kwa Katiba kwamba,- na itiliwe maanani- kwamba elimu ya kutokea<br />

standard one mpaka standard eight iwe ni free, na iwe ni free. Sio eti kwamba tunaambiwa ni bure, na hali sisi wazazi huku<br />

tunaambiwa tutoe shilingi mia tano. Hiyo sio bure. Kwa hivyo iwe ni elimu ya bure, vile tulikuwa tukisoma tu zamani. Zamani sisi<br />

tuliposoma, hakuna siku tuliambiwa kwamba utanunua ruler, utanunua vitabu, hivyo vitu ulikuwa ukivipata darasani, mpaka<br />

rubber unapata. Lakini siku hizi tunaambiwa elimu ni ya bure, lakini mtoto kesho anakuja anakwambia kwamba baba,<br />

nimefukuzwa school fees, unashindwa hii school fees mnasema ni ya bure, inatokea wapi. Tafadhali elimu kama ni ya bure, iwe<br />

ndani ya Katiba ni ya bure.<br />

Jambo la sita,- na nitamalizia hapo-, ni kuhusu vyama vya upinzani. Mimi ninapendekeza kwamba tuwe na vyama vya upinzani<br />

vitatu vyenye nguvu. Vitatu pekee yake vyenye nguvu. Hivi vyama vingine vyote vifagiliwe viwekwe kando. Na hivi vyama<br />

vitatu, serikali iwe ikivigharimia tukienda kwa uchaguzi. Na hiyo pia, tukiwa na vyama vichache kama hivyo, tutapoteza ile neno<br />

ambalo kila wakati tunaimbiwa: “ukabila”. Kwa sababu tukiwa na vyama vitatu, tutajumuisha makibila arobaini na mbili yote ya<br />

Kenya na ambapo neno ‘ukabila’ litapotea. Ukabila unatokea kwa sababu, vyama ni vingi na kila kabila kitakuwa na chama

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!