09.03.2013 Views

verbatim report of - ConstitutionNet

verbatim report of - ConstitutionNet

verbatim report of - ConstitutionNet

SHOW MORE
SHOW LESS

You also want an ePaper? Increase the reach of your titles

YUMPU automatically turns print PDFs into web optimized ePapers that Google loves.

Edward Aringo: Mimi naweza kupiga asante kwa serikali ya Kenya kuanza mtindo mpya kama huu...<br />

Com. Nunow: Majina yako kwanza, na ukaribie microphone.<br />

Edward Aringo: Jina langu ni Edward Aringo. Nashukuru serikali kufunguka na hii serikali kufunguka ni Mungu ndiye anatoa<br />

mwangaza. Siku Kenya ilipata uhuru, 1963 December, ilikuwa furaha mingi, wakapea President authority and power. Hii ndio<br />

ilikuwa kitu kibaya cha kwanza kumpa Kenya, ikijua namna ya kuendesha serikali. Maana nataja Mungu, amekwisha ona watu<br />

wengi wanaumia. Na yeye ndiye aliumba watu, ndio akatoa mwangaza waanze sheria kuwa kila kitu ikuwe inatumiwa na<br />

sheria. Wananchi wake wafurahie matunda ya uhuru. Kwa maana siku hizi, ni watu wachache wanao furahia matunda ya<br />

uhuru. Maanake katika Kenya a ¼ ya watu katika Kenya wanafurahia matunda ya na ¾ wana-suffer.<br />

Ya pili ni hii; Ukienda katika location, mshtakiwa anatakiwa atoe pesa kwa sub-chief, na yule mwenye kushtaki pia atoe. Sasa<br />

utajua ni nani ameshtakiwa?<br />

Na kwa koti naona mtu mmoja ndiye anashtaki mtu kwa makosa, na huyo mshtakiwa halipi tena kwa koti. Hii ni kinyume cha<br />

sheria na inafanyika, na watu wengi wanaumia. Na pengeni usipotoa wanasema tunahimiza kesi yako haiwezi kufanyika, na<br />

wewe ndio ulishtakiwa. Ndio maanake nashukuru hii sheria mpya ikuwe inaendesha vitu katika sheria bila kufikiria au<br />

kuonyesha mapendeleo.<br />

Ya pili, nasikia watu wanataja mambo ya chang'aa, pombe na polisi Hii sheria nataka ikuwe hivi, polisi wakija kufanya<br />

inspection katika nyumba ya mtu, aliiba chupa au aliiba jembe, wasije kuhangaisha mwenye nyumba ati kila kitu mtu wanataka<br />

receipt, alinunua namna gani. Ikuwe sheria wanakuja kwa ile kitu kinasikika aliiba. Kwa maana wanaingia katika nyumba,<br />

wengine wanachukua yule bwana wanamtia nje kwa room ya kukaa, na wengine wanaingia katika bedroom, wanachafua vitu<br />

huko kumbe hao ndio wanaiba hivyo vitu. Hiyo yote nashukuru, serikali itie katika sheria. Wakija kutafuta jembe ikuwe<br />

jembe. Hapana radio, leta receipt, kitu fulani, lete receipt, hapana.<br />

Ya tatu, katika Bunyore hapa, nasikia wanazungumuza mambo ya Bunyore na Nyanza. Miaka miwili imepita Luanda county<br />

council ilipewa kuzunguka six square miles kutoka Luanda. Wakaanza kutia signboard pale mileage inafika. Na watu wa<br />

Nyanza waling'oa hiyo signboard, wakatupilia mbali. Nikashindwa kujua hiyo kitu walitia halali au walitia kufuatana na sheria.<br />

Kwa sababu walinyamaza. Kama walijua walipewa six square miles, mpaka saa hii, sijaona hiyo signboard. Mimi ni mtu wa<br />

katikati ya mpaka wa Nyanza na Western.<br />

Ya nne...<br />

Com. Nunow: (Inaudible).<br />

74

Hooray! Your file is uploaded and ready to be published.

Saved successfully!

Ooh no, something went wrong!